GUSSIE
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 3,880
- 11,134
Members, Huu uzi ni kwa ajili ya kutoa ushauri, Maoni na Marekebisho kuhusu mfumo wetu wa elimu Tanzania.
Hoja zitakazotolewa hapa zitaunganishwa na kuwafikishia wahusika Bungeni na kwenye mamlaka ya Serikali.
Tujadili ni aina gani ya masomo tunayohitaji yafundishwe kwa watoto wetu, Watoto wetu wasome kwa miaka mingapi?
Tujadili mtoto amalizapo kila ngazi ya elimu awe na ujuzi na uwezo wa kufanya jambo gani?
Tujadili aina za shule tunazozihitaji kwa watoto wetu na aina ya walimu tunaowahitaji kwa ajili ya watoto wetu.
Mfumo wetu wa elimu umeundwa kwa mtoto kuanza chekechea akiwa na miaka mitatu mpaka mitano, Anaanza elimu ya msingi akiwa na miaka sita mpaka nane, Anaishi na elimu ya msingi kwa miaka saba, Baadae elimu ya upili ya Sekondari anaishi kwa miaka minne, Anajiunga na elimu ya juu ya Sekondari kwa mwaka moja na nusu mpaka miaka miwili, Baadae chuo Kikuu kwa shahada ya awali miaka mitatu mpaka mitano.
Kimahesabu mtoto anayesoma kufikia shahada ya awali ukiondoa udaktari na uinjinia anatumia miaka kumi na sita shule, 7+4+2+3=16
Je, ni sahihi mtoto kukaa miaka kumi na sita shule anaondoka bila ujuzi wowote ule.
Mtoto unampokea nyumbani tangu alipoanza kuwa bize akiwa na umri wa miaka minne, Anarudi mikononi mwako tena baada ya miaka kumi na sita bila ujuzi wowote.
Tunahitaji maoni yenu na ushauri hapa Jamiiforum, Uzoefu wa kila mmoja wetu unahitajika ili tutengeneze mfumo imara wa elimu kwa vizazi vijavyo.
Nina hakika huu uzi utatoa dira na maono kwa miaka mingi ijayo hapa JamiiForums.
Soma pia:
1) Mfumo wa elimu wa Nchi ya Ufini unavyolifanya Taifa hilo kuwa bora katika elimu Duniani; Tanzania inajifunza nini?
2) Muundo wa Elimu ya Tanzania
3) Kitila Mkumbo: Je, Tanzania tuna mtaala wa elimu?
4) Matatizo matatu katika Mfumo wetu wa Elimu
Hoja zitakazotolewa hapa zitaunganishwa na kuwafikishia wahusika Bungeni na kwenye mamlaka ya Serikali.
Tujadili ni aina gani ya masomo tunayohitaji yafundishwe kwa watoto wetu, Watoto wetu wasome kwa miaka mingapi?
Tujadili mtoto amalizapo kila ngazi ya elimu awe na ujuzi na uwezo wa kufanya jambo gani?
Tujadili aina za shule tunazozihitaji kwa watoto wetu na aina ya walimu tunaowahitaji kwa ajili ya watoto wetu.
Mfumo wetu wa elimu umeundwa kwa mtoto kuanza chekechea akiwa na miaka mitatu mpaka mitano, Anaanza elimu ya msingi akiwa na miaka sita mpaka nane, Anaishi na elimu ya msingi kwa miaka saba, Baadae elimu ya upili ya Sekondari anaishi kwa miaka minne, Anajiunga na elimu ya juu ya Sekondari kwa mwaka moja na nusu mpaka miaka miwili, Baadae chuo Kikuu kwa shahada ya awali miaka mitatu mpaka mitano.
Kimahesabu mtoto anayesoma kufikia shahada ya awali ukiondoa udaktari na uinjinia anatumia miaka kumi na sita shule, 7+4+2+3=16
Je, ni sahihi mtoto kukaa miaka kumi na sita shule anaondoka bila ujuzi wowote ule.
Mtoto unampokea nyumbani tangu alipoanza kuwa bize akiwa na umri wa miaka minne, Anarudi mikononi mwako tena baada ya miaka kumi na sita bila ujuzi wowote.
Tunahitaji maoni yenu na ushauri hapa Jamiiforum, Uzoefu wa kila mmoja wetu unahitajika ili tutengeneze mfumo imara wa elimu kwa vizazi vijavyo.
Nina hakika huu uzi utatoa dira na maono kwa miaka mingi ijayo hapa JamiiForums.
Soma pia:
1) Mfumo wa elimu wa Nchi ya Ufini unavyolifanya Taifa hilo kuwa bora katika elimu Duniani; Tanzania inajifunza nini?
2) Muundo wa Elimu ya Tanzania
3) Kitila Mkumbo: Je, Tanzania tuna mtaala wa elimu?
4) Matatizo matatu katika Mfumo wetu wa Elimu