Uchaguzi 2020 Tuikomboe Tanzania kupitia Lissu, hakuna nchi Duniani ina mifumo miwili ya lugha za kufundishia

Uchaguzi 2020 Tuikomboe Tanzania kupitia Lissu, hakuna nchi Duniani ina mifumo miwili ya lugha za kufundishia

Ndomaaana watoto wao wanawapeleka English medium na international schools ambako hawafundishi kwa kiswahili,hawataki kubadili policy ya lugha ya kufundishia ili RAIA washindwe kuwa direct contact with globalization
 
Mnyonge mnyogeni haki yake apewe, Lissu leo amenigusa kwenye swala la lugha ya kufundishia. Jambo hili limekuwa mwiba kwenye elimu na maisha ya Watanzania miaka na miaka.. Ni ukweli usiofichika kwamba lugha ya kufundishia ni tatizo kubwa sana kwenye mfumo wetu wa elimu. Magufuli mwenyewe ni mhanga Mawaziri wetu ni wahanga, Wabunge ni wahanga. Tuunge mkono chadema vijana wetu wapone.

Magufuli huongea kwa Kiswahili na kuhubiri kukuza Kiswahili si kwamba anakipenda sana. sababu kubwa ni kwamba hajui English vizuri, Ingawa alikua mwalimu na PHD aliandika kwa kizungu. Yeye mwenyewe ni mfano mzuri wa halihalisi na shida tuliyonayo kwenye elimu yetu. Lakini cha kushangaza hajachukua hatua kundoa shida hii inayoliamiza tafa. Tundu lisu ameona tatizo na yupo tayari kulitatua.Tumunge mkono Lisu tuiokoe Tanzani.

Kwenye hili la elimu tuambiane ukweli. Hatutaendelea kwa kuhimiza vijana wawe wamachinga, wajaze mitaa wakichuuza vitu vya mchina wakati maduka yapo. Leo Barabara, Reli nk ni wageni wanajenga. kwani nani alienda kujenga Reli China au Korea? Kijana akitoka na zero form 4 utampeleka wapi? CCM imetuangusha kwa tangu Uhuru. Tanzania tunahitaji mabadiliko.

Vijana wetu wengi wanashindwa kupata maarifa ya kutosha mashuleni na vyuoni kwa sababu tu hawaelewi lugha inayotumika kuwafunza. Mfano;mtihani wa kitato cha 4 si mgumu kiasi cha zaidi ya nusu ya wahitimu kupata alama (division) 4 na 0.

Wawekezaji wakija Tanzania wanashindwa kupata wafanyakazi wanaoweza kuwasilana nao vizuri na wenye weledi na marifaya ya kutosha kwenye lugha. Matokeo yake wanaamua kuajiri Wakenya kwenye nafasi za juu. Uliza Managers kwenye makampuni makubwa hapa kwetu ni akina nani. Tunge mkono Lisu Tupate Tanzania mpya.

Tanzania itaweza tu kusonga mbele endapo tutaamua kuborosha elimu yetu itowe wasomi wenye viwango vya kimataifa na sio kupelka watoto shule kwa mazoea tu lakini watoka watupu.

Hakuna nchi yoyote Duniani amboyo ina mifumo miwili ya lugha za kufundia kama ilivyo kwa Tanzania. Wanachi waliona tatizo hilo wakamua kuazisha shule zinazofundisha kwa Kingereza ili kuziba pengo, hivyo Tanzania hakuna watoto wanafunzwa kwa Englishi na Wale wa Kiswahili.

Tundu Lissu na CHADEMA ameamua kulivalia njuga suala hli tumuunge mkono.
Hakuna mtu hapo mkuu tuikomboe kwani nchi imetekwa?
 
LISU NI MTU ANAYELETWA DUNIANI KILA BAADA YA MIAKA 100.TUKIMKOSA MTU KAMA LISU KUWA KIONGOZI ITAKUWA NI KOSA KUBWA SANA AMBALO WATANZANIA TUTAKUJA JUTIA SANA MBELENI.
 
