Tuhuma za Yanga, Simba kununua ubingwa, TFF, Bodi ya Ligi, mnaziba masikio

Tuhuma za Yanga, Simba kununua ubingwa, TFF, Bodi ya Ligi, mnaziba masikio

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Ukifuatilia mitandaoni kwa sasa watu wa soka kuna kelele fulani hivi zimekuwa zikiendelea kwa kasi, ilianza kimya kimya, lakini taratibu zinaenda zinashika kasi.

Timu fulani kubebwa au timu hii inatengenezewa mazingira ya ubingwa ni maneno ambayo yanasikika sana mtaani na mitandaoni.

Awali, moja kati ya wadhamini wa Yanga walikuwa wakitajwatajwa kuwa wanahusika katika kupitia mlango wa nyuma kutengeneza mazingira ya timu yao kushinda. Hakuna aliyejitokeza hadharani kulizungumzia hilo kama ni kweli au la.

Baada ya mchezo wa Simba dhidi ya Tanzania Prisons, jana, Haji Manara akaposti picha ya refa wa mchezo huo na kuandika: Vp GSM anahusika au? Caption haina uhusiano na Picha ya juu, huwa napenda tu kuwapost Waungwana Marefarii wetu 🤪.”

Kwa tafsiri ya kawadia ni kuwa anamaanisha wale waliokuwa wakidai wao wanashinda kwa mkono wa GSM wana maoni gani kwa ushindi wa Simba hasa kwa refa wa mchezo husika.

Upande wa pili, Ahmed Ally naye akaweka post akidai kuwa kuna waamuzi wanne msimu huu wamefungiwa au kupewa adhabu katika michezo ambayo maamuzi yao yalionekana kuwabeba Yanga.

Kuna mifano mingi lakini hiyo ndiyo ya karibu.

Hoja yangu ni kuwa inamaana hiki kinachoendelea kwa sasa ni ununuaji wa mechi au ununuaji wa ubingwa? Hata kama ni utani, utani gani wa kuambiana kuwa kuna mazingira ya rushwa.

TFF na Bodi ya Ligi wapo kimya, wanasubiri mambo yawe mabaya ndiyo watoe tamko au wachukue hatua?

Ni kweli kuna timu au kuna watu wananunua mechi? Wanawahonga waamuzi au waamuzi wanafanya makosa kwa kuwa uwezo wao ni mdogo? Kitendo cha Manara na Ahmed Ally kutoa kauli tata kama hizo inamaanisha wanajua michezo michafu wanayofanya pande zote au ni nini kinaendelea?

Kuna kitu hapo hakipo sawa, TFF waamke kabla hali haijawa mbaya.
 
yaani kwa penati ile waliopewa simba fc dhini ya Tz prison na matukio mengine kama hayo, adi mwisho wa msimu huu hii premium league yetu inaweza kuwa ndiyo 'most corrupted league' kwa msimu huu duniani, takukuru, polisi, tff, bodi ya ligi, UWT woote wako kimyaa wakichekea mirungura kutembea tuu
 
yaani kwa penati ile waliopewa simba fc dhini ya Tz prison na matukio mengine kama hayo, adi mwisho wa msimu huu hii premium league yetu inaweza kuwa ndiyo 'most corrupted league' kwa msimu huu duniani, takukuru, polisi, tff, bodi ya ligi, UWT woote wako kimyaa wakichekea mirungura kutembea tuu
Kuna tatizo sehemu na wahusika wapo kimya kama hawaoni kwa kuwa uchafu mwingi unawagusa wao, labda mpaka itokee 'mbuzi ale zaidi ya urefu wa kamba yake', ndiyo wataona kuna tatizo.
 
Kuna mechi moja nyuma nyuma huko ilisemekana kwamba kuna tajiri wa Simba aliwahonga baadhi ya wachezaji wa Yanga akiwemo Morrison alipokuwa bado yuko Yanga na kuifanya Simba ishinde 4-0, ila kuhonga ni kuhonga tu uhonge refa uhonge wachezaji ni ufisadi ule ule.
 
Kuna mechi moja nyuma nyuma huko ilisemekana kwamba kuna tajiri wa Simba aliwahonga baadhi ya wachezaji wa Yanga akiwemo Morrison alipokuwa bado yuko Yanga na kuifanya Simba ishinde 4-0, ila kuhonga ni kuhonga tu uhonge refa uhonge wachezaji ni ufisadi ule ule.
Walipopigwa kono la Nyani( 5 , 0) mwaka 2012 na 6, 0 mwaka 1977 ni wachezaji gani wa usukuleni waliohongwa na simba?
 
Majibu yote yanaweza yakawa sahihi. Rushwa kwa hao waamuzi, na uwezo wao unaweza kuwa ni mdogo!
Lakini pia baadhi ya waamuzi wanaweza kutoa maamuzi tata kwa sababu tu ya unazi wao kwa hivyo vilabu! Unakuta mwamuzi ni shabiki wa moja ya hizo timu! Kwa hali hiyo, anaweza asipewe hiyo rushwa! Ila akaamua tu kupindisha sheria.

Mfano mzuri ni yule mwamuzi aliye chezesha mechi ya Yanga na Namungo! Na mwamuzi wa jana wa mechi ya simba na Prisons alishawahi kufungiwa pia miaka michache iliyopita, baada ya kufanya maamuzi yaliyo inufaisha simba kama alivyofanya jana! Na kwa bahati mbaya sana anaitwa Ahmada Simba! ☹️
 
Walipopigwa kono la Nyani( 5 , 0) mwaka 2012 na 6, 0 mwaka 1977 ni wachezaji gani wa usukuleni waliohongwa na simba?
Nakumbuka mwaka 1977 aliyehongwa alikuwa ni mlinda mlango wa Yanga wa wakati huo Bernard Madale tena ilisemwa sana kipindi hicho, ya mwaka 1912 sina uhakika.
 
Fun enough kuna likitu linaitwa waziri wa michezo na..,, limpo lio tuu wakati tim kama Tz prison na geita gold fc zikionewa waamuzi kiwazi wazi kabisa huku na lenyewe likitafuna kwa urefu wa kamba yake…… pambafu kabisa
 
Back
Top Bottom