Tukibaki Hai, Tutasimulia

Tukibaki Hai, Tutasimulia

TUKIBAKI HAI, TUTASIMULIA - 22

Na Steve B.S.M

Baada ya kitambo kidogo, hali ilitulia.

Mpelelezi kwa kutumia weledi wake wa kazi, akaanza kujenga mazingira ya kupata kile kilichomfanya afunge safari kutoka New York.

Mwanamke yule mzee, ambaye alikuja kujitambulisha kama mama wa mtoto aliyetangazwa kuuawa, akiwa anashukwa na machozi mengi, akaeleza namna mambo yalivyotokea.

Alivuta mafua mapesi, akatazama chini.

Macho yake yalikuwa mekundu sana. Uso wake umepwaya kama mtu anayejutia jambo au ametingwa na kitu fulani kizito.

Akiwa ametulia vivyo, aonekana kama yu mbali kimawazo, akaeleza namna gani alivyokuwa anampenda mwanaye.

Alikuwa ni kama tunu kwake, haswa ukizingatia hakubahatika kupata mtoto mwingine zaidi ya huyo.

Alisema,

"Alikuwa ndo' dunia yangu ya pekee. Furaha yangu. Sikujihisi mpweke ninapokuwa naye karibu. Alikuwa akinipenda na mimi nilijitahidi kadiri nilivyoweza kuurejesha upendo huo kwake."

Baada ya hapo, akaeleza namna gani swala la mwanaye kujinyonga lilivyomuacha katika bumbuwazi kwani hakuliona likitokea katika siku za usoni.

Alisema,

"Aliondoka kwenda chuo kama ilivyokuwa siku za kawaida. Sikuona ajabu wala dalili yoyote ile. Baadae majira ya saa mbili usiku, nikiwa na mashaka kwa kukawia kwake kurudi nyumbani nikamtafuta rafiki yake, Ronelle, kumuuliza kwasababu simu ya mwanangu haikuwa inapatikana.

Ajabu nilipompigia akasema hakuwa naye na hakumwona kabisa siku hiyo chuoni. Na kwa kudhania labda hajafika chuo, basi akaendelea na mambo yake kama kawaida.

Tukiwa katika hali hiyo ya sintofahamu, mimi na baba yake tukafanya jitihada za kuwasiliana na chuo. Hawakuwa na majibu.

Tulipotaka kupeleka taarifa kwenye vyombo vya usalama, tukaambiwa kiutaratibu ni mpaka pale siku kadhaa, angalau mbili, zitakapopita bila mrejesho wa mhusika basi ndo watalifanyia kazi shauri letu.

Japo tulieleza sababu ya kuwa na hofu, kwamba binti yetu si mtu wa kutoka na kuchangamana na watu, bado hatukuweza kuwashawishi.

Walishikilia msimamo wao.

Sitakuja kusahau, ni kesho yake majira ya asubuhi, nakuja kupata taarifa ya mwanangu kujinyonga.

Mwili wake ulikutwa mbali na chuo, ukiwa umekabwa na kitanzi, unaning'inia bila uhai."

Mama alipofika hapo, akashindwa kuzungumza kwa kama dakika tatu.

Uchungu ulimkaba kooni.

Alihisi kuna donge kubwa linalosugua kwenye shina la shingo yake na kifua.

Mpelelezi akapata kazi ya ziada ya kumtuliza.

Baada ya dakika hizo, sasa akapata kuendelea.

Akamweleza Mpelelezi kwamba aliushuhudia mwili wa mtoto wake ukiwa mochwari. Shingo yake imekuwa nyekundu kwa kubanwa na kamba ngumu.

Walifanya maandalizi ya msiba, lakini waliporejea tena mochwari hawakukuta mwili wa mtoto wao.

Walifanya kila jaribio, kila eneo waliloweza kufika lakini hamna kilichopatikana.

Mwili ulipotea mochwari katika mazingira ya ajabu mno.

Si kamera za hospitali wala walinzi walioweza kutoa majibu ya kueleweka.

Kote huko walisema hamna wanachokijua. Kilichofanyika ni 'attendant' wa zamu pamoja na security kusimamishwa kwaajili ya uchunguzi lakini baadae, baada ya majuma manne, walirejeshwa kazini kama kawaida.

Hivyo walichofanya, wakatengeneza tu kaburi katika mji wa Colma, mji tengefu kwaajili ya shughuli za mazishi ndani ya Jimbo la California.

Kutoka hapa San Fransisco mpaka huko ni takribani maili 3.23.

Walifanya hivyo kwasababu jiji la San Fransisco, tangu mwaka 1900, lilipiga marufuku shughuli za mazishi ndani ya maeneo yake kwasababu ya ukosefu wa sehemu sahihi kwaajili ya ibada hizo.

Ndani ya jiji hilo maarufu, kuna makaburi mawili tu, yale ya kitaifa (ya kiserikali) na yale ya Mission Dolores ambayo yapo chini ya wakatoliki.

Huko, Colma, wakaweka jeneza lisilokuwa na kitu kama sehemu tu ya kumbukumbu ya mtoto wao ambaye hawakupata kuuona mwili wake.

Alisema,

"Tuliona ni sahihi kufanya hilo kwaajili ya kuheshimu na kuonyesha uwepo wake duniani kisha akaondoka kama wapendwa wengine."

Alifuta kwanza machozi kabla hajendelea kunena mengine.

Naye Mpelelezi alikuwa naye sambamba kuhakikisha hamna anachokosa.

Masikio yake na ubongo wake vilikuwa hai kuliko kawaida.

Mwanamke yule akasema ya kwamba hata pale walipojitahidi huku na kule ili wapate kitu, matokeo yake mume wake akaaga dunia katika ajali ya hit-and-run.

Aligongwa kisha gari likatokomea likimuacha anamwagika damu kama fonteini barabarani.

