Tufanye nini na hizi clip zinazopotosha Historia ya Tanzania?

Tufanye nini na hizi clip zinazopotosha Historia ya Tanzania?

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Kuna clip inazunguka mitandaoni ikieleza mengi kuhusu Tanganyika.
Kubwa linaloshtua watu wengi ni kusema imani kuu nchini ni Ukristo.
Nimeandika makala hiyo hapo chini kutanabaisha kuhusu historia ya Tanganyika nikijaribu kueleza imekuwaje tumefikia hali hii:

MEETING OF THE MINDS​

Alikuwa Dr James Kwegyir Aggrey, Mwafrika kutoka Ghana ndiye mtu aliyemtia Kleist hamu ya kuingia katika siasa. Dr Aggrey alikuja Tanganyika mwaka 1924.

Dr Aggrey alikuwa katika Phelps-Stokes Commissions iliyokuwa imeundwa kuchunguza elimu ya Waafrika.

Ilikuwa katika kipindi hiki akiwa ndani ya kamisheni hii ndipo alipokuja Tanganyika. Dr Aggrey alikataliwa kupanga New Africa Hotel kwa kuwa alikuwa mtu mweusi.

Ikabidi Gavana Donald Cameron amtafutie chumba Government House ajisitiri kwa malazi.

Wakati huu alipokuwa Dar es Salaam ndipo Dr Agrrey alipokutana na Kleist.
Dr Aggrey alimtunukia Kleist moja ya vitabu vyake na akakitia sahihi yake.

Hakuna hata mtoto mmoja wa Kleist ambae anakumbuka jina la kitabu hiki.

Kleist alikithamini kitabu hiki na kilipamba shubaka lake la vitabu kwa miaka mingi.

Mwaka wa 1929 Kleist na baadhi ya rafiki zake wa karibu kama Mzee bin Sudi, ambaye wazazi wake walikuwa Wamanyema kutoka Belgian Congo, Ibrahim Hamis - Mnubi ambaye baba yake alitoka Daffur nchini Sudan, Zibe Kidasi, Ali Said Mpima - Mzaramo, Suleiman Majisu, Raikes Kusi, Rawson Watts na Cecil Matola - Myao kutoka Masasi walianzisha African Association, Matola akiwa President na Kleist Secretary.

Historia ya uhuru wa Tanganyika iligeuzwa ikawa historia ya Julius Kambarage Nyerere.

Historia ya TANU ikawa historia ya mtu mmoja.

Hili lilifanikiwa kwa kuwa tulikaa kimya lau kama walikuwapo wazalendo wenyewe walioupigania uhuru kwa hali na mali zao.

Sasa tueleze harakati za uhuru wapi zilianzia.
Tunaweka picha ya Dictionary of African Biography (DAB).

Kinawekwa kipande kifupi kinachomweleza Dr. Kwegyir Aggrey (1875 - 1927) kisha ndani ya Kamusi hilo hilo tunatoa na kumwekea mtazamaji wa clip yetu kipande kifupi cha Kleist Abdallah Sykes (1894 - 1949).

Wazalendo hawa waliotajwa ndani ya Kamusi hilo tunaeleza hawamo katika historia rasmi ya Tanganyika.

Mazungumzo kati ya Waafrika hawa wawili Dar-es-Salaam mwaka wa 1924 ndiyo yalisababisha Kleist kuunda African Association mwaka wa 1929 kisha kuunda Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) mwaka wa 1933.

Vyama vyote hivi viwili vilitawaliwa na Waislam.

Watafute wazalendo hawa katika historia ya Tanganyika hutowakuta popote.
Jambo la kusikitisha ni kuwa watu waliamini kuwa ile historia iliyokuwa ikisomeshwa ndiyo historia ya kweli.

332955155_3398442657098751_5156298518240527622_n.jpg

Kleist Abdallah Sykes
333027833_3114434315528253_5075425198623726105_n.jpg

Dr. Kwegyir Aggrey

332914989_1164916214133995_6225086038975879163_n.jpg

Dictionary of African Biography
(DAB)​

Picha ya juu ni Kleist Abdallah Sykes, inayofuata ni Dr. Kwegyir Aggrey na chini ni Dictionary of African Biography.

