Na idhaa ya biashara ilikuwa inaanza kwenye kumi na robo hivi,pia nakumbuka matangazo ya radio yakikata gafla kabla hayajarudi tena kulikuwa na kaspecial alarm kanagonga kama dk moja hivi halafu matangazo yanarudi kwa mtangazaji kuomba radhi kwa kukatika matangazoUpo sahihi,idhaa ya biashara ilikuwa ni special kwa mashirika ya umma - kabla mtangazaji hajaanza mambo yake alikuwa anatuomba tuburudike kwa Muziki.
Unakumbuka kipindi cha Muziki na BP cha uncle J Nyaisanga, kila jumatano saa 1:15 jioni, hapo ndio tulikuwa tunapata vitu vipya kabisa toka majuu?
jumapili sa nane mchana nakumbuka ilikuwa NIPE HABARI,kikitangazwa na mkurugenzi DAVID WAKATI...ndio kipindi pekee ambacho Wakati alikuwa anatangaza,ukimsikia sauti yake mara nyingi itakuwa kuna jambo zito la kitaifa.
kweli mkuu ni kitambo kirefu inawezekana nami nimechanganyaKwa kweli ilikuwa ni zamani, lakini sidhani kama Jumapili kulikuwa na kipindi cha aina hiyo hiyo mida, najua kulikuwa na kipindi cha kanisa asubuhi kulikuwa na makengele yanalia, kisha kulikuwa na kipindi cha watoto mashuleni, zilipendwA, salamu za wagonjwa kisha habari,
Kwa jioni nadhani kuliwa na cheichei, kipindi cha dini, nadhani na club rahaleo show
Inawezekana kaka ni muda umepita kwa kweli
Yes, unaanika battery halafu huchezi mbali...Yes madam,ukifumba na kufumbua macho unazikuta kwenye radio ya jirani anasikilizia mpira wa simba na yanga...
huyu mzee si ndio yuko star tv dar sasa hivi!Kile kilikuwa chini ya Angalieni Mpendu
Ndio kaka, ni mtaalamu sana wa lughahuyu mzee si ndio yuko star tv dar sasa hivi!
Nina Uncle wangu anaitwa Chupaki,alikuwa anapenda sana kubandika magazeti ya katuni chumbani kwake.Huenda ndicho chanzo cha jina lakeenzi ile ukiwa na lips kubwa wanakuita chupaki,siku hizi lips kubwa ni "Fasheni" kwa wadada wa dot com.
Umenichekesha madam,ila na mimi nilikuwa na likitabu kubwa ambamo nilikuwa nazikata hizo katuni na kuzibandika pia na picha za mpira,lakini mimi namshukuru mungu nimenusurika kuitwa chupaki.Nina Uncle wangu anaitwa Chupaki,alikuwa anapenda sana kubandika magazeti ya katuni chumbani kwake.Huenda ndicho chanzo cha jina lake
Aksante mkuuMchezo wa mzee Jangala ikidhaminiwa na pombe aina ya chibuku, nakumbuka nyimbo, idara yetu ya uhamiaji nalo jukumu kubwa saanaaaa kuwakaribishaa kuwasafirishaa na kulinda mipaka yetu[emoji441][emoji443][emoji443][emoji445][emoji445]
Watoto wasafi moyonii ni nyoota za macho ya wazaziiiiii[emoji445][emoji445][emoji445][emoji443][emoji443][emoji441]
Shamba aaanii shambaani shambaani mazaoo boora shambaani, haya twendenii shaambanii wananchi tukaalimeee [emoji443] [emoji444] [emoji446] [emoji447]
Wanawakee wa Tanzania wazuuuriii saaaanaaa, wanawakeeee tanzaniaa maendeleo tanzaniaaaa[emoji445][emoji443][emoji441][emoji443][emoji445]
Kuleni chakula boora cha kuujenga muili naku.... Pa kulala pawe boraa[emoji443][emoji445][emoji441]
Wakati umewadia wa salam za wagonjwa hosipitalinii leo tunawapa poleee, ajuaye bwana Mungu kwa mfu kuwa mzima mgonjwa kuwa salamaa leo tunawapa polee[emoji445][emoji445][emoji443][emoji445][emoji445][emoji441]
Wananchiiiii tujifunzeni ushirikaaaaa wananchi tujifunzeni ushirikaaaaa [emoji441][emoji445][emoji445][emoji445][emoji445]
Jamani vitaa imetangazwaa jamaaa wananchi wote tuwe imara, vijijini na mjini msisite kuwasema walanguzi[emoji445][emoji445][emoji445]
Matangazo sasa
1. Tumaa vifurushiii barua na pesa vitu mbalimbali vifike harakaaa tena kwa uhakikaaa, itumie sasaa shirika la posta na simu tanzaaaaniaaa ndio tegemeo letuu.
2. Hebu jitokezeee jioneshe simamaa mbelee za watuuu
3. Tairi general kutoka arushaaa tanzaaaaniaaa
4. Revolaaa revolaaaaa revolaaaaaa revolaaaaaaaa
5. Wee acha kula mali ya umma wee acha kujitafuna tafuna weeeee, wachaaaaaaaaa
6. Tumia chibuku ndio pombe bora, radha ya chibuku hujulikana, sifa moja na nyinginezo ni kulinda hadhi ya mnywaji
7. Komoooooaaaaa aaa komooooaaaa komoaaaa
8. Benki ya akiba ya posta ndio yako, benki ya akiba ya posta ni kwa watanzaniaaa woooote wakubwa kwa wadogo... Wananchi unaweza kufungua akaunti ya kawaaida, akaunti ya muda na akaunti ya muda maaalum.. Usingoje kesho ooo fungua akaunti yako leooo
Watangazaji hahaha Mama Deborah, Dominic Chilambo
Nimejikuta napata sweet memories tu
AksanteDah Mengi
Usomaji wa taarifa wa habari ulikuwa wa makini. Sisi tukiwa wadogo tulikuwa tunabashiri wasomaji.
Na hii ndio Taarifa ya Habari isomwayo na ...... David Wakati, SS. Nkamba/ Juma nGondae/ jamani we
Kipindi cha klabu raha leo Shooooooow!
Salamu kwa wagonjwa!
Mchana mwema
Kipindi cha wafanyakazi jamani- Wimbo wa Msondo-n Nidhamu ya kazi ni msingi wa mafanikio.......( mwenye clip hiyo aiweke)
Pwagu na Pwaguzi
Mchezo wa Redio jamani wanaact kama vile unawaona!! Wasanii hao wangekuwepo leo wangepata hela sana!
Nami pia na mdogo wangu tulikuwa tunabandika za Chakubanga. Sasa kuna mjomba wetu alikuwa nje ya nchi alipokuja alifurahia saana na kuzisoma zote. Natamani ningekitunza mpaka leo. lakini baadae walianzisha kama kitabu hivi cha Chakubanga. jamani old is gold!Umenichekesha madam,ila na mimi nilikuwa na likitabu kubwa ambamo nilikuwa nazikata hizo katuni na kuzibandika pia na picha za mpira,lakini mimi namshukuru mungu nimenusurika kuitwa chupaki.
Basi mimi ntakuita kimoyo moyo kaka yanguUmenichekesha madam,ila na mimi nilikuwa na likitabu kubwa ambamo nilikuwa nazikata hizo katuni na kuzibandika pia na picha za mpira,lakini mimi namshukuru mungu nimenusurika kuitwa chupaki.
Nipeni nguo nifueee....komoaaaTangazo la KOMOA!