SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,797
- 25,177
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sawa mkuu tunakuamini.Hutojutia.
Endelea tivu jamanii huyu bwana mlemavu sio yule aliyekutana naye kwenye bus akachukua simu ya mpelelezi
Asnt sn maana kule UMUGHAKA kaingia mitini[emoji23]TUKIBAKI HAI, TUTASIMULIA - 27
Na Steve B.S.M
Basi baada ya kitambo kidogo, ndege ikatua ndani ya jiji la San Fransisco na Mpelelezi akatafuta mahali sawia pa kujipumzisha, ilikuwa ni ndani ya hoteli moja yenye hadhi ya kati, hapo aka-book chumba chenye kujitosheleza alafu akajitupia kitandani akiwa na tarakilishi yake.
Yalikuwa ni majira ya saa nne ya usiku, ndege ilitumia masaa sita na dakika ishirini na kitu kutokea New York mpaka kufika kwenye jiji hili ndani ya jimbo la California.
Taratibu akiwa hapo kitandani, akaanza kupitia kesi zile za maiti kupotea mochwari, moja baada ya nyingine, akizitazama kwa umakini na akijaribu kuzisoma mazingira yake, akaandika kila kilicho cha muhimu katika kesi hizo.
Alikuwa anatafuta ni nini kinachofanana katika kesi zote hizi, na baada ya muda mfupi wa kuzikagua na kuzilinganisha akabaini jambo, watu wote waliouawa walikuwa ni wanafunzi, watatu kati yao walikuwa wanasoma chuo, wawili wakiwa high school.
Swala hili likampa mafikirisho mapya, kwanini wanafunzi? Alijaribu kufuatilia wanafunzi hao kwa tovuti za chuo na shule walizokuwa wanasoma, akagundua ni wanafunzi walokuwa werevu sana kitaaluma, mara kadha wa kadha waliwakilisha taasisi zao katika mashindano mbalimbali ya kitaaluma wakaibuka washindi.
Hapo akajikuta anataka kufahamu jambo, basi upesi akampigia simu mwenzake, afisa yule mnene mwenye kuvalia miwani anayemsaidia kwenye mambo haya ya upembuzi, na baada ya simu kuita kidogo ikapokelewa.
"Hey Travis!" Mpelelezi alisalimu na kuuliza, "Upo wapi?"
Travis akamjibu yu mahali amepumzika anajiburudisha kabla ya kurejea nyumbani, basi akamsihi,
"Kesho utakapokuwa kazini, naomba unitumie anwani za makazi ya wale watu ulioniambia, tafadhali usisahau, ni muhimu."
Travis akamwondoa shaka, atafanya hivyo, na huo ukawa mwisho wa mazungumzo yao, qkafunga mashine yake na kwenda kuoga ili atoke, alidhamiria kwenda Casino akajiburudishe na michezo kadhaa ya kamari, lakini leo akilenga kushinda zaidi kwani alikuwa na njaa na pesa.
Hakujua hapa San Fransisco atakaa kwa muda gani, hivyo kumudu mahitaji yake huku mshahara wake ukiwa nusu, ni lazima atafute njia mbadala ya kupata pesa.
Alitoka chumbani kwake, akashika ngazi kushuka chini. Aliposhuka ngazi kadhaa, akasikia sauti za watu wawili wakizoza huko chini, mmoja mwanamke na mwingine mwanaume.
Sauti ya kike akaitambua ni ya mhudumu, kwani si muda mrefu alizungumza naye kwaajili ya kujipatia hifadhi ya chumba kwahiyo bado anaikumbuka vizuri, lakini hii ya mwanaume hakuwa anaifahamu, alihisi ni ngeni masikioni.
Akashuka ngazi sita akizidi kusikia sauti za watu hao, na saa hii akili yake ikaanza kubishana na nafsi yake kuhusu sauti ile ya kiume.
Alihisi anaijua, hapana, akakataa haijui, mara akahisi anaijua, ila ... hapana, hapana, akasema tena na nafsi yake, siijui sauti hii, kidogo akasema anaijua, na akabaki hapa alipozidi kushuka ngazi.
Kadiri alivyokuwa anaisikia sauti hii ndivyo akili yake ikazidi kumwaminisha kuwa anaijua, na kweli alikuwa anaijua, sauti hii ya kiume ilikuwa ni ya yule mwanaume mlemavu alokutana naye kwenye ndege!
Hakutaka kuamini hili, ila ndo' ulikuwa ukweli wenyewe, ilikuwa ni sauti ya yule bwana mlemavu wa kule kwenye ndege! ... Ina maana yupo hapa?
Sababu hiyo ikamfanya aongeze kasi zaidi katika kushuka ngazi, alitaka kujua hiki anachokiwaza ni kweli au lah.
Alipofika chini hakuamini macho yake, ni kweli kabisa vile alivyokuwa anafikiria, pale mapokezi alikuwapo bwana yule mlemavu katika miwani yake meusi!
