Tudai uchaguzi wa haki badala ya kudai kuibiwa baada ya chaguzi

Tudai uchaguzi wa haki badala ya kudai kuibiwa baada ya chaguzi

Si kuwa kina Heche Tarime, Jongwe Mbeya, Bonnie Yai Ubungo na wengine Tunduma huko, tamaa kali ya aina za kina Bulaya imewaingia hawaoni Wala hawasikii?

Hawa wenye maridhiano yao nao je
Tatizo la CHADEMA lipo katika haya uliyoandika hapa.
Kati ya viongozi wake sioni viongozi walio na moto thabiti, pengine nikimuondoa Lissu, na wengine wachache nisiowajua vizuri zaidi.

Wengi wa viongozi hawa hawana tofauti kubwa na wale walioko ndani ya CCM yenyewe.
 
Hata Nelson Chamisa na CCC Zimbabwe waliamini na kusema kama ulivyoandika.

Usisahau:

1. Mahakama ni zao
2. Polisi, tume na wale wengine wote ni wao.

Kwani Jecha ilikuwa je?

"Atakayekwenda kwenye uchaguzi hivi, asitwambie baadaye kaibiwa."

Tukubaliane hili sasa.
Usinielewe vsivyo.
Sijasema popote CHADEMA wakubali upuuzi ufanyike wakati wa uchaguzi huo. Hili la kuzuia uchaguzi tambua lilianzia wapi, kabla ya kuenea kama lilivyo sasa.

Ninachokazia tu hapa, ni kuwa hiyo Katiba Mpya CHADEMA walishaliachia hilo lipite tokea siku nyingi kwa kulaghaiwa tu na Samia.
Sasa hivi wimbo huo wa katiba mpya ni aibu kabisa kuliweka hilo mbele kudanganya wasio na akili kichwani.
 
Tatizo la CHADEMA lipo katika haya uliyoandika hapa.
Kati ya viongozi wake sioni viongozi walio na moto thabiti, pengine nikimuondoa Lissu, na wengine wachache nisiowajua vizuri zaidi.

Wengi wa viongozi hawa hawana tofauti kubwa na wale walioko ndani ya CCM yenyewe.

Alipo LIssu tupo.

Mwabukusi, Mdude na Slaa ni mfano wa kuigwa.

CCM hataachia madaraka kirahisi.
 
Usinielewe vsivyo.
Sijasema popote CHADEMA wakubali upuuzi ufanyike wakati wa uchaguzi huo. Hili la kuzuia uchaguzi tambua lilianzia wapi, kabla ya kuenea kama lilivyo sasa.

Ninachokazia tu hapa, ni kuwa hiyo Katiba Mpya CHADEMA walishaliachia hilo lipite tokea siku nyingi kwa kulaghaiwa tu na Samia.
Sasa hivi wimbo huo wa katiba mpya ni aibu kabisa kuliweka hilo mbele kudanganya wasio na akili kichwani.

Hili la kuzuia uchaguzi binafsi sijalisikia mbali ya uzi huu.

Kama lipo, ni muhimu wadau tujuane. Kwa idadi tuliyopo tunatosha sana.

"Tindo hakuna katiba mpya, hakuna uchaguzi."

Kama mmeshahonga kachukueni pesa zenu.
 
Alipo LIssu tupo.

Mwabukusi, Mdude na Slaa ni mfano wa kuigwa.

CCM hataachia madaraka kirahisi.
Sasa tuanzie hapo, kwa kuwatambua wapiganaji halali wa mapambano haya, tuachane na huu uigizaji mwingi tunaouona hata huko ndani ya CHADEMA yenyewe; lakini, aaah, si ndio CHADEMA tegemeo pekee kwa sasa angalau kuwasumbua CCM, nani mwingine aliyepo sasa hivi?

Tuwachangie mawazo na hali na mali pengine watazinduka na kuona nafasi ya kipekee kabisa iliyopo mbele yao ya kuiondolea Tanzania mkosi huu wa CCM.
 
