Tukibaki Hai, Tutasimulia

Tukibaki Hai, Tutasimulia

TUKIBAKI HAI, TUTASIMULIA - 27




Na Steve B.S.M





Basi baada ya kitambo kidogo, ndege ikatua ndani ya jiji la San Fransisco na Mpelelezi akatafuta mahali sawia pa kujipumzisha, ilikuwa ni ndani ya hoteli moja yenye hadhi ya kati, hapo aka-book chumba chenye kujitosheleza alafu akajitupia kitandani akiwa na tarakilishi yake.

Yalikuwa ni majira ya saa nne ya usiku, ndege ilitumia masaa sita na dakika ishirini na kitu kutokea New York mpaka kufika kwenye jiji hili ndani ya jimbo la California.

Taratibu akiwa hapo kitandani, akaanza kupitia kesi zile za maiti kupotea mochwari, moja baada ya nyingine, akizitazama kwa umakini na akijaribu kuzisoma mazingira yake, akaandika kila kilicho cha muhimu katika kesi hizo.

Alikuwa anatafuta ni nini kinachofanana katika kesi zote hizi, na baada ya muda mfupi wa kuzikagua na kuzilinganisha akabaini jambo, watu wote waliouawa walikuwa ni wanafunzi, watatu kati yao walikuwa wanasoma chuo, wawili wakiwa high school.

Swala hili likampa mafikirisho mapya, kwanini wanafunzi? Alijaribu kufuatilia wanafunzi hao kwa tovuti za chuo na shule walizokuwa wanasoma, akagundua ni wanafunzi walokuwa werevu sana kitaaluma, mara kadha wa kadha waliwakilisha taasisi zao katika mashindano mbalimbali ya kitaaluma wakaibuka washindi.

Hapo akajikuta anataka kufahamu jambo, basi upesi akampigia simu mwenzake, afisa yule mnene mwenye kuvalia miwani anayemsaidia kwenye mambo haya ya upembuzi, na baada ya simu kuita kidogo ikapokelewa.

"Hey Travis!" Mpelelezi alisalimu na kuuliza, "Upo wapi?"

Travis akamjibu yu mahali amepumzika anajiburudisha kabla ya kurejea nyumbani, basi akamsihi,

"Kesho utakapokuwa kazini, naomba unitumie anwani za makazi ya wale watu ulioniambia, tafadhali usisahau, ni muhimu."

Travis akamwondoa shaka, atafanya hivyo, na huo ukawa mwisho wa mazungumzo yao, qkafunga mashine yake na kwenda kuoga ili atoke, alidhamiria kwenda Casino akajiburudishe na michezo kadhaa ya kamari, lakini leo akilenga kushinda zaidi kwani alikuwa na njaa na pesa.

Hakujua hapa San Fransisco atakaa kwa muda gani, hivyo kumudu mahitaji yake huku mshahara wake ukiwa nusu, ni lazima atafute njia mbadala ya kupata pesa.

Alitoka chumbani kwake, akashika ngazi kushuka chini. Aliposhuka ngazi kadhaa, akasikia sauti za watu wawili wakizoza huko chini, mmoja mwanamke na mwingine mwanaume.

Sauti ya kike akaitambua ni ya mhudumu, kwani si muda mrefu alizungumza naye kwaajili ya kujipatia hifadhi ya chumba kwahiyo bado anaikumbuka vizuri, lakini hii ya mwanaume hakuwa anaifahamu, alihisi ni ngeni masikioni.

Akashuka ngazi sita akizidi kusikia sauti za watu hao, na saa hii akili yake ikaanza kubishana na nafsi yake kuhusu sauti ile ya kiume.

Alihisi anaijua, hapana, akakataa haijui, mara akahisi anaijua, ila ... hapana, hapana, akasema tena na nafsi yake, siijui sauti hii, kidogo akasema anaijua, na akabaki hapa alipozidi kushuka ngazi.

Kadiri alivyokuwa anaisikia sauti hii ndivyo akili yake ikazidi kumwaminisha kuwa anaijua, na kweli alikuwa anaijua, sauti hii ya kiume ilikuwa ni ya yule mwanaume mlemavu alokutana naye kwenye ndege!

Hakutaka kuamini hili, ila ndo' ulikuwa ukweli wenyewe, ilikuwa ni sauti ya yule bwana mlemavu wa kule kwenye ndege! ... Ina maana yupo hapa?

Sababu hiyo ikamfanya aongeze kasi zaidi katika kushuka ngazi, alitaka kujua hiki anachokiwaza ni kweli au lah.

Alipofika chini hakuamini macho yake, ni kweli kabisa vile alivyokuwa anafikiria, pale mapokezi alikuwapo bwana yule mlemavu katika miwani yake meusi!

Akastajaabu ... Ni namna gani anagumiana na bwana huyu katika mazingira yanayofanana?

Alisimama hapo akitazama, akabaini bwana huyo anataka kuchukua chumba hoteli hiyo, na kweli yule dada wa mapokezi akampatia gharama na bwana huyo akaingia mfukoni kutoa pesa. Alitoa pesa kadhaa na kumpatia huyo dada, naye akapatiwa funguo za chumba nambari 112.

Hiko ni chumba cha pembeni kabisa na kile cha Mpelelezi kwani yeye anakaa chumba nambari 111!

Mpelelezi, akiwa amepigwa na butwaa na akisikia haya yote yanayoendelea hapa, akasimama wima kama mshumaa akiwa ameyatoa macho yake kwa bwana yule mlemavu huku akili yake ikiwa inawaka kwa tafakari.

