Tukifanya Hivi, Kina Mwamposa na Manabii kuwa Walipa Kodi Wakubwa

Tukifanya Hivi, Kina Mwamposa na Manabii kuwa Walipa Kodi Wakubwa

Nashindwa kuelewa kwanini TRA wanashindwa kuiga kwa Ruto wa Kenya na kuongeza mapato kutoka katika wimbi hili la mitume na manabii walioanzisha biashara ya Maji, chumvi, vitambaa nk wakiviita vya upako na kupata fedha nyingi sana kama biashara isiyo kodi wala cost of production. Msome Rais Ruto alivyoamua.

"Nimeongea na watendaji wa serikali yangu kuhusu baadhi ya wahubiri kucheza na imani za wakenya. Kuanzia sasa yule anataka kuuza maji asajiliwe na mamlaka ya maji, yule anataka kuuza mafuta asajiliwe na food and drugs authority, na yule anataka kuuza mbegu asajiliwe wizara ya kilimo. Watambulike kama wafanyabiashara, na serikali ijue wanauza ngapi kwa siku na walipe kodi. Huku kwa kanisa wabaki wanaoeneza neno la Mungu, sio wafanyabiashara. Hatuwezi kuruhusu imani za wakenya kuchezewa na wakora wachache, wanaotaka kujitajirisha kupitia shida za waumini wetu" William Samoei Ruto, Rais wa Kenya.
Nakubali 100 kwa 100. Hawa wanaojiita manabii na mitume wamegeuza dini kuwa biashara. Hakuna kuhubiri neno la mungu ila ni kukusanya sadaka na mafungu ya kumi. Tena yanakusanywa mabilioni kila siku bila ya risiti wala kodi
Je TRA inalijua hili au ni kuwakamua wananchi kwa tozo na VAT
Lipa kodi kwa maendeleo ya nchi ni msemo usio na maana yeyote wakati hawa manabii uchwara wanatajirika bila ya kulipa kodi
Tujifunze kutoka Kenya
 
Naona hii imekata sawa kabisa, nao walipe tu kodi nchi ipate mapato. Sidhani kama litakuwa tatizo kwao.
 
Hoja iko hivi?
Kodi hutozwa kwenye mambo matatu tu yaan, business, investment, employment. Chochote nje ya hapo hakitozeki Kodi (out of scope)
Sasa unatakiwa uje na sheria itakayosema na iwe strictly construed ili inmase mwamposa.
No intendment in tax laws, words must clearly be stated.
SASA EBU NISAIDIE HIYO SHERIA ITAKAAKAJE KIASI KWAMBA SADAKA AU MICHANGO kanisan itofautishe na mambo ya mwamposa?
Utaishia kutunga sheria mfu kwan haitaweza kufanya kazi.

Inatakiwa hivi unapowashtaki mwamposas useme ni kivipi arrangement ya transactions zake za maji na mafuta namna ambavyo fall within tax laws na sio kihisia.

Sasa mwamposa si atasena toeni sadaka nitawagawia maji MUNGU alioniruhusu niwagawie...
Wale wa 5,000 watapewa maji , chin ya hapo hatawapo ...hajairuka sheria yeyote
Yaani ukitoa 5000 ndo utapewa maji? Hiyo ina tofauti gani na biashara ya maji? Tofauti ni kuita upako tu? Je huyu mchuuzi wa maji akiita maji ya upako je atasamehewa kodi naye?
 
Katoliki pia wanayo maji ya kawaida wanachota bombani au kisimani,au mtoni au kwenye dimbwi na kuweka chumvi kidogo ambayo hayana hata viwango vya TBs ukiingia kanisani unachovya mkono na kupiga ishara ya msalaba wakatoliki wanaamini ni maji matakatifu sembuse Kwa Mwamposya ya Hill water au ya Uhai yenye nembo ya TBS yupi bora hapo?

