Tufanye Check-Up Mara kwa Mara


hahahahaha kwelI kabisa mkuu
 
Duh! Kazi kweli kweli. pole Profesa kwa kipimo hicho!
 
Sekundi chache za kupima Prostate zinaweza kuokoa maisha yako!
 
Mods kuachia mada ya namna hii ni kumkosea heshima rais wetu! Mnashiriki kumdhalilisha kiongozi wa nchi. Mtoa mada anastahili kushtakiwa kwa kumdhalilisha rais!
 
Mkuu naona umeifurahia sana mada, wewe na mtoa mada huwa mnafanya chekups za namna hiyo mara kwa mara

Ndiyo ninafanya check-up kila mwaka. Na ninafurahi daktari anaponiambia prostate yangu haina tatizo! Mungu akubariki. :smile-big:
 
Mods kuachia mada ya namna hii ni kumkosea heshima rais wetu! Mnashiriki kumdhalilisha kiongozi wa nchi. Mtoa mada anastahili kushtakiwa kwa kumdhalilisha rais!

Aisei, nia yangu si kumdhalilisha Rais. Nia yangu ni kuokoa maisha yenu. Prostate Cancer inatibika ukiiwahi. Lakini utajuaje kama unayo au huna kama huendi kupima? :sick:Mungu akubariki.
 
.. Zekidon ndomana mkuu kaenda nje kutibiwa maana kama ndiyo hivyo angetibiwa muhimbili ingekuws balaaa,
hata uwe jeneralI, billgates, prezidah etc kidole hakikwepeki kutokana na maelezo ya wataalam hapa
 
Last edited by a moderator:
Aisei, nia yangu si kumdhalilisha Rais. Nia yangu ni kuokoa maisha yenu. Prostate Cancer inatibika ukiiwahi. Lakini utajuaje kama unayo au huna kama huendi kupima? :sick:Mungu akubariki.
Kichwa maji
 
Mhnnnnn......ugonjwa fedhea! Haijarishi unaunwa nini na wapi, cha msingi kutibiwa. Zingatieni ushauri. Huku nilipo razima ku-check kila mwaka vinginevyo ajira hakuna. Nikasikia once check up hiyo ilikuwa ikifanywa na mwanamama daktari bingwa. Nahisi kulikuwa na malalamiko kidogo juu ya hilo maana huduma hiyo ilisitishwa. Kwa elimu hii nitaiibua tena. Bora afya njema.....hayo mengine ni kwa kuwa tunao uzima na afya njema.

Asante mkuu, usijari maana posts nyingine zaweza kukukera.

Asante pia kwa mods maana uzi huu ungekuwa huko hoja mchanganyiko nami nisingeuona.

Watani zetu magamba wautembelee pia ndo wajue facts za jf!
 
Mods kuachia mada ya namna hii ni kumkosea heshima rais wetu! Mnashiriki kumdhalilisha kiongozi wa nchi. Mtoa mada anastahili kushtakiwa kwa kumdhalilisha rais!
Hii nchi ya ovyo kweli.

Pinda alisema mafisadi wakikamatwa nchi itayumba, huo ugonjwa watanzania wameumwa wengi kwa miaka mingi lakini sasa wamepona.

Fistula wameumwa mama zetu wengi tu na sasa wamepona, Kinachofanyika sasa kupitia huu ugonjwa najua wengi watajitokeza kupima na kutibiwa bila wasiwasi maana wanajua yoyote anaweza kuupata.

Ushauri wangu MH. awe ni balozi wa huu ugonjwa ili watu wengi watibiwe na asisite kutoa ushuhuda pale inapobidi.
 
siyo kidogo mkuu nime elewa sana tu, ila swali lingine dogo, mkuu sasa ugonjwa huo unatofauti gani na mabusha kwa wanaume kuvimba (..........) au tofauti?

Asante kwa kunielewa mkuu,sasa kwa swali lako dogo hilo ni kwamba tatizo hilo la mabusha kuvimba linaitwa Hydrocele.
Tofauti ni kwamba hiyo Hydrocele ni collection ya maji, generally in the tunica vaginalis of the testes (Hivyo inasababisha uvimbe mkubwa kwenye scrotum,wakati Hiyo BPH yaani benign prostatic hyperplasia ni uvimbe kwenye tezi (gland) ambayo iko ndani.Hyperplasia maana yake ni kuongezeka kwa idadi ya cells (an increase in number of cells) na hivyo kusababisha uvimbe.

Hydrocele utaiona mwenyewe ule uvimbe wa scrotum wakati BPH mara nyingi lazima ufanye rectal examination (kuingiza kidole kwenye njia ya choo) na hata kufanya ultrasound kujua size ya uvimbe huo.

Kumbuka BPH ni idadi ya cells kuongezeka (hyperplasia) au cells kuvimba (hypertroph) wakati HYDROCELE ni collection ya maji kwenye scrotum.
 

Matola, sio kila mtu ni mbumbumbu...kama mleta mada alikuwa na nia ya dhati ya kuelemisha namna Prostate cancer inavyokuwa diagnised kwa nini ameacha aina nyingine ya vipimo?

Labda nikusadies, unaweza kupima kwa kufanya DRE exam (njia aliyotaja mleta mada) au PSA (blood tets). Kwanini ameacha kusema kuhusu PSA test? Na amejuaje kuwa rais ametumia DRE na PSA test?

Mwisho, nilidhani mada (kama heading ya thread inavyosema) inahusu umuhimu wa kufanya check-up mara kwa mara. Lakini inaelekea nia ilikuwa kuelezea DRE test!
 
Ngoja nimsaidie kidogo mtoa mada, ukifanyiwa checkup mara kwa mara ni vizuri kwa sababu ukikutwa nayo utatolewa na utaendelea vizuri sana na maisha yako. Ukijagundulika unayo na imeshakuwa kubwa mara nyingi hugeuka kuwa cancer kwa sababu hutolewa( biopys ) sijui kama nimeandika sawa wataalam watanisaidia ili ipimwe kama imefika stage gani wajue utapewa matibabu gani kama stage ni mbaya utaishia ocean road na kwa kuwa itakuwa imeguswa ndio balaa kubwa kifo kinakuhusu tena cha maumivu sana. Nimeshauguza mgonjwa wa hiyo kitu alichelewa bila kujua tatizo la ugonjwa alimripotia dokta wake mara kwa mara ishu ya mkojo kutoka mara kwa mara, lakini dokta akamwambia ni kwa sababu unatumia dawa za moyo, mwisho anakuja kumpima anamwambia umechelewa imekuwa kubwa, kwa matatizo aliyoyapata kifo cha maumivu alichokufa, nisingependa kuona mwanaume mwingine anapitia hayo maumivu, nawaomba wanaume kapimeni tu kwani kidole kina shida gani? Maana hili gonjwa sikia tu cancer inakufanya ukojoe kwa kutumia mpira na ni damu inatoka kuchanganyika na mkojo, acheni hapa naandika nasikia uchungu si ya kuyashudia. Labda mtu aende ocean road kutembelea wagonjwa akute wa ugonjwa huu ataelewa na ataenda kuinama mwenyewe.
 
Check up nchi hii ngumu kaka... Walioko mahututi wenyewe matibabu mgogoro sasa check up so ndio balaa kabisa?
 
Kupigwa dole hospitali za hapa nchini ni noma,lazima ivume kwenye vyombo vyote vya habari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…