Alimuwaza sana bwana yule, je alikuwa ni mtu wa kawaida? Hakupata jibu, lakini juu ya yote aliona kuna haja ya dhati ya kumtilia bwana huyu maanani.

Maanani ya karibu.

Mhudumu alimuuliza,

"Ungependa nikusindikize?"

Bwana yule akatabasamu kisha akasema, "itakuwa vema zaidi."

Basi yule dada akatoka katika dawati lake na kuongozana na huyu bwana akimsaidia kumshika, wakaelekea kwenye ngazi, hapo wakapishana na Mpelelezi wao wakipanda juu.

Mpelelezi akawatazama mpaka wakaishilia, alisikia maongezi kidogo kisha akasikia mtu akishuka ngazi upesi, alikuwa ni yule dada wa mapokezi baada ya kumaliza kazi yake, hapo naye akatoka zake hotelini kuelekea nje.

Alipofika huko, hakuchukua muda mrefu kupata taksi, akakwea na kuelekea Casino.

Lakini barabarani alijikuta akimuwaza mtu yule hotelini.

***

"Hapana, inatosha!" Travis alimkatazama mhudumu kuongeza kinywaji kingine mezani kwani alikuwa ametosheka sasa, akalipia 'bill' yake na kunyanyuka akitazamia kueleka nyumbani kwake majira yakiwa ni saa tano ya kuitafuta saa sita ya usiku.

Aliliendea gari lake katika eneo la maegesho, akajiweka ndani na kutikisa kwanza kichwa chake kuona kama kipo sawa, alihisi pombe zimemzidia lakini baada ya kufanya hivyo akajiaminisha yuko sawa, anaweza kuendesha gari na kufika nyumbani salama, basi akatia moto gari yake kwa kutekenya ufinguo, lakini kabla hajaenda popote akastaajabu amekabwa shingo na mikono tokea nyuma!

Mikono minene yenye misuli ya kutosha.

Mikono hiyo ilimkaba kwanguvu kiasi kwamba akayatoa macho yake nje kana kwamba matufe.

Kabla hajafanya chochote, kitambaa cheupe kikafunika pua na mdomo wake, hakuchukua muda akapoteza fahamu, mara punde gari nalo likaondoka lisijulikane wapi linaelekea.

***

Taiwan, Majira ya saa sita usiku ...

Baada ya kutema moshi wa sigara nje, bwana Taiwan alisafisha koo lake kisha akamwambia mwenzake aliyekuwapo kando,

"Inabidi tuibuke na mpango haraka, la sivyo mambo yataharibika kabisa."

Bwana huyu, yaani Taiwan, alikuwa amevalia sweta la mistarimistari lenye kofia juu yake, chini alivalia viatu vyeusi vya wazi.

Pembeni yake, rafiki yake, bwana Yu, alikuwa amevalia shati jeusi, tai nyeusi na suruali nyeusi ya kitambaa iliyomkaa vema, chini ana viatu vyeusi aina ya moka.

Kitu pekee kilichokuwa na rangi tofauti na mavazi yake ilikuwa 'kaua' kadogo kekundu kalichokuwapo upande wake wa kushoto wa kifua, naye bwana huyu alikuwa anavuta sigara kama mwenzake, Taiwan.

"Sasa tutafanyaje?" Bwana Yu akauliza. Macho yao yote yalikuwa yanatazama maji ya bahari yakiwa yanahakisi mwanga wa mataa ya jiji hili, taa hizo za rangi mbalimbali zilifanya eneo hili kupendeza na kuvutia machoni.

Bwana Yu aliuliza tena,

"Kama akigundua Kiellin amefariki, atakuelewa kweli?"

"Hilo halina shaka," Taiwan akamjibu na kuongezea, "nilishajipanga kwaajili ya kitu kama hiko, nitamweleza mtoto alifariki si punde baada yeye kuanza safari ya kuja huku, na kwasababu nilikuwa nikimwambia hali mbaya ya Kiellin, basi haitakuwa ngumu kunielewa."

Akaeleza pia ni namna gani mwili wa Kiellin ulikuwa umetunzwa tangu kifo chake akimpatia daktari maelekezo yote pamoja na fedha nzuri.
Alimhakikishia Yu kuwa Mitchelle hatobaini lolote lile, hata kuhisi kama Kiellin alishafariki masiku kadhaa nyuma.

Alisema,

"Kinachoniumiza kichwa ni kuhusu huu mnada. Lazima tufanye jambo upesi ili tuweze kupata pesa ya maana, na kwa leo nimeonana na Chi gang. Wanataka mzigo ule na wameahidi kutupatia pesa kubwa mno kama tukifanikisha kuwapatia."

Hapo Yu akamtazama Taiwan, macho yake yaliwaka tamaa, akauliza,

"Tutapata kiasi gani?"

Taiwan akamwambia ni mamilioni ya madola, na punde tu watakapozitia kimyani basi hawatakuwa na haja ya kumfanyia kazi mtu yeyote yule mpaka kifo kitakapowakuta uzeeni!

Hakika ofa yao ikamtoa Yu udenda, lakini akili yake haikuwa nyuma kumkumbusha juu ya hatari ya deal hili, akauliza,

"Lakini tutaweza vipi na huku safe ya kutunzia mali ikiwa ina uwezo wa kufunguliwa na mtu mmoja pekee dunia nzima?"

"Ni kweli!" Taiwan akamjibu, kisha kabla hajaongeza neno akavuta kwanza mkupuo mmoja wa sigara na kuutemea moshi puani kama bomba za gari kubwa alafu akasema, "ndo' maana nmekuambia tunahitaji mpangokazi, Yu. Kazi ipo kwetu sasa, kwani uhakika wa pesa toka kwa genge la Chi ni asilimia mia moja na moja!"