Wote wanaita maji matakatifu
Unaonekana kichwa chako cheupe sana, kwani hayo maji wanayochovya Katoliki kwa ajili ya kufanya ishara ya msalaba, wanakunywa kama kwa Mwamposa wanavyokunywa maji yake ya miujiza?

Na kwani hayo maji wakatoliki wanauza, kama Mwamposa anavyouza maji yake ya miujiza?
 
Sadaka na Kikumi ni tofauti na kuuza maji na mafuta ya upako. Hizo ni biashara ambazo zinafanyika kanisani kwa mitume. Hivyo zipo liable for taxation. Mambo ya kusema toeni sadaka niawape mafuta hiyo sio sadaka ni uyapeli. Sadaka unaitoa kwa hiari na hupewi chochote in return.

Yaani ukitoa 5000 ndo utapewa maji? Hiyo ina tofauti gani na biashara ya maji? Tofauti ni kuita upako tu? Je huyu mchuuzi wa maji akiita maji ya upako je atasamehewa kodi naye?
Yaan ukitoa 40,000 ya mchango wa jumuiya ndio mtoto atabatizwa? utapata huduma ya padri kwenye mazishi ya mwanafamilia wako....hiyo sio biashara kama ya mwamposa?
 
Ulipaswa kwanza kuelewa tulianzia wapi na niliyekuwa namjibu,usingekuja na hili swali maana hata siwezi kujibu kwakuwa umerukia kati kati.
Kwanza Mkuu nitake radhi sijarukia swali nilikuwa nafuatilia mlolongo wote mwanzo mpaka mwisho nilichoona hapo mifano yako yote ulikuwa unawatolea Wakatoliki ukionyesha kama Wakatoliki wapo sahihi kuliko Dini/ madhehebu mengine
 
Na TRA wapo wakiwakaba akina mama ntilie, nchi ya ajabu sana hii, hawa matapeli wa dini ni wajasiria dini kwelikweli wanatengeneza na kuharamisha pesa zao huku TRA na vyombo vya dola vikiangalia kushoto.
Ila tuwe wakweli Rais akianza kuwafuatilia kina Mwamposa wote nyinyi si mtasema kwa sababu Rais huyu ni Muislamu aupendi Ukristo?
 
TRA kodi inasoma ya PAYE ya hao wachungaji wa makanisa yote yawe katoliki,Lutheran, Pentecoste au lolote kipato chao wanachopewa wao direct kinakatwa kodi kitokanacho na sadaka za waumini ? Kiitwe fungu la kumi ,posho or whatever ? Ni income from employment kwao .Kodi wanalipa?

Dawa yao TRA iwashukie kama mwewe Kuwa how do you survive source ya income yako for survival unaitoa wapi? Kama sadaka za waumini au mafungu ya kumi huo mshahara walipe kodi na wapigiwe toka siku wamekuwa wachungaji ,mapadre au massista kanisa husika lilipe arrears za kodi

Ili wakome kunyooshea kidole wengine akina Mwamposya or whoever makanisani
Kukomesha huo ujinga

Wanatupa mawe kwingine wakati wanaishi nyumba za vioo.Patachimbika.
Umeambiwa wakifanya Biashara ya kuuza Chumvi,Maji,KEKI,juisi, mafuta ambazo ni bidhaa za viwandani zinazouzwa na wafanyabiashara WENGINE wanaolipa Kodi Tena Kwa Bei nafuu .

Hapo kipi hakieleweki. ACHENI kuliangamiza Taifa Kwa kushabikia majizi na Mafisadi ndio Maana kanisa haliwezi kuikemea serikali iliyojaa majizi matokeo yake inayatumia majizi Kwenda kuzindua miradi Yao ya Wizi . Mtumie na Nabii Wa Mungu anawatumia Walafi na Mafisadi Wa Mali za umma na majizi ya kura na wauaji kweda kuzindua na kubariki Miradi waliyoipata madhebahuni kama kweli ni halali. Si Bora angemchukua mtumie mwenzake kama Mwigira au Kakobe au Lusekelo au Pengo au Malasusa akazindue na kutakasa miradi yake Binafsi. Huoni Hapo kuna somo la wazi kuwa piga pesa zako mapema waumini Wakiwa Bado wamelala. Wakizinduka kumeshakucha.

