Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Na tuseme AmeeenMWENYEZI MUNGU aendelee kubariki kipaji chako Mr[emoji123]
Thnx much mkali wa hizi kazi[emoji120]
Tuendelee na chombo mkuu.Na Steve B. S. M [emoji106]
Nimeshafika kugawa burudani.Stive w end uje basiii
DoneTUKIBAKI HAI, TUTASIMULIA - 22
Na Steve B.S.M
Baada ya kitambo kidogo, hali ilitulia.
Mpelelezi kwa kutumia weledi wake wa kazi, akaanza kujenga mazingira ya kupata kile kilichomfanya afunge safari kutoka New York.
Mwanamke yule mzee, ambaye alikuja kujitambulisha kama mama wa mtoto aliyetangazwa kuuawa, akiwa anashukwa na machozi mengi, akaeleza namna mambo yalivyotokea.
Alivuta mafua mapesi, akatazama chini.
Macho yake yalikuwa mekundu sana. Uso wake umepwaya kama mtu anayejutia jambo au ametingwa na kitu fulani kizito.
Akiwa ametulia vivyo, aonekana kama yu mbali kimawazo, akaeleza namna gani alivyokuwa anampenda mwanaye.
Alikuwa ni kama tunu kwake, haswa ukizingatia hakubahatika kupata mtoto mwingine zaidi ya huyo.
Alisema,
"Alikuwa ndo' dunia yangu ya pekee. Furaha yangu. Sikujihisi mpweke ninapokuwa naye karibu. Alikuwa akinipenda na mimi nilijitahidi kadiri nilivyoweza kuurejesha upendo huo kwake."
Baada ya hapo, akaeleza namna gani swala la mwanaye kujinyonga lilivyomuacha katika bumbuwazi kwani hakuliona likitokea katika siku za usoni.
Alisema,
"Aliondoka kwenda chuo kama ilivyokuwa siku za kawaida. Sikuona ajabu wala dalili yoyote ile. Baadae majira ya saa mbili usiku, nikiwa na mashaka kwa kukawia kwake kurudi nyumbani nikamtafuta rafiki yake, Ronelle, kumuuliza kwasababu simu ya mwanangu haikuwa inapatikana.
Ajabu nilipompigia akasema hakuwa naye na hakumwona kabisa siku hiyo chuoni. Na kwa kudhania labda hajafika chuo, basi akaendelea na mambo yake kama kawaida.
Tukiwa katika hali hiyo ya sintofahamu, mimi na baba yake tukafanya jitihada za kuwasiliana na chuo. Hawakuwa na majibu.
Tulipotaka kupeleka taarifa kwenye vyombo vya usalama, tukaambiwa kiutaratibu ni mpaka pale siku kadhaa, angalau mbili, zitakapopita bila mrejesho wa mhusika basi ndo watalifanyia kazi shauri letu.
Japo tulieleza sababu ya kuwa na hofu, kwamba binti yetu si mtu wa kutoka na kuchangamana na watu, bado hatukuweza kuwashawishi.
Walishikilia msimamo wao.
Sitakuja kusahau, ni kesho yake majira ya asubuhi, nakuja kupata taarifa ya mwanangu kujinyonga.
Mwili wake ulikutwa mbali na chuo, ukiwa umekabwa na kitanzi, unaning'inia bila uhai."
Mama alipofika hapo, akashindwa kuzungumza kwa kama dakika tatu.
Uchungu ulimkaba kooni.
Alihisi kuna donge kubwa linalosugua kwenye shina la shingo yake na kifua.
Mpelelezi akapata kazi ya ziada ya kumtuliza.
Baada ya dakika hizo, sasa akapata kuendelea.
Akamweleza Mpelelezi kwamba aliushuhudia mwili wa mtoto wake ukiwa mochwari. Shingo yake imekuwa nyekundu kwa kubanwa na kamba ngumu.
Walifanya maandalizi ya msiba, lakini waliporejea tena mochwari hawakukuta mwili wa mtoto wao.
Walifanya kila jaribio, kila eneo waliloweza kufika lakini hamna kilichopatikana.