Yu alimtazama Taiwan akaona jambo usoni kwake, aliamini bwana huyo ana jambo ameshalipanga kichwani, akataka kulifahamu.

Akauliza,

"Wewe umepanga nini, Taiwan?" Na hapa ndo' akawa amefika mahali ambapo Taiwan alikuwa anangoja, mahali pa kujieleza mawazo yake, bwana huyo akatabasamu kwanza kisha akanyonya sigara yake, moshi huu wa sasa ulikuwa ni muhimu sana kuliko aliouvuta awali kwani aliiona picha fulani kichwani kwake, picha ambayo iliambatana na matumaini makubwa, hivyo moshi huu aliusikia kabisa ukipenya mwilini mwake, na alipoutoa alihisi ahueni kubwa.

Akasema,

"Yu, mpango wangu ni kabambe sana, lakini kutimia nahitaji watu, vipi utanisaidia?"

Aliuliza hivyo akimtazama Yu, Yu naye akatabasamu kama jibu lake, alikuwa radhi kwenye mpango huo, lakini kama ilivyokuwa awali, hakuyaacha mashaka yake nyuma, akauliza,

"Na utammudu vipi, Mitchelle? Kwa namna ulivyokuwa unaniambia kumhusu mtu huyo ni wazi ni mtu hatari. Utafanikiwa kumkabili?"

"Ndo' maana nikakwambia nina mpango kabambe, hukuelewa?" Taiwan akasema akiitupa sigara yake chini, alishamaliza kuinyonya na sasa kimebakia kipisi, akakikanyaga kukizima.

Akaongeza,

"Niamini mimi, Yu. Sema kama nilivyokuambia hapo mwanzo, nahitaji watu, watu, watu."

"Unawahitaji kama wangapi?" Yu akauliza.

"Zaidi ya hamsini." Taiwan akajibu akiweka mkono wake mfukoni, macho yake yanatazama bahari.

Yu akamuahidi ataifanya kazi hiyo, ndani ya siku moja tu kila kitu kitakuwa tayari.

Basi usiku wao ukaisha hivyo, mipango na matumaini mwanana, lakini kwa upande ule wa pili tulipotokea, mambo yakiwa kinyume kabisa.

Katika majira ya asubuhi ya saa mbili hivi, habari zilishamfikia kila mmoja katika ofisi kuu ya polisi jijini New York kuwa mmoja wa maafisa habari wa ofisi hiyo kubwa inayoheshika nchini Marekani, amekutwa akiwa hana uhai katika mazingira ya kutatanisha!

Bwana huyo, kama mbuzi wa kafara, alichinjwa koo lake na kitu chenye ncha kali kisha akatelekezwa katika gari lake maeneo ya Manhattan.

Hapo pamoja naye, ulikutwa ujumbe kwenye kioo cha mbele cha gari, ujumbe ulioandikwa kwa damu iliyoshukiwa kuwa ya marehemu, ukisomeka,

"Suits and tie."


***
 
TUKIBAKI HAI, TUTASIMULIA - 27




Na Steve B.S.M






Basi baada ya kitambo kidogo, ndege ikatua ndani ya jiji la San Fransisco na Mpelelezi akatafuta mahali sawia pa kujipumzisha, ilikuwa ni ndani ya hoteli moja yenye hadhi ya kati, hapo aka-book chumba chenye kujitosheleza alafu akajitupia kitandani akiwa na tarakilishi yake.

Yalikuwa ni majira ya saa nne ya usiku, ndege ilitumia masaa sita na dakika ishirini na kitu kutokea New York mpaka kufika kwenye jiji hili ndani ya jimbo la California.

Taratibu akiwa hapo kitandani, akaanza kupitia kesi zile za maiti kupotea mochwari, moja baada ya nyingine, akizitazama kwa umakini na akijaribu kuzisoma mazingira yake, akaandika kila kilicho cha muhimu katika kesi hizo.

Alikuwa anatafuta ni nini kinachofanana katika kesi zote hizi, na baada ya muda mfupi wa kuzikagua na kuzilinganisha akabaini jambo, watu wote waliouawa walikuwa ni wanafunzi, watatu kati yao walikuwa wanasoma chuo, wawili wakiwa high school.

Swala hili likampa mafikirisho mapya, kwanini wanafunzi? Alijaribu kufuatilia wanafunzi hao kwa tovuti za chuo na shule walizokuwa wanasoma, akagundua ni wanafunzi walokuwa werevu sana kitaaluma, mara kadha wa kadha waliwakilisha taasisi zao katika mashindano mbalimbali ya kitaaluma wakaibuka washindi.

Hapo akajikuta anataka kufahamu jambo, basi upesi akampigia simu mwenzake, afisa yule mnene mwenye kuvalia miwani anayemsaidia kwenye mambo haya ya upembuzi, na baada ya simu kuita kidogo ikapokelewa.

"Hey Travis!" Mpelelezi alisalimu na kuuliza, "Upo wapi?"

Travis akamjibu yu mahali amepumzika anajiburudisha kabla ya kurejea nyumbani, basi akamsihi,

"Kesho utakapokuwa kazini, naomba unitumie anwani za makazi ya wale watu ulioniambia, tafadhali usisahau, ni muhimu."

Travis akamwondoa shaka, atafanya hivyo, na huo ukawa mwisho wa mazungumzo yao, qkafunga mashine yake na kwenda kuoga ili atoke, alidhamiria kwenda Casino akajiburudishe na michezo kadhaa ya kamari, lakini leo akilenga kushinda zaidi kwani alikuwa na njaa na pesa.

