Tufikie hatua tutumie akili na tuambiane ukweli. Wazungu wanatuua kirahisi tu

Tufikie hatua tutumie akili na tuambiane ukweli. Wazungu wanatuua kirahisi tu

Wazungu wakitaka kuiangamiza Afrika,hawaitaji kutumia chanjo yoyote au kuja kimya kimya,
Walifanya hivyo 1884,mkutano wa berlin,wakaigawa Afrika,ukoloni,utumwa,kwa miaka zaidi ya mia!
Wazungu walisambaratisha Dola ya kisoviet,
Kwame Nkurumah,Lumumba,Samora,Savimbi,Ghadafi wote Hawa walisambaratishwa na wazungu,wakati Iraq na Libya zinatwangwa na mabomu Afrika nzima ilifyata mkia,hakuna aliyesema kitu,Kama Wazungu(Usa,UK,Canada,Austaria,New Zealand,Japan,)wanaitetemesha Urusi,Iran,Korea,mpaka zinashika adabu,sembuse vi nchi 52 vya Afrika,
Ukikusanya uchumi wa nchi zote hizi za Afrika,hazifikii uchumi wa India,
Jimbo moja la USA lina uchumi mkubwa kuriko nchi nyingi za Afrika,
Sie hatuzalishi kitu ambacho wazungu hawawezi kupata kwingine,sie sio wanuhimu sana kwao,
Hizi porojo za Jiwe,ni upuuzi mtupu,Magari,Ndege,vyote vinatoka kwao,sie kaI yetu ni kuzaa tu
 
1. KWANZA, chanjo ya COVID 19 hakuna anayeweza kuizuia isiingie katika kila nchi. Hapa Tanzania hata tupige kelele za namna gani, itaingia na Magufuli hana ubavu Wa kuzuia kwa sbb na yeye ni mtu tu kama mimi na we we..

2. PILI, kama hili la chanjo hii ni ishu ya imani, hebu tujiulize tangu lini watanzania milioni 60 tumekuwa na imani moja? Si kila mtu ana imani yake na mungu wake? Kwani Magufuli kawa in charge wa imani ya kila Mtanzania?

3. TATU, kwa sisi wakristo, tunaamini kuwa haya hayana budi kutukia na kumkuta kila mtu. Aliyesimama imara kiimani kwa Mungu muumba, hawezi kupokea chanjo hii iwapo kweli itathibitika ni kinyume na mapenzi ya Mungu...!

4. NNE, maswala ya imani Mungu kayaacha wazi mtu achague mwenyewe njia anayotaka kuiendea. Tukichagua kuwa upande wa Mungu, HAKIKA TUTAPONA..

Tukichagua kumtumukia shetani, tutaangamia tu. Maana imeandikwa hivyo..

Mungu wetu muumba, ni very Democratic. Hamlazimishi mtu kuja kwake. Isipokuwa ameweka njia zote wazi. Akatupa utashi na akili za kuchagua lililo jema...

Mungu huruhusu mambo fulani yenye kuumiza ili kupima imani yetu....

Kama chanjo ya COVID 19 imebeba alama ya ANT-CHRIST yaani 666 na kila mtu akajua hivyo, kwanini uogope kukutana nayo na kisha kuikataa? Imani yako itakuwa iko wapi sasa kama hili halitakuja?

Nasema tena, hakuna mtu wa kuzuia hili. Si Rais Magufuli wala nani. Anayeweza kuzuia baya lolote lisimpate ni mtu mwenyewe binafsi kupitia IMANI YAKE katika Mungu. Huyu atazuia na atapona...!!
 
Mtu anaenda shuleni ila akirudi nyumbani anakua hayawani kuliko wasioenda shule. Hii nchi bora tufute shule tu hazina msaada kwenye kuwakomboa watu kifikra
 
Sawa basi kama ni hivyo huyo Raisi wenu wa CCM angeongelea MADHARA ya chanjo na sio kuongea na kuzua uongo kuhusu NIA ya chanjo ya Corona

Ifikie mahali muwe na shukrani mnasaidiwa mangapi na hao mnao waita MABEBERU ???
 
Back
Top Bottom