Hata kanisa Katoliki Karine zilizopita liliuza vyeti vya msama Wa dhambi Kwa hamasa kubwa na KUWADANGANYA watu kuwa YESU akiaja atauliza vyeti vya msamaha Wa dhambi. Biashara hiyo ilipingwa na Padri Martín Luther na kuitwa mzushi na Muasi mpaka kutangaziwa kifo na papá.

Karne hii watu hawasomi Biblia wanasubiri kusomewa na kupewa tafsiri za kizushi na Hadithi za kutunga. Mafuta ya upako ndiyo hayo hayo yanattumiwa na Waganga na maustadhi kutibu na yanatengenezwa na Wataalamu Wa majini Jambo ambalo kwenye Ukristo halipo. Dawa ya mapepo ni jina la YESU SIO mafuta Wala Maji ya Kiwandani. Maji watu walishamwagiwa Kwa njia ya ubatizo na mafuta Kwa Sasa ni Roho Mtakatifu. Magonjwa yalikwisha Kwa kupigwa na kuteswa Kwake YESU Kristo na kumwaga damu yake.
Come on !! Wakristo Wa Leo nani aliyewaloga ?Kwa Nini mnarudi Tena kwenye Zama za Giza na kuangamizwa Kwa kukosa maarifa ya kumjua Kristo aliye asili ya hekima na maarifa Yote?
 
Acha uongo yanauzwa kati ya 1000 au 2000 na pesa inaenda kwenye uendeshaji wa huduma za Kanisa.Kuna umeme unawaka pale,Kuna Redio analipia TCRA,Kuna Wafanyakazi na wachungaji wanalipwa pia nk.
Sasa ulitaka pesa atoe wapi?
Mbona kwenye makanisa ya KKKT na Moravian na ata Katoliki Huwa kunakuwa na minada makanisani muumini analeta Kuku wa Tshs 20000 na anauzwa kwa 200000,apo inakuaje Mkuu.Au ndiyo kunywa anye Kuku,akinya Bata kaarisha?
Umesema mnada Wa sadaka sio mnada Wa kuwatamgazia watu wiki nzima kuwa Njooni kutakua na mnada Wa upako na uponyaji ? Na Maji yanawekwa Sehemu watu wanauza Kwa lengo la uponyaji!!

Inaonekana chuki inatokana na Kudhani kuwa Yale makanisa ya watu Binafsi yanapata nguvu KIROHO na kiimani kupitia toba lakini wengi hawajui kuwa Nyuma yake ni kulea dhambi Kwa kulinganisha na makanisa makongwe yanayojiendesha kitaasisi.

Minada inayofanywa kwanye makanisa ya KKKT na Roma pesa zake zinasimamiwa na kamati za Fedha na kuratibiwa na miongozo ya kanisa SIO Mali ya mchungaji na familia yake.
Ndio Maana hayo makanisa yanatoa misaada Kwa watu wasiojiweza kitaasisi na Kuna bajeti maalumu Kwa ajili hiyo lakini pia watu wengi wansomeshwa na makanisa hayo na kukata elimu ya Theolojia NJE na ndai ya nchi na kuweza kutanua wigo Wa wasomi na Ajira Kwa Vijana na Hata watu wazima. Kuna Taasisi za huduma za tiba kama Hospitali na zahanati za makanisa hayo na SIO Mali ya Mchungaji Wala askafu na MKE wake na Watoto wake Bali ni Mali ya Taasisi akistaafu analipwa Haki zake na Taasisi inapata mtumisi Mwingine. Hapo ni taaisi . Yesu alijenga taasisi ndio Maana alikua na Mhasibu na wasaidizi wake ambao walikua wanafanya KAZI kitaasisi na kurudisha Taarifa kwake na walipotoka kujibinafsishia taasisi iwe Mali Yao pale walipomkuta MTU anatoa Pepo Kwa jina lake wakajaribu Kumkataza Kwa sababu hayupo kwenye kundi lile Yesu aliwaambia wamwache Maana yupo upande Wao na SIO kinyume chao.

