Tufumue mfumo wetu wa soka kwa kuingia mkataba na Ujerumani

Tufumue mfumo wetu wa soka kwa kuingia mkataba na Ujerumani

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Tanzania tumekuwa tunahangaika kutafuta dawa ya matatizo yetu ya mpira. Uzuri mmoja katika soka letu tuna desturi nzuri ya timu za Simba na Yanga ambapo ni mtaji mzuri sana. Kwenye timu ya taifa au mashindano ya kimataifa ya vilabu tumeendelea kuwa dhaifu ukiacha mafanikio ya mara kwa mara ya Simba 🤣😂

Leo nitagusia dawa mojawapo kwa upande wa timu ya taifa.

Nchi hii inabidi turudi square one kwenye soka letu. Tubadilishe kabisa ufahamu wetu wa jinsi tunavyocheza mchezo huu. Kuangalia mpira wa EPL umetuharibu zaidi, Waingereza wanapenda sana mpira ila ligi yao na style yao siyo sahihi kwetu.

Ushauri wangu tuingia mkataba na nchi kama Ujerumani (SIYO UINGEREZA) na waanzishe Academy yao hapa.

Ujerumani ndiyo nchi iliyofanikiwa kubadilisha kabisa style yao ya mpira na sasa wako level ya juu kabisa hadi anaeeza kumpiga Brazil goli 7.

Hii leo tunaleta kocha wa Ufaransa, kesho tunaleta Mwingereza, keshokutwa Mbrazil ni kuwachanganya tu wachezaji. Tukumbuke wachezaji wetu hawana foundation nzuri ya mpira kuweza kumeza mabadiliko haya yote ya kimfumo.

Ikiwezekana, hata vilabu vyetu vyote visisitizwe kuchukua programs zitakazoletwa na wataalamu hao wa Kijerumani ili kujenga style inayoshabihiana. Inakuwa rahisi mchezaji anapofikia timu ya taifa, anakuwa zile basic concept ameanza kuzipata. Hili liendani na kupeleka makocha na wakufunzi Ujerumani ( au hiyo Academy iwe pia na program ya makocha).

Ningesema Spain au Uholanzi ila naenda na Ujerumani maana tuna historia nao zaidi na wameonyesha uwezo wa kubadilisha mpira wao. Pia naona kama Ujerumani alichukua sehemu ya style za Spain na Uholanzi.

Kutokea hapo tutakuwa na wachezaji wa kuuza kwenye ligi kubwa duniani (ingawa wengine watabadili uraia ila hilo haliepukiki) na mwisho wa siku tutapata wachezaji wazuri wa timu ya taifa.
 
Tanzania tumekuwa tunahangaika kutafuta dawa ya matatizo yetu ya mpira. Uzuri mmoja katika soka letu tuna desturi nzuri ya timu za Simba na Yanga ambapo ni mtaji mzuri sana. Kwenye timu ya taifa au mashindano ya kimataifa ya vilabu tumeendelea kuwa dhaifu ukiacha mafanikio ya mara kwa mara ya Simba [emoji1787][emoji23]

Leo nitagusia dawa mojawapo kwa upande wa timu ya taifa.

Nchi hii inabidi turudi square one kwenye soka letu. Tubadilishe kabisa ufahamu wetu wa jinsi tunavyocheza mchezo huu. Kuangalia mpira wa EPL umetuharibu zaidi, Waingereza wanapenda sana mpira ila ligi yao na style yao siyo sahihi kwetu.

Ushauri wangu tuingia mkataba na nchi kama Ujerumani (SIYO UINGEREZA) na waanzishe Academy yao hapa.

Ujerumani ndiyo nchi iliyofanikiwa kubadilisha kabisa style yao ya mpira na sasa wako level ya juu kabisa hadi anaeeza kumpiga Brazil goli 7.

Hii leo tunaleta kocha wa Ufaransa, kesho tunaleta Mwingereza, keshokutwa Mbrazil ni kuwachanganya tu wachezaji. Tukumbuke wachezaji wetu hawana foundation nzuri ya mpira kuweza kumeza mabadiliko haya yote ya kimfumo.

Ikiwezekana, hata vilabu vyetu vyote visisitizwe kuchukua programs zitakazoletwa na wataalamu hao wa Kijerumani ili kujenga style inayoshabihiana. Inakuwa rahisi mchezaji anapofikia timu ya taifa, anakuwa zile basic concept ameanza kuzipata. Hili liendani na kupeleka makocha na wakufunzi Ujerumani ( au hiyo Academy iwe pia na program ya makocha).

Ningesema Spain au Uholanzi ila naenda na Ujerumani maana tuna historia nao zaidi na wameonyesha uwezo wa kubadilisha mpira wao. Pia naona kama Ujerumani alichukua sehemu ya style za Spain na Uholanzi.

Kutokea hapo tutakuwa na wachezaji wa kuuza kwenye ligi kubwa duniani (ingawa wengine watabadili uraia ila hilo haliepukiki) na mwisho wa siku tutapata wachezaji wazuri wa timu ya taifa.
Sikiliza wewe soko ni pesa, angalia Waarabu anagalia Egypt wanafanya vyema kwa sababu ya uchumi wa nchi yao ni mzuri sana.