Akastajaabu ... Ni namna gani anagumiana na bwana huyu katika mazingira yanayofanana?
Alisimama hapo akitazama, akabaini bwana huyo anataka kuchukua chumba hoteli hiyo, na kweli yule dada wa mapokezi akampatia gharama na bwana huyo akaingia mfukoni kutoa pesa. Alitoa pesa kadhaa na kumpatia huyo dada, naye akapatiwa funguo za chumba nambari 112.
Hiko ni chumba cha pembeni kabisa na kile cha Mpelelezi kwani yeye anakaa chumba nambari 111!
Mpelelezi, akiwa amepigwa na butwaa na akisikia haya yote yanayoendelea hapa, akasimama wima kama mshumaa akiwa ameyatoa macho yake kwa bwana yule mlemavu huku akili yake ikiwa inawaka kwa tafakari.
Alimuwaza sana bwana yule, je alikuwa ni mtu wa kawaida? Hakupata jibu, lakini juu ya yote aliona kuna haja ya dhati ya kumtilia bwana huyu maanani.
Maanani ya karibu.
Mhudumu alimuuliza,
"Ungependa nikusindikize?"
Bwana yule akatabasamu kisha akasema, "itakuwa vema zaidi."
Basi yule dada akatoka katika dawati lake na kuongozana na huyu bwana akimsaidia kumshika, wakaelekea kwenye ngazi, hapo wakapishana na Mpelelezi wao wakipanda juu.
Mpelelezi akawatazama mpaka wakaishilia, alisikia maongezi kidogo kisha akasikia mtu akishuka ngazi upesi, alikuwa ni yule dada wa mapokezi baada ya kumaliza kazi yake, hapo naye akatoka zake hotelini kuelekea nje.
Alipofika huko, hakuchukua muda mrefu kupata taksi, akakwea na kuelekea Casino.
Lakini barabarani alijikuta akimuwaza mtu yule hotelini.
***
"Hapana, inatosha!" Travis alimkatazama mhudumu kuongeza kinywaji kingine mezani kwani alikuwa ametosheka sasa, akalipia 'bill' yake na kunyanyuka akitazamia kueleka nyumbani kwake majira yakiwa ni saa tano ya kuitafuta saa sita ya usiku.
Aliliendea gari lake katika eneo la maegesho, akajiweka ndani na kutikisa kwanza kichwa chake kuona kama kipo sawa, alihisi pombe zimemzidia lakini baada ya kufanya hivyo akajiaminisha yuko sawa, anaweza kuendesha gari na kufika nyumbani salama, basi akatia moto gari yake kwa kutekenya ufinguo, lakini kabla hajaenda popote akastaajabu amekabwa shingo na mikono tokea nyuma!
Mikono minene yenye misuli ya kutosha.
Mikono hiyo ilimkaba kwanguvu kiasi kwamba akayatoa macho yake nje kana kwamba matufe.
Kabla hajafanya chochote, kitambaa cheupe kikafunika pua na mdomo wake, hakuchukua muda akapoteza fahamu, mara punde gari nalo likaondoka lisijulikane wapi linaelekea.
***
Taiwan, Majira ya saa sita usiku ...
Baada ya kutema moshi wa sigara nje, bwana Taiwan alisafisha koo lake kisha akamwambia mwenzake aliyekuwapo kando,
"Inabidi tuibuke na mpango haraka, la sivyo mambo yataharibika kabisa."
Bwana huyu, yaani Taiwan, alikuwa amevalia sweta la mistarimistari lenye kofia juu yake, chini alivalia viatu vyeusi vya wazi.
Pembeni yake, rafiki yake, bwana Yu, alikuwa amevalia shati jeusi, tai nyeusi na suruali nyeusi ya kitambaa iliyomkaa vema, chini ana viatu vyeusi aina ya moka.
Kitu pekee kilichokuwa na rangi tofauti na mavazi yake ilikuwa 'kaua' kadogo kekundu kalichokuwapo upande wake wa kushoto wa kifua, naye bwana huyu alikuwa anavuta sigara kama mwenzake, Taiwan.
"Sasa tutafanyaje?" Bwana Yu akauliza. Macho yao yote yalikuwa yanatazama maji ya bahari yakiwa yanahakisi mwanga wa mataa ya jiji hili, taa hizo za rangi mbalimbali zilifanya eneo hili kupendeza na kuvutia machoni.
Bwana Yu aliuliza tena,
"Kama akigundua Kiellin amefariki, atakuelewa kweli?"
"Hilo halina shaka," Taiwan akamjibu na kuongezea, "nilishajipanga kwaajili ya kitu kama hiko, nitamweleza mtoto alifariki si punde baada yeye kuanza safari ya kuja huku, na kwasababu nilikuwa nikimwambia hali mbaya ya Kiellin, basi haitakuwa ngumu kunielewa."
Akaeleza pia ni namna gani mwili wa Kiellin ulikuwa umetunzwa tangu kifo chake akimpatia daktari maelekezo yote pamoja na fedha nzuri.