Tukitazama haya mambo kishabiki na kimahaba Kama Siasa na Mipira tunamsaidia Shetani kuliangamiza kanisa na Ukristo Kwa Kasi kubwa sana na tunakula na Wakristo Wa hovyohovyo walijatana makanisani lakini ni watu waovu kupita kisasi.

Maji hayajaletwa na waumini kama Sadaka Ili yauzwe mnada lakini MTU anayalinganisha na bidhaa Kama malimbuko au Sadaka wanazopeleka Kanisani na kuuzwa mnada kwenye makanisa mengine.

Watu wanasubiri kanisa la KKKT,Anglican na Roma wapambane na mapadri na wachungaji Wao wamwagiwe Tindikali na kuuawa kule Zanzibar mpaka Hapo Wazanzibari watakapokaa na KUELEWA na Kutoa uhuru na kuamua kujiunga na Ukristo Kwa hiyari Yao . Kisha Manabii Feki watajitikeza kuwa Wametumwa Kwenda kuwapa upako Wazanzibar na watayaponda na kusema kuwa makanisa ya KKKT na Rima hayana Mungu Wala Roho Mtakatifu.

Hubirini Injili bila woga Wala kujali maisha yenu mafupi maeneo yasiyo na Wakristo Ili watu wamjue Kristo Mfano kule Kusini na mikoa ya Pwani, Somalia, Sudani na Zanzibar na Pemba na Hata Mashariki ya MBALI
 
Ruto atakuwa one term present

Alikuwa kutwa anazurura makanisani kutqfura kura hadi ya vichochoni kumbe tapeli akapata kura kageuka kupiga vita waliompa kura

Akimaliza kipindi chake Uhuru Kenyatta atarudi kwenye madaraka ya uraisi Ruto atakuwa one term president

Wanasiasa hawana loyal members makanisa ndio yanao Ruto ahesabu kuwa atakuwa president kipindi kimoja tu vaada ya hapo kwa heri
Acha uzushi fuatilia , Ruto kabla ya kuingia kwenye Siasa alikua ni MTU Wa Dini sana na alikua anatumia muda wake Mwingi kuhubiri na MKE wake.Mungu alimuinua Kwa KAZI ya kulirejesha kanisa la Kristo na Haki kwenye Taifa la Kenya. SIO muda mrefu Kenya watatuuzia mahindi na chakula mana Mungu anapomuinua Kiongozi anayemtii analiariki Taifa hilo.

Hata Waisraeli walikua wanajenga hekalu kupitia Wafalme waliokuwa wanaumia kuona hekalu la Mungu limebaki magofu. Na Mungu alikua anawapa nguvu na uwezo pale wafalme wanapoguswa na kulijenga upya hekalu .

Kusema kuwa Ruta alipewa kuwa Kwa kampeni za makanisa sana hivyo akae kimya ni kumkosea Heshima mana alikua hiyo Tangu mwanzo .
Amepata Kibali Cha kulirejesha kanisa kwenye misingi ya Kristo Hata kama Atakaa madarakani mwaka mmoja lakini KAZI ya Mungu ameifanya ya kutetea injili ya Kweli inayompa Heshima ni utukufu Yesu Kristo Badala ya mafuta na Chumvi.
 