Hakujua hapa San Fransisco atakaa kwa muda gani, hivyo kumudu mahitaji yake huku mshahara wake ukiwa nusu, ni lazima atafute njia mbadala ya kupata pesa.

Alitoka chumbani kwake, akashika ngazi kushuka chini. Aliposhuka ngazi kadhaa, akasikia sauti za watu wawili wakizoza huko chini, mmoja mwanamke na mwingine mwanaume.

Sauti ya kike akaitambua ni ya mhudumu, kwani si muda mrefu alizungumza naye kwaajili ya kujipatia hifadhi ya chumba kwahiyo bado anaikumbuka vizuri, lakini hii ya mwanaume hakuwa anaifahamu, alihisi ni ngeni masikioni.

Akashuka ngazi sita akizidi kusikia sauti za watu hao, na saa hii akili yake ikaanza kubishana na nafsi yake kuhusu sauti ile ya kiume.

Alihisi anaijua, hapana, akakataa haijui, mara akahisi anaijua, ila ... hapana, hapana, akasema tena na nafsi yake, siijui sauti hii, kidogo akasema anaijua, na akabaki hapa alipozidi kushuka ngazi.

Kadiri alivyokuwa anaisikia sauti hii ndivyo akili yake ikazidi kumwaminisha kuwa anaijua, na kweli alikuwa anaijua, sauti hii ya kiume ilikuwa ni ya yule mwanaume mlemavu alokutana naye kwenye ndege!

Hakutaka kuamini hili, ila ndo' ulikuwa ukweli wenyewe, ilikuwa ni sauti ya yule bwana mlemavu wa kule kwenye ndege! ... Ina maana yupo hapa?

Sababu hiyo ikamfanya aongeze kasi zaidi katika kushuka ngazi, alitaka kujua hiki anachokiwaza ni kweli au lah.

Alipofika chini hakuamini macho yake, ni kweli kabisa vile alivyokuwa anafikiria, pale mapokezi alikuwapo bwana yule mlemavu katika miwani yake meusi!

Akastajaabu ... Ni namna gani anagumiana na bwana huyu katika mazingira yanayofanana?

Alisimama hapo akitazama, akabaini bwana huyo anataka kuchukua chumba hoteli hiyo, na kweli yule dada wa mapokezi akampatia gharama na bwana huyo akaingia mfukoni kutoa pesa. Alitoa pesa kadhaa na kumpatia huyo dada, naye akapatiwa funguo za chumba nambari 112.

Hiko ni chumba cha pembeni kabisa na kile cha Mpelelezi kwani yeye anakaa chumba nambari 111!

Mpelelezi, akiwa amepigwa na butwaa na akisikia haya yote yanayoendelea hapa, akasimama wima kama mshumaa akiwa ameyatoa macho yake kwa bwana yule mlemavu huku akili yake ikiwa inawaka kwa tafakari.

Alimuwaza sana bwana yule, je alikuwa ni mtu wa kawaida? Hakupata jibu, lakini juu ya yote aliona kuna haja ya dhati ya kumtilia bwana huyu maanani.

Maanani ya karibu.

Mhudumu alimuuliza,

"Ungependa nikusindikize?"

Bwana yule akatabasamu kisha akasema, "itakuwa vema zaidi."

Basi yule dada akatoka katika dawati lake na kuongozana na huyu bwana akimsaidia kumshika, wakaelekea kwenye ngazi, hapo wakapishana na Mpelelezi wao wakipanda juu.

Mpelelezi akawatazama mpaka wakaishilia, alisikia maongezi kidogo kisha akasikia mtu akishuka ngazi upesi, alikuwa ni yule dada wa mapokezi baada ya kumaliza kazi yake, hapo naye akatoka zake hotelini kuelekea nje.

Alipofika huko, hakuchukua muda mrefu kupata taksi, akakwea na kuelekea Casino.

Lakini barabarani alijikuta akimuwaza mtu yule hotelini.

***

"Hapana, inatosha!" Travis alimkatazama mhudumu kuongeza kinywaji kingine mezani kwani alikuwa ametosheka sasa, akalipia 'bill' yake na kunyanyuka akitazamia kueleka nyumbani kwake majira yakiwa ni saa tano ya kuitafuta saa sita ya usiku.

Aliliendea gari lake katika eneo la maegesho, akajiweka ndani na kutikisa kwanza kichwa chake kuona kama kipo sawa, alihisi pombe zimemzidia lakini baada ya kufanya hivyo akajiaminisha yuko sawa, anaweza kuendesha gari na kufika nyumbani salama, basi akatia moto gari yake kwa kutekenya ufinguo, lakini kabla hajaenda popote akastaajabu amekabwa shingo na mikono tokea nyuma!

Mikono minene yenye misuli ya kutosha.

Mikono hiyo ilimkaba kwanguvu kiasi kwamba akayatoa macho yake nje kana kwamba matufe.

Kabla hajafanya chochote, kitambaa cheupe kikafunika pua na mdomo wake, hakuchukua muda akapoteza fahamu, mara punde gari nalo likaondoka lisijulikane wapi linaelekea.

***

Taiwan, Majira ya saa sita usiku ...

Baada ya kutema moshi wa sigara nje, bwana Taiwan alisafisha koo lake kisha akamwambia mwenzake aliyekuwapo kando,

"Inabidi tuibuke na mpango haraka, la sivyo mambo yataharibika kabisa."