Mwili ulipotea mochwari katika mazingira ya ajabu mno.
Si kamera za hospitali wala walinzi walioweza kutoa majibu ya kueleweka.
Kote huko walisema hamna wanachokijua. Kilichofanyika ni 'attendant' wa zamu pamoja na security kusimamishwa kwaajili ya uchunguzi lakini baadae, baada ya majuma manne, walirejeshwa kazini kama kawaida.
Hivyo walichofanya, wakatengeneza tu kaburi katika mji wa Colma, mji tengefu kwaajili ya shughuli za mazishi ndani ya Jimbo la California.
Kutoka hapa San Fransisco mpaka huko ni takribani maili 3.23.
Walifanya hivyo kwasababu jiji la San Fransisco, tangu mwaka 1900, lilipiga marufuku shughuli za mazishi ndani ya maeneo yake kwasababu ya ukosefu wa sehemu sahihi kwaajili ya ibada hizo.
Ndani ya jiji hilo maarufu, kuna makaburi mawili tu, yale ya kitaifa (ya kiserikali) na yale ya Mission Dolores ambayo yapo chini ya wakatoliki.
Huko, Colma, wakaweka jeneza lisilokuwa na kitu kama sehemu tu ya kumbukumbu ya mtoto wao ambaye hawakupata kuuona mwili wake.
Alisema,
"Tuliona ni sahihi kufanya hilo kwaajili ya kuheshimu na kuonyesha uwepo wake duniani kisha akaondoka kama wapendwa wengine."
Alifuta kwanza machozi kabla hajendelea kunena mengine.
Naye Mpelelezi alikuwa naye sambamba kuhakikisha hamna anachokosa.
Masikio yake na ubongo wake vilikuwa hai kuliko kawaida.
Mwanamke yule akasema ya kwamba hata pale walipojitahidi huku na kule ili wapate kitu, matokeo yake mume wake akaaga dunia katika ajali ya hit-and-run.
Aligongwa kisha gari likatokomea likimuacha anamwagika damu kama fonteini barabarani.
Alichokuja kuambulia ni mwili wa mumewe ukiwa umepasuka kichwa, vipandevipande vya kutosha kabisa kwenye mfuko mdogo wa rambo.
Hapo Mpelelezi akapata taswira halisinya namna gani mwanamke huyu alikuwa anateseka.
Viatu vyake vilikuwa vikubwa mno kuviingia.
Alikuwa na kila sababu ya kulia akaeleweka na dunia nzima.
Hakumaliza, akaendelea akisema hakukoma kutafuta haki yake.
Alikodisha mpelelezi binafsi wa kuchunguza maswahibu haya baada ya kutumia polisi kushindikana, lakini mpelelezi huyo hakufika mbali.
Baada ya majuma mawili tangu ampe kazi hiyo, akapata taarifa kuwa bwana huyo amekutwa amejinyonga katika makazi yake.
Pembeni aliacha ujumbe wa wapi mwili wake upelekwe na kuhifadhiwa lakini hakusema nini kilipelekea maamuzi hayo ya kushtua.
"Kampuni yake ilikuwa katika kilele cha mafanikio," Mwanamke alisema, "ilikuwa ni ajabu kwake kuacha yote hayo na kutamatisha uhai wake."
Baada ya hapo, alikata tamaa ya kuendelea kutafuta tena.
Alipoteza matumaini.
Alijitenga na maisha na maisha yakajitenga na yeye.
Hata sasa anashangaa nini kilichomleta bwana huyu mpelelezi katika kesi hiyo ya miaka iliyopita.
Kesi ambayo alishaambiwa kuwa imefungwa rasmi muda tu.
Aliuliza,
"Kuna kitu mmepata? ... Mmejua nini kilimkuta mwanangu na mume wangu?"
Mpelelezi akashusha kwanza pumzi maana hakujua hata aanzie wapi katika maswali hayo.
Alichofanya ni kumpatia mwanamke huyo matumaini kwamba anaweza akapata kitu katika juhudi zake.