YEHODAYA hebu ngoja kidogo, viwanda vya maji vinalipa kodi kama kawaida na yeye ananunua huko.
Lakini kifuatacho naye anauza nasikia yale maji ya elfu moja anauza elfu 5 mpaka 10. That's where tunasema faida hiyo iwe taxed.
Tupo pamoja mkuu? Hata maduka yetu ya mtaani faida yao ya kuuza maji inatozwa kodi.
Huu ndio ujinga unasikia? Nenda pale kaulize , huu ujinga ndio niliukataa nikapita pale nikauliza maji nikaambiwa buku nikachukua nikanyw taratibu ,nikaondoka. kunavitu sio vya kusikia. mwamposa Hana tofauti na wanaouza maji barabarani na wao lipe kodi?
 
Wacheni kupotosha ili kumlinda huyo jamaa yenu.

Makanisa hufanya harambee kwa kuuza vitu kwa lengo la kupata pesa zitakazotumika kwa shughuli fulani hapo kanisani, kama ujenzi, ukarabati wa jengo, hakuna harambee inayofanywa bila sababu.

Kwa mantiki hiyo, sasa hebu tuambie, Mwamposa akiuza maji na mafuta, hizo pesa huwa anazipeleka wapi?na kufanyia kitu gani?
Wewe unazijua shughuli za mwamposa kama ausali kwake? Mimi mwenyewe sijui shughuli za kanisa la jirani kabisa na nyumbani kwangu , nitawezaje kujua shughuli za mwamposa tuache ujuaji wa kijinga
 
Unaweza kusema hapa posho wanazolipana wafanyakazi wa serikali even hao TRA kuna wakati hufanya vikao vyao wakajilipa posho huwa zinakatwa kodi?

Una chuki kubwa sana na RC bro kuwachukia hakukuongezei chochote kwenye maisha yako ya kiroho zaidi ya kupoteza muda sasa nakushauri kaa chini kunywa maji kidogo(sijui yatakuwa ni ya mwamposa au vipi utajua mwenyewe) kisha tafakari je ni sahihi kwa mwamposa kuwauzia watu Hill Water 1litre ya Tsh 500/= mtaani kwa gharama ya 5,000/= hapo Kawe na popote kwenye matamasha yake?
Hawa watu wamejawa na roho chafu sana.Kuna mmoja hua anaabudu kanisa Fulani la mtume mmoja bilionea alihama mpaka Chumba anacholala mumewe ate ameambiwa Mume wake mi pepo.
Yaani mumewe alikua msomi na kusomesha watoto wake na kutokana na jina la huyo baba Watoto wake walipata KAZI kwenye taasisi kubwa na kuwa na mafanikio makubwa sana hasa Watoto Wa Kike. Mama akawa anasali kwenye makanisa Binafsi na kumtenga Yule baba eti ni Pepo na Watoto Wa kiume wakawa upande Wa mama . Alihama Chumba kisa Yule baba alikua anakunywa pombe . Yule baba alikua mstarabu sana na nyumba yake alijenga mpaka kaunter na kuweka vinyenywaji ndani Kwa ajili ya kunywa na marafiki zake. Mume waliyeoana na kuishi ZAIDI ya miaka 35 anaibuka ghafla na kumwita Pepo na kuhama Chumba.

Hawa waumini Wa makanisa Binafsi ni watu wanaojengewa Chuki na kujazwa mapepo machafu ya Chuki na ujinga na kupofushwa macho kama mafarisayo na masadukayo. Wengi hawaelewani mpaka na majirani. Hawawezi kutenda mema Kwa majirani Wala NduguHawana msingi Wowote Wa mafundisho ya Yesu ya kumpenda Jirani Yako kama nafsi Yako . Kwa kweli ni majanga Matupu . Tofuti kabisa na Wasabato wanamsimamo sana ya Dini lakini Wana upendo Kwa WENGINE wasio Wa Imani Yao pamoja na k utofautiana Imani Yao.

