Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

...Dominick Chilambo...
Hatupo nae sasa.... Nakumbuka nilisikia sauti yake ya mwisho..live... Tukuyu Stars ilikua uanjan...

RTD ...ilirusha...
RIP.
 
Mie nlikuwa napenda kile kitangazo "Wewe acha kula mali ya uma, wewe acha kujitafunatafuna kama punguani, wewe!" Teh! Teh!
 
saa moja jioni kipindi cha kahawa....lol.....na kale kanyimbo chake..."kahawa ni zao lenye faida kubwa"".....cjui nini nini......!!!! au wakati wa adhuhuri hapo kitu cha dongo kipo jikoni kitu ndani ya chungu hadi kina abuu wanapata harufu yake....lol
 
kipindi cha majira saa tatu na ule wimbo wa kuashiria kipindi kinaanza na lile tangazo la sabuni ya komoa"nipeni maji nifueee komoa sabuni ya komoa komoa"ilikua burudani tosha
 
..hihi je: boomuu boomuu bomuuu eeehhh....watu wote wanazaaa....bwana bomuuu kazidiiishaa weee....!!!
afu kulikuwa na kipindi flani hivi majira ya saa moja usiku kilikuwa kinahusu igizo la kuhamasisha mambo ya maji...kuna mzee mmoja hivi alikuwa mbishi vibayaaa....sijui kilikuwa kinaitwaje kile kipindi!!
 
Deborah mwenda (mama na mwana) ua jekundu,mazungumzo baada ya habari. karibun watotoo woote,tufurahi watotoo wotee.
 
Sikiliza bwana umemeeee cjui ilikuwa ni kila juma ngap ah kitambo sana
 
Alafu kuna kialarm fulan kilikuwa kinapga kama ikitokea mitambo kukorofisha au umeme ukikatka rtd.Nduuuu nduuuu ndu ndu ndu nduuuu.Kinadumu kama dk 2 au 3 then afta hapo kumradhi za kumwaga zinafata.Ha ha ha ha ha
 
Bustani ya malenga unaikumbuka? Enz hzo saa 6 mchana njaa inauma sana dizain bi mkubwa au mfanyakaz yupo jikon anapka ugali na mboga fulan huipendiiii.Bas na yale mashairi ndo yanazd kuongeza unenge na hasira fulan.Ha ha ha mbaya zaidi jiran unaskia harufu ya mikarangizo ya kufa mtu kwenda huwez mana bi mkubwa anakukomalia usile kwa watu.Ha ha ha very funny
 
Mwaka ilipovunjika jumuia ya Afrika Mashariki yale mazungumzo baada ya habari kuhusu NYAN'GAU.Klabu raha leo shoo ambapo bendi zilitoa nyimbo zao mpya walizorekodi rtd.Mikingamo kilijaa unafiki kwa kuwatoa kafara vidagaa na kuyaacha mapapa na nyangumi.Pwagu na Pwaguzi.Kijaruba na Abdala Mlawa.External service Ras T (sasa Baba T wa EA radio) alikuwa na kipindi cha muziki wa reggae siku ya ijumaa au jmosi.Na msituko waliopata wasikilizaji wa kipindi cha michezo mtangazaji maarufu wa kipindi marehemu Abdul Masudi Jawewa alipoacha kazi rtd na kwenda ajiliwa kwa Virani.Matangazo ya moja kwa moja(live) siku kiongozi wa chama cha wapigania uhuru wa msumbiji FRELIMO marehemu Samora Machel alipokuwa akiwasuta hadharani wasaliti wa harakati hizo kutokea nachingwea.Matangazo ya moja kwa moja ya mazishi ya marehemu Edward Sokoine na Cardinal Rugambwa.NITARUDI BAADAE.
 
Huyu jamaa hata kama mko na mambo yenu mlikuwa mnalazimika kuacha na kumsikiliza , ole wao watoto wapige kelele wakati Tesha ananguruma!



me too, kumbe utoto sio mbali 25 yrs back naona niko pembeni ya redio baada ya mama na mwana mpira........



Where is Salama Mfamao??



U see may be we can always love our country kwa kukumbushana enzi hizo,,,,,...sio leo!

Namkumbuka Tesha.
Nakumbuka siku anatangaza kustaafishwa u RPC bwana Maji.
Namnukuu:
"Habari kamili, Dar es Salaam.
Serikali imemstaafisha kwa manufaa ya umma, kamanda wa Polisi wa mkoa wa Dar es Salaam, Bwana Tryphone Maji."
 
Juma Ngondae, Salim Mbonde na Abdul Ngarawa walikuwa wataalam wa "Mazungumzo baada ya habari",
yakiratibiwa kwa karibu na Paul Sozigwa.
 
Jacob Tesha, alipokuwa akisoma habari nilikuw nageuka kumtazama Baba. Sauti nzito. Debora Mwenda enzi za Mama na Mwana, hadithi ya Ua jekundu na Binti Chura. Ah! Watu wamesahau Adili na Nduguze. Saa nane na dakika 2 kila jumapili. Acha tu, wakati huo Nyerere alikuwa hai.

Ni Jumamosi aisee, si J2. Marudio J3, saa 11.02 jioni.
 
Nikipindi cha pili cha pili hapa wao sifuri sisi moja na utamsikia tukifungwa timu ya taifa alikuwa hata hasemi goooooooooooo utasikia washatufunga. namna gani hapa jamaa alitakiwa kutumia hata ulimi kuweka ule mpira kimiani. Ahmedi Kampira na mpira lalalalalalalalalaaaaa ah namna gani Juma Mgunda anashindwa kuona milingoti mitatu hapa.
Kwenye maguu kumi nane ana weka mpira ule Edward Chumila na na simba wanafanya mabadiliko namuona kocha mchezaji anaingia hapa heeeee he Chumila kwa guu lake la kushoto anapiga mpira ule anaingiza majalo moja pale ile inaitwa banana chop gooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooo a namna gani hapa mpira unagonga mtambaaaaa panya wasikilizaji ..................... nikikumbuka enzi hizo sipati jibu

I like this!
 
safi sana Mkuu - memory nzuri - tumewakumbuka wengi sababu wakati huo Radio ilikuwa moja tu - mi nilipenda kipindi cha michezo - mbili kasoro robo na majira saa tatu na jambo asubuhi----

Sikonge kuna wimbo huu nafikiri utaukumbuka

--- kumekuchaa jamaa kumekuchaaa ----majogoo vijijini wanawikaa----wananchi amkeni tufanye kazi sasaaa......tusonge mbeleee - tosonge mbeleee

Nikisikia unapigwa basi najua tayari kumekucha kweli - kujiandaa kwenda shule....Hapa nakumbuka ujamaa ujamaa vile duh.

Hapo ulipoandika "wananchi" kulikuwa na neno "wazalendo"
 
Back
Top Bottom