Hili la kuzuia uchaguzi binafsi sijalisikia mbali ya uzi huu.

Kama lipo, ni muhimu wadau tujuane. Kwa idadi tuliyopo tunatosha sana.

"Tindo hakuna katiba mpya, hakuna uchaguzi."

Kama mmeshahonga kachukueni pesa zenu.
Ni vigumu sana kujua mawazo yote yanayowekwa humu JF na wachangiaji mbalimbali, kwa wingi wa michango hiyo ilivyo.

Hili la kuzuia uchaguzi hata kabla CHADEMA (Mnyika kulitaja), tayari lilishawekwa humu ndani ya JF, siyo kama mada inayojitegemea, bali kama mchango ndani ya mada nyinginezo.

Ukitaka nitafute mchango huo nilioupendekeza CHADEMA waufuate, wakati Magufuli angali hai, itabidi nifanye hivyo. Na si hivyo tu, hadi mapendekezo ya namna ya kuzuia uchaguzi usifanyike yaliwekwa.
 
Sasa tuanzie hapo, kwa kuwatambua wapiganaji halali wa mapambano haya, tuachane na huu uigizaji mwingi tunaouona hata huko ndani ya CHADEMA yenyewe; lakini, aaah, si ndio CHADEMA tegemeo pekee kwa sasa angalau kuwasumbua CCM, nani mwingine aliyepo sasa hivi?

Tuwachangie mawazo na hali na mali pengine watazinduka na kuona nafasi ya kipekee kabisa iliyopo mbele yao ya kuiondolea Tanzania mkosi huu wa CCM.

Kumwondoa CCM hakuwezi kuwa lelemama.

Lazima kutambua:

1. Kwenye hali ya sasa anaweza kutoka je?
2. Tukifanikiwa kupata katiba mpya anatakiwa kutoka je?

CCM siyo wajinga. Tayari hawafungii makampuni yenye kudaiwa au faini.

Tayari wanafukuza watendaji serikalini kwa kadi zao kurudishwa.

Tunayo mengi ya kujifunza kwa Raila Odinga.
 
Ni vigumu sana kujua mawazo yote yanayowekwa humu JF na wachangiaji mbalimbali, kwa wingi wa michango hiyo ilivyo.

Hili la kuzuia uchaguzi hata kabla CHADEMA (Mnyika kulitaja), tayari lilishawekwa humu ndani ya JF. Ukitaka nitafute mchango huo nilioupendekeza CHADEMA waufuate, wakati Magufuli angali hai, itabidi nifanye hivyo. Na si hivyo tu, hadi mapendekezo ya namna ya kuzuia uchaguzi usifanyike yaliwekwa.

Kama ilivyo safari ya mbinguni hayupo mwenye kuwahi au kuchelewa.

Tupe nyuzi zenye hayo. Tujikite huko.

Kuzuia uchaguzi ni hatua njema.

CCM kutoka madarakani yataka njia zote overt and covert. Wasio tayari hata wakikaa pembeni hatutawa miss.

"Enough is enough."

Habari ndiyo hiyo.
 
Kumwondoa CCM hakuwezi kuwa lelemama.

Lazima kutambua:

1. Kwenye hali ya sasa anaweza kutoka je?
2. Tukifanikiwa kupata katiba mpya anatakiwa kutoka je?

CCM siyo wajinga. Tayari hawafungii makampuni yenye kudaiwa au faini.

Tayari wanafukuza watendaji serikalini kwa kadi zao kurudishwa.

Tunayo mengi ya kujifunza kwa Raila Odinga.
Yapo ya kujifunza toka kwa Raila, lakini huyo siyo mfano mzuri hata kidogo. Bahati yake ni moja tu kwamba analo kundi la watu wa kabila lake waliko nyuma yake kufa na kupona. Hapa watu kama hao hawapo.