Alichokuja kuambulia ni mwili wa mumewe ukiwa umepasuka kichwa, vipandevipande vya kutosha kabisa kwenye mfuko mdogo wa rambo.

Hapo Mpelelezi akapata taswira halisinya namna gani mwanamke huyu alikuwa anateseka.

Viatu vyake vilikuwa vikubwa mno kuviingia.

Alikuwa na kila sababu ya kulia akaeleweka na dunia nzima.

Hakumaliza, akaendelea akisema hakukoma kutafuta haki yake.

Alikodisha mpelelezi binafsi wa kuchunguza maswahibu haya baada ya kutumia polisi kushindikana, lakini mpelelezi huyo hakufika mbali.

Baada ya majuma mawili tangu ampe kazi hiyo, akapata taarifa kuwa bwana huyo amekutwa amejinyonga katika makazi yake.

Pembeni aliacha ujumbe wa wapi mwili wake upelekwe na kuhifadhiwa lakini hakusema nini kilipelekea maamuzi hayo ya kushtua.

"Kampuni yake ilikuwa katika kilele cha mafanikio," Mwanamke alisema, "ilikuwa ni ajabu kwake kuacha yote hayo na kutamatisha uhai wake."

Baada ya hapo, alikata tamaa ya kuendelea kutafuta tena.

Alipoteza matumaini.

Alijitenga na maisha na maisha yakajitenga na yeye.

Hata sasa anashangaa nini kilichomleta bwana huyu mpelelezi katika kesi hiyo ya miaka iliyopita.

Kesi ambayo alishaambiwa kuwa imefungwa rasmi muda tu.

Aliuliza,

"Kuna kitu mmepata? ... Mmejua nini kilimkuta mwanangu na mume wangu?"

Mpelelezi akashusha kwanza pumzi maana hakujua hata aanzie wapi katika maswali hayo.

Alichofanya ni kumpatia mwanamke huyo matumaini kwamba anaweza akapata kitu katika juhudi zake.

Angalau sasa amepata mwanga wa pa kuendea.

Kufikia hapo alitaka kujua hospitali ambayo mwili wa binti ulipelekwa, tarehe ambayo mwili ulitoweka, jina la ile kampuni binafsi ambayo iliyokuwa inahusika na upelelezi, na jina la mpelelezi huyo aliyefikwa na mauti akiwa anafanya kazi yake.

Alipovipata akashukuru, lakini kabla hajaondoka mwanamke huyo akampatia kijidaftari kidofo chenye jalada la pinki.

Akamwambia,

"Hii ni diary yake niliyopata kumnunulia. Pengine ukitazama unaweza kupata kitu."

Mpelelezi akaichukua.

Diary ambayo ndo' hii anayo mkononi hivi sasa.

Lakini hakuondoka huko bila kupewa onyo na mwanamke yule mzazi wa binti aliyekufa.

Onyo hilo hakuliacha kulisikia hata sasa.

"Kuwa makini na uhai wako."

Katika yote hayo, bado alikuwa na shauri la kurudi San Fransisco, California, siku za karibuni.

Alimini kabisa kuwa kule ndipo njia ilipo ya kufika anapopataka.

Akiwa taratibu anapitiq diary hiyo akitafuta kama kuna lolote anaweza kuambulia, simu yake ya mezani ikaita.

Alipopokea, akasikia sauti ya mkuu wake wa kitengo.

Alimwambia anamuhitaji ofisini maramoja. Akatii agizo.

Akaelekea huko ambapo alimkuta mkuu wake akiwa ameketi kwa kuegemaza mguu wake wa kushoto juu ya wa kulia.

Mezani kulikuwa na kisosi chenye kipisi kidogo cha sigara kinachoishilia moto.

Bwana huyo aliyekuwa amevalia suti rangi ya damu ya mzee, alikuwa ametulia vema ndani ya kiti chake kikubwa na kirefu chenye nyama za kutosha.

Alimtazama Mpelelezi, bila ya kusema jambo lolote, kisha akavuta droo ya meza yake kubwa, akatoa bahasha ya kaki, kimo cha wastani.

Akaiweka bahasha hiyo mezani akisema,

"Nadhani huu ndo' uamuzi sahihi kwa sasa."

Mpelelezi akaidaka bahasha hiyo asijue kinachoendelea.

Kabla hajaifungua, akaambia arejeshe bunduki ya polisi pamoja na beji yake rasmi. Hivyo vitabakia kituoni mpaka pale atakapopewa taarifa rasmi.

Mkuu alitoa angalizo,,

"Kwa sasa hauruhusiwi kujihusisha na kazi yoyote ya polisi. Hauna ithibati hiyo. Umepewa likizo ya lazima wakati tukiwa tunakagua mwenendo wako. Wakati huo wote utakuwa raia wa kawaida na malipo ya mshahara wako yatakuwa nusu ya kawaida."

Mpelelezi alipotaka kujua sababu, akaambiwa kwa ufupi kuwa ni utovu wa nidhamu.

Baada ya hapo, mkuu wake akamtaka aende zake kwani ana shughuli nyingi za kufanya.

Mpelelezi alipotoka, mkuu akawasha sigara kwa kiberiti chake cha gesi alafu akavuta mikupuo mitatu mikubwa.

Mikupuo ambayo aliivuta kwa hisia zote.

Mapafu yake yalipojaa, akautema moshi nje kana kwamba bomba la trekta.

Muda si mrefu, ofisi yake nzima ikajawa na moshi mnene.


****

Brookhaven, New York.

Saa kumi na moja jioni.

Dr. Lambert alifungua kifungo cha kola ya shati lake, kisha akashusha pumzi ndefu ya unafuu.

Sasa alikuwa anahema.

Mbali na uchovu wa kazi alofanya kutwa nzima, bado hakuwa tayari kwenda nyumbani.