Alimhakikishia Yu kuwa Mitchelle hatobaini lolote lile, hata kuhisi kama Kiellin alishafariki masiku kadhaa nyuma.
Alisema,
"Kinachoniumiza kichwa ni kuhusu huu mnada. Lazima tufanye jambo upesi ili tuweze kupata pesa ya maana, na kwa leo nimeonana na Chi gang. Wanataka mzigo ule na wameahidi kutupatia pesa kubwa mno kama tukifanikisha kuwapatia."
Hapo Yu akamtazama Taiwan, macho yake yaliwaka tamaa, akauliza,
"Tutapata kiasi gani?"
Taiwan akamwambia ni mamilioni ya madola, na punde tu watakapozitia kimyani basi hawatakuwa na haja ya kumfanyia kazi mtu yeyote yule mpaka kifo kitakapowakuta uzeeni!
Hakika ofa yao ikamtoa Yu udenda, lakini akili yake haikuwa nyuma kumkumbusha juu ya hatari ya deal hili, akauliza,
"Lakini tutaweza vipi na huku safe ya kutunzia mali ikiwa ina uwezo wa kufunguliwa na mtu mmoja pekee dunia nzima?"
"Ni kweli!" Taiwan akamjibu, kisha kabla hajaongeza neno akavuta kwanza mkupuo mmoja wa sigara na kuutemea moshi puani kama bomba za gari kubwa alafu akasema, "ndo' maana nmekuambia tunahitaji mpangokazi, Yu. Kazi ipo kwetu sasa, kwani uhakika wa pesa toka kwa genge la Chi ni asilimia mia moja na moja!"
Yu alimtazama Taiwan akaona jambo usoni kwake, aliamini bwana huyo ana jambo ameshalipanga kichwani, akataka kulifahamu.
Akauliza,
"Wewe umepanga nini, Taiwan?" Na hapa ndo' akawa amefika mahali ambapo Taiwan alikuwa anangoja, mahali pa kujieleza mawazo yake, bwana huyo akatabasamu kwanza kisha akanyonya sigara yake, moshi huu wa sasa ulikuwa ni muhimu sana kuliko aliouvuta awali kwani aliiona picha fulani kichwani kwake, picha ambayo iliambatana na matumaini makubwa, hivyo moshi huu aliusikia kabisa ukipenya mwilini mwake, na alipoutoa alihisi ahueni kubwa.
Akasema,
"Yu, mpango wangu ni kabambe sana, lakini kutimia nahitaji watu, vipi utanisaidia?"
Aliuliza hivyo akimtazama Yu, Yu naye akatabasamu kama jibu lake, alikuwa radhi kwenye mpango huo, lakini kama ilivyokuwa awali, hakuyaacha mashaka yake nyuma, akauliza,
"Na utammudu vipi, Mitchelle? Kwa namna ulivyokuwa unaniambia kumhusu mtu huyo ni wazi ni mtu hatari. Utafanikiwa kumkabili?"
"Ndo' maana nikakwambia nina mpango kabambe, hukuelewa?" Taiwan akasema akiitupa sigara yake chini, alishamaliza kuinyonya na sasa kimebakia kipisi, akakikanyaga kukizima.
Akaongeza,
"Niamini mimi, Yu. Sema kama nilivyokuambia hapo mwanzo, nahitaji watu, watu, watu."
"Unawahitaji kama wangapi?" Yu akauliza.
"Zaidi ya hamsini." Taiwan akajibu akiweka mkono wake mfukoni, macho yake yanatazama bahari.
Yu akamuahidi ataifanya kazi hiyo, ndani ya siku moja tu kila kitu kitakuwa tayari.
Basi usiku wao ukaisha hivyo, mipango na matumaini mwanana, lakini kwa upande ule wa pili tulipotokea, mambo yakiwa kinyume kabisa.
Katika majira ya asubuhi ya saa mbili hivi, habari zilishamfikia kila mmoja katika ofisi kuu ya polisi jijini New York kuwa mmoja wa maafisa habari wa ofisi hiyo kubwa inayoheshika nchini Marekani, amekutwa akiwa hana uhai katika mazingira ya kutatanisha!
Bwana huyo, kama mbuzi wa kafara, alichinjwa koo lake na kitu chenye ncha kali kisha akatelekezwa katika gari lake maeneo ya Manhattan.
Hapo pamoja naye, ulikutwa ujumbe kwenye kioo cha mbele cha gari, ujumbe ulioandikwa kwa damu iliyoshukiwa kuwa ya marehemu, ukisomeka,
"Suits and tie."
***
Umeridhika enhAsante tivu
Tumeambiwa tushukuru kwa chochote kile kidogo au kikubwaUmeridhika enh
Sawa. Ila niambie tu, umeridhika?Tumeambiwa tushukuru kwa chochote kile kidogo au kikubwa
Sijaridhika mimi tivuSawa. Ila niambie tu, umeridhika?