Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Wanabodi,

Baada ya Kifo cha Mtangazaji Nguli nchini, Uncle J. Nyaisanga, naomba kuchukua fursa hii, kufanya reflection ndogo ya Watangazaji wa RTD waliotangulia mbele ya haki. Jee unawakumbuka?, unakumbuka vipindi vyao?!, unawakumbuka kwa lipi?!.

Naomba nisizungumzie kulitowatoa duniani, wala hatima ya familia zao walizoziacha huku nyuma maana sio tuu nitazidi kuogopa, bali pia tutazidi kuumia!. Just imagine, kijitaasisi kidogo kama RTD chenye ofisi yake pale BH-Pugu Road kupoteza idadi kubwa hivi ya watumishi wake (tena hawa ninaowataja ni Watangazaji tuu!, achilia watumishi wengine!. Sii bure!, ila lazima tukubali ni kazi ya Mungu, na kazi ya Mungu haina makosa!.

Hii list sio walikufa lini ni random, nikiwakumbuka wengine nitawaongeza!
Tukianzia na

  1. David Wakati
  2. Abdul Masudi (Jawewa)
  3. Eli Mbotto
  4. Stephen Mlatie
  5. Siwatu Luanda
  6. Salama Mfamao
  7. Salim Seif Nkamba (Mjomba)
  8. Michael Katembo
  9. Nelly Kidella
  10. Halima Mchuka,
  11. Omar Jongo
  12. Tumboi Tamimu Risasi
  13. Mohamed Ng'ombo
  14. Abisai Stephen (Uronu)
  15. Stephen Lymo.
  16. Nadhir Mayoka
  17. Juma Ngodae
  18. Rukia Machumu
  19. Karim Besta
  20. Henrick Michael Libuda
  21. Idrissa Sadalah
  22. Bati Kombwa
  23. Iddi Rashid Mchatta
  24. Dominic Chilambo
  25. Hassan Mkumba
  26. Khadija Said
  27. Ally Saleh
  28. Kwegier Munthali
  29. Leonard Mtawa
  30. Khalid Ponera
  31. Ben Kiko

Jee unawakumbuka?, unakumbuka vipindi vyao?!, unawakumbuka kwa lipi?!.
Pia sio vibaya kuwaulizia wale watangazaji wa siku nyingi ambao hatujui walipo, ili kama nao wametangulia tuyaingize majina yao.

RIP All the Fallen Heroes wa Tasnia ya Utangazaji Tanzania!,

Pascal.

Asanteni kwa taarifa, nime update list, sasa idadi ya Watangazaji wa iliyokuwa Radio Tanzania, Dar es Salaam (RTD) wamefika 31!, kwa taasisi moja, waliofanya kazi ndani ya jengo moja (BH) pale Pugu Rd, vifo vya watu 31, ni vingi mno!.

Pascal.
 
Wanabodi,

Baada ya Kifo cha Mtangazaji Nguli nchini, Uncle J. Nyaisanga, naomba kuchukua fursa hii, kufanya reflection ndogo ya Watangazaji wa RTD waliotangulia mbele ya haki. Jee unawakumbuka?, unakumbuka vipindi vyao?!, unawakumbuka kwa lipi?!.

Naomba nisizungumzie kulitowatoa duniani, wala hatima ya familia zao walizoziacha huku nyuma maana sio tuu nitazidi kuogopa, bali pia tutazidi kuumia!. Just imagine, kijitaasisi kidogo kama RTD chenye ofisi yake pale BH-Pugu Road kupoteza idadi kubwa hivi ya watumishi wake (tena hawa ninaowataja ni Watangazaji tuu!, achilia watumishi wengine!. Sii bure!, ila lazima tukubali ni kazi ya Mungu, na kazi ya Mungu haina makosa!.