Aliketi katika gari lake akingoja jambo. Macho yake yalikuwa yanatazama 'rearview mirror'' (kioo juu ya kichwa cha dereva) kwa umakini ingali akijitahidi kujiweka 'comfortable' kadiri awezavyo.

Mzee huyu alikuwa amevalia shati jeupe la mikono mifupi. Shati lenye mistari midogomidogo ya rangi ya zambarau.

Shati hilo alilichomekea kwenye suruali yake nyeusi ya kitambaa iliyobanwa na mkanda mnene wa kahawia.

Alingojea hapo kwa kama dakika sita ndo akamwona mtu katika kioo.

Alipotazama vema kiooni, akabaini ni mtu aliyekuwa anamngoja, yaani Dr. Jean.

Bwana huyo mfupi alikuwa amevalia shati jeusi lenye nyotanyota ndogo nyeupe zinazometa. Sarawili ya kadeti, rangi ya kahawia ilokoza, na viatu vikubwa vya ngozi.

Bwana huyo alitembea kuja uwelekeo wa gari la Dr. Lambert, lakini alipopiga hatua kadhaa alibadili mwelekeo wake akielekea upande mwingine.

Alifanya hayo akiwa hana utambuzi wowote kama mwenzake yu kwenye gari anamngoja.

Hapo ikampasa Dr. Lambert ashuke upesi kwenye gari lake na kujaribu kumpungia.

Hakuona.

Ikabidi amuite.

Bwana huyo akageuka na kumwona Dr. Lambert akiwa anapunga mkono kumwita. Akapaza sauti,

"Leo sielekei huko. Unaweza kwenda!"

Kisha akaendelea zake kana kwamba hamna kilichotokea.

Alipotembea kidogo simu yake ikaita mfukoni. Alipotoa kutazama, ni Dr. Lambert.

Akapokea.

"Ebu acha ujinga," sauti ya Dr. Lambert ilifoka na kuamrisha, "Njoo kwenye gari langu upesi!"

Alafu simu ikakata.

Bwana huyo akaona isiwe tabu, akaitikia wito.

Aliketi kwenye kiti cha pembeni ya Dr. Lambert alafu akauliza nini sababu ya wito huo.

Lakini akamsihi Dr. Lambert azingatie muda kwani ana mahali anapotakiwa kuwapo si muda mrefu toka sasa.

Dr. Lambert akajikuta anatabasamu.

"Wewe bwana," akasema akisontea kidole kwa mwenziwe. "Umekuwa wa kunipandishia mabega sasa, sio?"

Dr. Jean hakujibu kitu. Lambert akaendelea kumweleza ni namna gani yeye ni mkubwa katika lile 'deal' alilomtambulisha.

Namna gani alivyoanza 'misheni' hiyo na mpaka hapo alipofikia leo, hivyo Jean anapaswa kumsikiza na kumheshimu sana.

Katika hayo yote aliyojinasibu, Jean hakutia neno lolote, badala yake aliuliza,

"Hiko ndo' umeniitia?"

Dr. Lambert akashusha pumzi ya hasira. Alihisi kifua kinataka kupasuka.

Alijitahidi kumudu hasira zake kwa kuhema mara kadhaa, pumzi ndefu, kisha akarejea kwa upole.

Aliuliza,

"Ni nini mlijadili na Mitchelle siku ile kwenye gari? Nataka kujua."

Jean akatabasamu, kisha akajibu,

"Siko tayari kukwambia. Je, una lingine?"

Mbali na jibu hilo, macho yake yalimkera mno Dr. Lambert. Bwana huyo alikuwa anamtazama kwa mboni za dhihaka.

Basi dokta akajikuta akishika usukani kwa hasira.

Hajakaa vema, Dr. Jean akafungua mlango na kwenda zake.


**

Kuna nini kinaendelea kwa Dr. Jean?

Nini alizungumza na Mitchelle kwa siri siku ile alipokutanishwa naye?
 
TUKIBAKI HAI, TUTASIMULIA - 22

Na Steve B.S.M

Baada ya kitambo kidogo, hali ilitulia.

Mpelelezi kwa kutumia weledi wake wa kazi, akaanza kujenga mazingira ya kupata kile kilichomfanya afunge safari kutoka New York.

Mwanamke yule mzee, ambaye alikuja kujitambulisha kama mama wa mtoto aliyetangazwa kuuawa, akiwa anashukwa na machozi mengi, akaeleza namna mambo yalivyotokea.

Alivuta mafua mapesi, akatazama chini.

Macho yake yalikuwa mekundu sana. Uso wake umepwaya kama mtu anayejutia jambo au ametingwa na kitu fulani kizito.

Akiwa ametulia vivyo, aonekana kama yu mbali kimawazo, akaeleza namna gani alivyokuwa anampenda mwanaye.

Alikuwa ni kama tunu kwake, haswa ukizingatia hakubahatika kupata mtoto mwingine zaidi ya huyo.

Alisema,

"Alikuwa ndo' dunia yangu ya pekee. Furaha yangu. Sikujihisi mpweke ninapokuwa naye karibu. Alikuwa akinipenda na mimi nilijitahidi kadiri nilivyoweza kuurejesha upendo huo kwake."

Baada ya hapo, akaeleza namna gani swala la mwanaye kujinyonga lilivyomuacha katika bumbuwazi kwani hakuliona likitokea katika siku za usoni.

Alisema,

"Aliondoka kwenda chuo kama ilivyokuwa siku za kawaida. Sikuona ajabu wala dalili yoyote ile. Baadae majira ya saa mbili usiku, nikiwa na mashaka kwa kukawia kwake kurudi nyumbani nikamtafuta rafiki yake, Ronelle, kumuuliza kwasababu simu ya mwanangu haikuwa inapatikana.

Ajabu nilipompigia akasema hakuwa naye na hakumwona kabisa siku hiyo chuoni. Na kwa kudhania labda hajafika chuo, basi akaendelea na mambo yake kama kawaida.

