Tujadili Mfumo wa Elimu utakaotufaa Tanzania. Maoni yataunganishwa na kufikishwa Bungeni na Serikalini

Tujadili Mfumo wa Elimu utakaotufaa Tanzania. Maoni yataunganishwa na kufikishwa Bungeni na Serikalini

Darasa I-III
Uraia, Kiswahili na Hisabati

IV-VII
Hisabati, Kiswahili, Historia na Ufundi stadi (LEVEL 1)

Form I-IV (LEVEL 2-3)

Hisabati, Kiswahili, Historia na Ufundi stadi
Form V-VI

Hisabati, Kiswahili, Historia na Ufundi stadi (LEVEL 4-6)
Naona umeamua kumtengeneza mswahili

Yaani somo la kiingereza umetupilia
Mbali
 
Serikali iwawezeshe ma professor na research funds nchi haiwezi endelea kama hamna research za maana zinazofanyika
 
Elimu ya chuo wafanye malekebisho sana maana apana kitu pale asa wanao somea uwalimi na shelia wengi upoteza muda
 
Wakafanye case study ya elimu inayo tolewa china,singapore,malaysia na n.k

Halafu waunganishe study na kuja na elimu tendaji ZAIDI kuliko upuuzi Huu uliopo!!!

Mitihani ya Necta ifutwe ibaki mitihani ya faculty husika ndio isimamie na Sio lazima mitihani ifanane bali mazingira yaangaliwe na uzalishaji eneo husika!!!
 
1. Elimu ya msingi ingebakia kwa maboresho ya kuwepo na namna mtoto atajifunza elimu ya msingi vzur na kuifahamu vyema nchi yake kuanzia jiografia, uchumi, siasa

2. Elimu inayofuata iwe ni ya vitendo zaidi(ujuzi + maarifa) ili imuandae mtoto na mazingira halisia ya nchi yake

3. Tuangalie nchi inahitaji sana wataalamu katika sekta hizo na zipewe kipaumbele na siyo kila mwaka vyuoni courses ni zile zile Na admissions zinafanyika kwa wingi tuu.

Nb: Ujerumani tu diploma yake kwa huku kwetu nahs ndo kama mtu mwenye PhD
 
Wakafanye case study ya elimu inayo tolewa china,singapore,malaysia na n.k

Halafu waunganishe study na kuja na elimu tendaji ZAIDI kuliko upuuzi Huu uliopo!!!

Mitihani ya Necta ifutwe ibaki mitihani ya faculty husika ndio isimamie na Sio lazima mitihani ifanane bali mazingira yaangaliwe na uzalishaji eneo husika!!!
Kula tisa
 
Upper second ya kukariri??
Wewe unayo upper ipi ya kuelewa mkuu. Nimechomekea na elimu ya wabunge ama viongozi wetu jamani mbali na elimu darasa ya watt wetu.

Vipi wewe mwenye kuelewa wa upper highest second umelifanyia Nini Taifa lako.

Ambao hata wamekariri wanatibu watu wanajenga nyumba unazotumia kila siku. Ni wahasibu na ma hr wapo wanafanya kazi mbalimbali nje na ndani ya nchi.
 
Advance (form 5 na 6) zifutwe, ni mambo ya kale
Binafsi nikijiassses najilaumu kwanini nilienda advance, sio kwamba ngumu ni nyepesi sana, ila nikiwaza nilivyokuwa nakomaa na ma organic chemistry, unaambiwa sijui uprove existance ya OH , sijui benzene. Tunaishia kukariri TU kwasababu hauwezi hakuna practical ya hayo mambo. Bora ningeenda diploma Sasa hivi ningekuwa hata mtaalamu mzuri wa magari. Kama upo chuo na una lengo la kujiajiri kwa unachikisomea unaweza ukaelewa
 
Members, Huu uzi ni kwa ajili ya kutoa ushauri, Maoni na Marekebisho kuhusu mfumo wetu wa elimu Tanzania.

Hoja zitakazotolewa hapa zitaunganishwa na kuwafikishia wahusika Bungeni na kwenye mamlaka ya Serikali.

Tujadili ni aina gani ya masomo tunayohitaji yafundishwe kwa watoto wetu, Watoto wetu wasome kwa miaka mingapi?

Tujadili mtoto amalizapo kila ngazi ya elimu awe na ujuzi na uwezo wa kufanya jambo gani?

Tujadili aina za shule tunazozihitaji kwa watoto wetu na aina ya walimu tunaowahitaji kwa ajili ya watoto wetu.