Kwa hali ilivyo sasa hivi hapa nchini, kutokana na kudidimia kulikofikiwa na CCM, CHADEMA wanayo nafasi nzuri kuliko wakati mwingine wowote wa kuwaondoa madarakani.

Kinachotakiwa tu, ni kwa CHADEMA kujipanga vizuri.
Kuna mfano mzuri wanaoweza kuuangalia wakitazama nyuma kidogo ya historia yao na kuanzia hapo.
Wakati ule wa Kikwete walipopata wabunge wengi zaidi Bungeni, pamoja na kwamba palikuwepo na mazingira magumu katika uchaguzi ule.

Warudi nyuma, waangalie walichofanya wakati ule, na kuweka mikakati ya kuzidisha zaidi na kuiondoa CCM.

Inawezekana sana safari hii kuiondoa CCM madarakani. Wananchi wenyewe wapo tayari kwa hilo..

Ndiyo maana tunawahimiza, wajizatiti tokea sasa kwa kuweka mikakati itakayowezesha hayo yatokee.
Haya siyo maneno matupu, wafungue tu akili na kuwa tayari kupokea ushauri na kuufanyia kazi.
 
Kama ilivyo safari ya mbinguni hayupo mwenye kuwahi au kuchelewa.

Tupe nyuzi zenye hayo. Tujikite huko.

Kuzuia uchaguzi ni hatua njema.

CCM kutoka madarakani yataka njia zote overt and covert. Wasio tayari hata wakikaa pembeni hatutawa miss.

"Enough is enough."

Habari ndiyo hiyo.
Hii ni 'process', na CHADEMA wakubali kuanzia sasa kusuka mikakati hiyo.

Waanzie mwanzo kabisa kujua na kutambua wanayofanya CCM kuharibu chaguzi zote wanazoshiriki wao.

Hiyo ni hatua ya kwanza kabisa. Katiba iliyopo pamoja na ubovu wake siyo nyenzo mojawapo ya kuhalalisha uvurugaji wa uchaguzi.
CCM wanapovuruga uchaguzi, wanavunja katiba hiyo hiyo, pamoja na ubovu huo. Kwa hiyo CHADEMA wawe tayari kukataa kwa nguvu uhalifu huo unaofanywa na CCM.

Sasa ujue, binafsi mimi ni mtu mwenye kupenda kufuata taratibu zilizo ainishwa. Kwa hiyo hapa mwanzo kabisa ni lazima CHADEMA wafanye 'Home work' yao vizuri kabla hatujarukia mambo mengineyo wanayoweza kuyafanya kuhakikisha kwamba haki zao hazidhurumiwi safari hii.

Wakati ni huu, siyo baadae.
 
Yapo ya kujifunza toka kwa Raila, lakini huyo siyo mfano mzuri hata kidogo. Bahati yake ni moja tu kwamba analo kundi la watu wa kabila lake waliko nyuma yake kufa na kupona. Hapa watu kama hao hawapo.

Kwa hali ilivyo sasa hivi hapa nchini, kutokana na kudidimia kulikofikiwa na CCM, CHADEMA wanayo nafasi nzuri kuliko wakati mwingine wowote wa kuwaondoa madarakani.

Kinachotakiwa tu, ni kwa CHADEMA kujipanga vizuri.
Kuna mfano mzuri wanaoweza kuuangalia wakitazama nyuma kidogo ya historia yao na kuanzia hapo.
Wakati ule wa Kikwete walipopata wabunge wengi zaidi Bungeni, pamoja na kwamba palikuwepo na mazingira magumu katika uchaguzi ule.

Warudi nyuma, waangalie walichofanya wakati ule, na kuweka mikakati ya kuzidisha zaidi na kuiondoa CCM.

Inawezekana sana safari hii kuiondoa CCM madarakani. Wananchi wenyewe wapo tayari kwa hilo..

Ndiyo maana tunawahimiza, wajizatiti tokea sasa kwa kuweka mikakati itakayowezesha hayo yatokee.
Haya siyo maneno matupu, wafungue tu akili na kuwa tayari kupokea ushauri na kuufanyia kazi.