Tukiwa katika hali hiyo ya sintofahamu, mimi na baba yake tukafanya jitihada za kuwasiliana na chuo. Hawakuwa na majibu.

Tulipotaka kupeleka taarifa kwenye vyombo vya usalama, tukaambiwa kiutaratibu ni mpaka pale siku kadhaa, angalau mbili, zitakapopita bila mrejesho wa mhusika basi ndo watalifanyia kazi shauri letu.

Japo tulieleza sababu ya kuwa na hofu, kwamba binti yetu si mtu wa kutoka na kuchangamana na watu, bado hatukuweza kuwashawishi.

Walishikilia msimamo wao.

Sitakuja kusahau, ni kesho yake majira ya asubuhi, nakuja kupata taarifa ya mwanangu kujinyonga.

Mwili wake ulikutwa mbali na chuo, ukiwa umekabwa na kitanzi, unaning'inia bila uhai."

Mama alipofika hapo, akashindwa kuzungumza kwa kama dakika tatu.

Uchungu ulimkaba kooni.

Alihisi kuna donge kubwa linalosugua kwenye shina la shingo yake na kifua.

Mpelelezi akapata kazi ya ziada ya kumtuliza.

Baada ya dakika hizo, sasa akapata kuendelea.

Akamweleza Mpelelezi kwamba aliushuhudia mwili wa mtoto wake ukiwa mochwari. Shingo yake imekuwa nyekundu kwa kubanwa na kamba ngumu.

Walifanya maandalizi ya msiba, lakini waliporejea tena mochwari hawakukuta mwili wa mtoto wao.

Walifanya kila jaribio, kila eneo waliloweza kufika lakini hamna kilichopatikana.

Mwili ulipotea mochwari katika mazingira ya ajabu mno.

Si kamera za hospitali wala walinzi walioweza kutoa majibu ya kueleweka.

Kote huko walisema hamna wanachokijua. Kilichofanyika ni 'attendant' wa zamu pamoja na security kusimamishwa kwaajili ya uchunguzi lakini baadae, baada ya majuma manne, walirejeshwa kazini kama kawaida.

Hivyo walichofanya, wakatengeneza tu kaburi katika mji wa Colma, mji tengefu kwaajili ya shughuli za mazishi ndani ya Jimbo la California.

Kutoka hapa San Fransisco mpaka huko ni takribani maili 3.23.

Walifanya hivyo kwasababu jiji la San Fransisco, tangu mwaka 1900, lilipiga marufuku shughuli za mazishi ndani ya maeneo yake kwasababu ya ukosefu wa sehemu sahihi kwaajili ya ibada hizo.

Ndani ya jiji hilo maarufu, kuna makaburi mawili tu, yale ya kitaifa (ya kiserikali) na yale ya Mission Dolores ambayo yapo chini ya wakatoliki.

Huko, Colma, wakaweka jeneza lisilokuwa na kitu kama sehemu tu ya kumbukumbu ya mtoto wao ambaye hawakupata kuuona mwili wake.

Alisema,

"Tuliona ni sahihi kufanya hilo kwaajili ya kuheshimu na kuonyesha uwepo wake duniani kisha akaondoka kama wapendwa wengine."

Alifuta kwanza machozi kabla hajendelea kunena mengine.

Naye Mpelelezi alikuwa naye sambamba kuhakikisha hamna anachokosa.

Masikio yake na ubongo wake vilikuwa hai kuliko kawaida.

Mwanamke yule akasema ya kwamba hata pale walipojitahidi huku na kule ili wapate kitu, matokeo yake mume wake akaaga dunia katika ajali ya hit-and-run.

Aligongwa kisha gari likatokomea likimuacha anamwagika damu kama fonteini barabarani.

Alichokuja kuambulia ni mwili wa mumewe ukiwa umepasuka kichwa, vipandevipande vya kutosha kabisa kwenye mfuko mdogo wa rambo.

Hapo Mpelelezi akapata taswira halisinya namna gani mwanamke huyu alikuwa anateseka.

Viatu vyake vilikuwa vikubwa mno kuviingia.

Alikuwa na kila sababu ya kulia akaeleweka na dunia nzima.

Hakumaliza, akaendelea akisema hakukoma kutafuta haki yake.

Alikodisha mpelelezi binafsi wa kuchunguza maswahibu haya baada ya kutumia polisi kushindikana, lakini mpelelezi huyo hakufika mbali.

Baada ya majuma mawili tangu ampe kazi hiyo, akapata taarifa kuwa bwana huyo amekutwa amejinyonga katika makazi yake.

Pembeni aliacha ujumbe wa wapi mwili wake upelekwe na kuhifadhiwa lakini hakusema nini kilipelekea maamuzi hayo ya kushtua.

"Kampuni yake ilikuwa katika kilele cha mafanikio," Mwanamke alisema, "ilikuwa ni ajabu kwake kuacha yote hayo na kutamatisha uhai wake."

Baada ya hapo, alikata tamaa ya kuendelea kutafuta tena.

Alipoteza matumaini.

Alijitenga na maisha na maisha yakajitenga na yeye.

Hata sasa anashangaa nini kilichomleta bwana huyu mpelelezi katika kesi hiyo ya miaka iliyopita.

Kesi ambayo alishaambiwa kuwa imefungwa rasmi muda tu.

Aliuliza,

"Kuna kitu mmepata? ... Mmejua nini kilimkuta mwanangu na mume wangu?"

Mpelelezi akashusha kwanza pumzi maana hakujua hata aanzie wapi katika maswali hayo.

Alichofanya ni kumpatia mwanamke huyo matumaini kwamba anaweza akapata kitu katika juhudi zake.

Angalau sasa amepata mwanga wa pa kuendea.

Kufikia hapo alitaka kujua hospitali ambayo mwili wa binti ulipelekwa, tarehe ambayo mwili ulitoweka, jina la ile kampuni binafsi ambayo iliyokuwa inahusika na upelelezi, na jina la mpelelezi huyo aliyefikwa na mauti akiwa anafanya kazi yake.

