Tukiachana na Fibre Cables, hiki ni kisababishi kingine cha ukosefu wa intaneti

Tukiachana na Fibre Cables, hiki ni kisababishi kingine cha ukosefu wa intaneti

Mzee acha kushika watu masikio...

Kuna double fiber cuts kwa ISPs ambao ni major suppliers wa internet Tanzania (Seacom na Eassy), cut ya kwanza ilitokea mwaka huu mwanzoni na impact haikuwa kubwa sababu ya uwepo wa second link ya kusini...
Naunga mkono hoja 🤣😁
 
View attachment 2989833
Picha: Internet Fibre Cable ndani ya bahari ya Hindi ambayo Watanzania walio wengi waliaminishwa kuwa huenda ikawa na matatizo yaliyopelekea tatizo la internet

=================

Umekuwa ukipata shida ya mtandao kwenye hizi siku mbili-tatu ndani ya hii weekend? Umejiuliza kwa nini na kulaumu sana mtandao wako?

Usilaumu sana hili tatizo limesababishwa na "Geomagnetic Instability" Huku ni kuyumba-yumba kwa mawimbi ya umeme na sumaku kwenye anga la Dunia. Ngoja nikueleweshe.

Dunia ina mawimbi ya sumaku na umeme, kuanzia ardhini hadi kwenye anga lake, kuna sehemu huko angani inaitwa "Ionosphere", ni ukanda wenye chaji za umeme zinazotembea, ambazo huweka msawazo sawa kati ya umeme na nguvu ya mvutano kuunda mawimbi fulani ambayo huzingira Dunia na kuilinda.

Ukanda huu hulinda dunia dhidi ya joto kali na mawe ambayo huja kuipiga dunia, yakifika kwenye ukanda ule huweza kuungua na ndipo huwa tunaona moto wa vimondo vikikatiza angani usiku.

Nguvu hii ya umeme na sumaku ambayo huzunguka Dunia ndiyo husaidia katika mawasiliano ya wireless kwa kutumia satellite.

Vifaa kama simu, TV, Vingamuzi nk huunganishwa na Satellites kuweza kuwasiliana na mawimbi ya mawasiliano hupita kwenye ukanda wa umeme na sumaku unaozunguka Dunia.

Ukanda huu ukivurugika mawasiliano huharibiwa au kuvurugika kwa muingiliano au mawimbi hushindwa kusafiri kwenye anga, hii kitu tunaita "Transmission Interference"

Kuvurugika kwa mawimbi hayo ya sumaku (Geomagnetic Instability) ndicho kilichotokea na kufanya mawasiliano yayumbe kwa kiasi fulani karibu kote Duniani. Hiyo instability imesababishwa na "Geomagnetic Storm"

Hapa sasa kuna story ndefu kidogo. Tuifupishe namna hii.

Ukifatilia kwenye vyanzo vya habari vikubwa kama BBC, CNN, FoxNews, AlJazeera, NYtimes, NatGeo, NASA nk utaona kuna habari zilizogonga vichwa vya habari zikisema watu wameshuhudia kumeta-meta kwa anga kwenye ukanda wa kaskazini (Northern Hemisphere)

View attachment 2989837

Kumeta-meta kwa anga kumeonekana London, California, Baadhi ya miji Canada, na baadhi ya maeneo mengine huko Ulaya na Urusi. Kuna kitu kama mwanga wa ajabu unameta-meta angani majira ya usiku au jioni Jua linapozama, unaitwa "Aurora"

Wakati huo huo, NOAA– National Oceanic and Atmospheric Administration, shirika la hali ya hewa la Marekani lenye uhusiano wa mazingira ya kimataifa limetoa majibu ya kipimo cha Solar Flare iliyopigwa picha na NASA kufikia kiwango cha G5.

Solar Flare ni nini?
Hii ni aina ya Volcano inayolipuka kwenye Jua, Jua limeundwa na plasma ya moto sana kuanzia kwenye kiini chake mpaka kwenye uso wake, mchakato wake wa kulipuka kuunda joto unaofanyika kwa kuungana kwa Helium na Hydrogen wakati mwingine husababisha mlipuko ambao unatoka nje ya Jua kama ilivyo Volcano.
View attachment 2989838

Kama ilivyo Volcano ya huku, ujiuji wa moto huruka juu ya mlima na huitwa Lava, kule kwenye Jua ule ujiuji huwa ni plasma ya moto sana na ikiruka juu inakuwa na gesi za mtoto, mionzi mikali, punjepunhje za charge na umeme, ambazo husambaa kwenye anga lote la Jua.