Binafsi nimeandika mada kadhaa kwa nini Raila ni mfano mzuri wa kujifunza. Ya msingi:

1. Raila ana uzoefu wa kuipambania haki kwa miongo mingi.
2. Raila kapigania haki tangia enzi ymza chama kimoja, tume za uchaguzi zisizokuwa huru hadi kwenye tume zilizo huru.
3. Raila amewahi ku prevail mahakamani kuhusiana na uchaguzi mkuu.
4. Raila kapambana tokea nje ya chama tawala, ndani ya chama tawala, na pia akiwa na rais aliyeko madarakani madarakani.
5. Raila anajua maana ya agenda ya kudumu, dhidi ya marafiki na maadui katika siasa.
6. Raila anajua kuhamasisha umma. Kudhania kundi lake ni la wajaluo tu itakuwa kutojitendea haki.

Ikumbukwe pamoja naye Raila leo ni Uhuru Kenyatta, Martha Karua, Kalonzo Musyoka na vigogo wengi wengine na vyama vyao ambapo wala si wajaluo.

"Ngoma hii inapendeza kuzicheza kutokea ndani si kutokea nje. Ni Imani yangu aghalabu, yetu kutokea ndani; kuwa hadi leo hakuna lisilofahamika ndani ya Chadema."

Ideas?! Hapana! Ninadhani tatizo kubwa ni kutokukubaliana na Hali halisi.

Niliwahi kuandika mada yenye msingi huu kuwa ilipo Chadema haihitaji mawazo tena. Inahitaji kuchukua hatua tu ndicho kilichobakia.

Ni aibu kuwa chama chenye wanachama 8m+:

a) kinashindwa vipi kufanya maandamano au migomo yenye madanikio?
b) kinashindwa vipi kuzuia uchafuzi wa chaguzi?
c) kinashindwa vipi kushinikiza agenda zaje?
d) nk.

Kwenye chama hiki la kwanza sasa la kufanya ilikuwa ni kupanga safi sahihi za uongozi kidemokrasia na kwa uwazi kabisa kupitia primaries kama kwake Beberu.

Ni muhimu viongozi wenye uthubutu wakakabidhiwa chama, wenye kusita wakapisha damu mpya. Damu mpya ipo na haitakaa kwisha.

"Tusiandike kuwashauri Chadema sisi kama outsiders. Tuandike kujishauri wenyewe kama wenye shughuli."

Utamu wa Ngoma .... tena yakhe!
 
Hii ni 'process', na CHADEMA wakubali kuanzia sasa kusuka mikakati hiyo.

Waanzie mwanzo kabisa kujua na kutambua wanayofanya CCM kuharibu chaguzi zote wanazoshiriki wao.

Hiyo ni hatua ya kwanza kabisa. Katiba iliyopo pamoja na ubovu wake siyo nyenzo mojawapo ya kuhalalisha uvurugaji wa uchaguzi.
CCM wanapovuruga uchaguzi, wanavunja katiba hiyo hiyo, pamoja na ubovu huo. Kwa hiyo CHADEMA wawe tayari kukataa kwa nguvu uhalifu huo unaofanywa na CCM.

Sasa ujue, binafsi mimi ni mtu mwenye kupenda kufuata taratibu zilizo ainishwa. Kwa hiyo hapa mwanzo kabisa ni lazima CHADEMA wafanye 'Home work' yao vizuri kabla hatujarukia mambo mengineyo wanayoweza kuyafanya kuhakikisha kwamba haki zao hazidhurumiwi safari hii.

Wakati ni huu, siyo baadae.

Utamu wa Ngoma ni kuwamo kuicheza. Mfano mzuri ni kwenye hii vita vyao Ukraine:

Wa Ukraine wenyewe ni lazima kuamka kujipigania. Congo ni lazima kuamka kujipigania. Vinginevyo tegemea hujuma na maanguko makuu.