Hii list sio walikufa lini ni random, nikiwakumbuka wengine nitawaongeza!
Tukianzia na

  1. David Wakati
  2. Abdul Masudi (Jawewa)
  3. Eli Mbotto
  4. Stephen Mlatie
  5. Siwatu Luanda
  6. Salama Mfamao
  7. Salim Seif Nkamba (Mjomba)
  8. Michael Katembo
  9. Nelly Kidella
  10. Halima Mchuka,
  11. Omar Jongo
  12. Tumboi Tamimu Risasi
  13. Mohamed Ng'ombo
  14. Abisai Stephen (Uronu)
  15. Stephen Lymo.
  16. Nadhir Mayoka
  17. Juma Ngodae
  18. Rukia Machumu
  19. Karim Besta
  20. Henrick Michael Libuda
  21. Idrissa Sadalah
  22. Bati Kombwa
  23. Iddi Rashid Mchatta
  24. Dominic Chilambo
  25. Hassan Mkumba
  26. Khadija Said
  27. Ally Saleh
  28. Kwegier Munthali
  29. Leonard Mtawa
  30. Khalid Ponera

Jee unawakumbuka?, unakumbuka vipindi vyao?!, unawakumbuka kwa lipi?!.
Pia sio vibaya kuwaulizia wale watangazaji wa siku nyingi ambao hatujui walipo, ili kama nao wametangulia tuyaingize majina yao.

RIP All the Fallen Heroes wa Tasnia ya Utangazaji Tanzania!,

Pascal.

Kuna vitu viwili hapa, eidha umri wangu haujaenda sana kama ninavyodhani au hawa ni wakongwe wa zamani sana. Yaani angalau kwa mbaaaaali nimewahi sikia jina la Omar Jongo pia Halima mchuka. Namkumbuka Sued Mwinyi na Nkamia mpirani. Ila nina uhakika hao kwenye list walikuwa balaaa.
 
kaka Pasco...

Ndugu yetu Ben Kiko naye kapendwa zaidi na Maulana na anaingia kwenye katika list ya wapendwa wetu waliotangulia mbele za haki...

Hakika ni majonzi tele...

www.jamiiforums.com/habari-na-hoja-mchanganyiko/750143-tanzia-ben-kiko-afariki-dunia-2.html#post11011066
[h=3]Mkuu Watu8, Asante kwa taarifa, nime update list, sasa idadi ya Watangazaji wa iliyokuwa Radio Tanzania, Dar es Salaam (RTD) wamefika 31!, kwa taasisi moja, waliofanya kazi ndani ya jengo moja (BH) pale Pugu Rd, vifo vya watu 31, ni vingi mno!.[/h]
Pasca
 
Kuna vitu viwili hapa, eidha umri wangu haujaenda sana kama ninavyodhani au hawa ni wakongwe wa zamani sana. Yaani angalau kwa mbaaaaali nimewahi sikia jina la Omar Jongo pia Halima mchuka. Namkumbuka Sued Mwinyi na Nkamia mpirani. Ila nina uhakika hao kwenye list walikuwa balaaa.
Barafu, utakuwa dogo, enzi hizo redio ilikuwa moja tuu, RTD, na kulikuwa hakuna TV, hivyo wale wa zamani, haya ni majina ya kawaida sana!, na huo uliowataja, wa zamani ni Jongo, wengine ni wa juzi kati!.

Pascal.
 
Wadau hivi Jacob Tesha yuko wapi siku hizi?
 
[h=3]Mkuu Watu8, Asante kwa taarifa, nime update list, sasa idadi ya Watangazaji wa iliyokuwa Radio Tanzania, Dar es Salaam (RTD) wamefika 31!, kwa taasisi moja, waliofanya kazi ndani ya jengo moja (BH) pale Pugu Rd, vifo vya watu 31, ni vingi mno!.[/h]
Pasca

Dada Yetu Restuta Bukoli sijaona jina lake.
 
Kharid Ponela nae ametutoka lini jamani, RIP watangazaji wote wa RTD, sitokuja kumsahau Siwatu Luanda, yule dada alivyokufaga nilitoaga machozi
Mkuu Ram, Ponera alitutoka siku nyingi!, ila Siwatu alitangulia sana!, alikuwa na mguu hatari!.

RIP Ponera, RIP Siwatu.

Pascal.
 