Huyo Lissu hana uelewa wa nini anaongea.

Afrika ya kusini wana lugha 11 zinazofundishwa mashuleni, mbona kiuchumi wametuacha mbali sana!!?.

Tuendelee tu kuwa maskini kwa uvivu wetu halafu lugha ziwe ndio sababu ya uhalalishaji.
 

Attachments

  • 1803589E-79B9-48C1-9F5F-F988668749EF.MP4
    13.6 MB
Dunia ina maajabu yake wana JF! Yaliyonipata wkat naingia form one sintosahau!!,

Ile nimeingia darasani tu, Juma tatu asubuhi! sikuamini ni Kiingredhaa! mwanzo/ mwisho wa somo! mbona jasho la mavi lilinibana bila kutaka! Nilijiona mjinga wa Dunia nzima, hasa pale kwenye self introduction/kujitambulisha, sikujua nini kinaendelea, bahati nzuri nilikaa katikati nikaiga wenzangu wa mbele! jamani nilifadhaika kimwili na kiroho! ukiwa na Bp waweza kufa!

Nilicho ambulia! ni darasa kusema kwa pamoja, Yeees!!.... Noor!!! baaasi!!! nilitamani kurudi nyumbani! lkn sasa Home! mbali safari ya siku 4, nta mwambia nini Baba mzazi, Mzee kauzu anakuzodoa Mezani wakati wa mlo, mbele ya mama wa kambo, na wadogo zangu! msosi utapanda kweli? Sometimes baada ya maombi usiku? anakusema kupitia Biblia hasa kitabu cha Methali;


Any way Kwa hasira nilikariri Dictionary yoooote! nikarudia tena na tena! Grammar niliijua badaye! Anwani ya Mzazi nikabadili ili asiipate report ya Masomo yangu, Barua za tabia yangu na maendeleo ya masomo zilikwenda kwingine kusikojulikana! bila kujali nimefanya vizuri au vibaya mpaka nikamaliza Shule ya Sec.

Huko mbele ikawa tabia no kujua taarifa ya masomo yangu! mpaka nilipoanza kazi rasmi, na nikakata mazoea na home! bila mzazi kujua maendeleo yangu, alisikiaga tu mwanao yuko chuo kikuu!

kukariri Ilinisaidia, presentations, Semina naingia kwa kujiamini km Kenya! wana JF Kiiingredha usipokijua weeee! asikudanganye mtuu! ni Maradhi mabaya sana, sitaki, sipendi, sitamani sidhanii yakupate yale yaliyonipata...wewe unayesoma hapa! ukiweza soma hata lugha saba za kimataifa!

Jiwe, Ndarichako hawafurahii na yanayowakuta. Watu ni km, Nyerere, Mkapa bana wanaongea mpaka wana nesa nesa hivi! Wazungu wanawakubali sana.
 
Hatuwezi tukaiuza nchi mchana kweupe kwa kumpa kibaraka ..... Wa mabepari ..... Simwamini kabisa Lissu ana maslahi tofauti kura yangu kwa JPM
 
Shida sio kuongea kinge, shida ni kuwa mwanafunzi hawaelew wanachofundishwa shuleni. Mtu anatakiwa also english waikati huo huo masomo mengine yanafundishwa kwa kiengereza!

Tuwe na lugha moja tu tokea chekechea mpaka chuo, km ni kiswahili bas ni mwanzo mwisho na ndo wachina wanafanya hivyo na english huwa somo la giada. Like wise kwa kiengereza.