Alipovipata akashukuru, lakini kabla hajaondoka mwanamke huyo akampatia kijidaftari kidofo chenye jalada la pinki.

Akamwambia,

"Hii ni diary yake niliyopata kumnunulia. Pengine ukitazama unaweza kupata kitu."

Mpelelezi akaichukua.

Diary ambayo ndo' hii anayo mkononi hivi sasa.

Lakini hakuondoka huko bila kupewa onyo na mwanamke yule mzazi wa binti aliyekufa.

Onyo hilo hakuliacha kulisikia hata sasa.

"Kuwa makini na uhai wako."

Katika yote hayo, bado alikuwa na shauri la kurudi San Fransisco, California, siku za karibuni.

Alimini kabisa kuwa kule ndipo njia ilipo ya kufika anapopataka.

Akiwa taratibu anapitiq diary hiyo akitafuta kama kuna lolote anaweza kuambulia, simu yake ya mezani ikaita.

Alipopokea, akasikia sauti ya mkuu wake wa kitengo.

Alimwambia anamuhitaji ofisini maramoja. Akatii agizo.

Akaelekea huko ambapo alimkuta mkuu wake akiwa ameketi kwa kuegemaza mguu wake wa kushoto juu ya wa kulia.

Mezani kulikuwa na kisosi chenye kipisi kidogo cha sigara kinachoishilia moto.

Bwana huyo aliyekuwa amevalia suti rangi ya damu ya mzee, alikuwa ametulia vema ndani ya kiti chake kikubwa na kirefu chenye nyama za kutosha.

Alimtazama Mpelelezi, bila ya kusema jambo lolote, kisha akavuta droo ya meza yake kubwa, akatoa bahasha ya kaki, kimo cha wastani.

Akaiweka bahasha hiyo mezani akisema,

"Nadhani huu ndo' uamuzi sahihi kwa sasa."

Mpelelezi akaidaka bahasha hiyo asijue kinachoendelea.

Kabla hajaifungua, akaambia arejeshe bunduki ya polisi pamoja na beji yake rasmi. Hivyo vitabakia kituoni mpaka pale atakapopewa taarifa rasmi.

Mkuu alitoa angalizo,,

"Kwa sasa hauruhusiwi kujihusisha na kazi yoyote ya polisi. Hauna ithibati hiyo. Umepewa likizo ya lazima wakati tukiwa tunakagua mwenendo wako. Wakati huo wote utakuwa raia wa kawaida na malipo ya mshahara wako yatakuwa nusu ya kawaida."

Mpelelezi alipotaka kujua sababu, akaambiwa kwa ufupi kuwa ni utovu wa nidhamu.

Baada ya hapo, mkuu wake akamtaka aende zake kwani ana shughuli nyingi za kufanya.

Mpelelezi alipotoka, mkuu akawasha sigara kwa kiberiti chake cha gesi alafu akavuta mikupuo mitatu mikubwa.

Mikupuo ambayo aliivuta kwa hisia zote.

Mapafu yake yalipojaa, akautema moshi nje kana kwamba bomba la trekta.

Muda si mrefu, ofisi yake nzima ikajawa na moshi mnene.


****

Brookhaven, New York.

Saa kumi na moja jioni.

Dr. Lambert alifungua kifungo cha kola ya shati lake, kisha akashusha pumzi ndefu ya unafuu.

Sasa alikuwa anahema.

Mbali na uchovu wa kazi alofanya kutwa nzima, bado hakuwa tayari kwenda nyumbani.

Aliketi katika gari lake akingoja jambo. Macho yake yalikuwa yanatazama 'rearview mirror'' (kioo juu ya kichwa cha dereva) kwa umakini ingali akijitahidi kujiweka 'comfortable' kadiri awezavyo.

Mzee huyu alikuwa amevalia shati jeupe la mikono mifupi. Shati lenye mistari midogomidogo ya rangi ya zambarau.

Shati hilo alilichomekea kwenye suruali yake nyeusi ya kitambaa iliyobanwa na mkanda mnene wa kahawia.

Alingojea hapo kwa kama dakika sita ndo akamwona mtu katika kioo.

Alipotazama vema kiooni, akabaini ni mtu aliyekuwa anamngoja, yaani Dr. Jean.

Bwana huyo mfupi alikuwa amevalia shati jeusi lenye nyotanyota ndogo nyeupe zinazometa. Sarawili ya kadeti, rangi ya kahawia ilokoza, na viatu vikubwa vya ngozi.

Bwana huyo alitembea kuja uwelekeo wa gari la Dr. Lambert, lakini alipopiga hatua kadhaa alibadili mwelekeo wake akielekea upande mwingine.

Alifanya hayo akiwa hana utambuzi wowote kama mwenzake yu kwenye gari anamngoja.

Hapo ikampasa Dr. Lambert ashuke upesi kwenye gari lake na kujaribu kumpungia.

Hakuona.

Ikabidi amuite.

Bwana huyo akageuka na kumwona Dr. Lambert akiwa anapunga mkono kumwita. Akapaza sauti,

"Leo sielekei huko. Unaweza kwenda!"

Kisha akaendelea zake kana kwamba hamna kilichotokea.

Alipotembea kidogo simu yake ikaita mfukoni. Alipotoa kutazama, ni Dr. Lambert.

Akapokea.

"Ebu acha ujinga," sauti ya Dr. Lambert ilifoka na kuamrisha, "Njoo kwenye gari langu upesi!"

Alafu simu ikakata.

Bwana huyo akaona isiwe tabu, akaitikia wito.

Aliketi kwenye kiti cha pembeni ya Dr. Lambert alafu akauliza nini sababu ya wito huo.

Lakini akamsihi Dr. Lambert azingatie muda kwani ana mahali anapotakiwa kuwapo si muda mrefu toka sasa.