Jua lina Anga kama ilivyo Dunia yenye Atmosphere, anga la Jua huitwa Corona. Corona ni gesi za moto sana, ni ukanda wenye joto na mionzi mikali kuweza kuyeyusha chuma, umeme wake huweza kuyeyusha Dunia na isionekane.

Volcano ya Jua (Solar Flare) inapoteka, ujiuji wa plasma na gezi kutoa kwenye uso wa Jua, husukuma gezi zote za moto zilizo kwenye Corona ziweze kutanuka na kutembea kutoka kwenye ukanda wa Jua na kusambaa kwenye anga lingine karibu na Jua.

Solar Flare ni mlipuko wa volcano kwenye Jua. Alafu kule kusambaa kwa moto wa Corona kunaitwa "Coronal Mass Ejection (CME)" ni ketendo cha zile gesi za moto na umeme pamoja na magnetic field za Jua kusambaa kuelekea mbali.

Kama Flare itakuwa ni kubwa kiwango cha kusukuma hizo material za Corona kuondoka kabisa kwenye anga la Jua, zile material zitaanza kusambaa angani kote kama upepo uliobeba umeme, na nguvu ya mionzi kuelekea Sayari zilizo karibu na Jua. Upepo huo wa moto unaitwa "Solar Wind"

Solar Wind nyingi huifikia sayari ya Mercury karibu kila siku, kwa sababu iko karibu na Jua, kuna baadhi ya nyakati Solar Wind hufika huku Duniani na zinakuwa hazina nguvu ya kuharibu zaidi, sana sana hutokea ongezeko la joto na kutokea kwa Aurora hafifu.

Aurora–kule kumeta-meta kwa rangi mbalimbali angani, kunaonekana-ga Northern Hemisphere– inatokea kwa zile punjepunhje za gesi zilizo kwenye anga letu, kuchomwa na mionzi ya umeme unaotengenezeka kwenye Geomagnetic Storm.

Nilikwambia anga letu kule juu kuna chembechembe za umeme na sumaku zilizo kwenye (equilibrium) msawazo sawa kwa ajili ya kulinda Dunia, chini kidogo kuna ukanda wa gesi wa kulinda hiyo mionzi isichome viumbe wa Duniani unaitwa Ozone.

Chini kidogo ya Ozone ndipo kuna hizi gesi tunazopumua na kuendeshea maisha, sasa ule moto na ions za umeme na joto ukiweza kushuka chini kidogo utaanza kuunguza zile gesi mfano Ammonia, Nitrates, Hydrogen, Oxygen nk na moto wa hizo gesi huwa una rangi mbalimbali.

Kwa hiyo, Geomagnetic Storm ikitokea, inasababisha msawazo kuparaganyika (Instability) lile joto linaweza kushuka chini kidogo na kuanza kusumbua gesi kadhaa ambazo tutaona zikiungua huku zikitoa rangi mbalimbali angani, zile rangi angani huitwa Aurora.

Hiyo Geomagnetic Storm ni kitu kama kimbunga kinachoambatana na joto na mionzi ya umeme kinachotokea baada ya kuparaganyika kwa magnetic field ya Dunia.

Magnetic field ya Dunia sana sana kuja kuona imeparaganyika mpaka iwe inasumbuliwa na Magnetic field za Jua ambazo zinafika huku kupita Solar Wind.

Unakumbuka Solar Wind nimekwambia zinatokana na nini?
Ni Coronal Mass Ejection; kufyatuka kwa maada za moto mpaka kusambaa kwenye anga lote karibu na Jua.

Sayari zote zilizo karibu na Jua hupokea hicho kimbunga cha moto mkali na mionzi,
Cosmological Symmetry imeiweka Dunia mbali na Jua kwa kilomita Milioni 150, la sivyo tungeshaungua-ga mda mrefu.

Kwa hiyo ndo hivyo. NASA ile ujumaa walitoa ripoti ya kwamba vinasa taarifa vyao vya angani vimeona Jua likilipuka Flare ambayo imeelekea kabisa ukanda ilipo Dunia kwa sasa, hivyo kama kuna madhara yanaweza kutufikia.

