Tukibaki Hai, Tutasimulia

Tukibaki Hai, Tutasimulia

Saaana,alafu ukizingatia Mitchelle alikubali kurudi hatarini(kukamatwa) kwasaabu yake,akiamini she's like family to her.
Nahis yule partner wake Ferdinand atakuja muokoa,kifo chake kilikua cha mchongo. Hopefully bado yuko hai.
Eeh najiiliza Ferdy yuko wapi?
 
TUKIBAKI HAI, TUTASIMULIA - 36



Ingawa Jennifer alimsaliti, akimuuza kwa watesi wake kama alivyofanya Yuda kwa Yesu, lakini bado alisikia kitu ndani yake, hakikuwa kingine bali hisia ya uchungu, akasogelea kwa ukaribu zaidi kuta hii iliyomtenganisha yeye na mlinzi, macho yake yanametameta lakini ndita amezikunja, akauliza,

"Alikuwa na nani?"

"Nani?" Mlinzi akauliza, macho yake yalikuwa yapo juu ya ile sahani ya chakula alokuwa anaitamani, hata akili yake ilikuwapo huko, masikio yakafa ganzi.

"Jennifer!" Mitchelle akarudia kwa sauti ya mkazo. "Mara yake ya mwisho alikuwa na nani?"

Mlinzi akamtazama.

"Sasa mimi najuaje? Nipo na wewe hapa kutwa nzima, najuaje ya huko duniani?"

"Mbona umefahamu kuwa amekufa?"

"Nimesikia wenzangu wanaongea, wale majamaa walokuja hapa asubuhi. Amekutwa amekufa ndani ya chumba chake cha hoteli, mlango unaotazamana na chumba cha daktari."

Mitchelle aliendea sahani ya chakula akaitwaa na kurejea nayo alipokuwa amesimama, akamwonyeshea mlinzi akisema,

"Nipo tayari kukupatia, sio tu leo hata siku zote n'takazokuwamo humu, ninachotaka ni taarifa tu toka kwako."

Mlinzi akamtazama kwa macho ya mashaka kisha akaitazama sahani ile ilokuwamo mkononi mwa mfungwa wake, akauliza,

"Nitakuaminije?"

"Una rimoti, si ndio?" Mitchelle akamuuliza na kuongezea swali juu yake, "nitafanya nini ukiwa na rimoti hiyo? Unajua kabisa kuwa ukibonyeza kitufe hiko basi sitakuwa na tija tena."

Mlinzi akajipapasa mfukoni, kweli hakuwa na kitu chochote isipokuwa 'mafunguo' na kadi, rimoti haikuwa pamoja naye lakini hakutaka kuukubali unyonge huo, akasema kwa kujiamini,

"Ukileta janja janja yoyote nitabonyeza kitufe hiko kwa nusu saa nzima, nadhani utakuwa ushakauka kwa umauti!"

Mitchelle akatikisa kichwa, mlinzi akatazama kando na mbali yake, hakika alikuwa mwenyewe, alipohakikisha hilo akamgeukia tena Mitchelle na kumuuliza,

"Unataka taarifa gani?"

Mitchelle akamwambia kile anakihitaji, bwana mlinzi akamsikiliza kwa umakini, alipomaliza akampatia chakula kwa kupitia kidirisha kidogo kilichokuwapo langoni, mlinzi akakitwaa na kumuahidi atamrejea baadae.

Akaenda zake.


****


Alipoweka sigara yake kubwa chini, boss mkubwa alimtazama mwenziwe aliyekuwa ameketi katika meza hii, sigara yake akaisiginia kwenye kisosi kisha akatemea moshi pembeni, moshi mzito, alafu akasema, "Tuna miezi miwili tu, kila kitu inabidi kiwe kimeshakamilika, unajua kuna mkutano mkubwa wa UN mbele yetu na huo ndo' 'target' yetu kubwa."

Kando ya bwana huyo alokuwa anaongea naye walikuwapo wanaume wengine wawili, wote walikuwa wamevalia suti nyeusi, macho yao yanatazama kiti kikubwa kilichokaliwa na boss mkubwa, nyuso zao zina umakini kana kwamba waliambiwa kinachoongelewa hapa basi kinajiri kwenye mtihani hapo baadae, mbali na hao wanaume alikuwapo mwingine alosimama, bwana yule wa miraba minne, alikuwa amesimama kwa utulivu, hatikisiki wala kuyumba, kidevu amekinyanyua juu, mikono ameikutanisha kwenye kiuno chake.

"... Kabla ya mkutano huo inabidi tuwe tumeshageuza adui yetu kuwa silaha yetu kubwa. Kila mtu hapa anajua ni namna gani mwanamke yule ana uwezo wa ajabu, tunakumbuka vema namna gani alivyofanikiwa kutokomeza kabisa jeshi letu kabla hatujaja kusimama upya, namna gani tulivyopoteza wanaume mamia kwa mamia kwenye mikono yake, laiti akiwa mikononi mwetu basi hatutazuilika na mtu yeyote!"