Dr. Lambert akajikuta anatabasamu.

"Wewe bwana," akasema akisontea kidole kwa mwenziwe. "Umekuwa wa kunipandishia mabega sasa, sio?"

Dr. Jean hakujibu kitu. Lambert akaendelea kumweleza ni namna gani yeye ni mkubwa katika lile 'deal' alilomtambulisha.

Namna gani alivyoanza 'misheni' hiyo na mpaka hapo alipofikia leo, hivyo Jean anapaswa kumsikiza na kumheshimu sana.

Katika hayo yote aliyojinasibu, Jean hakutia neno lolote, badala yake aliuliza,

"Hiko ndo' umeniitia?"

Dr. Lambert akashusha pumzi ya hasira. Alihisi kifua kinataka kupasuka.

Alijitahidi kumudu hasira zake kwa kuhema mara kadhaa, pumzi ndefu, kisha akarejea kwa upole.

Aliuliza,

"Ni nini mlijadili na Mitchelle siku ile kwenye gari? Nataka kujua."

Jean akatabasamu, kisha akajibu,

"Siko tayari kukwambia. Je, una lingine?"

Mbali na jibu hilo, macho yake yalimkera mno Dr. Lambert. Bwana huyo alikuwa anamtazama kwa mboni za dhihaka.

Basi dokta akajikuta akishika usukani kwa hasira.

Hajakaa vema, Dr. Jean akafungua mlango na kwenda zake.


**

Kuna nini kinaendelea kwa Dr. Jean?

Nini alizungumza na Mitchelle kwa siri siku ile alipokutanishwa naye?
Done
Waiting enthusiastically
 
TUKIBAKI HAI, TUTASIMULIA - 23

Na Steve B.S.M

East Hampton, New York.

Saa tano usiku


Gari dogo la wagonjwa, lenye rangi nyeupe na nyekundu, lilikuwa linakimbia katika 'highway likitoa sauti kali ya king'ora.

Juu ya gari hilo, kulikuwa na taa nyekundu na za bluu, zikiwakawawaka kuusindikiza msafara huu wa majanga.

Na kwa sababu ya hiyo, magari yaliyokuwapo barabarani yakawa yanapisha kutoa nafasi kwa gari hilo kuwahi huko linapoelekea.

Likavuka na kuyapita magari mengine kwa kasi.

Mara lilikuwa kushoto na mara kulia ... Kulia na mara tena kushoto.

Dereva, mwanaume mwenye makamo ya miaka arobaini na ushee, alishikilia usukani wake kwanguvu akiwa anatazama barabara kwa umakini mkubwa.

Uso wake mnene ulipambwa na masharubu meusi, kidevu chenye chengachenga za ndevu na macho makubwa ya mduara.

Macho ambayo yalifura kwa ndita, yakikodolea lami asije akaleta maafa.

Mwilini alikuwa na sare nyeusi yenye nembo sawa na gari hili. Nembo ya afya. Kichwani akiwa na kofia nyeusi pia yenye nembo sawasawa.

Pembeni yake, kiti cha pembeni, alikuwa ameketi bwana aliyevalia sawa na yeye, lakini yeye akiwa mchanga zaidi.

Kijana barobaro mwenye mwili mwembamba. Uso wake mrefu, kidevu chake kina ncha kali, masikio yake mapana na macho yake yamejawa na hofu.

Alikuwa anaogopa kasi ya gari hili.

Alitazama mbele kwa kukodoa, mkono wake wa kushoto ukiwa umeshikilia kwanguvu 'handle' juu ya dirisha la mlango wa gari.

Alitamani kusema jambo, lakini asingeweza.

Kwa nyuma yao, baada tu ya kuvuka kigingi kinachotenganisha watu wa mbele ya gari na nyuma ya gari, kulikuwapo na watu wanne.

Mmoja alikuwa ni mke wa Bryson.

Alikiwa amevalia gauni jepesi la kulalia, rangi ya bluu iliyokoza. Miguuni mwake ana viatu vya wazi vyenye manyoya mengi.

Nywele zipo timtim.

Uso ameukunja akimtazama mtoto wake aliyekuwa amejilaza juu ya kitanda kirefu chembamba.

Mtoto Cecy.

Amefunikwa na 'mask' ya kumsaidia kuhema, pembeni yake wakiwa wamesimama wataalamu wawili, mwanaume na mwanamke, wanaohangaikia hiki na kile kuhakikisha uhai unabaki katika mwili wa mtoto huyo.

Wataalamu hao walikuwa wamevalia sare lakini tofauti na wale waliokuwapo mbele ya gari.

Wao walijivalia makoti meupe, mafupi yanayoishia magotini.

Walikuwa wako 'busy' kwelikweli. Mara wamshike mtoto kifuani ... mara watazame mashine iliyokuwa inapiga kelele za ku-bip ... mara waongeze jambo katika mashine ... Mara wajadili.

Wakiwa wanafanya hayo, mama mtoto alikuwa anatazama kwa macho yake mekundu.

Macho yanayovuja machozi.

Macho yanayoonyesha hofu kuu iliyomea ndani yake.

Mikono yake ilikuwa inatetemeka. Kila alivyokaa, hakujihisi 'comfortable' kabisa, hivyo akawa anabadilibadili mikao kila mara.

Jasho, taratibu, linamchuruza kwenye paji lake la uso.

Mkono wake wa kuume ulikuwa umeshikilia simu ambayo ilikuwa hewani muda wote huo.

Upande wa pili wa mawasiliano alikuwamo mumewe akiwa anapashana naye habari juu ya kinachoendelea hapa.

Lakini ni kama dakika nne sasa zimepita, hawajazungumza kitu.

Simu bado ipo hewani ...

Kidogo sauti ya Bryson ikauliza,

"Bado hajaamka?"

Mwanamke, badala ya kujibu, akashikwa na uchungu uliotibuliwa na swali hilo.