Wadau hivi Jacob Tesha yuko wapi siku hizi?
Jakob Tesha yupo, ni mstaafu, mara mwisho alikuwa wizara ya Habari na Vijana na Utamaduni. Sasa hivi yeye na Edda Sanga wana kampuni ya ushauri wa habari, wanaishauri Mlimani Radio na TV.

Pascal.
 
Dada Yetu Restuta Bukoli sijaona jina lake.
Mkuu Masuke, naomba tukumbushane details, alikuwa ni mtangazaji wa lini, vipindi vyake, na alitangulia lini mbele ya haki, ila sio lazima kutaja kilichomtanguliza!.

Pascal.
 
Mimi nakumbuka kipindi cha mama na mwana japo sifahamu kama mama yetu yu hai alitusimulia hadith ya adili na nduguze, kidogo nakipindi cha kombola tulikua kambi ya umishumta bahi sokoni muda huo mwalimu ndyo aliutumia kutuamsha kuanza mazoezi,daa kweli sasa tumezeeka.
 
Mkuu Masuke, naomba tukumbushane details, alikuwa ni mtangazaji wa lini, vipindi vyake, na alitangulia lini mbele ya haki, ila sio lazima kutaja kilichomtanguliza!.

Pascal.

Nakumbuka alikuwa anaripoti kutoka Shinyanga hasa kipindi cha majira asubuhi na usiku, na wakati TBC1 (TVT wakati huo) ilivyoanza akawa anaripoti kwenye taarifa za habari za TV kutokea Shinyanga huko huko.

Sikumbuki hasa ni miaka ipi alianza kutangaza, hata mwaka aliofariki exactly sikumbuki ninachokumbuka ni kwamba alifariki kipindi cha Kikwete inaweza kuwa kati ya 2006 na 2007 kwa sababu Kikwete alihudhuria ule msiba na mazishi yalifanyika mkoani mwanza sehemu moja inaitwa Kisesa.
 
Nakumbuka alikuwa anaripoti kutoka Shinyanga hasa kipindi cha majira asubuhi na usiku, na wakati TBC1 (TVT wakati huo) ilivyoanza akawa anaripoti kwenye taarifa za habari za TV kutokea Shinyanga huko huko.

Sikumbuki hasa ni miaka ipi alianza kutangaza, hata mwaka aliofariki exactly sikumbuki ninachokumbuka ni kwamba alifariki kipindi cha Kikwete inaweza kuwa kati ya 2006 na 2007 kwa sababu Kikwete alihudhuria ule msiba na mazishi yalifanyika mkoani mwanza sehemu moja inaitwa Kisesa.
Masuke, asante kwa taarifa, kumbe huyu ni Mtangazaji wa RTD ya juzi ilipokuwa TBC!, hawa karibu wote ni watangazaji wa zamani iliyokuwa RTD kabla haijawa TBC.

Hata hivyo nimemuongeza kwenye list.

Thanks.

Pascal
 
Mimi nakumbuka kipindi cha mama na mwana japo sifahamu kama mama yetu yu hai alitusimulia hadith ya adili na nduguze, kidogo nakipindi cha kombola tulikua kambi ya umishumta bahi sokoni muda huo mwalimu ndyo aliutumia kutuamsha kuanza mazoezi,daa kweli sasa tumezeeka.
Udaa, Kipindi cha Mama na Mwana ni cha Deborah Mwenda, sasa hivi amestaafu, ila anaendelea na kipindi TBC-1
 
Masuke, asante kwa taarifa, kumbe huyu ni Mtangazaji wa RTD ya juzi ilipokuwa TBC!, hawa karibu wote ni watangazaji wa zamani iliyokuwa RTD kabla haijawa TBC.

Hata hivyo nimemuongeza kwenye list.

Thanks.

Pascal

Ameanza kutangaza wakati huo ikiitwa RTD.
 
michael katembo kipindi cha mkoa kwa mkoa duh mara ya kwanza nausikia wimbo wa kila munu ave na kwao. zamaniiii
 
Huyu alikuwa sister wangu sana, wimbo wake wa mwisho kabla hajaanza kuumwa uliitwa "Ousmane Bakayoko", siku ya kifo chake nilimpigia wimbo "Salama" wa Marijani Rajab

Nkizisikia nyimbo hizi, namkumbuka sana Salama!.