Watu wanapata changamoto mavyuoni including myself. Kwahiyo tuchague lugha moja, english au swahili. SWALI NI, KISWAHILI KINAJITOSHELEZA KUFUNDISHIA MASHULENI NA CHUO KIKUU KAMA WACHINA WANAVOFANYA?
Mimi nakuelewa kuna wanafunzi wanapata shida kwenye kuchanganya lugha mbili. Kwa upande wangu, sidhani kama lugha mbili ambazo ni kiswahili kwenye shule ya msingi na kingereza sekondari au chuo ni shida. Ukiwa shule ya msingi unasomeshewa somo la kingereza kwenye madarasa yote mpaka utakapofika darasa la saba. Na hii inatakiwa pale unapofika sekondari, basi angalau unajuwa kutumia lugha ya kingereza na pia una hazina ya lugha mbili yani
kiswahili na kingereza. Tatizo sio hiyo system, tatizo ni quality ya ufundishaji, walimu tuaowapa dhamana ya kufundisha watoto, wao wenyewe hawana uwezo wa kufundisha mtu mpaka akaekewa. Tulitafuta hiyo shida ya quality of education pamoja na nyenzo za kutisha, utaona matokeo yanavyokuwa tofauti. Ikiwa kija wa kitanzania anakwenda China au Russia haongei hata neno moja ya hizo lugha, anajifunza lugha na anasoma mpaka anapata shahada yake, kwanini akiwa hapa nyumbani hawezi kutumia lugha mbili?
 
Unaposema duniani sijui una maana gani mimi nimesoma Austria wale wana mifumo mitatu ya kufundishia Kijerumani, kifaransa na kiingereza mimi na wanafunzi wengine tulisoma mfumo wa kiingereza lakini tulisoma kijerumani na kifaransa kama masomo mengine. Bahati mbaya ni kwamba hatujaweza kujitosheleza kuwa na vitabu vya kufundishia masomo yote kwa kiswahili shule ya msingi mpaka chuo kikuu na hata lugha ya kiswahili bado haijajitosheleza misamiati ya maneno ya kitaalamu kwenye sayansi ya uvumbuzi na maabara nadhani hata kimahakama
 
Mbona unaongea kama vile watu wote wanaishi daresalam au watu wote wana uwezo kifedha.Lugha ni zaidi ya kuongea na kuandika.Lugha ndo msingi wa maendeleo nahili sio jambo jepesi jepesi kama unavyolichukulia.
Tatizo sio unaishi wapi, tatizo ni mwanafunzi anatakiwa kupewa nyenzo zote ikiwa na pamoja na walimu wenye weledi wa juu, vitabu, vitendea kazi, madarasa nk. Huwezi kusema mwanafunzi kashidwa kusoma kama hujampa ushirikiano wa kutosha na vifaa vitakavyo msaudia kutimiza malengo yake.
 
Kwa sisi werevu hatuwezi kumpa kura yetu Lissu piga ua. Ila kwa wale wadukuwaji ndo mtakaompa kura lissu. Kila la heri kutuuza watanzania.
Una werevu gani wewe punguani kama kuuzwa ushauzwa zamani kama ulikuw hujui ndio maana unapewa elimu ya kuunga unga usitoke hilo tongo tongo lililo kwenye jicho lako kalaghabaho
 
Unatoa mifano ya nchi ambazo kuanzia mazingira ya mwalimu,mwanafunzi na shule yenyewe yako vizuri.Hebu itazame tanzania alafu niambie hicho ulichokiandika kama kinawezekana hapa bongo kwa hali iliyopo sasa.Kwasababu hapa changamoto sio uwezo mdogo tu wa mwalimu kufundisha bali ata mwanafunzi mwenyewe anaweza kau na uwezo mdogo kutokana na changamoto kadha wa kadha zakimazingira,lishe n.k.
Kama mnajua changamoto za elimu ni pamoja na mazingira kwa nini mdanganye watanzania kwa taarifa za uongo??
 
Wewe mwanasaccos hapo Afrika ya Kusini tu wameamua Kiswahili kuingizwa kwenye mtaala wao wakufundishia kwenye shule zao!! Wewe unadharau Kiswahili!!
Napenda sana kutumia akili ndugu...sasa tunasubiri nini kufuta Kiingereza tukomae na Kiswahili kama wachina wanavyotumia lugha yao
 
Back
Top Bottom