Akaukunja uso wake maradufu machozi yakishuka mithili ya mto.

Mafua yakamparamia na kwikwi zikamkaba koo kiasi kwamba ikawa shida hata kuhema.

Kwa hayo tu, mumewe akajua kuwa hali si shwari.

Ilikuwa ipo wazi.

Ikampasa ajivike 'uanaume' kumtia mkewe moyo kuwa yote yatakuwa sawa. Asipoteze tumaini.

Wakati huo naye, bwana Bryson, akiwa katika gari lake binafsi, anajaribu kadiri awezavyo kufukuzia gari hili la wagonjwa.

Katika gari hilo alikuwamo na mtoto wake Cellina, pacha wa yule ambaye yumo katika gari la wagonjwa akiwa hoi, hajitambui.

Bwana huyu, alikanyaga pedeli ya mafuta kwa uzito wa mguu wake akijitahidi kuuweka umakini barabarani kadiri awezavyo.

Kwa mbali kidogo tu, alikuwa analiona gari lile lililombeba mtoto wake pamoja na mkewe.

Kwenye kiti cha pembeni yake, mtoto Cellina alikuwa amekaa kimya kwa kutulia sana.

Alivalia gauni rangi ya pinki lenye mauamaua na vijikatuni kadhaa vinavyochekelea na kufurahi.

Macho yake yalibeba hofu akionekana yu mbali kwa tafakari.

Si bure alikuwa anamuwaza mwenziwe, mama yake au wote kwa pamoja.

Yeye ndo' alikuwa mtu wa kwanza kumwona mwenzie akiwa amedondoka chini ghafla na kupoteza fahamu, wakiwa wanacheza tu chumbani.

Ilikuwa ni swala la kufumba na kufumbua ... anashuhudia mwenzie akiwa anatoka damu kichwani baada ya kujibamiza vibaya.

Sasa picha hiyo haikutoka kichwani mwake.

Alihofia sana japo baba yake alijaribu mno kumtuliza na kumtia matumaini kwa nguvu zote kwani alijua hali hiyo ni mbaya kwa mtoto huyu haswa ukizingatia afya ya moyo wake.

Muda kidogo wakafika hospitali, Cecy akashushwa na kupokelewa na wahudumu ambao walikuwa 'chap' sana.

Wakamhamishia kwenye kitanda chenye magurudumu na kumwingiza moja kwa moja kwenye chumba cha dharura.

Huo ukawa mwisho wa familia yake kumwona, kwani walitakiwa kungoja nje ya chumba ili wawapatie fursa wataalamu kufanya kazi yao huko ndani.

Wakakaa kwenye viti wakingojea kwa kihoro.

Wakiwa hapo wanasali na kuomba yote yawe kheri.

Bryson alimkumbatia mkewe na mwanae, Cellina, akajikuta anashindwa kuzuia chozi kudondoka.

Kama si kuutukuza uanaume wake basi angejikuta chini anagaragara jwa uchungu. Lakini baba akifanya hivyo, wengine itakuaje?

Wakakaa hapo kwa lisaa lizima, ndipo dokta akaja akihitaji kuonana na wahusika.

Alikuwa ni mwanaume mwenye makamo ya miaka thelathini. Mweusi, mrefu, nadhifu na mkakamavu.

Koti lake ni jeupe na shingoni ana kifaa cha kupimia mapigo ya moyo, 'stethoscope'.

Aliomba waelekee ofisini na wahusika wake hawakuwa na hiyana, wakaelekea huko.

Walipofika na kutulia, dokta akachukua maelezo ya wahusika akitaka kujua nini kilitokea na kama swala hilo ni la kawaida kwa mgonjwa.

Baada ya kupata maelezo aliyoyahitaji, ndipo sasa akaeleza kuwa mtoto Cecy ni mhanga mkubwa wa tatizo la moyo.

Kwa kawaida, moyo una valvu nne lakini kwa mtoto Cecy chemba moja haifanyi kazi vema na hiyo ndo' sababu mapigo yake ya moyo yamekuwa si ya kueleweka (irregular beats).

Tatizo hilo ndo' hupelekea mtoto kuvimba miguu, kupata kizunguzungu, kuzirai na kupata uchovu wa mara kwa mara.

Lakini pia mtoto yupo hatarini na ugandaji wa damu, kiharusi, moyo kufeli kabisa na hata kupelekea kifo endapo kama tatizo halitapata ufumbuzi haraka.

Alipoyasema hayo, kwa kutumia taaluma yake akatoa ushauri kwa wazazi hawa kuwa njia bora ya kumnusuru mtoto huyo na matatizo haya makubwa ni kufanya upasuaji mkubwa.

Upasuaji wa kupandikiza kifaa kitakachomsaidia kuongoza moyo wake kuwa na mapigo ya kawaida.

Hiyo ndo' itakuwa tiba pekee ya tatizo hili kwa sasa.

Daktari aliwatoa hofu kwamba mtoto anaendelea vema, lakini bado ataendelea kuwa katika uangalizi wa karibu mpaka pale watakapoona ana ahueni ya kutosha.

Baada ya maelezo hayo, bwana Bryson, maramoja, akaanza kufuatilia taratibu ya upasuaji wa mtoto.

Alitaka kujua gharama na utaratibu wake ili ajue namna gani anaweza kulivaa hili.

Alipopata taarifa za kutosha, akarejea kwa mkewe aliyekuwa ameketi kumngoja muda wote huo.

Hapo akaketi kama mtu aliyetoka kukimbia mbio za ushindani, kwani alishusha pumzi ndefu akifyagia jasho katika paji lake la uso.

Alipoketi akatulia sana akiyatafakari mambo. Huenda alisahau hata mkewe yupo hapo na hajaongea naye juu ya kilichosibu.

Mkewe alipomgusa kumshtua, bwana huyo akakurupuka. Hapo akarejea fahamuni.