Angalau sasa amepata mwanga wa pa kuendea.
Kufikia hapo alitaka kujua hospitali ambayo mwili wa binti ulipelekwa, tarehe ambayo mwili ulitoweka, jina la ile kampuni binafsi ambayo iliyokuwa inahusika na upelelezi, na jina la mpelelezi huyo aliyefikwa na mauti akiwa anafanya kazi yake.
Alipovipata akashukuru, lakini kabla hajaondoka mwanamke huyo akampatia kijidaftari kidofo chenye jalada la pinki.
Akamwambia,
"Hii ni diary yake niliyopata kumnunulia. Pengine ukitazama unaweza kupata kitu."
Mpelelezi akaichukua.
Diary ambayo ndo' hii anayo mkononi hivi sasa.
Lakini hakuondoka huko bila kupewa onyo na mwanamke yule mzazi wa binti aliyekufa.
Onyo hilo hakuliacha kulisikia hata sasa.
"Kuwa makini na uhai wako."
Katika yote hayo, bado alikuwa na shauri la kurudi San Fransisco, California, siku za karibuni.
Alimini kabisa kuwa kule ndipo njia ilipo ya kufika anapopataka.
Akiwa taratibu anapitiq diary hiyo akitafuta kama kuna lolote anaweza kuambulia, simu yake ya mezani ikaita.
Alipopokea, akasikia sauti ya mkuu wake wa kitengo.
Alimwambia anamuhitaji ofisini maramoja. Akatii agizo.
Akaelekea huko ambapo alimkuta mkuu wake akiwa ameketi kwa kuegemaza mguu wake wa kushoto juu ya wa kulia.
Mezani kulikuwa na kisosi chenye kipisi kidogo cha sigara kinachoishilia moto.
Bwana huyo aliyekuwa amevalia suti rangi ya damu ya mzee, alikuwa ametulia vema ndani ya kiti chake kikubwa na kirefu chenye nyama za kutosha.
Alimtazama Mpelelezi, bila ya kusema jambo lolote, kisha akavuta droo ya meza yake kubwa, akatoa bahasha ya kaki, kimo cha wastani.
Akaiweka bahasha hiyo mezani akisema,
"Nadhani huu ndo' uamuzi sahihi kwa sasa."
Mpelelezi akaidaka bahasha hiyo asijue kinachoendelea.
Kabla hajaifungua, akaambia arejeshe bunduki ya polisi pamoja na beji yake rasmi. Hivyo vitabakia kituoni mpaka pale atakapopewa taarifa rasmi.
Mkuu alitoa angalizo,,
"Kwa sasa hauruhusiwi kujihusisha na kazi yoyote ya polisi. Hauna ithibati hiyo. Umepewa likizo ya lazima wakati tukiwa tunakagua mwenendo wako. Wakati huo wote utakuwa raia wa kawaida na malipo ya mshahara wako yatakuwa nusu ya kawaida."
Mpelelezi alipotaka kujua sababu, akaambiwa kwa ufupi kuwa ni utovu wa nidhamu.
Baada ya hapo, mkuu wake akamtaka aende zake kwani ana shughuli nyingi za kufanya.
Mpelelezi alipotoka, mkuu akawasha sigara kwa kiberiti chake cha gesi alafu akavuta mikupuo mitatu mikubwa.
Mikupuo ambayo aliivuta kwa hisia zote.
Mapafu yake yalipojaa, akautema moshi nje kana kwamba bomba la trekta.
Muda si mrefu, ofisi yake nzima ikajawa na moshi mnene.
****
Brookhaven, New York.
Saa kumi na moja jioni.
Dr. Lambert alifungua kifungo cha kola ya shati lake, kisha akashusha pumzi ndefu ya unafuu.
Sasa alikuwa anahema.
Mbali na uchovu wa kazi alofanya kutwa nzima, bado hakuwa tayari kwenda nyumbani.
Aliketi katika gari lake akingoja jambo. Macho yake yalikuwa yanatazama 'rearview mirror'' (kioo juu ya kichwa cha dereva) kwa umakini ingali akijitahidi kujiweka 'comfortable' kadiri awezavyo.