Bwana huyu, yaani Taiwan, alikuwa amevalia sweta la mistarimistari lenye kofia juu yake, chini alivalia viatu vyeusi vya wazi.

Pembeni yake, rafiki yake, bwana Yu, alikuwa amevalia shati jeusi, tai nyeusi na suruali nyeusi ya kitambaa iliyomkaa vema, chini ana viatu vyeusi aina ya moka.

Kitu pekee kilichokuwa na rangi tofauti na mavazi yake ilikuwa 'kaua' kadogo kekundu kalichokuwapo upande wake wa kushoto wa kifua, naye bwana huyu alikuwa anavuta sigara kama mwenzake, Taiwan.

"Sasa tutafanyaje?" Bwana Yu akauliza. Macho yao yote yalikuwa yanatazama maji ya bahari yakiwa yanahakisi mwanga wa mataa ya jiji hili, taa hizo za rangi mbalimbali zilifanya eneo hili kupendeza na kuvutia machoni.

Bwana Yu aliuliza tena,

"Kama akigundua Kiellin amefariki, atakuelewa kweli?"

"Hilo halina shaka," Taiwan akamjibu na kuongezea, "nilishajipanga kwaajili ya kitu kama hiko, nitamweleza mtoto alifariki si punde baada yeye kuanza safari ya kuja huku, na kwasababu nilikuwa nikimwambia hali mbaya ya Kiellin, basi haitakuwa ngumu kunielewa."

Akaeleza pia ni namna gani mwili wa Kiellin ulikuwa umetunzwa tangu kifo chake akimpatia daktari maelekezo yote pamoja na fedha nzuri.
Alimhakikishia Yu kuwa Mitchelle hatobaini lolote lile, hata kuhisi kama Kiellin alishafariki masiku kadhaa nyuma.

Alisema,

"Kinachoniumiza kichwa ni kuhusu huu mnada. Lazima tufanye jambo upesi ili tuweze kupata pesa ya maana, na kwa leo nimeonana na Chi gang. Wanataka mzigo ule na wameahidi kutupatia pesa kubwa mno kama tukifanikisha kuwapatia."

Hapo Yu akamtazama Taiwan, macho yake yaliwaka tamaa, akauliza,

"Tutapata kiasi gani?"

Taiwan akamwambia ni mamilioni ya madola, na punde tu watakapozitia kimyani basi hawatakuwa na haja ya kumfanyia kazi mtu yeyote yule mpaka kifo kitakapowakuta uzeeni!

Hakika ofa yao ikamtoa Yu udenda, lakini akili yake haikuwa nyuma kumkumbusha juu ya hatari ya deal hili, akauliza,

"Lakini tutaweza vipi na huku safe ya kutunzia mali ikiwa ina uwezo wa kufunguliwa na mtu mmoja pekee dunia nzima?"

"Ni kweli!" Taiwan akamjibu, kisha kabla hajaongeza neno akavuta kwanza mkupuo mmoja wa sigara na kuutemea moshi puani kama bomba za gari kubwa alafu akasema, "ndo' maana nmekuambia tunahitaji mpangokazi, Yu. Kazi ipo kwetu sasa, kwani uhakika wa pesa toka kwa genge la Chi ni asilimia mia moja na moja!"

Yu alimtazama Taiwan akaona jambo usoni kwake, aliamini bwana huyo ana jambo ameshalipanga kichwani, akataka kulifahamu.

Akauliza,

"Wewe umepanga nini, Taiwan?" Na hapa ndo' akawa amefika mahali ambapo Taiwan alikuwa anangoja, mahali pa kujieleza mawazo yake, bwana huyo akatabasamu kwanza kisha akanyonya sigara yake, moshi huu wa sasa ulikuwa ni muhimu sana kuliko aliouvuta awali kwani aliiona picha fulani kichwani kwake, picha ambayo iliambatana na matumaini makubwa, hivyo moshi huu aliusikia kabisa ukipenya mwilini mwake, na alipoutoa alihisi ahueni kubwa.

Akasema,

"Yu, mpango wangu ni kabambe sana, lakini kutimia nahitaji watu, vipi utanisaidia?"

Aliuliza hivyo akimtazama Yu, Yu naye akatabasamu kama jibu lake, alikuwa radhi kwenye mpango huo, lakini kama ilivyokuwa awali, hakuyaacha mashaka yake nyuma, akauliza,

"Na utammudu vipi, Mitchelle? Kwa namna ulivyokuwa unaniambia kumhusu mtu huyo ni wazi ni mtu hatari. Utafanikiwa kumkabili?"

"Ndo' maana nikakwambia nina mpango kabambe, hukuelewa?" Taiwan akasema akiitupa sigara yake chini, alishamaliza kuinyonya na sasa kimebakia kipisi, akakikanyaga kukizima.

Akaongeza,

"Niamini mimi, Yu. Sema kama nilivyokuambia hapo mwanzo, nahitaji watu, watu, watu."

"Unawahitaji kama wangapi?" Yu akauliza.

"Zaidi ya hamsini." Taiwan akajibu akiweka mkono wake mfukoni, macho yake yanatazama bahari.

Yu akamuahidi ataifanya kazi hiyo, ndani ya siku moja tu kila kitu kitakuwa tayari.

Basi usiku wao ukaisha hivyo, mipango na matumaini mwanana, lakini kwa upande ule wa pili tulipotokea, mambo yakiwa kinyume kabisa.

Katika majira ya asubuhi ya saa mbili hivi, habari zilishamfikia kila mmoja katika ofisi kuu ya polisi jijini New York kuwa mmoja wa maafisa habari wa ofisi hiyo kubwa inayoheshika nchini Marekani, amekutwa akiwa hana uhai katika mazingira ya kutatanisha!