Watu wa anga na taarifa za bahari, NOAA, wakasema kulingana na vipimo vyao wanaiweka hiyo Flare kwenye kizio cha G5 (Hii inahitaji elimu nyingine kuielewa)

Kwa kipimo hicho, NASA wakarudi na majibu kuwa nguvu ya Solar Wind kutokana na Volcano hiyo inaweza kutufikia ikasababisha Aurora na hata kuvuruga mfumo wa mawasiliano ya Satellites.

Kufika Jumamosi Mei 11, baadhi ya nchi za kaskazini zilikuwa zimeshaona Aurora, na makampuni ya mawasiliano yanayohusiana na mfumo wa kimawasiliano wa Satellites za Marekani za Pentagon yalianza kukumbana na Traffic Interference kwenye online transmitter zao. Kufika jumapili ya leo makampuni mengine yanayohusiana na Satellite za urusi na Ujerumani nayo yameanza kuona mtafaruko kwenye mawasiliano yao.

Matatizo mbalimbali ya kimtandao yanaweza kuendelea kwa siku tano mbeleni, heat wave inaweza kutokea kwa nchi za Ulaya na America Kaskazini.

Vimbunga na mvua kubwa zinaweza kuendelea kwenye ukanda wetu wa Kitropiki na Ikweta, au Joto kali la ghafla kwa siku chache.
MYUMBISHOO
 
Mimi binafsi na Conspiracy zangu naamini hii ni sabotage kutoka starlink ili watu wahamie net za satellite
 
Mada ina knowledge kubwa inaandikwaje Kwa ufupi. Ikiwa huwezi kusoma tafuta mada fupifupi usome zipo nyingi
 
View attachment 2989833
Picha: Internet Fibre Cable ndani ya bahari ya Hindi ambayo Watanzania walio wengi waliaminishwa kuwa huenda ikawa na matatizo yaliyopelekea tatizo la internet

=================

Umekuwa ukipata shida ya mtandao kwenye hizi siku mbili-tatu ndani ya hii weekend? Umejiuliza kwa nini na kulaumu sana mtandao wako?

Usilaumu sana hili tatizo limesababishwa na "Geomagnetic Instability" Huku ni kuyumba-yumba kwa mawimbi ya umeme na sumaku kwenye anga la Dunia. Ngoja nikueleweshe.

Dunia ina mawimbi ya sumaku na umeme, kuanzia ardhini hadi kwenye anga lake, kuna sehemu huko angani inaitwa "Ionosphere", ni ukanda wenye chaji za umeme zinazotembea, ambazo huweka msawazo sawa kati ya umeme na nguvu ya mvutano kuunda mawimbi fulani ambayo huzingira Dunia na kuilinda.

Ukanda huu hulinda dunia dhidi ya joto kali na mawe ambayo huja kuipiga dunia, yakifika kwenye ukanda ule huweza kuungua na ndipo huwa tunaona moto wa vimondo vikikatiza angani usiku.

Nguvu hii ya umeme na sumaku ambayo huzunguka Dunia ndiyo husaidia katika mawasiliano ya wireless kwa kutumia satellite.

Vifaa kama simu, TV, Vingamuzi nk huunganishwa na Satellites kuweza kuwasiliana na mawimbi ya mawasiliano hupita kwenye ukanda wa umeme na sumaku unaozunguka Dunia.

Ukanda huu ukivurugika mawasiliano huharibiwa au kuvurugika kwa muingiliano au mawimbi hushindwa kusafiri kwenye anga, hii kitu tunaita "Transmission Interference"

Kuvurugika kwa mawimbi hayo ya sumaku (Geomagnetic Instability) ndicho kilichotokea na kufanya mawasiliano yayumbe kwa kiasi fulani karibu kote Duniani. Hiyo instability imesababishwa na "Geomagnetic Storm"

Hapa sasa kuna story ndefu kidogo. Tuifupishe namna hii.