Unaingia ushirikiano na Ujerumani iweje? Uwanjani mnaingia kuchangia vilabu? Yanga na Simba pale kwa mkapa kama zinakutana na timu za mikoani huwa hata nusu uwanja unajaa?

Jezi mnamudu kununua jezi mpya kila msimu ili club ipate pesa?

Sikiliza soka ni pesa na si vinginevyo, kama mashabiki wenyewe hawachangii cluba kwa kuingia uwanjani na kununua jezi unategemea miujiza ipi?
 
Kwa hiyo nchi za kiafrika zilizofanikiwa kisoka zinacheza stahili ya kijerumani?
 
Akili kisoda wewe,
Nikadhani unasema tupeleke vijana huko hata 100 kwenye academy zao ili baadae tuwe na kizazi kipya chenye exposure ya timu za Ulaya wewe unatuletea mambo ya bongo
 
Sikiliza wewe soko ni pesa, angalia Waarabu anagalia Egypt wanafanya vyema kwa sababu ya uchumi wa nchi yao ni mzuri sana.

Unaingia ushirikiano na Ujerumani iweje? Uwanjani mnaingia kuchangia vilabu? Yanga na Simba pale kwa mkapa kama zinakutana na timu za mikoani huwa hata nusu uwanja unajaa?

Jezi mnamudu kununua jezi mpya kila msimu ili club ipate pesa?

Sikiliza soka ni pesa na si vinginevyo, kama mashabiki wenyewe hawachangii cluba kwa kuingia uwanjani na kununua jezi unategemea miujiza ipi?
Huo utafiti umeufanya wapi kuwa timu za nje zinategemea zaidi fedha kwenye jezi na viingilio? Kila siku nasema hapa, kuna watu mmejua juzi pesa inavyofanya kazi kwa hiyo kila siku mnawahubiria watu kuhusu pesa utadhani mmegundua kitu kipya.

Unapoongelea kwa Mkapa, ule uwanja si wa kuchezea mechi ndogo. Kwanza gharama zake ni kubwa hata kuutumia na hauko friendly kwa mechi ndogo maana mashabiki wako mbali na uwanja. Hizi timu zingejikunja zikajenga viwanja vyao vya kuingiza mashabiki hata 30,000 vingeweza kupata fedha nyingi sana in the long run kwa matangazo, ufadhili wa jina, kuuza vinywaji na chakula, nk. Huko ndiyo kuna hela ya maana.

Halafu supply ya ticket ikiwa ndogo, demand yake itakuwa kubwa na hiyo itaongeza thamani kwenye kuhudhuria mechi.
 
Akili kisoda wewe,
Nikadhani unasema tupeleke vijana huko hata 100 kwenye academy zao ili baadae tuwe na kizazi kipya chenye exposure ya timu za Ulaya wewe unatuletea mambo ya bongo
Wewe ndiyo taahira kabisa. Sasa nilichosema ni nini na wewe unasema nini? Unadhani kipi kitakuwa endelevu, kupeleka vijana 100, jambo ambalo kwanza haliwezekani au kufungua academy hapa na kuleta wakufunzi kutoka kwao?

Ghana walifanikiwa sana kwa kuwa na Academy kama hizo ndani ya nchi yao.
 
Akili kisoda wewe,
Nikadhani unasema tupeleke vijana huko hata 100 kwenye academy zao ili baadae tuwe na kizazi kipya chenye exposure ya timu za Ulaya wewe unatuletea mambo ya bongo
ht ukipeleka vjana 500 still haikuguarantee mafanikio,
 
Hapa dawa pekee ni Serikali kubeba gharama za kuwapeleka kwenye academy za nje, vijana wetu wenye vipaji katika michezo mbalimbali.

Baada ya hapo, vijana hao watafutiwe timu za kucheza huko huko! Na mwisho wa siku warudi kuja kuliwakilisha Taifa lao. Wakifanya hivi, basi hakutakuwepo tena na hizi siasa za Yanga na simba.
 
Wewe ndiyo taahira kabisa. Sasa nilichosema ni nini na wewe unasema nini? Unadhani kipi kitakuwa endelevu, kupeleka vijana 100, jambo ambalo kwanza haliwezekani au kufungua academy hapa na kuleta wakufunzi kutoka kwao?

Ghana walifanikiwa sana kwa kuwa na Academy kama hizo ndani ya nchi yao.
Shindaneni kwa matusi naona mnayaweza zaidi ya hoja kwa hoja
 
Akili kisoda wewe,
Nikadhani unasema tupeleke vijana huko hata 100 kwenye academy zao ili baadae tuwe na kizazi kipya chenye exposure ya timu za Ulaya wewe unatuletea mambo ya bongo
Wee nae ndio wale wale ...nyani haoni kundule🤣🤣🤣 katika hao 100 utapata mmoja au wawili ambao wanaweza cheza professional football.
 
Back
Top Bottom