Nawe Mkumbuke.

Marijani Raajab - Salama - YouTube

Pascal

Huo wimbo naupenda sana.
By the way Salama Mfamao alikuwa sister wako sana au "sister wako sana"?
 
Wanabodi,

Baada ya Kifo cha Mtangazaji Nguli nchini, Uncle J. Nyaisanga, naomba kuchukua fursa hii, kufanya reflection ndogo ya Watangazaji wa RTD waliotangulia mbele ya haki. Jee unawakumbuka?, unakumbuka vipindi vyao?!, unawakumbuka kwa lipi?!.

Naomba nisizungumzie kulitowatoa duniani, wala hatima ya familia zao walizoziacha huku nyuma maana sio tuu nitazidi kuogopa, bali pia tutazidi kuumia!. Just imagine, kijitaasisi kidogo kama RTD chenye ofisi yake pale BH-Pugu Road kupoteza idadi kubwa hivi ya watumishi wake (tena hawa ninaowataja ni Watangazaji tuu!, achilia watumishi wengine!. Sii bure!, ila lazima tukubali ni kazi ya Mungu, na kazi ya Mungu haina makosa!.

Hii list sio walikufa lini ni random, nikiwakumbuka wengine nitawaongeza!
Tukianzia na

  1. David Wakati
  2. Abdul Masudi (Jawewa)
  3. Eli Mbotto
  4. Stephen Mlatie
  5. Siwatu Luanda
  6. Salama Mfamao
  7. Salim Seif Nkamba (Mjomba)
  8. Michael Katembo
  9. Nelly Kidella
  10. Halima Mchuka,
  11. Omar Jongo
  12. Tumboi Tamimu Risasi
  13. Mohamed Ng'ombo
  14. Abisai Stephen (Uronu)
  15. Stephen Lymo.
  16. Nadhir Mayoka
  17. Juma Ngodae
  18. Rukia Machumu
  19. Karim Besta
  20. Henrick Michael Libuda
  21. Idrissa Sadalah
  22. Bati Kombwa
  23. Iddi Rashid Mchatta
  24. Dominic Chilambo
  25. Hassan Mkumba
  26. Khadija Said
  27. Ally Saleh
  28. Kwegier Munthali
  29. Leonard Mtawa
  30. Khalid Ponera
  31. Ben Kiko
  32. Restuta Bukholi

Jee unawakumbuka?, unakumbuka vipindi vyao?!, unawakumbuka kwa lipi?!.
Pia sio vibaya kuwaulizia wale watangazaji wa siku nyingi ambao hatujui walipo, ili kama nao wametangulia tuyaingize majina yao.

RIP All the Fallen Heroes wa Tasnia ya Utangazaji Tanzania!,

Pascal.

NB. Pia unaweza Kupata Taarifa za Baadhi ya Watangazi waliotutoka hapa.

Tribute to David Wakati, Kikwete, Mengi, Nchimbi na ...

Tribute to David Wakati: His Legacy Will Live On!
Mzee David Wakati Katutoka Leo Translate this page




Tribute To Uncle J. Nyaisanga: Jee Unamkumbuka kwa Lipi?!. Kuagwa ...

TBC haikumtendea haki marehemu David Wakati - Jamii Forums

  1. Tribute to Halima Mchuka: Alikuwa Mtu wa Watu!
    Halima Mchuka hatunae duniani - Page 2 - JamiiForums
    Hii RTD unaikumbuka? - JamiiForums
    Msiba wa halima mchuka hauna nafasi tbc - JamiiForums
    Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa RTD - Jamii Forums
    Topic: Nimewakumbuka hawa pia..................zamani... - Jamii ...


    Mtangazaji Maarufu wa RTD Amefariki Dunia Asubuhi Hii ..


Malima Ndelema
 
Back
Top Bottom