Bahati mbaya sana Chadema napo Pana vijana wengi kwenye Ile irodha ya wasio na mchango wowote kwenye mapambano. Wako kama chawa wa mama tu.

Vijana kama hao hawana mchango wowote na halipo bora kama kuwaweka pembeni.

Hatuwezi kuepuka kupeana makavu:

CHADEMA: Bila kuwapa Makavu hakuna Katiba Mpya
 
Binafsi nimeandika mada kadhaa kwa nini Raila ni mfano mzuri wa kujifunza. Ya msingi:

1. Raila ana uzoefu wa kuipambania haki kwa miongo mingi.
2. Raila kapigania haki tangia enzi ymza chama kimoja, tume za uchaguzi zisizokuwa huru hadi kwenye tume zilizo huru.
3. Raila amewahi ku prevail mahakamani kuhusiana na uchaguzi mkuu.
4. Raila kapambana tokea nje ya chama tawala, ndani ya chama tawala, na pia akiwa na rais aliyeko madarakani madarakani.
5. Raila anajua maana ya agenda ya kudumu, dhidi ya marafiki na maadui katika siasa.
6. Raila anajua kuhamasisha umma. Kudhania kundi lake ni la wajaluo tu itakuwa kutojitendea haki.

Ikumbukwe pamoja naye Raila leo ni Uhuru Kenyatta, Martha Karua, Kalonzo Musyoka na vigogo wengi wengine na vyama vyao ambapo wala si wajaluo.

"Ngoma hii inapendeza kuzicheza kutokea ndani si kutokea nje. Ni Imani yangu aghalabu, yetu kutokea ndani; kuwa hadi leo hakuna lisilofahamika ndani ya Chadema."

Ideas?! Hapana! Ninadhani tatizo kubwa ni kutokukubaliana na Hali halisi.

Niliwahi kuandika mada yenye msingi huu kuwa ilipo Chadema haihitaji mawazo tena. Inahitaji kuchukua hatua tu ndicho kilichobakia.

Ni aibu kuwa chama chenye wanachama 8m+:

a) kinashindwa vipi kufanya maandamano au migomo yenye madanikio?
b) kinashindwa vipi kuzuia uchafuzi wa chaguzi?
c) kinashindwa vipi kushinikiza agenda zaje?
d) nk.

Kwenye chama hiki la kwanza sasa la kufanya ilikuwa ni kupanga safi sahihi za uongozi kidemokrasia na kwa uwazi kabisa kupitia primaries kama kwake Beberu.

Ni muhimu viongozi wenye uthubutu wakakabidhiwa chama, wenye kusita wakapisha damu mpya. Damu mpya ipo na haitakaa kwisha.

"Tusiandike kuwashauri Chadema sisi kama outsiders. Tuandike kujishauri wenyewe kama wenye shughuli."

Utamu wa Ngoma .... tena yakhe!

Mkuu 'brazaj', yapo ya kujifunza toka kwa Raila, binafsi sioni kuwa mfano wa kuigwa na kuwa na manufaa hapa kwetu.
Tusipoteze lengo na kufifisha juhudi hapa hapa kwetu kwa kuweka nguvu nyingi kujaribu kuelewa yaliyoshindikana kwingine.

Tuweke 'focus' yetu kuwaondoa CCM madarakani kwa kuchangia mawazo, hali na mali kwa hawa tulionao hapa wanaojitahidi kuifanya kazi hiyo

Hayo ya waKenya tuwaachie wenyewe, mtindo wao ni wao pekee wanaouelewa.

Hebu kama unao uelewa wowote kuhusu Hichilema wa Zambaia alipitia mlango gani, labda tupe elimu kidogo tuone kama inatufaa nasi hapa.
 