Makanisa yaliyoanzia Marekani yalianza Kama uamsho Wa kuhubiri injili Duniani kote. Shetani hakulala akaingia HUKO HUKO kuleta injili ya utajirisho na MIUJIZA na kupoteza ule uamsho Wa kuwapeleka watu Mbinguni na Sasa anawapeleka Kuzimu Kwa mamilioni ya watu Huku upendo Wa watu ukiwa umepoa na kujazwa Chuki kubwa sana na tamaa ya Fedha na ngono.

Yani watu wanajazana makanisani kujikinga Kwa KUTUMIA Maji na Chumvi. Ukiwauliza mbona hawajabatizwa au kujazwa Roho Mtakatifu hawana Majibu ZAIDI ya kusema mbona Roma na KKKT wanatoa Sadaka nyingi hawakatwi Kodi pasipo kujua kuwa Hayo makanisa yanamchango mkubwa sana kwenye maendeleo ya jamii nzima kupitia Sadaka na SIO biashara bidhaa ya Maji au sukari au Chumvi au soda au Energy drink.

Msingi Wa Sadaka Upo katika kuwahudumia wanyonge na yatima katika uhitaji Wao. Ndio Maana hakuna mwarabu mwenye maisha magumu Hata kama ni tahira na hajasoma elimu ya Dunia Kwa sababu ya kugawana zaka Kwa Kila mahitaji bila riba Wala masharti magumu ya kuvunja Ndoa za watu na kuendeleza zinaa Kwa wake za watu .ZAIDI watapewa mitaji na kuwa na uwezo Wa kulea familia ZAO na Hata Vijana kuoa . Hiyo ni Dini inayofanana sana na misingi ya Imani aliyoishi baba Wa Imani Mzee wetu Ibrahimu na uzao wake akiwemo Yesu na mlezi wake Mzee Joseph na mama yake Mariam.
Hii mihemko ya kimarekani imeleta shida sana mana haiwajali watu kwenye jamii nzima Bali MTU Mmoja anayejiita mtume basi anaamua kuwa upako uwe ni Maji au ni juisi au vitambaa au Sabúni au mafuta yaliyotengenezwa Kiwandani kama bidhaa nyingine zinazouzwa kibiashara. Hayauzwi Kama Sadaka Bali Kwa Bei ya faidi ambayo WENGINE hawawezi kuifikia . Babu wa Loliondo Kwa Sababu alifanyia huduma yake Kijiji Kwa majani ya miti ambayo Hata sayansi inathibitisha kuwa ni dawa Hao Hao mitume walimpinga na kusema kuwa ni Pepo na ushirikina Kwa sabau tu hakuwa na suti Kali na mavyombo Mkubwa ya Muziki na makumbwa.
 
Nabii mkuu Tanzania👇😁😁😁
 
Unaweza kusema hapa posho wanazolipana wafanyakazi wa serikali even hao TRA kuna wakati hufanya vikao vyao wakajilipa posho huwa zinakatwa kodi?

Una chuki kubwa sana na RC bro kuwachukia hakukuongezei chochote kwenye maisha yako ya kiroho zaidi ya kupoteza muda sasa nakushauri kaa chini kunywa maji kidogo(sijui yatakuwa ni ya mwamposa au vipi utajua mwenyewe) kisha tafakari je ni sahihi kwa mwamposa kuwauzia watu Hill Water 1litre ya Tsh 500/= mtaani kwa gharama ya 5,000/= hapo Kawe na popote kwenye matamasha yake?
Yale maji yanauzwa buku
Kama ulinunua 5000 umepigwa na wahuni
 
Kama TRA hawakatwi hizo posho wanatakiwa kukatwa na wabunge pia
Posho ni income TRA kama kweli usemacho hawako sahihi wakatwe kodi za vikao wao na wabunge

Posho ni income kwa receiver iwe ya kikao cha TRA au mbunge au posho ya padre au mchungaji au Askofu au nabii au mtume ni taxable income

Kama haiko taxable iwe taxable
Ni kweli lakini Wabunge hawafanyi Biashara ya Kununua maji na kuyauza kwenye mikutano majimboni Kwako au kule Bungeni. Wakifanya Biashara hiyo ya kuuza hangachifu na mafuta ya zeituni na sabuni za mshindi basi watakadiriwa Kodi kama wafanyabiashara WENGINE .