Ukifatilia kwenye vyanzo vya habari vikubwa kama BBC, CNN, FoxNews, AlJazeera, NYtimes, NatGeo, NASA nk utaona kuna habari zilizogonga vichwa vya habari zikisema watu wameshuhudia kumeta-meta kwa anga kwenye ukanda wa kaskazini (Northern Hemisphere)

View attachment 2989837

Kumeta-meta kwa anga kumeonekana London, California, Baadhi ya miji Canada, na baadhi ya maeneo mengine huko Ulaya na Urusi. Kuna kitu kama mwanga wa ajabu unameta-meta angani majira ya usiku au jioni Jua linapozama, unaitwa "Aurora"

Wakati huo huo, NOAA– National Oceanic and Atmospheric Administration, shirika la hali ya hewa la Marekani lenye uhusiano wa mazingira ya kimataifa limetoa majibu ya kipimo cha Solar Flare iliyopigwa picha na NASA kufikia kiwango cha G5.

Solar Flare ni nini?
Hii ni aina ya Volcano inayolipuka kwenye Jua, Jua limeundwa na plasma ya moto sana kuanzia kwenye kiini chake mpaka kwenye uso wake, mchakato wake wa kulipuka kuunda joto unaofanyika kwa kuungana kwa Helium na Hydrogen wakati mwingine husababisha mlipuko ambao unatoka nje ya Jua kama ilivyo Volcano.
View attachment 2989838

Kama ilivyo Volcano ya huku, ujiuji wa moto huruka juu ya mlima na huitwa Lava, kule kwenye Jua ule ujiuji huwa ni plasma ya moto sana na ikiruka juu inakuwa na gesi za mtoto, mionzi mikali, punjepunhje za charge na umeme, ambazo husambaa kwenye anga lote la Jua.

Jua lina Anga kama ilivyo Dunia yenye Atmosphere, anga la Jua huitwa Corona. Corona ni gesi za moto sana, ni ukanda wenye joto na mionzi mikali kuweza kuyeyusha chuma, umeme wake huweza kuyeyusha Dunia na isionekane.

Volcano ya Jua (Solar Flare) inapoteka, ujiuji wa plasma na gezi kutoa kwenye uso wa Jua, husukuma gezi zote za moto zilizo kwenye Corona ziweze kutanuka na kutembea kutoka kwenye ukanda wa Jua na kusambaa kwenye anga lingine karibu na Jua.

Solar Flare ni mlipuko wa volcano kwenye Jua. Alafu kule kusambaa kwa moto wa Corona kunaitwa "Coronal Mass Ejection (CME)" ni ketendo cha zile gesi za moto na umeme pamoja na magnetic field za Jua kusambaa kuelekea mbali.

Kama Flare itakuwa ni kubwa kiwango cha kusukuma hizo material za Corona kuondoka kabisa kwenye anga la Jua, zile material zitaanza kusambaa angani kote kama upepo uliobeba umeme, na nguvu ya mionzi kuelekea Sayari zilizo karibu na Jua. Upepo huo wa moto unaitwa "Solar Wind"

Solar Wind nyingi huifikia sayari ya Mercury karibu kila siku, kwa sababu iko karibu na Jua, kuna baadhi ya nyakati Solar Wind hufika huku Duniani na zinakuwa hazina nguvu ya kuharibu zaidi, sana sana hutokea ongezeko la joto na kutokea kwa Aurora hafifu.

Aurora–kule kumeta-meta kwa rangi mbalimbali angani, kunaonekana-ga Northern Hemisphere– inatokea kwa zile punjepunhje za gesi zilizo kwenye anga letu, kuchomwa na mionzi ya umeme unaotengenezeka kwenye Geomagnetic Storm.

Nilikwambia anga letu kule juu kuna chembechembe za umeme na sumaku zilizo kwenye (equilibrium) msawazo sawa kwa ajili ya kulinda Dunia, chini kidogo kuna ukanda wa gesi wa kulinda hiyo mionzi isichome viumbe wa Duniani unaitwa Ozone.

Chini kidogo ya Ozone ndipo kuna hizi gesi tunazopumua na kuendeshea maisha, sasa ule moto na ions za umeme na joto ukiweza kushuka chini kidogo utaanza kuunguza zile gesi mfano Ammonia, Nitrates, Hydrogen, Oxygen nk na moto wa hizo gesi huwa una rangi mbalimbali.