Utamu wa Ngoma ni kuwamo kuicheza. Mfano mzuri ni kwenye hii vita vyao Ukraine:

Wa Ukraine wenyewe ni lazima kuamka kujipigania. Congo ni lazima kuamka kujipigania. Vinginevyo tegemea hujuma na maanguko makuu.

Bahati mbaya sana Chadema napo Pana vijana wengi kwenye Ile irodha ya wasio na mchango wowote kwenye mapambano. Wako kama chawa wa mama tu.

Vijana kama hao hawana mchango wowote na halipo bora kama kuwaweka pembeni.

Hatuwezi kuepuka kupeana makavu:

CHADEMA: Bila kuwapa Makavu hakuna Katiba Mpya
Dah!

Sijui ni vipi tunatofautiana katika kutoa mifano mizuri ya kuwaiga, wakati sote tukiwa tunakubaliana vizuri kabisa katika hoja kuu!
"Ukraine" pamoja na kuamka kujipigania wao, lakini waliingizwa kwenye kichaka kabla hawajagundua kuwa wanaingizwa huko. Hiyo vita imekwisha kuwa balaa kwa nchi yao. Ni bora wangechukua tahadhari kungali mapema zaidi kwa kuelewa hali yao halisi ilivyokuwa toka mwanzo.

Sijui ni Congo ipi unaizungumzia wewe, kama ni hii hii DRC, hii hii iliyokuwa ya Kabila na sasa hivi Tshisekedi. Kama ndiyo yenyewe hiyo, nikupe mfano mahsusi wa ujinga wa ajabu sana waafrika tulio nao. Wanajeshi wa Umoja wa Mataifa wamekaa hapo zaidi ya miaka ishirini, hawafanyi lolote la maana, bali wakizalisha watoto tu haramu, na huku wakilipwa pesa nyingi.
Pesa zote zile zilizotumika kuweka jeshi hilo hapo zingetumika kujenga jeshi imara la waCongo wenyewe hali ingekuwa ni tofauti kabisa na ilivyo sasa.

Kwa bahati nzuri, wananchi wenyewe ndio wamewaamsha akili viongozi wao kuondokana na upuuzi ule.

Kwa hiyo, nikubaliane na wewe juu ya" kuwapa makavu" viongozi wa CHADEMA, pengine ndipo akili zitakapowaingia kichwani.
Hao vijana unaowasema wewe, wapo hivyo kwa sababu ya kukosa uongozi unaowaongoza vizuri kufuata maelekezo ya chama.
Si ajabu wengi wa hao vijana hawana tofauti kubwa na wale tunaowaona kule CCM, kazi yao ni kusubiri tu, chama kichukue madaraka ili wateuliwe uongozi katika ngazi mbalimbali, kama wanavyofanya CCM sasa hivi.
Wapo, wanasubiri tu matunda bila kuvuja jasho.
 
Zimbabwe tayari wapinzani wanadai kuibiwa uchaguzi.

Gabon uchaguzi wao ni leo:

"Huko kwenye mtandao wa internet, TCRA ya huko tayari imeshafanya yake."

Zaidi mno Serikali ya huko imepiga marufuku uwepo wa waangalizi na wanabari wa kimataifa.

1. Twendeni mahakamani,
2. Kampeni zetu ziwe na mwelekeo thabiti - uchaguzi wa haki,
3. Tuunganishe nguvu na wengine wengi, letu kuwa moja:

Ikapate kueleweka waziwazi sasa, kuwa:

"Hakuna katiba mpya, hakuna uchaguzi mkuu (2024 wala 2025)."

Chaguzi za wizi za nini?
_________
Internet cut in Gabon on election day - NetBlocks
hapo ndipo mnapo feli, kuwa bila katiba mpya hakuna uchaguzi?kwa style ya mawazo haya mtakalia mayowe tu kila kukicha badala ya kutumia mikutano yenu ya hadhara kwa manufaa bora ya watanzania nyie mnakalia migomo uchwara ,mkisusa wenzenu wanakula kilaini bila jasho.Tumieni mikutano yenu kwa kuwaeleza wananchi namna ya kuwapa maendeleo na si matusi ,kejeli wala uchochezi wa kuvuruga amani ya taifa hili.wekeni sera zenu vyema na mziishi.
 