Mfumo wetu wa elimu umeundwa kwa mtoto kuanza chekechea akiwa na miaka mitatu mpaka mitano, Anaanza elimu ya msingi akiwa na miaka sita mpaka nane, Anaishi na elimu ya msingi kwa miaka saba, Baadae elimu ya upili ya Sekondari anaishi kwa miaka minne, Anajiunga na elimu ya juu ya Sekondari kwa mwaka moja na nusu mpaka miaka miwili, Baadae chuo Kikuu kwa shahada ya awali miaka mitatu mpaka mitano.

Kimahesabu mtoto anayesoma kufikia shahada ya awali ukiondoa udaktari na uinjinia anatumia miaka kumi na sita shule, 7+4+2+3=16

Je, ni sahihi mtoto kukaa miaka kumi na sita shule anaondoka bila ujuzi wowote ule.

Mtoto unampokea nyumbani tangu alipoanza kuwa bize akiwa na umri wa miaka minne, Anarudi mikononi mwako tena baada ya miaka kumi na sita bila ujuzi wowote.

Tunahitaji maoni yenu na ushauri hapa Jamiiforum, Uzoefu wa kila mmoja wetu unahitajika ili tutengeneze mfumo imara wa elimu kwa vizazi vijavyo.

Nina hakika huu uzi utatoa dira na maono kwa miaka mingi ijayo hapa JamiiForums.

Soma pia:

1) Mfumo wa elimu wa Nchi ya Ufini unavyolifanya Taifa hilo kuwa bora katika elimu Duniani; Tanzania inajifunza nini?

2) Muundo wa Elimu ya Tanzania

3) Kitila Mkumbo: Je, Tanzania tuna mtaala wa elimu?

4) Matatizo matatu katika Mfumo wetu wa Elimu
Mambo makubwa 2 naona yafanyike.
1. Shule zote kuanzia msingi mpaka sekondari form six pamoja na masomo ya kawaida pia wasome masomo ya lazima kama somo la biashara, kilimo(agribusiness), machenics, uchumi na sanaa mfano uchoraji, upishi, ususi n.k

2. Masomo yote 75% yawe practical na hiyo 25% theory. Mtoto ajengewe self competency ya fani sio taka taka za hivi sasa.


Japo vichwa vya viongozi wetu vimejaa michongo ya posho na trip allowance tuombe Mungu itokee mabadiriko ya mfumo wa elimu maana ni aibu tupu.
 
Kufanyike mabdiliko katika sehemu 3 muhimu
1) Lugha ya kufundishia
2) Mitaala ya kufundishia
3) Muda wa kuwa shuleni

1. Lugha ya kufundishia
Kiuhalisia watanzania walio wengi wako huru sana kujifunza kwa lugha ya kiswahili na hili mimi mwenyewe ni shuhuda maana kipindi nasoma ngazi ya elimu ya upili na ya juu mwalimu alikua na kazi 2 kuu akiwa darasani: ya kwanza ni kutafsiri dhana (concept) iliyo kwenye mada husika kwa lugha ya kiswahili na pili ni kuifanya dhana ieleweke kwa wanafunzi.

Hii inafanya walimu kutumia nguvu nyingi sana kutoa elimu kwa kutumia Kiswanglish na kwa upande wa lugha haifanyi mwanafunzi kuwa na uwezo (competent) kwenye matumizi ya lugha yeyote iwe kiingereza au kiswahili.

Kwa kutumia kiswahili itawafanya wanafunzi kuwa huru (confortable) zaidi wakati wa jujifunza pia kuwa na uwezo mzuri katika matumizi sahihi ya lugha ya kiswahili.

Pia baada ya maisha ya shule kiuhalisia huku makazini watanzania tulio wengi tunafikiri sana kwa kiswahili vichwani mwetu lakini utendaji mara nyingi tunautafsiri uwe kwa kiingereza ili tuendane na mifumo iliyopo.

Hii inapunguza ufanisi kwa kiwango kikubwa sana. Kwa hiyo kupata ufanisi matumizi ya lugha mama katika kufikiri na kutenda ni muhimu sana.

Najua pia kunaweza kuwa na mashaka kidogo kwenye utimilifu wa lugha ya kiswahili kama lugha ya kufundishia na pia ugumu unaoonekana katika misamiati mbalimbali iliyo katika lugha ya kiswahili; ila ukweli ni kwamba hakuna lugha iliyo timilifu katika elimu na ndio maana hata kiingereza kimeazima misamiati mingi katika kada mbalimbali kama baolojia, fizikia na sheria kutoka lugha ya kilatini, kigiriki nk.