Bwana huyo, kama mbuzi wa kafara, alichinjwa koo lake na kitu chenye ncha kali kisha akatelekezwa katika gari lake maeneo ya Manhattan.

Hapo pamoja naye, ulikutwa ujumbe kwenye kioo cha mbele cha gari, ujumbe ulioandikwa kwa damu iliyoshukiwa kuwa ya marehemu, ukisomeka,

"Suits and tie."


***
Asnt sn maana kule UMUGHAKA kaingia mitini[emoji23]
 
TUKIBAKI HAI, TUTASIMULIA - 28


Na Steve B.S.M




"Namba unayopiga haipatikani ..."

Ilikuwa ni mara ya tatu sasa Mpelelezi anausikia ujumbe huu lakini bado hakuamini masikio yake, akapiga tena na tena, bado majibu ni yaleyale, namba unayopiga haipatikani kwa sasa.

Akasonya akishika kiuno, majira sasa ni saa tatu asubuhi, amesimama nje ya hoteli alofikia akiwa anatazama barabara kuu inayokatiza hapo, barabara hiyo ilikuwa na wingi wa magari pia na wingi wa watu wanaoenda na kurudi.

Alisimama hapo akiwa anatazama huku na kule, akili yake ipo mbali sana japo macho yake yanaangaza hapa, kichwani alikuwa anatafakari ni nini kimetokea na muda mwingine akiwa anadhani pengine anaota.

Alifungua simu yake akaingia mtandaoni, moja kwa moja akaelekea kwenye tovuti ya kupata habari za jiji la New York, si kwamba hakuingia huko hapo mwanzo, hapana, alishaingia kama mara nane sasa, na si tu sehemu moja, bali tovuti mbalimbali lakini bado hakuwa ameridhika.

Akajaribu tena kupiga simu, yaleyale, simu haipatikani, akang'ata meno yake kwa hasira, kidogo tu akiwa hapohapo, kabla hajafanya kingine, akahisi kitu kimegusa mguu wake wa kushoto, upesi akageuka.

Kumbe ilikuwa ni fimbo, fimbo ya mtu mlemavu asiyeona, fimbo ndefu rangi yake nyeupe.

Kutazama uso, akamwona bwana yule mlemavu ambaye anaishi naye hotelini hapa, bwana huyo alikuwa amevalia suruali nyeusi ya kitambaa, chini ana raba za kawaida sana, hata shati lake la juu halikuwa limenyooshwa, limejikunjakunja kana kwamba limekamuliwa na baunsa, usoni mwake, kama kawaida, alikuwa amevalia miwani meusi.

Bwana huyo alikuwa akitembea akiwa ametanguliza fimbo yake mbele kama macho, lakini alipogusa mtu alihisi kitu akasema upesi,

"Samahani sana, bwana."

Kisha akatabasamu kiwepesi na kuendelea na safari yake kana kwamba hakuna kilichotokea, Mpelelezi akabaki akimtazama bwana huyo namna akienda zake, hakukoma kumtazama mpaka anaishilia akijiuliza mtu huyu ni wa wapi na huku San Fransisco alipokuja hana ndugu kiasi amefikia hotelini? Na kama ni biashara basi ni biashara gani hiyo?

Kwa muda kidogo bwana huyo akawa amemsahaulisha mawazo yake ya awali, mawazo ya kuwaza kifo cha kutatanisha cha Travis, bwana yule alipoishia, akasimamisha taksi iliyokuwa inakatiza, akakwea na safari ikaanza.

Akiwa katika gari hilo, kando ya dirisha, alifungua simu yake akanyookea moja kwa moja kwenye kategoria ya picha, huko akatafuta kidogo na kuangukia kwenye fali alilolutunza kwa jina 'diary'.

Akalifungua na kuanza kutazama ...

Humo kulijaa picha za diary ile alopatiwa na yule mama ambaye mwanaye alifariki, diary ambayo ilikuwa na matukio ya yule mwanamke ambaye picha yake inatumika kwenye kitambulisho cha mtuhumiwa wa mauaji ya The DL.

Mpaka safari inakoma, Mpelelezi alikuwa anasoma diary hiyo kwakupitia picha za simu yake, alikuwa anazipitia kwa umakini kana kwamba anazifanyia mtihani baadae.

Aliposhuka, aliweka simu yake mfukoni akatazama nyumba iliyosimama mbele yake, ilikuwa ni ghorofa ya sakafu kadhaa, rangi yake dhahabu iliyopauka.

Akaingia humo na kunyookea mlango nambari 64, akagonga hapo, sauti ya kike ikaitikia, kidogo mlango ukafunguka akachungulia msichana mwenye makamo ya miaka ishirini hivi, nywele zake ndefu rangi ya bia, macho yake gololi na 'lips' zake nyembamba sana, akamuuliza Mpelelezi,

"Naweza kukusaidia?"

Mpelelezi akaeleza adhma yake. Alionyeshea picha ya kijana fulani katika simu yake kisha akasema anahitaji maongezi machache kuhusu kifo cha mtu huyo.

Alipofanya hivyo, msichana yule akakodoa, uso wake ukapara kwa hofu, akatazama kama Mpelelezi yu na watu wengine, akaona yu mwenyewe, basi upesi akaufunga mlango wake lakini kabla hajafanikiwa, Mpelelezi akauzuia kwa mkono.

"Naomba tuongee tafadhali!"

Msichana yule akakataa katakata, hakutaka kusikia lolote toka kwa Mpelelezi bali kuondoka kwake tu, akalazimisha kufunga mlango kwanguvu zake zote Mpelelezi akimzuia, ilikuwa ni kama igizo la futuhi.

