Tujikumbushe Mashairi tuliyoyapenda shule ya msingi

Tujikumbushe Mashairi tuliyoyapenda shule ya msingi

Nyumbani kwako kuzuri, japokuwa ni pangoni
Nyumba yako ni johari, ya mwenzako sitamani,
Hata pawe pa tajiri, hapafai maisha
Nyumbani kwako johari, kwingine usitamani.


Uipende nyumba yako, utaona raha yake, Kisha penda ndugu yako, kwako apaone kwake
Dunia mahangaiko, usipende pekepeke, Nyumbani kwako johari, kwingine usitamani.
 
Nyumbani kwako kuzuri, japokuwa ni pangoni
Nyumba yako ni johari, ya mwenzako sitamani,
Hata pawe pa tajiri, hapafai maisha
Nyumbani kwako johari, kwingine usitamani.


Uipende nyumba yako, utaona raha yake, Kisha penda ndugu yako, kwako apaone kwake
Dunia mahangaiko, usipende pekepeke, Nyumbani kwako johari, kwingine usitamani.
Japo siku bahatika kulisoma lakini liko poa
 
Wanangu Wa faida mpo?
.
Kuna vitu vinafanya wakati Fulani mtu mzima utamani kurudi utotoni
Ingawa ni ngumu ki nadharia (mawazo) yanaweza kukurudisha na ukajikuta Una tabasamu peke yako njiani
.
Nakumbuka moja ya vitu vilivyo ni Fanya niipende shule ili kuwa ni pamoja na kukaa makundi na kusoma hadithi mbalimbali na baadae kuulizana maswali ya hadithi husika.
.
Lakini pia ile Mwalimu anakuja ghafla darasani kisha anamchagua mwanafunzi yeyote aimbe shairi na akikosea basi viboko vinamiminwa

Basi ikawa kila unaporudi home unakariri haswa mashairi ili kesho na wewe uonekane konki
Mashairi yalikua murua Sana na haya ni mfano tu
[emoji652]
"BABA NA MAMA SALAMU
nyumbani nawatumia
Siwezi kupiga simu
Niko Mbali na dunia
Bila Shaka mwafahamu
Jela Nina tumikia
Sina Wa kumlaumu niliyataka mwenyewe"
[emoji654]
"NIKIMALIZA KUSOMA
Nitafanya kazi gani
Nipende kuwa rubani
Kazi nzuri ya heshima
Nirushe ndege angani
Inifikishe salama
Nikimaliza kusoma nitafanya kazi gani"

[emoji654]

"CHITEMO MIMI MASIKINI
uvivu wangu nyumbani
Nikiwa huru njiani nakufa
Nakufa hapa kwanini
Sadiki sasa hashiba
Chakula kingi kwa baba
Nirudi tena kwa baba nakufa hapa kwanini"

Ebwana tupia nawewe shairi lako pendwa tujikumbushe zile nyakati za dhahabu kabisa
Mm nayakumbuk ya olevel CHEKA CHEKA
 
Mimi panya ni mwepesi, hadi mnanidharau.
Vipi leo iwe kesi, mimi kuzamisha dau.
Dau kazamisha ng'ombe, ndipo likafanya pindu.
Kichwani ana mapembe, mgongoni ana nundu.

Kitambo sana
Mimi panya ni mwepesi, hadi mnanidharau.
Vipi leo iwe kesi, mimi kuzamisha dau.
Dau kazamisha ng'ombe, ndipo likafanya pindu.
Kichwani ana mapembe, mgongoni ana nundu.

Kitambo sana
Mkuu hili shairi kama unalikumbuka lote naomba ulimalizie aisee
 
aisee umenikumbusha mbali sana braza

nilipewa kipande hiki kukariri ili nije kuimba siku ya kufunga shule

tulikua std 5 mwaka 2000
 
Back
Top Bottom