Tuendako hali inatisha. Sasa maharage yanakimbilia kilo moja elfu 4 (4,000)

Tuendako hali inatisha. Sasa maharage yanakimbilia kilo moja elfu 4 (4,000)

je parle

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2018
Posts
2,022
Reaction score
3,919
Jana nafika dukani usiku kununua maharage kilo naambiwa 3,800 na kesho huenda tukapandisha kuwa elfu 4 kamili.

Nimeshindwa kuelewa shida ipo wapi maana mwezi wa nne yalikuwa 1,700 yakapanda 2,000 hadi 2,400 sasa huku tunapoenda tutakula tu ugali na kachumbari. Vitu vyote vimekuwa juu mno, kama unaishi kwenu huwezi kulijua hili.

Ukienda sokoni unaweza kuzimia, maana nazi nzuri inaanza 1,400 mihogo ndio usiseme, viazi vitamu ndio usiulize hata bei mana ndoo ndogo ilikuwa elfu 5 hadi 7 sasa hivi ni elfu 12.

Hii nchi tunapoenda tutauana kwa njaa, watu hawashibi ndio maana wana kuwa na stress za hapa na pale.

Note, nadhani wakulima mwaka huu watajenga maghorofa kama madalali sio wanaopandisha bei.
 
Tule Mboga za majani mchicha haujapanda bei Bado

Mchele umeshuka Bei huku Tandika kilo-moja 2400/ 2200 unapata so ukitaka nunua chakula nenda sokoni Mkuu

Pia hapo nyumbani waambie waishi kwa bajeti kula maharage kila siku sio chakula Bora hata mchicha
 
Wakulima walime basi au wamechoka?
Wanalima je wakati hakuna mvua ?

Wanalima je wakati hawana pesa ya pembe jeo?

Msimu ulio pita mvua ilikua haba.

Watu hawakupata mavuno ya kutosha

Hiyo nikwa mikoa ya nyanda zajuu kusini.

Bado kwa mikoa ya Kanda ya ziwa wanako pata mvua misimu miwili Nako imebuma.

Mbaya zaidi 2020 /2021 wakulima wengi walipata hasara na kushindwa kurudi shambani Kutokana na uwepo wa Bei hafifu.

Hii Khali imeanzia mbali Huku watu wakitazama na kushangilia.

Kila mmoja alikaa kimya kwakujiona hausiki kwanamna yeyote.

Acha tupambane na Khali zetu.
 
Wanalima je wakati hakuna mvua ?

Wanalima je wakati hawana pesa ya pembe jeo?

Msimu ulio pita mvua ilikua haba.

Watu hawakupata mavuno ya kutosha

Hiyo nikwa mikoa ya nyanda zajuu kusini.

Bado kwa mikoa ya Kanda ya ziwa wanako pata mvua misimu miwili Nako imebuma.

Mbaya zaidi 2020 /2021 wakulima wengi walipata hasara na kushindwa kurudi shambani Kutokana na uwepo wa Bei hafifu.

Hii Khali imeanzia mbali Huku watu wakitazama na kushangilia.

Kila mmoja alikaa kimya kwakujiona hausiki kwanamna yeyote.

Acha tupambane na Khali zetu.
Kazi ya kilimo Ni sawa na kuwa Mwalimu unabidi kujitoa Sana malipo atalipa Mungu.
 
Watu mnakejeli tu huu uzi , ni kweli kabisa wanaoishi vijijini ndio wanatambua hali jinsi ilivyo ngumu, ukichanganya na haya matozo yasiyokuwa na kichwa wala miguu yaani moto unawaka kweli kweli, kwa mnaoshinda kwenye viyoyozi na kulipwa miposho isiyoeleweka lazima mlete kejeli tu na dharau, vyakula sio vimepanda tu bei havishikiki.
 
Back
Top Bottom