Msichana huyo alipoona hana uwezo wa kumshinda nguvu Mpelelezi, akapaza sauti ya kuomba msaada, sauti yake ilikuwa kali na nyembamba yenye kuumiza sikio, Mpelelezi aliposikia hayo akaachia mlango upesi kutazama mazingira yake ya usalama.

Hakutaka kuleta zengwe hapa, anafahamu fika hakuwa na kitambulisho wala chochote cha kumtambulisha kama yeye ni mwanausalama, hivyo hakuwa na uhalali wowote wa kuwa hapo.

Akatoka hapo haraka akielekea chini lakini wakati huo baadhi ya majirani walishatoka kwenye viota vyao kutazama kinachoendelea, walimtazama Mpelelezi akienda zake na Mpelelezi kama asiyejua kilichoendelea hapa, akatembea kama mtu aliye katikati ya jiji, hakujali watu, ni kama vile hakuwa anawaona, alipofika chini akaitisha taksi na kuketi kitako.

Akiwa ndani ya gari alitazama anwani nyingine ya kuitembelea kisha akampatia dereva maelekezo na gari likaelekea huko.

Njiani akaendelea kusoma ile 'diary' kwenye simu yake, hakutaka kuwaza kitu kingine kabisa, mawazo yake yalikuwa hapo kwa asilimia zote, na kweli baada ya muda mawazo yake yakalipa, kuna jambo akaona humo, jambo la muhimu kuliandika chini, akafanya hivyo katika simu yake hiyohiyo ...

Alitazama orodha ya anwani za kutembelea akaona imesheheni, alikuwa na sehemu nyingi za kwenda na watu wengi wa kuongea nao, kazi ndo' kwanza ilikuwa inaanza, tena katika kipindi chake kibaya kazini.

Alichoomba ni huko kwengine kusilete matata kama hapa alipotoka, la sivyo ... Akatikisa kichwa, lakini alijikuta akitabasamu pale alipokumbuka mkasa wa yule msichana, namna walivyokuwa wanagombania mlango ilikuwa kituko haswa, lakini kila kitu kina sababu, aliamini msichana yule alikuwa na sababu ya kukataa kuongea naye na ni jukumu lake kujua sababu hiyo ni ipi ...

Basi gari likatokomea katika barabara yake ...

***

"Umepata taarifa?" Aliuliza bwana akiwa anaketi chini, mkononi alikuwa amebebelea glasi yenye kinywaji rangi ya dhahabu, glasi inachuruza kwa baridi.

Bwana huyu si mgeni machoni petu, la hasha, alikuwa ni yule mwanaume ambaye alitambulishwa kama mume kwa yule mwanamke ambaye alikutana na Mpelelezi katika uwanja wa kuchezea kamari, yaani Casino.

Mwanaume huyu ambaye tulimwona siku ile akiwa ameukunja uso kumkuta Mpelelezi pamoja na Mwanamke yule ndani, hapa alikuwa na uso wa binadamu wa kawaida kama mimi na wewe, alipoketi alimpatia mtu aliyekaa naye mkabala glasi hiyo alokuja nayo kisha yeye akawa mtupu isipokuwa chupa yake ya maji mezani.

Mtu huyo aliyekuwa naye mkabala si mwingine bali ni yule mwanamke ... mwanamke mrembo mwenye utashi wa kucheza kamari kiasi cha kumshtua Mpelelezi, alikuwa amekaa ndani ya blauzi na pensi fupi ya jeans, uso wake una 'make-up' ya kiasi.

Alikunywa kile alicholetewa kwa fundo moja kisha akaiweka glasi mezani, ndipo akauliza,

"Taarifa gani?"

"Yule bwana yupo San Fransisco," akasema yule mwanaume akiwa anamtazama Mwanamke huyo kwa macho ya mkazo, hata alipokunywa maji yake bado alikuwa anamtazama kwa kumkazia mboni.

"Oooh ..." Mwanamke akaitikia, lakini macho yake hayakuonyesha mshangao wowote kama ilivyokuwa kwenye kauli yake, alikuwa anatazama glasi yake ya kinywaji mezani kama mtu anayefikiria jambo.

Mwanaume akasema,

"Hii ndo' fursa yetu sasa ya kurekebisha makosa."

"Makosa yapi?" Mwanamke akauliza macho yake yakimtazama mwenziwe.

"Hujui makosa yapi?" Mwanaume akastaajabu. "Ulipata nafasi nzuri lakini hukufanya uliyotakiwa kufanya, nilistaajabu kumkuta bwana yule akiwa hai katika nyumba yako!"

"Najua ninachokifanya, Jerry!" Mwanamke akawaka. Aliyatoa macho yake kiasi kuonyesha msisitizo wa anachokisema, Mwanaume akatabasamu, halikuwa tabasamu la furaha.

"Ni kipi hiko? Tulipewa kazi moja tu, moja tu!"

"Na nitaifanya. Sawa?"

"Kama ulilenga hivyo, Evelyn, kwanini ulihitaji msaada wangu siku ile?"

Siku ile ...

Siku ile?

Siku ipi hiyo? ...

Ngoja kidogo,

Ilikuwa ni majuma kadhaa yaliyopita, siku ambayo Mwanamke huyu, Evelyne, alikuwa katika gari majira ya saa tatu usiku akiwa anatazama dirishani.

Hakuwa mwenyewe, pembeni yake alikuwapo huyu mwanaume, Jerry, akiwa ametulia kama chai ndani ya chupa, naye macho yake yalikuwa yanatazama nje, ni bayana kuna kitu walikuwa wanangojea hapa.

