Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Upo sahihi,idhaa ya biashara ilikuwa ni special kwa mashirika ya umma - kabla mtangazaji hajaanza mambo yake alikuwa anatuomba tuburudike kwa Muziki.
Unakumbuka kipindi cha Muziki na BP cha uncle J Nyaisanga, kila jumatano saa 1:15 jioni, hapo ndio tulikuwa tunapata vitu vipya kabisa toka majuu?
Na idhaa ya biashara ilikuwa inaanza kwenye kumi na robo hivi,pia nakumbuka matangazo ya radio yakikata gafla kabla hayajarudi tena kulikuwa na kaspecial alarm kanagonga kama dk moja hivi halafu matangazo yanarudi kwa mtangazaji kuomba radhi kwa kukatika matangazo
 
jumapili sa nane mchana nakumbuka ilikuwa NIPE HABARI,kikitangazwa na mkurugenzi DAVID WAKATI...ndio kipindi pekee ambacho Wakati alikuwa anatangaza,ukimsikia sauti yake mara nyingi itakuwa kuna jambo zito la kitaifa.

Kwa kweli ilikuwa ni zamani, lakini sidhani kama Jumapili kulikuwa na kipindi cha aina hiyo hiyo mida, najua kulikuwa na kipindi cha kanisa asubuhi kulikuwa na makengele yanalia, kisha kulikuwa na kipindi cha watoto mashuleni, zilipendwA, salamu za wagonjwa kisha habari,
Kwa jioni nadhani kuliwa na cheichei, kipindi cha dini, nadhani na club rahaleo show

Inawezekana kaka ni muda umepita kwa kweli
 
Kwa kweli ilikuwa ni zamani, lakini sidhani kama Jumapili kulikuwa na kipindi cha aina hiyo hiyo mida, najua kulikuwa na kipindi cha kanisa asubuhi kulikuwa na makengele yanalia, kisha kulikuwa na kipindi cha watoto mashuleni, zilipendwA, salamu za wagonjwa kisha habari,
Kwa jioni nadhani kuliwa na cheichei, kipindi cha dini, nadhani na club rahaleo show

Inawezekana kaka ni muda umepita kwa kweli
kweli mkuu ni kitambo kirefu inawezekana nami nimechanganya
 
Acha kabisa kwa kweli hizo zilikuwa enzi, hao watangazaji walikuwa na uwezo wa kutengeneza sauti na kizifanya ziwe pich kabisa, hadithi kama ya UA JEKUNDU, yule mama alikuwa anasimulia kama senema vile

Kwa kweli ulikuwa sahihi kutengeneza picha za hao watangazji kwa kutumia sauti na hiyo ilikuwa kwa kila mtoto
 
Ni kweli Ben kiko aliripoti kwa namna ya kutukatisha tamaa watanzania kutoka mstari wa mbele wa mapambano dhidi ya Nduli Idd Amin Dadaa.
Fundi mitambo wa kutumainiwa na kutegemewa RTD walikuwa, crispin Lugongo, Noel Namaloe, Ally Said Tunku......
Watangazaji wa mpira wenye utani wa jadi na kuwa kivutio kikubwa kwa wasikilizaji walikuwa Ahmed Jongo na mwenzake wa simba.

Kipindi cha misakato kikiandaliwa kwa ustadi mkubwa. Vipindi kama malenga wetu, kijaluba, mkoa kwa mkoa, vijana leo n.k vilikuwa na mvuto wa pekee.

Mama na mwana, chei chei shangazi,pwagu na pwazi (p & p co. Ltd) mzee jangala, kidole, kiatu, mzee mundu (kwa udhamini wa kibuku) havitapata mpinzani japo havipo hewani.

Majira, mikingamo, salamu za wagonjwa, taarifa za habari, kila mtu alipenda kuvisikiliza

Tangazo la mabati ya galco nalikumbuka sana. Revola, philips ndio yenyewe......., National, n.k

Watangazaji walikuwa mahiri sana, kina Juma Ngondae, Julius Nyaisanga, Salim Mbonde, S. S. Nkamba, Abdul Ngarawa, Eda Sanga, Mikidadi Mahmud, Jackob Tesha.............

Mazungumzo baada ya habari yamewajia kutoka redio tanzania dar es salaam.
 
Nina Uncle wangu anaitwa Chupaki,alikuwa anapenda sana kubandika magazeti ya katuni chumbani kwake.Huenda ndicho chanzo cha jina lake
Umenichekesha madam,ila na mimi nilikuwa na likitabu kubwa ambamo nilikuwa nazikata hizo katuni na kuzibandika pia na picha za mpira,lakini mimi namshukuru mungu nimenusurika kuitwa chupaki.
 