Mzee huyu alikuwa amevalia shati jeupe la mikono mifupi. Shati lenye mistari midogomidogo ya rangi ya zambarau.
Shati hilo alilichomekea kwenye suruali yake nyeusi ya kitambaa iliyobanwa na mkanda mnene wa kahawia.
Alingojea hapo kwa kama dakika sita ndo akamwona mtu katika kioo.
Alipotazama vema kiooni, akabaini ni mtu aliyekuwa anamngoja, yaani Dr. Jean.
Bwana huyo mfupi alikuwa amevalia shati jeusi lenye nyotanyota ndogo nyeupe zinazometa. Sarawili ya kadeti, rangi ya kahawia ilokoza, na viatu vikubwa vya ngozi.
Bwana huyo alitembea kuja uwelekeo wa gari la Dr. Lambert, lakini alipopiga hatua kadhaa alibadili mwelekeo wake akielekea upande mwingine.
Alifanya hayo akiwa hana utambuzi wowote kama mwenzake yu kwenye gari anamngoja.
Hapo ikampasa Dr. Lambert ashuke upesi kwenye gari lake na kujaribu kumpungia.
Hakuona.
Ikabidi amuite.
Bwana huyo akageuka na kumwona Dr. Lambert akiwa anapunga mkono kumwita. Akapaza sauti,
"Leo sielekei huko. Unaweza kwenda!"
Kisha akaendelea zake kana kwamba hamna kilichotokea.
Alipotembea kidogo simu yake ikaita mfukoni. Alipotoa kutazama, ni Dr. Lambert.
Akapokea.
"Ebu acha ujinga," sauti ya Dr. Lambert ilifoka na kuamrisha, "Njoo kwenye gari langu upesi!"
Alafu simu ikakata.
Bwana huyo akaona isiwe tabu, akaitikia wito.
Aliketi kwenye kiti cha pembeni ya Dr. Lambert alafu akauliza nini sababu ya wito huo.
Lakini akamsihi Dr. Lambert azingatie muda kwani ana mahali anapotakiwa kuwapo si muda mrefu toka sasa.
Dr. Lambert akajikuta anatabasamu.
"Wewe bwana," akasema akisontea kidole kwa mwenziwe. "Umekuwa wa kunipandishia mabega sasa, sio?"
Dr. Jean hakujibu kitu. Lambert akaendelea kumweleza ni namna gani yeye ni mkubwa katika lile 'deal' alilomtambulisha.
Namna gani alivyoanza 'misheni' hiyo na mpaka hapo alipofikia leo, hivyo Jean anapaswa kumsikiza na kumheshimu sana.
Katika hayo yote aliyojinasibu, Jean hakutia neno lolote, badala yake aliuliza,
"Hiko ndo' umeniitia?"
Dr. Lambert akashusha pumzi ya hasira. Alihisi kifua kinataka kupasuka.
Alijitahidi kumudu hasira zake kwa kuhema mara kadhaa, pumzi ndefu, kisha akarejea kwa upole.
Aliuliza,
"Ni nini mlijadili na Mitchelle siku ile kwenye gari? Nataka kujua."
Jean akatabasamu, kisha akajibu,
"Siko tayari kukwambia. Je, una lingine?"
Mbali na jibu hilo, macho yake yalimkera mno Dr. Lambert. Bwana huyo alikuwa anamtazama kwa mboni za dhihaka.
Basi dokta akajikuta akishika usukani kwa hasira.
Hajakaa vema, Dr. Jean akafungua mlango na kwenda zake.
**
Kuna nini kinaendelea kwa Dr. Jean?
Nini alizungumza na Mitchelle kwa siri siku ile alipokutanishwa naye?
KhaDaah tivu ndogo
Kafupi bwana siku zote hizo ulizotuacha
Siku moja tu?Kafupi bwana siku zote hizo ulizotuacha
Mbona mimi hujanitag mkuu
Hapo sawaSiku moja tu?
Ngoja nitulie, tuendelee.