Baada ya muda kidogo, Jerry, yaani huyu mwanaume akauliza,

"Una uhakika atakuja hapa?"

Kisha akatazama saa yake ya mkononi.

Mwanamke yule, yaani Evelyne, akiwa anaendelea kutazama nje, akamtoa shaka mwenzake, bado aliamini mtu wake atakuja kama walivyokubaliana hata kama ni kwa kuchelewa.

"Kwa namna nilivyoongea naye mara ya mwisho, naamini kabisa atakuja."

Kweli, haikupita dakika kumi baada ya hiyo kauli, wakamwona mwanaume akiwa anatembea kwa kasi, Jerry alikuwa wa kwanza kumwona, akamnyooshea kidole akiuliza,

"Sio yule?"

Kutazama, ni Mpelelezi, bwana huyo alikuwa ameshuka toka kwenye gari la kukodi si muda, sasa anatazamia kuingia ndani ya Casino.

"Anajua amechelewa, unaweza ukaona tu mwendo wake," alisema Mwanamke ndani ya gari kisha akafungua mlango na kushuka, nyuma yake akifuatiwa na Jerry.

Waliingia ndani, wakasimama kwa mbali walipojihakikishia kumwona Mpelelezi, walikuwa wanamtazama kwa umakini kuhakikisha hapotei machoni mwao, kidogo wakamwona mhudumu akiwa na Mpelelezi, papohapo Evelyne akamtazama Jerry kwa kumpa ishara kisha akafungua pochi yake na kumkabidhi kitu mwanaume huyo, Jerry alipopokea, akaondoka kumfuata yule mhudumu aliyeongea na Mpelelezi, wakati huo Evelyne akiwa anatazama.

Baada ya muda kidogo, Jerry akarejea na kumwambia Evelyne kuwa kazi imekamilika, kila kitu kimeenda kama kilivyopangwa, Evelyne akampongeza, wakangoja kwa dakika kadhaa wakiwa wanamtazama Mpelelezi kwa mbali, muda ulipowadia, Evelyne akaaga na kwenda moja kwa moja kumfuata Mpelelezi.

Alipokuwepo huko, Jerry alikuwa anatazama kila kitu, macho yake hayakubanduka hata sekunde, aliangalia kila kinachoendelea.

Baada ya muda kidogo, akaona Mpelelezi anadondoka, hapo Evelyne akamtazama na upesi akasogea katika eneo la tukio, akambeba Mpelelezi wakijinasibu wapo naye pamoja kisha wakatoka zao kwenda nje.

Jerry akiwa amembebelea Mpelelezi begani, nyuma yake Evelyne akiwa anatembea kwa upesi, walinyookea kwenye gari lao wakampakia Mpelelezi humo na kuondoka.

Hawakwenda mbali, Jerry akashuka na kumwacha Evelyne peke yake kwenye gari, alimwambia kuna mahali anapaswa kwenda na asubuhi watapata kuonana, basi Mwanamke akiwa katika usukani, akaenda zake akiwa amembebelea Mpelelezi nyuma kana kwamba mzigo.

Lakini akiwa anaenda alikuwa akikaa kumbuka kauli ya Jerry, ya kwamba amtupie mwanaume huyo mahali salama baada ya dakika thelathini kupita kwani hatokuwa na uhai tena.

Kinyume na hapo akanyookea na mwanaume huyo nyumbani akiwa bado ni mzima, anahema japo hana fahamu, huko akamtua na kumpeleka moja kwa moja chumbani.

Kesho yake asubuhi, Jerry alipokuja, anastaajabu kumwona Mpelelezi sebuleni, na alipopata wasaa wa kuzoza na Evelyne kule chumbani aliuliza ni kivipi mwanaume yule alikuwa mzima ingali walimuwekea dawa kali kwenye kinywaji.

Majibu ya Evelyne hayakueleweka, Jerry akahitimisha kuwa dawa ilikuwa imebadilishwa, haikuwa ile waliyoipanga kwani kwa ukali wake uhai wa Mpelelezi ungekuwa historia hivi sasa.

Lakini kwanini Evelyne alifanya hivyo? Hakuna aliyejua bali yeye mwenyewe, sasa anapata nafasi ya pili, nafasi ya sasa hivi, nafasi ya leo hii, Jerry anamsisitiza lakini kama haitoshi simu inaita, anampatia Evelyne aongee nayo, ilikuwa ni simu ya kazi.

Mtu ambaye hakumjua ni nani mpaka pale aliposikia sauti yake.

Mtu huyo akamweleza kuwa hapo alipo yupo nyuma ya gari la kukodi alilomo Mpelelezi, anamfuatilia kwa kitambo sasa, na atakapopata wasaa basi ataimaliza kazi yake upesi bila kusita.

Kabla Evelyne hajaongezea neno, simu ikakatwa, akamtazam Jerry kwa mshangao.

"Hata mimi sikufahamu hilo!" Jerry akajitetea akiwa ameyatoa macho.

Evelyne akasema,

"Kwahyo hapa tuongeapo, kipofu muuaji yupo kazini?"

"Ndio," Jerry akajibu kwa kujiamini, "si umesikia mwenyewe?"

Evelyne akanyanyuka upesi na kwenda zake, hata kinywaji chake hakumaliza, Jerry akajribu kumwita lakini hakufua dafu, mwanamke alienda zake kana kwamba ni kiziwi, hakuna anachosikia.



***.


nini kinaendelea hapa?
 
Back
Top Bottom