Tukio la kusisimua nililolishuhudia kwa macho yangu katika msitu wa Nairoto

Tukio la kusisimua nililolishuhudia kwa macho yangu katika msitu wa Nairoto

Pale nilipo kaa (kuwangoja washkaji) usingizi ulinipitia nililalaa mpaka nilipo amshwa na makelele ya washkaji.

Sijui nilitumia muda gani kwenye usingizi ule ila nilipo angalia saa ilikua ni saa 6 mchana.

Nilipo amka nilikutana na kijua kikali utadhani niko Sudan, yani mpaka nguo nilizo vaa zilishaanza kunyauka.

Chakwanza niliwauliza kuhusu yule mmalawi, nikaambiwa bado wako camp wanaendelea kungoja mvua iishe waanze kazi.

Nilipo wauliza vipi kama mvua imeisha huko walikotoka, wakaniambia mvua imenyamaza sasa hivi baada ya kuvuka lile korongo.

Yani kumbe mvua inaanzia kwenye korongo kwenda matandani, ila kulimaliza korongo mvua hakuna.

Tulitembea mpaka kijijini, hakuna alie jua kua mimi nina dhahabu mbeleni.

Tuliingia kijijini saa 2 usiku, hapo tukalala.
Ila kwakua tulisha fika kijijini, kila mtu aliendelea kimpango wake.

Pale kijijini kila mtu anaham ya kujua kulikoni huko porini.
Nakumbuka nilitulia kwenye kiosk cha jamaa flani hivi, kila mtu alikua ananiuliza kuhusiana na porini.

Usiku kucha nilikesha kwenye kile kiosk cha jamaa nikila Royal gin (hii ni pombe kali sana) mpaka kuna kucha.

Kwakua nilikua na pesa ya kutosha niliyo chukua kwenye lile duka la marehem, hivyo ilikua mwendo wa kujimiminia pombe.

Kuna dem alinitamani nika lale kwake, lakini nilikataa kwa kuhofea asiniibie dhahabu yangu.

Migodini wanawake ndio wanaongoza kutuibia wachimbaji.

Kilicho fanyika nikumpa pombe mpaka dem akakimbia.

Asubuhi, sikutaka kulemba, na pombe zangu kichwani, nikakamata piki piki mpaka Montepuez.

Montepuez, hapa ndio kuna soko la madini yote.

Nikaingia kwa msirilanka nikapima dhahabu.

Dhahabu ilikua na uzito wa gram 112, kila gram kwa kipindi kile ilikua 2000 miticais sawa na laki moja shilingi kwa wakati huo.

Nikachukua 224,000 miticais, hapo akili yote inamuaza mama Abuu (Shemeji yenu)

Nakumbuka nilinunua piki piki na mazaga mengine kama nguo.

Nikatuma kama 60,000 miticais (sawa na Milioni tatu kipindi hicho) kwa mama yangu Tanzania, maisha yakaendelea.

MWISHO.

Naahidi kuwahabarishine matukio mbali mbali yanayo / yatayo tokea hapa mgodini nilipo.

Kumbuka kwa sasa naishi Tete, Muatiz, ila kwa hizi mvua zilizo anza kunyesha, nategemea kurudi Cabo del Gado wilaya ya Montepuez, nikatafute Ruby.

Hapa nangoja hii kazi iishe, nione kama nitaokoa chochote kinisogeze kwenye Ruby.
Ahsanteni na kwaherini.
Kwahiyo mkuu ukapiga kama million 11 ... Je vipi mkuu unamawazo ya siku 1 kuja kuachana na kazi ya uchimbaji kufanya biashara zingine au haujafikiria kuhusu hilo
 
Ahsante mponcha.
Ushawahi kuingia ndani ya fonka?
Mule ni kama umeshajizika tayari.
Usiku wa leo nitakua humo.
mkuu kila la kheri angalia duara likijikopa lisilale na wewe mbele.....mambo yakiwa mabaya jifiche kwenye fonka....huko mkiwa mnashuka chini mnavaa koboko?!....na ukitaka kumsemesha mtu aliyeko duarani unamwambia "hapo chini, achama!!!!" au?!..
usisahau kupiga sample kabla hujafanya maamuzi na mwisho uwe makini na matufe ukihila ni bahati yako.....ukichumera au ukiporora ndo maisha.....ukienda maluja angalia kulia na kushoto kwanza ...

kila la kheri murah...
 
Mkuu nairoto sikuwahi kurudi tena.
Mshikaji wa kimalawi tulikutana miaka miwili mbele, Mwaja.
Hakunifanya kitu kwasababu Pele Mwaja mimi nilikua na kundi la wauni walio kua wanasumbua pale.
Nilimuahidi kumlipa (kuepusha zogo) lakini sikuwahi kumlipa, na mpaka leo sijui yuko wapi.

Kuhusu wale jamaa, sijui kilicho endelea nyuma, ila mpaka leo Nairoto watu wanachimba, lakini dhahabu hazitoki kama zamani.
Asante kwa story nzuri na ya kusisimua. So hujawahi rudi Nairoto tena? Yule mmalawi hukuwahi kutana nae tena? Je ile mvua iliwahi isha na jamaa wakaendelea kupiga kazi? Vip sasa upatikananaji wa dhahabu huko Nairoto? Kuna sehem nimesoma kuna wazungu wamewekeza huko wanadai bado wanafanya utafiti wa dhahabu!!
 