Ninaposomesha historia ya utaifa wa Tanganyika huanza kwa kuwapa wanafunzi wangu rejea katika Dictionary of African Biography (DAB) niwaambia wamsome Dr. Aggrey wakimaliza wamsome Kleist Sykes.

Kipande hiki nimekipa jina: ''Meeting of the Minds.''
 
Sawa. Imani kubwa hapa nchini ni Uislamu. Waislamu ndio waliongoza mapambano yote ya kudai uhuru. Ukoo wa Sykes ulikuwa na nafasi ya kipekee katika mapambano hayo. Kinachosikitisha ni kuwa Nyerere aliwasahau kabisa baada ya uhuru na maisha yao kama ilivyokuwa kwa waislamu wengi yalikuwa duni.

Kabla ya uhuru waislamu walikuwa na shule na hospitali nyingi ambazo Nyerere alizitaifisha ili kuwapa nafasi wakristu wenzake wafikie kiwango cha elimu na ustaarabu wa waislamu. Hakuishia hapo, alihakikisha kuwa maksi zote za vijana wa kiislamu katika mitihani zilikuwa zinabadilishwa na kupewa wakristu. Nyerere huyo huyo alitaifisha mali za waislamu na kuwapa wakristu.

Hali hiyo iliendelezwa na Mkapa ambae aliondoa mazuri yote yaliyofanywa na Mwinyi. Mkapa alifikia hatua ya kuchukua chuo kikuu cha taasisi ya serikali na kukikabidhi kwa wakristu wenzake. Hali ilikuwa nzuri kidogo wakati wa Jakaya lakini John alipoingia aliharibu tena. Sasa hivi kidogo inaenda vizuri baada ya Mheshimiwa Samia kuwa Rais. Hawa wakristu hasa wakatoliki sio watu wa kuwafanyia masihara kabisa.

Amandla...
 
Dunia tunaishi kwa hisani ya ukristo. Mungu ndiyo ana hukumu, fanya dhambi ila Mungu mwenye nguvu atakuhumu.

Iran mwanamke hajafunika kichwa wanamuua. Wewe hauna dhambi mpaka umuue mwenzako? Dini ina mahakama? Ahaaa

Wewe ni nani unihukumu mimi? Ingekuwa dini ni ya Mungu huko Uarabuni ambako uislam umezaliwa ingekuwa ni sehemu salama za kuishi na zingekuwa zimebarikiwa sana.

Pale Zanzibar, watu wakifunga wanaanza kuchapa watu viboko. Ule saa 9 au saa 10 halafu saa 7 mchana umuone mtu anakula ubebe kiboko anakutamanisha.

Umefunga kula au umefunga ili uache dhambi? Imani yako kwanini iwe kero kwangu?

Mimi ni mpagani (sina dini)
 
Puna,
Limepita hilo ndugu yangu.
Clip hiyo hapo chini:


Mzee Mohamed hiyo Clip ina makosa mengi,pia naamini kabisa anayezungumza sio Mtanzania. Ni ya kuipuuza tu Mzee wangu.
 
Mzee Mohamed hiyo Clip ina makosa mengi,pia naamini kabisa anayezungumza sio Mtanzania. Ni ya kuipuuza tu Mzee wangu.
Puna,
Haya si ya kupuuza.
Haya ni ya kurekebishwa
 
Kumbe umeitoa Tiktok! Umeona hilo la dini lakini la lugha hukuliona. Tiktok ni kama jina lake lilivyo. Ruksa mtu yeyote kujisemea anachotaka. Hakuna mtu makini anayewachukulia serious.

Amandla...
Fundi...
Mimi nawachukulia kwa uzito utakiwao.
 
Unaangalia kila kitu kwa miwani ya dini inakua ngumu kuKuchukulia seriously.

Kiarabu ni official language TZ? Kama ni official language Znz, kwanini hujalalamika huyo mtu kusema ni official language hadi TZ mainland?
 
Kama Kiarabu ni official language Zanzibar basi ni ruksa kutumika katika Baraza la Mapinduzi na mawasiliano ya kiserikali.

Amandla...
 
Back
Top Bottom