Mchezo wa mzee Jangala ikidhaminiwa na pombe aina ya chibuku, nakumbuka nyimbo, idara yetu ya uhamiaji nalo jukumu kubwa saanaaaa kuwakaribishaa kuwasafirishaa na kulinda mipaka yetu[emoji441][emoji443][emoji443][emoji445][emoji445]

Watoto wasafi moyonii ni nyoota za macho ya wazaziiiiii[emoji445][emoji445][emoji445][emoji443][emoji443][emoji441]

Shamba aaanii shambaani shambaani mazaoo boora shambaani, haya twendenii shaambanii wananchi tukaalimeee [emoji443] [emoji444] [emoji446] [emoji447]

Wanawakee wa Tanzania wazuuuriii saaaanaaa, wanawakeeee tanzaniaa maendeleo tanzaniaaaa[emoji445][emoji443][emoji441][emoji443][emoji445]

Kuleni chakula boora cha kuujenga muili naku.... Pa kulala pawe boraa[emoji443][emoji445][emoji441]

Wakati umewadia wa salam za wagonjwa hosipitalinii leo tunawapa poleee, ajuaye bwana Mungu kwa mfu kuwa mzima mgonjwa kuwa salamaa leo tunawapa polee[emoji445][emoji445][emoji443][emoji445][emoji445][emoji441]

Wananchiiiii tujifunzeni ushirikaaaaa wananchi tujifunzeni ushirikaaaaa [emoji441][emoji445][emoji445][emoji445][emoji445]

Jamani vitaa imetangazwaa jamaaa wananchi wote tuwe imara, vijijini na mjini msisite kuwasema walanguzi[emoji445][emoji445][emoji445]


Matangazo sasa
1. Tumaa vifurushiii barua na pesa vitu mbalimbali vifike harakaaa tena kwa uhakikaaa, itumie sasaa shirika la posta na simu tanzaaaaniaaa ndio tegemeo letuu.

2. Hebu jitokezeee jioneshe simamaa mbelee za watuuu

3. Tairi general kutoka arushaaa tanzaaaaniaaa

4. Revolaaa revolaaaaa revolaaaaaa revolaaaaaaaa

5. Wee acha kula mali ya umma wee acha kujitafuna tafuna weeeee, wachaaaaaaaaa

6. Tumia chibuku ndio pombe bora, radha ya chibuku hujulikana, sifa moja na nyinginezo ni kulinda hadhi ya mnywaji

7. Komoooooaaaaa aaa komooooaaaa komoaaaa

8. Benki ya akiba ya posta ndio yako, benki ya akiba ya posta ni kwa watanzaniaaa woooote wakubwa kwa wadogo... Wananchi unaweza kufungua akaunti ya kawaaida, akaunti ya muda na akaunti ya muda maaalum.. Usingoje kesho ooo fungua akaunti yako leooo

Watangazaji hahaha Mama Deborah, Dominic Chilambo
Nimejikuta napata sweet memories tu
Aksante mkuu
 
Dah Mengi
Usomaji wa taarifa wa habari ulikuwa wa makini. Sisi tukiwa wadogo tulikuwa tunabashiri wasomaji.
Na hii ndio Taarifa ya Habari isomwayo na ...... David Wakati, SS. Nkamba/ Juma nGondae/ jamani we
Kipindi cha klabu raha leo Shooooooow!
Salamu kwa wagonjwa!
Mchana mwema
Kipindi cha wafanyakazi jamani- Wimbo wa Msondo-n Nidhamu ya kazi ni msingi wa mafanikio.......( mwenye clip hiyo aiweke)
Pwagu na Pwaguzi
Mchezo wa Redio jamani wanaact kama vile unawaona!! Wasanii hao wangekuwepo leo wangepata hela sana!
Aksante
 
Umenichekesha madam,ila na mimi nilikuwa na likitabu kubwa ambamo nilikuwa nazikata hizo katuni na kuzibandika pia na picha za mpira,lakini mimi namshukuru mungu nimenusurika kuitwa chupaki.
Nami pia na mdogo wangu tulikuwa tunabandika za Chakubanga. Sasa kuna mjomba wetu alikuwa nje ya nchi alipokuja alifurahia saana na kuzisoma zote. Natamani ningekitunza mpaka leo. lakini baadae walianzisha kama kitabu hivi cha Chakubanga. jamani old is gold!
 
Umenichekesha madam,ila na mimi nilikuwa na likitabu kubwa ambamo nilikuwa nazikata hizo katuni na kuzibandika pia na picha za mpira,lakini mimi namshukuru mungu nimenusurika kuitwa chupaki.
Basi mimi ntakuita kimoyo moyo kaka yangu
 
Ratiba ya ndege kipindi cha ATC hewanii saa nne na robo usiku,duh eti leo tuna ndege moja!
 
Back
Top Bottom