Kwa hiyo, Geomagnetic Storm ikitokea, inasababisha msawazo kuparaganyika (Instability) lile joto linaweza kushuka chini kidogo na kuanza kusumbua gesi kadhaa ambazo tutaona zikiungua huku zikitoa rangi mbalimbali angani, zile rangi angani huitwa Aurora.

Hiyo Geomagnetic Storm ni kitu kama kimbunga kinachoambatana na joto na mionzi ya umeme kinachotokea baada ya kuparaganyika kwa magnetic field ya Dunia.

Magnetic field ya Dunia sana sana kuja kuona imeparaganyika mpaka iwe inasumbuliwa na Magnetic field za Jua ambazo zinafika huku kupita Solar Wind.

Unakumbuka Solar Wind nimekwambia zinatokana na nini?
Ni Coronal Mass Ejection; kufyatuka kwa maada za moto mpaka kusambaa kwenye anga lote karibu na Jua.

Sayari zote zilizo karibu na Jua hupokea hicho kimbunga cha moto mkali na mionzi,
Cosmological Symmetry imeiweka Dunia mbali na Jua kwa kilomita Milioni 150, la sivyo tungeshaungua-ga mda mrefu.

Kwa hiyo ndo hivyo. NASA ile ujumaa walitoa ripoti ya kwamba vinasa taarifa vyao vya angani vimeona Jua likilipuka Flare ambayo imeelekea kabisa ukanda ilipo Dunia kwa sasa, hivyo kama kuna madhara yanaweza kutufikia.

Watu wa anga na taarifa za bahari, NOAA, wakasema kulingana na vipimo vyao wanaiweka hiyo Flare kwenye kizio cha G5 (Hii inahitaji elimu nyingine kuielewa)

Kwa kipimo hicho, NASA wakarudi na majibu kuwa nguvu ya Solar Wind kutokana na Volcano hiyo inaweza kutufikia ikasababisha Aurora na hata kuvuruga mfumo wa mawasiliano ya Satellites.

Kufika Jumamosi Mei 11, baadhi ya nchi za kaskazini zilikuwa zimeshaona Aurora, na makampuni ya mawasiliano yanayohusiana na mfumo wa kimawasiliano wa Satellites za Marekani za Pentagon yalianza kukumbana na Traffic Interference kwenye online transmitter zao. Kufika jumapili ya leo makampuni mengine yanayohusiana na Satellite za urusi na Ujerumani nayo yameanza kuona mtafaruko kwenye mawasiliano yao.

Matatizo mbalimbali ya kimtandao yanaweza kuendelea kwa siku tano mbeleni, heat wave inaweza kutokea kwa nchi za Ulaya na America Kaskazini.

Vimbunga na mvua kubwa zinaweza kuendelea kwenye ukanda wetu wa Kitropiki na Ikweta, au Joto kali la ghafla kwa siku chache.
Huu ni uwongo
 
Internet hatutumii kabisa satelite mzee. Ni fiber kwa asilimia kubwa sana. Na fiber ni glass. Hakuna umeme wala sumaku kwenye fiber. Ishu ni fiber kukatika baharini ndo maana internet inasumbua. Hayo mambo unayoyasema yangukua na ukweli basi TVs ndo zingeathirika coz hizo ndo zinatumia satelite communication
 
Internet hatutumii kabisa satelite mzee. Ni fiber kwa asilimia kubwa sana. Na fiber ni glass. Hakuna umeme wala sumaku kwenye fiber. Ishu ni fiber kukatika baharini ndo maana internet inasumbua. Hayo mambo unayoyasema yangukua na ukweli basi TVs ndo zingeathirika coz hizo ndo zinatumia satelite communication
Hii post ya kwanza thread hii imejaa upotoshaji, halafu muandishi kaiandika kwa madoido na kujiamini kama anajua alichoandika. Kaandika hivyo kwenye hadhira ya watu wengi wasiojua kuhakiki habari, wakisikia mtu anaeleza kitu kwa mbwembwe nyingi, wanafikiri zile mbwembwe ndiyo ujuzi.

Kumbe ujinga na uongo tu.
 
madude kama haya nilikuwa namfatilia sana Prof. Mishio Kaku theoretical physicist mmoja hivi na kuna kipindi cha television kinaitwa Through the Wormhole cha bwana Morgan Freeman
 
Aisee hii mada kuisoma na kuielewa inataka utulivu wa hali ya juu sana
 
Back
Top Bottom