Hii lugha gani [emoji3][emoji3]
Hiyo ni lugha ya kichimbaji hiyo
Maloja-kujisaidia porin
Kuhila - kupata madini
Duarani - shimo
Moko - sururu
Matufe - udongo unao meguka kwenye kuta za shimo na unaweza kukujeruhi vibaya au kukuuwa kabisa ukikukuta huko chini

Nmepata bahat ya kukaa na wachimbaji sehem tofaut ila naona lugha yao ni moja labda kwakua wanahamahama na wanakutana
 
Zamani sana pale jirani na kwa bamkubwa Chamwino kuna kakijiji kanaitwa nzuguni,kuliibuka Chimbo dhahabu inatema mi dogo tu wa 12-14,
nilikua najichanganya sana na maanko wangu alafu walikua watu wa vagi na ubwiii ile mbaya,
sasa walinipenda kwasababu mlinzi wao huko wakipakaza,likianzishwa nzegembe mi nachukua wallet na mali zote zinazohamishika kisha nayeya home.
Machimbo yalipoanza Nzuguni tulienda hawakuniacha bodyguard wao.
Duh kufika kule nilichoka jamaa anachosimulia ni kweli kabisa.
uzinzi,pombe,bangi, kila aina ya uasi unaukuta .ushangae sasa machimbo hata mwezi hayana.
sisi tulikua na kagroup ketu mtu nne wote mayanki tu na tulikua tunachakata vumbi tu lile.
siku kadhaa tukapatapata vimawe viduuchu yani kwenda kuuza tukagawana kahela kadogodogo tu.
Ila mi niliridhika nikasepa nikawaacha maanko maana wao hata ndoto ya kurudi hawana ilikua km wamefika nyumbani,sio hata wachimbaji wao ilikua ni pary pary tu.bangi pombe mabibi na daily wana hela wale jamaa aisee
Ila walikua mafundi malori wazuri sana KAUDO pale na Madereva.
Ule mgodi ulikatika ghafla tu,upo hapo Chamwino pembeni kushoto ukiwa unaenda kwa baba mkubwa.
Sio kwamba baba mkubwa anachimba kisirisiri?
 
huna hata haya kusimulia kutoroka jeshi jinga wewe. kwa hiyo hapo umeridhika kula ugali wa shikamoo mama
ndio nyie tunawaimbaga kwenye chenja mananga wakubwa
Watt wa kishua hao matifu ya kijesh hawayawezi wameshazoea kudekezwa na dady na mamy hata ukimpiga na ukubwa wake wanaenda kukusemea kwa mummyyy
 
Hiyo ni lugha ya kichimbaji hiyo
Maloja-kujisaidia porin
Kuhila - kupata madini
Duarani - shimo
Moko - sururu
Matufe - udongo unao meguka kwenye kuta za shimo na unaweza kukujeruhi vibaya au kukuuwa kabisa ukikukuta huko chini

Nmepata bahat ya kukaa na wachimbaji sehem tofaut ila naona lugha yao ni moja labda kwakua wanahamahama na wanakutana
Matufe yamenitisha
 
Mkuu Cabo del Gado ni kubwa, ina wilaya 16.
Akina Ali mbabe wanazingua kuanzia wilaya ya Mocimbua, Muedumbe, kisanga na Makumia.

Mimi naenda wilaya ya Montepuez, hii iko mbali kidogo na huko.
Alafu huku mimi ndio huwa nakaa sana, nikitoka ni kwaajili ya mlio.

Hapa Mwatizi ilinileta dhahabu ya Ngorongoza, lakini naona ni pagumu, wacha nikatafute Ruby kwanza.

Kuhusu kudhaniwa ali mbabe, hilo kweli lina tokea, tena Watanzania kibao wako jela za huku kwa kudhaniwa ali mbambe.

Yupo mshikaji wa Dodoma, alisota miaka miwili jela, katoka mwaka jana, nasikia ndugu zake walikuja kumfatilia.

Hilo jimbo si ndo Alshabab wamelitwaa? Utayaweza mazingira ya mchakamchaka na milio ya risasi mara kwa mara?
Angalia tu usije ukahisiwa wewe ni miongoni mwao wakakumaliza askari wa Msumbiji
 
Hiyo ni lugha ya kichimbaji hiyo
Maloja-kujisaidia porin
Kuhila - kupata madini
Duarani - shimo
Moko - sururu
Matufe - udongo unao meguka kwenye kuta za shimo na unaweza kukujeruhi vibaya au kukuuwa kabisa ukikukuta huko chini

Nmepata bahat ya kukaa na wachimbaji sehem tofaut ila naona lugha yao ni moja labda kwakua wanahamahama na wanakutana
Umesahau fonka-shimo linalochimbwa ndani linaelekea pembeni horizontally kama mwanandani wa pembeni.Hii linatinduliwa kwa poncho na mtindo imara
 
Mkuu hii ni dunia nyingine.
Mara kibao nimejaribu kufanya hivyo lakini nashindwa.
Nikikaa home mwezi tu, nayamiss haya maisha.
Kuna kipindi najiuliza (hasa nikiwa kwenye hali mbaya) hivi nimezaliwa kuishi maporini?
Maana mifano naiona, wapo wazee tunachimba nao.

Mzee anakuhadithia machimbo miaka ya 1980 huko, yani hata sijazaliwa.

Kuna mzee alifuatwa na mwanae arudi home (mwanae ni mkubwa na ana pesa) mzee alikataa kata kata, mpaka yule mtoto akawaomba wazee wenzie (nao ni wachimbaji) wamshauri mzee akubali kurudi home, na mpaka sasa mzee tunae Migodini, sijui yuko poli gani.
Kwa nilivyokusoma naona umeshapata migao mingi sana pesa tena pesa kubwakubwa kwanini usirudi Tz ubadili maisha
 
Back
Top Bottom