Mkuu 'brazaj', yapo ya kujifunza toka kwa Raila, binafsi sioni kuwa mfano wa kuigwa na kuwa na manufaa hapa kwetu.
Tusipoteze lengo na kufifisha juhudi hapa hapa kwetu kwa kuweka nguvu nyingi kujaribu kuelewa yaliyoshindikana kwingine.

Tuweke 'focus' yetu kuwaondoa CCM madarakani kwa kuchangia mawazo, hali na mali kwa hawa tulionao hapa wanaojitahidi kuifanya kazi hiyo

Hayo ya waKenya tuwaachie wenyewe, mtindo wao ni wao pekee wanaouelewa.

Hebu kama unao uelewa wowote kuhusu Hichilema wa Zambaia alipitia mlango gani, labda tupe elimu kidogo tuone kama inatufaa nasi hapa.

Kwa nini model ya Raila naiona si ya kupuuza:

1. Raila kutokea upinzani kwenye Moi era alijiunga KANU. Kutokea huko akaibomoa KANU na kupelekea anguko lake.

Cha kujifunza hapa: kama CCM ina tu infiltrate, tunafanya nini ku wa infiltrate wao?

2. Kwamba Raila alijiunga KANU kwa malengo ya muda mrefu.

Cha kujifunza hapo tusiwaone walioko CCM kama wasaliti bali wengine kama wetu walioko kule kama uwekezaji. Overt na covert lazima kuwa na maana pana na halisi.

3. Kwamba Raila ni tayari Kuwa na timu tofauti. Hili ni jambo la msingi sana.

Cha kujifunza ni kutokushupaza shingo. Kwamba tulitofautiana na awaye yote in the course of struggle haipaswi kuwa ndiyo end of the road. Adui hawezi kuwa kudumu vivyo Kwa rafiki.

Raila ana mengi ya kutufunza kuliko Hichilema. Zingatia Zambia, Kaunda aliangushwa kwenye first multi party election.

Uchaguzi wa kumtoa KANU, CCM, ANC, ZANU PF, MPLA, RPF, NRM hauwezi kuwa sawa na wa Zambia au Malawi leo.

Ninakazia yapo mengi na Raila. Tufungue macho na masikio zaidi tutaweza kuona na kusikia.
 
hapo ndipo mnapo feli, kuwa bila katiba mpya hakuna uchaguzi?kwa style ya mawazo haya mtakalia mayowe tu kila kukicha badala ya kutumia mikutano yenu ya hadhara kwa manufaa bora ya watanzania nyie mnakalia migomo uchwara ,mkisusa wenzenu wanakula kilaini bila jasho.Tumieni mikutano yenu kwa kuwaeleza wananchi namna ya kuwapa maendeleo na si matusi ,kejeli wala uchochezi wa kuvuruga amani ya taifa hili.wekeni sera zenu vyema na mziishi.

Hapa ndipo mnapo feli Kwa kudhani hii ngoma ni ya kuchezwa na Lissu, Mbowe au Chadema fulani, kama vipi ya kuwakuta yawakute wao ila si ninyi. Ninyi ni watu wa kula matunda tu.

"Utamu wa ngoma ni kuingia kuzicheza."

Itambulike Chadema ilipo inahitaji vitendo si mawazo. Namma ya kuwatimua CCM madarakani hayupo asiyejua Hilo hadi sasa.
F4coIWrWkAI9Dlw.jpeg


Tofautisha kususa na kuusimamisha uchaguzi usiwepo.

Uchaguzi ambao wizi unaruhusiwa utashinda vipi wewe kama si mdau kwenye huo ujamba wazi?

Kwani unadhani Munangagwa kashinda uchaguzi au katangazwa tu kushinda?