Pia ugumu wa lugha ya kiswahili tunauona kwa sababu sio lugha inayotumika kutufunza tangu tungali wadogo kielimu mpaka tunapokomaa; ni kama tu mtoto wa kisukuma/kichaga ambaye anachanganyiwa lugha katika makuzi yake, akija kukutana na msukuma/mchaga anayeongea lugha ya ndani kabisa (mfano babu zeru wasiojua kabisa kiswahili) basi lazima atasema kisukuma/kichaga cha ndani ni kigumu sana.

2. Mitaala ya kufundishia
Kwa kiwango kikubwa sana mitaala ya elimu yetu imepitwa na wakati na haijumuishi mambo mengi ya sasa. Hili lipo kuanzia ngazi ya shule za msingi mpaka vyuo vikuu. Kuna ulazima sasa wa kuhuisha mitaala yetu iendane na wakati.

Pia sioni ulazima wa mwanafunzi kupata elimu jumuishi (kwa kusoma masomo mengi yasiyowiana) kwa kipindi kirefu na kusoma masomo maalumu (ya michepuo) kwa kipindi kifupi kwani yanadumaza ubunifu/uwezo wa uvumbuzi wa mwanafunzi husika.

Kwa mfano hakuna ulazima wowote wa kusoma masomo tisa au zaidi kwa miaka saba shule ya msingi halafu usome tena masomo tisa yakufanana nayo kwa miaka minne shule ya upili. Nadhani wanafunzi waanze kusomea michepuo mbalimbali baada ya muda usiozidi miaka saba tangu kuanza elimu ya msingi.

3. Muda wa kuwa shuleni
Kwa sasa maisha ya kielimu ya kijana wa Kitanzania yanatumia muda mwingi sana shuleni kujifunza mambo mengi ambayo hayatakuja kumsaidia baadae.

Napendekeza mwanafunzi asitumie zaidi ya miaka kumi na moja (11) shuleni kabla ya kufika elimu ya chuo kikuu kama ilivyo sasa ambapo ni miaka saba ya elimu ya msingi, miaka minne ya elimu ya upili na miaka miwili ya elimu ya juu (jumla ya miaka 13).

Kiuhalisia ni wakati sasa wa kuupunguza muda wa elimu ya msingi na elimu ya upili na kuongeza muda wa elimu ya juu; miaka minne inatosha kabisa kwa elimu ya msingi na miaka mitatu kwa elimu ya upili lakini elimu ya juu yapaswa iwe na walau miaka mitatu hadi minne ambapo mwanafunzi atasoma masomo ya michepuo na baada ya hapo ndipo aende chuo kikuu kusomea fani itakayowiana na kipaji na uwezo wake.

Kwa maana hiyo tunatazamia kijana wa miaka 20 mpaka 22 atakuwa ameshapata elimu na ujuzi wa kutosha kuanza kulijenga taifa letu.

Nawasilisha.
Nakuunga mkono hasa point ya 1 &2, just imagine tupo chuo first year bachelor, mwanafunzi wa engineering nafundishwa communication skills, halaf content yenyewe nakumbuka nilifundishwa darasa la 7 sijui la 6 Ile!. Kama issue ni kingereza lugha ya kimataifa au ya biashara, kwanini tusisome English course kabisa huku masomo mengine tunasoma Kwa lugha yetu( kiswahil)
 
Mimi kwa mawazo yangu,
Kwanza masomo yapunguzwe. Tukianza na elimu ya msingi, wasome masomo matano tu. kwa mchanganuo ufuatao:-

1. LUGHA [Kiswahili na kiingereza]

2.MAARIFA YA JAMII [Urai, Historia, na elimu ya mazingira na kujitambua]

3.STADI ZA KAZI [Kilimo, uvuvi, ufugaji na ufundi]

4.Sayansi [Jiografia,baiolojia,kemia na fizikia + kompyuta kozi(introduction)]

5. HESABU/HISABATI na BIASHARA
Kwa sekondari nako masomo yapunguzwe.

Wakimaliza shule ya msingi, wanapopangiwa kwenda sekondari basi wa speshelaizi na kombinesheni zao kabisa, yaani ukitoka shule ya msingi unapangiwa kwenda arts, science au business.

Masomo yawe kwa mchanganuo ufuatao:-

1.ARTS [LANGUAGE( kiswahili na kiingereza/kifaransa/kiarabu), + CIVICS and HISTORY + BASIC MATHEMATICS]

2. SCIENCE[PCM,PCB,PGM, CBG n.k + PURE MATHEMATICS]

3. BUSINESS[ECONOMIC, COMMERCE and ACCOUNTANCE + BASIC MATHEMATICS]

4. COMPUTER COURSE iwe kwa wote arts, science na business
-Kingine miaka ya kusoma nayo pia upunguzwe.

Kwa shule za msingi wanafunzi waanze shule wakiwa na miaka 7 baada ya kumaliza elimu ya awali ambayo kwasasa nayo pia iwe ya lazima.