Mkewe akamuuliza kinachoendelea naye akamweleza kila kitu.

Gharama za kufanya upasuaji ni kubwa mno, hata mfumo wake wa malipo kwa wale wanaotoa kidogokidogo (installments) bado si rafiki kwa wenye kiasi kidogo cha pesa, kwani muda wa kulipia ni mfupimfupi sana.

Kinachomuumiza zaidi kichwa, ana watoto wawili ambao wote wanahitajika kupata huduma hiyo ya upasuaji.

Fedha hiyo ni nyingi sana kiasi kwamba hata akitumia hati ya eneo lake la kazi kuomba mkopo bado haitatosha kukidhi mahitaji.

Sasa atapatia wapi hiyo pesa?

Alisema,

"Hata lile deal ninalofanya, pesa yake haifikii kiwango hiki, achilia mbali ndo' hiyohiyo ambayo pesa yake nimekuwa nikiitumia kwa muda wote huu."

Hapa pakawa na simanzi mbili.

Moja, ya mahututi ya mtoto na pili, mahututi ya kifedha.

Katika shauri hilo, mke akamshauri Bryson awasiliane na mtu yule anayempatia kazi ili amweleze shida zake. Huenda akamskiza na kumsaidia.

Alisema,

"Bryson, hatuwezi kuacha maisha ya watoto wetu yateketee. Hawa watoto ndo' kitu pekee tulichonacho ... Ndo' kitu pekee nilichonacho ... Kama unavyojua, sina uwezo wa kubeba mimba tena. Vipi nikiwapoteza hawa?"

Bryson akamtazama mwanaye Cellina. Alikuwa ametulia mapajani mwa mama yake, ameshapitiwa na usingizi kitambo.

Akayaangaza macho yake huku na kule. Watu kadha wa kadha wakikatiza na kuteta.

Lakini hamna aliyemzingatia hata mmoja. Mawazo yake yalikuwa mbali sana.

Mbali sana ...

Baada ya muda kidogo, akatoa simu yake mfukoni akatafuta jina Hilda na kupiga.

Alikumbuka kazi alompatia mwanamke huyo.

Zaidi alikumbuka kazi hiyo ina pesa yake taslimu punde itakapomalizika. Japo pesa hiyo si lukuki lakini si haba ... Si sawa na kutokuwa nacho kabisa.

Simu ikaita na kuita mpaka ikakata.

Akapiga tena.

Napo mchezo ukawa uleule ... Simu iliita mpaka ikakata.

Akalalama kwa hasira ...

Wakati upande wa pili, anayempigia akiwa analalama kwa raha tele kitandani.

Mwanamke huyo, yaani Hilda, akiwa hana moja wala mbili, alikuwa anajimwayamwaya katika kitanda chake kikubwa, hapo akiwa na mwanaume aliyekuwa anamkonga moyo.

Si mwingine bali Richie.

Wawili hao walikuwa wamezama katika dimbwi refu la huba kiasi kwamba hawakujali kabisa yanayoendelea duniani.

Kila mmoja alikuwa yuko 'busy' anashindana na mwenzake kuguna kwa raha wanazopeana.

Bryson akapiga simu mpaka akachoka.

Baada ya nusu saa, watu hawa walipomalizana, kila mmoja akiwa ameshusha alichokuwa amebeba, ndipo wakakumbuka simu zao.

Hilda, akiwa ameufunika mwili wake mnene kwa shuka tu, alitazama simu yake akakuta 'missed calls' za kutosha.

Naye Richie pia.

Wote walitafutwa na Bryson kwa muda tofautitofauti.

"Atakuwa anataka nini?" Richie akauliza.

Bwana huyo alikuwa amevalia nguo ya ndani tu. Mwili wake mkangafu wote ukiwa nje.

Hilda pasipo kujibu, akajaribu kumpigia boss wake na kidogo simu ikapokelewa.

Baada ya kulumbana kidogo kwa kutokupokea simu mapema, Bryson akaenda kwenye hoja iliyomfanya apige simu.

Akamuuliza Hilda kama ameshamaliza kazi alompa, naye Hilda akasema kwa upesi kuwa kazi imekwisha.

Kwa maana hiyo basi, Bryson akamtaka aiwasilishe kwake haraka iwezekanavyo.Hilda akasema kesho asubuhi atampatia.

Lakini haraka ya Bryson haikuweza kungoja tena. Alimsihi amtumie muda si mrefu kwa kupitia baruapepe.

Kisha akakata simu.

Akamwacha Hilda katika bumbuwazi.

Upesi akamuuliza Richie,

"Si umeshaimaliza?"

Richie akamwambia bado. Alitarajia ataimaliza mpaka kufikia kesho jioni.

Hilda akashika kichwa.

"Unasemaje, Richie?" Aliuliza akiwa ameyakodoa macho.

Kweli bwana huyo hakuwa amemaliza, na alitoka kumpongeza muda si mrefu kwa kazi alofanya!

Akamsihi upesi wachangake kwani kazi inahitajika iwe imetumwa kwa njia ya barua pepe muda si mrefu.

Kufumba na kufumbua Richie akawasha tarakilishi yake, kazi ikaendelea.

Akawa anachapa huku akiwa uchi wa kufunikwa na nguo ya ndani tu.

Lakini kila alipofanya kazi, muda ukazidi kuyoyoma akiwa bado yuko nyuma.

Kazi ni kubwa.

Wakawa wanangoja muda wowote simu itaita.

Lakini haikuita.

Wakaendelea kufanya kazi kwa haraka wanavyoweza.

Muda ukasonga.

Simu haikuita.

Kazi ikaendelea.

Simu haikuita.

Kidogo, mlango ndo' ukaita.

Ngo! Ngo! Ngo!

Hapa wakajikuta wanatazamana.

Mmoja yu ndani ya shuka na mwingine kwenye nguo ya ndani tu.


**
 
Back
Top Bottom