"Tunao uwezo wa kushinikiza uchaguzi kuwa wa haki."

Hii ni njia moja ambayo, inajulikana kuwa:

1. Chawa wa mama hawawezi kuipenda.
2. CCM na vibaraka wao hawawezi kuipenda.
3. Wasiojulikana hawawezi kuipenda.
4. Wenye uchu wa ubunge Chadema ba upinzani design ya kina Bulaya hawawezi kuipenda.
5. Nk

Kwani wewe ni yupi katika hao ndugu?
 
Dah!

Sijui ni vipi tunatofautiana katika kutoa mifano mizuri ya kuwaiga, wakati sote tukiwa tunakubaliana vizuri kabisa katika hoja kuu!
"Ukraine" pamoja na kuamka kujipigania wao, lakini waliingizwa kwenye kichaka kabla hawajagundua kuwa wanaingizwa huko. Hiyo vita imekwisha kuwa balaa kwa nchi yao. Ni bora wangechukua tahadhari kungali mapema zaidi kwa kuelewa hali yao halisi ilivyokuwa toka mwanzo.

Sijui ni Congo ipi unaizungumzia wewe, kama ni hii hii DRC, hii hii iliyokuwa ya Kabila na sasa hivi Tshisekedi. Kama ndiyo yenyewe hiyo, nikupe mfano mahsusi wa ujinga wa ajabu sana waafrika tulio nao. Wanajeshi wa Umoja wa Mataifa wamekaa hapo zaidi ya miaka ishirini, hawafanyi lolote la maana, bali wakizalisha watoto tu haramu, na huku wakilipwa pesa nyingi.
Pesa zote zile zilizotumika kuweka jeshi hilo hapo zingetumika kujenga jeshi imara la waCongo wenyewe hali ingekuwa ni tofauti kabisa na ilivyo sasa.

Kwa bahati nzuri, wananchi wenyewe ndio wamewaamsha akili viongozi wao kuondokana na upuuzi ule.

Kwa hiyo, nikubaliane na wewe juu ya" kuwapa makavu" viongozi wa CHADEMA, pengine ndipo akili zitakapowaingia kichwani.
Hao vijana unaowasema wewe, wapo hivyo kwa sababu ya kukosa uongozi unaowaongoza vizuri kufuata maelekezo ya chama.
Si ajabu wengi wa hao vijana hawana tofauti kubwa na wale tunaowaona kule CCM, kazi yao ni kusubiri tu, chama kichukue madaraka ili wateuliwe uongozi katika ngazi mbalimbali, kama wanavyofanya CCM sasa hivi.
Wapo, wanasubiri tu matunda bila kuvuja jasho.

Kutofautiana mawazo au hata Kwa mifano ni jambo la heri wala si tatizo.

Ukraine - hiyo itapiganiwa na wa Ukraine wenyewe. Ni chaka au si chaka hilo uamuzi wao ura prevail kama taifa. Ama kwa hakika ninayo heshima kubwa saba kwa kukomaa their way. Ni heri kufa ukipigania haki yako, kuliko kuishi ukiwa kwenye magoti ukiwanyenyekea watesi wako.

Congo DRC amani yao haitaletwa na MONUSCO, SADC, EAC, Angola au Uganda au majeshi yao hali wao wakicgeza ndombolo ya solo.

Tanzania hatutatoboa Kwa kuwaachia Lissu, Mbowe au Chadema tusiyokuwa tayari kujinasibu nayo kama yetu kinagaubaga.

Ninachoongelea hapa ni kuwa tuepuke kuwashauri Chadema sisi kama wakuja. Yaani sisi kutokea nje. Kwani huko nje ni wapi hasa? CCM au ACT?

"Tushauriane tukiwa ndani. Itapendeza zaidi."

Hii nchi inatuhitaji sote tena tukiwa ndani kweli kweli.

F4coIWrWkAI9Dlw.jpeg


Ushindi mbona hauko mbali?
 
Back
Top Bottom