-Shule ya msingi wasome miaka mitano ya darasani na mwaka mmoja wa stadi za kazi wakisubiri kuingia sekondari.

-Kwa sekondari wa wasome miaka minne ya darasani na mwaka mmoja wa stadi za kazi wakisubiri kuingia chuo.

-Baada ya hapo, chuo wasome miaka miwili/mitatu darasani mwaka mmoja kazi kwa vitendo.
Hayo ndo mawazo yangu.
Yes mda wa kufanya field week 10 hazitoshi, waweke mwaka kabisa au hata nusu mwaka
 
toa na kimbizaaa CCM madarakani, mambo mengine yatakaa sawaa tuu
 
Wakafanye case study ya elimu inayo tolewa china,singapore,malaysia na n.k

Halafu waunganishe study na kuja na elimu tendaji ZAIDI kuliko upuuzi Huu uliopo!!!

Mitihani ya Necta ifutwe ibaki mitihani ya faculty husika ndio isimamie na Sio lazima mitihani ifanane bali mazingira yaangaliwe na uzalishaji eneo husika!!!
China na Singapore wao utaratibu wao upo vipi?

Unaweza toa maoni yako hapa kidogo
 
China na Singapore wao utaratibu wao upo vipi?

Unaweza toa maoni yako hapa kidogo
Practical based education in relevance to natural environment and by improving production of raw materials for industries to manufacture goods for consumption!!ETI leo tuna upungufu wa mafuta ya kula hadi bei inapanda tu wakati tuna alizeti,michikichi,karanga,pamba nazi na n.k halafu watoto wanakariri atomic mass hadi chuo kikuu badala ya kuzalisha na kukuza uchumi!!!Pumba TUPU Mkuu!!!Tunaua viwanda VYA ndani kea kufundisha ujinga watoto wetu!!bado nyama na maziwa ku process Ili tuuze hadi nje!hata viwanda VYA nyama hatuna humu NCHINI!!!?TURUDI KWENYE MISINGI YA UZALISHAJI MKUU!!!cha kushangaza hatuna scheme za kutosha za umwagiliaji hapa NCHINI ETI tuna kilimo cha msimu mmoja tu !!hatuwezi production KWA style hiyo!!
 
Ntajikita zaidi kwenye mada zinazofundishwa kwenye masomo mbali mbaki:

Baadhi ya mada zimepitwa na wakati kwa mfano kwenye somo la historia sekondari kuna umuhimu gani wa kupoteza muda kusoma evolution of man,eti tumetokana na masokwe,kweli dunia ya sayansi na teknolojia bado tupo kwenye usokwe!

Kwenye masomo ya lugha,kisw na engl tujikite zaidi kwenye stadi nne za lugha ie speaking,listening,writing and reading

Na kwenye mtihani iwepo practical ya hizo stadi nne yani kama ni speaking mtoto ajue kuna maksi za kuongea ili tupime uwezo wake wa lugha.

Ni ajabu kukuta msomi wa chuo kikuu hajui kabisa kujieleza kwa lugha aliosoma kwa miaka zaidi ya kumi.tuwe serios basi

Kwenye stad ya writig tukazanie creative writing hiyo ipo form four,kwmba mtoto waweze kuandika liwaya,tamthilia,mashairi nk.angalieni kwenye issue ya vitabu vya kingeleza ie nnovels,play etc

Waandishi wengi sio watanzania chukua unanswered cries,three suitors,this time tomorrow etc sio wantanzania.

Je, utamaduni wetu utatambulishwa na nini kama sio kwenye fasihi yetu?
Mkuu kuliondoa SoMo la Historia nisawa na kuruhusi Giza Nene kwenye fikra za watanzania asiyejua atokako hawezi kujua aendako.
 
Mambo makubwa 2 naona yafanyike.
1. Shule zote kuanzia msingi mpaka sekondari form six pamoja na masomo ya kawaida pia wasome masomo ya lazima kama somo la biashara, kilimo(agribusiness), machenics, uchumi na sanaa mfano uchoraji, upishi, ususi n.k

2. Masomo yote 75% yawe practical na hiyo 25% theory. Mtoto ajengewe self competency ya fani sio taka taka za hivi sasa.


Japo vichwa vya viongozi wetu vimejaa michongo ya posho na trip allowance tuombe Mungu itokee mabadiriko ya mfumo wa elimu maana ni aibu tupu.
Kwa mtazamo huu labda walimu watoke nje ya nchi kama ilivyo ktk soka
 
Back
Top Bottom