"Lakini ..." Bwana mmoja akasema kwa shaka, "tutafanikiwa vipi katika hilo? Tutamwamini vipi mtu yule hata sasa kiasi cha kumtwika majukumu yetu nyeti?"

Boss mkubwa akagunia puani alafu akaegemea kiti chake kikubwa, macho yake yakamtazama mwanaume mwingine kwa namna ya kumpa ruhusa, naye mwanaume huyo akaongea akisema kuwa Mitchelle si binadamu wa kawaida, mbali na kwamba nje ana umbo la binadamu na hata matendo pia lakini ana mfumo kamili unaomwendesha, mfumo unaojitegemea, endapo watakapoweza kuumudu mfumo huo basi wataweza kumtumia kama mtumwa wao kama vile alivyotumika kuwaangamiza hapo kabla.

"Hatujajua ni nini kilitokea hapo nyuma lakini huenda mwanamke huyo aliharibu mfumo wake wa kiuendeshaji hivyo akaanza kujitegemea, kwa mujibu wa Dr. Lambert, tunaweza kumtengenezea upya mfumo wa kummudu japo ni zoezi kubwa lakini linawezekana."

"Na hilo ndo' linafanya daktari yule anaendelea kuwa hai hata sasa," akasema boss mkubwa, "yeye alishiriki katika kumtengeneza mwanamke huyu, japo si kwenye zoezi zima lakini angalau anajua wapi pa kuanzia na nani wa kuanza naye kulikamilisha hili."

"Tutaweza kweli kuuwahi mkutano huo ndani ya miezi miwili?" Bwana yule akauliza, boss akamtazama na kumwambia hiyo ndo' sababu ya yeye kuwaita hapo, kuharikisha mpango huo kadiri itakavyowezekana.

"Mtaongozana na Dr. Lambert kwenda US, huko mtafanya naye kila kitu kws ukaribu, kwa hap tulopofikia hatuwezi kumwamini yeye tu asilimia zote, nataka muwe naye karibu mno. Yeye atawaelekeza chakufanya, wapi pa kwenda na nani wa kumwona, pesa zitakazokuwa zinatumwa zitawafikia ninyi kabla ya mikono yake, na ninyi ndo' mtakaonipa taarifa ya kila jambo."

Baada ya kusema hayo, alitoa angalizo,

"Kuweni makini na yule bwana, nadhani mnajua kilichotokea juzi yake?"

Mabwana wakatikisa vichwa vyao kuonyesha wameelewa, boss mkubwa akasimama kuondoka zake.



Hiyo Juzi yake, majira ya saa za usiku, Kianjin Hotel, Taiwan. Majira ya usiku mzito.


Baada ya mhudumu kukatiza, mlango ukafunguka na kichwa cha Dr. Lambert kikachomoza nje, akatazama korido ndefu ya hoteli, pande zote mbili, hakukuwa na mtu isipokuwa mhudumu aliyekuwa anaishilia, akatoka ndani ya chumba chake na kuufuata mlango uliokuwa unatazamana naye, alikuwa amevalia nguo maalum wanayovaa watu watokapo kuoga, nguo yenye 'material' ya taulo ikiwa imebanwa na kamba kiunoni, akabisha hodi kwa kubonyeza kitufe cha kengele na muda si mrefu mlango ukafunguliwa na mwanamke aliyevalia taulo kifuani, ana tabasamu usoni mwake, si mwingine bali Jennifer, Dokta akaingia ndani na mlango ukafungwa upesi.

"Aah! Hata sasa bado hujalala?" Alisema Dr. Lambert akijimwaga kwenye kiti kama mzigo uliomzidia kuli, Jennifer akatabasamu kisha naye akaketi pembeni yake.

"Usiku huu ni mwanana sana," Dokta akasema akiupeleka mkono wake kiunoni mwa Jennifer, Jennifer akashtuka kidogo kisha akatabasamu na kuupokea mkono huo kwa mkono wake wa kushoto, dokta akaendelea akisema namna gani usiku huo ulivyokuwa bora, mosi wamepata fedha nyingi sana na pili wapo pamoja baada ya muda mrefu wa kutengana.

"Nilikuwa naingojea siku hii kwa muda mrefu sana, kuna muda nilidhani haitaweza kutokea lakini kweli hakuna lisilowezekana chini ya jua, sasa mtesi wetu yupo ndani na sisi tupo huru, kisasi cha aina gani hiki?"