Kodi halali kabisa ni Kwa wafanyabishara . Hata Kaisari alipoitawala Israel alilenga kupata kodi kutokana na eneo la njia kuu za Biashara kati ya Ulaya ,Asia na Afrika kupita Israel na Mashariki ya Kati.Wayahudi walidhani YESU atagoma KUTOA Kodi lakini akawaombia Kodi na pesa ni za sera na mfumo Wa Mtawala ambaye alikua ni Kaisari ndio MAANA AKASEMA ya Kaisari MPENI kaisari na ya Mungu MPENI Mungu .

Sasa kama Kanisa linafanya Biashara Badala ya kuhubiri mambo ya Mungu na KUTOA Sadaka kama maagizo ya MUNGU yanavyoelekeza basi ni Lazima Kaisari aende kuchukua kilicho chake. Na wale watakaofanya ya Mungu basi MUNGU atachukua kilicho chake.

Kodi ni Kwa Kaisari na Sadaka ni Kwa Mungu. Hiyo Hata utawala katili Wa Rumi ulijua Hilo. Hawakuchukua Sadaka za mahekalu Bali walikwenda Hekaluni kuchukua Kodi Kwa wafanyabiashara Baada ya Wayahudi kuligeuza hekalu kuwa Soko na Sehemu ya KUFANYA uovu na uhuni WOTE wa kibiashara walidhani kuwa watakwepa Kodi ya Kaisari. Walisababisha mpaka machangudoa kuwa yanajiuza kwenye viunga vya hekalu na wateja wao wakawa ni wafanyabiashara na Hata watu waliotoka MBALI Kwenda Hekaluni na baadhi ya wakuu Wa kidini . Ndio Maana yule Mwanamke Kababa alipokutwa anajiuza walimkamata na kumpeleka Kwa Yesu. Yesu akawaambia asiye na dhambi awe Wa kwanza kumpiga jiwe. Wakakimbia WOTE. Yesu alijua kuwa Wayahudi walikua wameshatoka kwenye misingi ya Manabii na Tourati kutokana na Kuiga Mila za Warumi na mambo ya Kirumi yaliyoonekana kama maendeleo na maisha ya kisasa Kwa wakati huo.
Ndivyo ILIVYO Sasa pia Wakristo wamepotoka na kujiegemeza kwenye utamaduni Wa magharibi na Mila ZAO na Kile wanachani kuwa ni maendeleo na Imani mpya iliyogubikwa na tamaa ya Fedha na starehe na anasa za Dunia.

Wakuza hangachifu za upako Wanafanya hivyo mana WANAJUA kuwa watu hawana Elimu ya Dini na theolojia ya kujua historia ya Ukristo na Dini nyingine na chimbuko lake na anguko lake Tangu Adamu na Mapito na nyakati zake KIROHO na kimwili.

Shetani katika MALENGO yake ya muda mrefu aliondoa masomo ya Dini mashuleni na kuacha masomo ya historia za kipagani na Sasa tunapata wasomi wengi wasiojali Wala kujua maandiko Kwa usahihi matokeo yake wakishafanikiwa ama Kwa Wizi au rushwa au udanganyifu wanakimbilia kujitakasa Kwa vitambaa na mafuta na Maji mana nafsi ZAO zimejaa hukumu na kujihukumu Usiku na mchana. Hawana Neno la Maarifa ndani mwao.
 
Back
Top Bottom