Dokta akamkumbatia Jennifer kwa nyuma, akauliza, "au kuna lolote unalonidai, mpenzi?" Kwa kutumia ishara, Jennifer akamjibu hamna analodai kisha akatabasamu na kumgeukia dokta, akambusu mdomoni.

"Nisamehe sana," akasema kwa mikono, "kuna muda nilikuwa nakutilia mashaka juu ya hili, nilistaajabu kwanini haukutaka kutumia sumu nikammaliza upesi kumbe ulikuwa na mpango kabambe, mpango wa kuishi ya kifahari mpaka kufa kwetu."

Dokta akatabasamu, tabasamu la majivuno, alijiona yupo juu ya dunia hii, anapaa pasipo mipaka, akamtazama Jennifer machoni na kumwambia, "unaweza kuamini kuwa mpango huo haujaisha?"

Baada ya hapo kilichofuata kilikuwa ni kuonyeshana mapenzi mazito kinyume kabisa na umri wao, huenda walijiandaa sana kwenye kila mazingira, mithili ya watoto wenye damu changa wakakabiliana na kiu zao, baada ya dakika thelathini wakawa wamejilaza kitandani wanatazama dari, miili yao imefunikwa na shuka, kila mtu anahema kwa purukushani, dokta anavuja jasho jingi sana, Jennifer akamgeukia na kumpa ishara ya mikono ikisema,

"Niambie basi kuhusu mpango wako, au sipaswi kuusikia?"

Kisha akauweka mkono wake kwenye kifua kongofu cha dokta, naye dokta akatasamu, akamgeukia mwanamke huyo na kumuuliza, "unahamu kubwa ya kuujua?"

Jennifer akajibu kwa kichwa, uso wake umejawa na hamu ya udadisi, punde dokta akauvuta mto ulokuwapo pembeni yake na kumfunika nao Jennifer usoni, kwa haraka akanyanyuka na kumkalia Jennifer kwa juu yake, akatumia nguvu zake zote kumziba mwanamke huyo asipate pumzi, mwanzo Jennifer alidhani ni mchezo lakini kadiri muda ulivyoenda akabaini haikuwa mzaha, ulikuwa ni mpambano wa kutetea uhai wake, lakini alikuwa ameshachelewa, hakujiweza tena kujinasua, alitapatapa kwa kadiri yake lakini hakufua dafu, dokta alimng'ang'ania kama ruba, haikupita muda akaishiwa na nguvu, mikono yake iliyokuwa inapambana ikalegea na kujitupia kando, dokta akajua kashamaliza kazi.

"Sehemu yako katika mpango wangu imeshakwisha," alisema dokta, mwili wake unavuja jasho maradufu ya awali kwa kazi alotoka kuifanya, akafuta paji lake la uso kwa kiganja kisha akajimwagia pembeni ya kitanda, akautazama mwili wa Jennifer, ulikuwa umelala mfu, akafuata nguo alokuja nayo humo mfukoni akatoa chupa ndogo akammiminia mwanamke huyo mdomoni na pembeni yake kidogo, alipomaliza akachukua kichupa cha pili toka mfukoni akakifungua na kujipakaza mikononi kisha kwa uangalifu akatoka katika chumba hiki baada ya kujihakikishia usalama koridoni, akarejea chumbani mwake alipofunga kwa 'lock' na kuzima taa kuwa kiza totoro.

Kidogo, baada ya kama dakika tano, mabwana mawili wakashika korido ya hoteli hii wakiwa wanatembea mwendo wa dharura, bwana mmoja alikuwa mrefu mwembamba na mwingine akiwa mfupi ila mwembamba pia, wote wamevalia suti nadhifu rangi yake nyeusi, mabwana hao walikomea kwenye mlango wa chumba kimoja wakatazamana usoni, bwana mrefu akatikisa kichwa, yule mfupi akaufungua mlango kwa kusogeza tu kitasa, mlango ukafunguka wakazama ndani, si punde wakawa wamesimama kando ya mwili wa Jennifer, mwili uliolala chini ukiwa hauna pumzi ndani yake, hapo yule bwana mrefu akaitoa simu yake mfukoni na kuipiga, punde simu ikapokelewa akasema,

"Amekufa. Amekwishamuua."

Baada ya hapo kukawa na ukimya mfupi kisha akauliza, "tufanye nini?" Punde kidogo akakata simu na kumwambia mwenzake, "tuondoke."

"Tunafanyaje?" Mwenzake akauliza, akamjibu huku akiutazama mwili wa Jennifer, "boss amesema haituhusu, tuache kama ilivyo."

"Hivyo tu?"

"Ndio. Ametusihi kazi yetu hapa ni kutazama tu. Hili lipo nje ya maslahi yetu."

Baada ya maongezi hayo mafupi, walichomoa vifaa vyao walivyovipachika, vifaa vya kunasia sauti, kisha wakaondoka zao.


***
 
Back
Top Bottom