Tukisema mfungo wa Ramadhan ni mwepesi na ni kubadili ratiba ya kula tunakosea?

Tukisema mfungo wa Ramadhan ni mwepesi na ni kubadili ratiba ya kula tunakosea?

Cha ajabu tukifunga sisi waislamu mayeumia na kuona wivu ni nyie wakristo ajabu iliyoje embu angalia mnavyotuhusudu hadi huyu mlimbwende kashindwa kujizuia
Hakuna anayeumia mkifunga infact tunashangaa,na ndicho alicholeta mtoa mada.
Unajua nyinyi huwa mna ujinga mmoja,mnataka kusifiwa kwa kila jambo,na ole wake anayekosoa basi anaona wivu ama ana chuki na uislam.

Ktk ukristo tumeambiwa imani bila matendo ni utumbo tu,wewe ni mbora katika nidhamu unaposali msikitini au unapofika mwezi wa ramadhani lakini ni kweli unamjua Mungu au unafanya kwa ajili ya waislam???

Leo hii hapa duniani hakuna jamii ngumu kuishi nayo kama ile yenye waislam,hata waislam wenyewe kwa wenyewe ni kipengere kukaa pamoja😀😀.
 
Hakuna anayelazimishwa ndio maana utakuta ikifika ramadhani hata baadhi ya wakristo wanafunga kuwasindikiza rafiki zao waislamu , ita kubadili ratiba au chochote ila tumewekewa utaratibu kwenye dini na tunaufuata kwa heshima kubwa duniani kote from europe to united states wanajua na kuheshimu kwamba sasa ni mwrzi wa ramadhani ila kwaresma hawaijui
Na huu ujumbe wa ramadhani kutoka kwa raisi wa dunia na huyu mwingine ni mtangazaji maarufu southafrica
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] sasa wanazuia watu kula hadharani kwann? Na mtu hajafunga au sio wa imani yenu?
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] sasa wanazuia watu kula hadharani kwann? Na mtu hajafunga au sio wa imani yenu?
Hiyo siyo sawa kwa jamii yenye watu wa dini tofauti , ila zanzibar wana tamaduni zao kidogo tofauti na huku bara , ndio maana kuna baadhi ya restaurants zipo wazi kuhudumia watu wa dini nyingine na watalii,
 
Hakuna anayeumia mkifunga infact tunashangaa,na ndicho alicholeta mtoa mada.
Unajua nyinyi huwa mna ujinga mmoja,mnataka kusifiwa kwa kila jambo,na ole wake anayekosoa basi anaona wivu ama ana chuki na uislam.

Ktk ukristo tumeambiwa imani bila matendo ni utumbo tu,wewe ni mbora katika nidhamu unaposali msikitini au unapofika mwezi wa ramadhani lakini ni kweli unamjua Mungu au unafanya kwa ajili ya waislam???

Leo hii hapa duniani hakuna jamii ngumu kuishi nayo kama ile yenye waislam,hata waislam wenyewe kwa wenyewe ni kipengere kukaa pamoja😀😀.
Ukiujua uislamu ukiachana na mnavyodanganyana huko na wachungaji feki ni raha sana ndio maana unaona watu wengi hata walioenda qatar tu worldcup waliishia kubadili dini maana walichokuwa wanadanganywa na walichokiona tofauti,
Na sisi waislamu swala tano ni kila siku lazima ndio maana unaona huyo mtangazaji wa kizulu kasifia hapo kwenye kusali huwa hakuna mjadala kwa waislamu hata duka au uende na pesa , fikiria mtu yupo southafrica amenote hivyo vitu
Na kuna huyu shaun king kutoka marekani juzi kasilimu baada ya kufanya research kuhusu uislamu kakuta tofauti na ujinga aliodanywa
Toa chuki jifunze kuhusu uislamu nakuahidi utaupenda
 

Attachments

  • Screenshot_20240323-230317_Instagram.jpg
    Screenshot_20240323-230317_Instagram.jpg
    151.7 KB · Views: 1
Qadhi mmoja wakati wa kusikiliza kesi kwenye mahakama, mwanamke aliyekuwa akitoa ushahidi wake alikuwa akitoa huku akibubujikwq na machozi sana mpaka mmoja wa masheikh akamwambia Qadhi; hutosheki na ushahidi wake? humuonei huruma kwa ushahidi wa huyu mwanamke mpaka hali aliyonayo ya kulia?

Qadhi akamjibu; sihukumu machozi, nahukumu haki.

Kwa hiyo ndugu yangu, mimi nimebahatika kukuona kwa nafasi mbalimbali ndani ya hii Jf. Nimebahatika kukuona kwa maudhui yanayohusu dini ya kiislam na uchangiaji wako nimeuona.

Watu wa aina yenu nawajua: Alaa kulli hall! Iwe mashariki ya ardhi na magharibi yake, hata iwe chembe ya mchanga haitoondoa maana kwamba wewe si mdini.
get the hell out if you are not open to criticism, humu jf tunahojiana kwa hoja, leta hoja mezani kupinga ama kusapoti, kama huwezi baki kuwa msomaji tu.
 
Hayo maandiko Wala hayawahusu wakristo

Hapo Yesu alipokuwa anaongea hayo kulikuwa hakuna mkristo hata mmoja

Yesu amezaliwa amekuta Wana waisrael wanafunga tokea enzi na enzi na ndio anaoongea nao hapo

Na kama hayo mandiko yanakuhu wewe mkristo tuambie wewe unafunga vipi ?

Masaa 12
Masaa 24
Wiki mzima
Mwezi mzima
Siku 40
Hayo maandiko Wala hayawahusu wakristo

Hapo Yesu alipokuwa anaongea hayo kulikuwa hakuna mkristo hata mmoja

Yesu amezaliwa amekuta Wana waisrael wanafunga tokea enzi na enzi na ndio anaoongea nao hapo

Na kama hayo mandiko yanakuhu wewe mkristo tuambie wewe unafunga vipi ?

Masaa 12
Masaa 24
Wiki mzima
Mwezi mzima
Siku 40
Kwahiyo wewe ni mwarabu?kisa unafata utamaduni wa kiarabu
 
Nadhani hakuna taifa lina watu wengi wanaopenda sifa za kipuuzi na kushadadia mambo ya kijinga kama Tanzania
 
Ukiujua uislamu ukiachana na mnavyodanganyana huko na wachungaji feki ni raha sana
Hakuna mchungaji feki wala OG huwa anajishughulisha na uislam,uislam mimi nausoma kila siku,na kadili ninavyoujua ndio nazidi kujua ni jinsi gani ulitokana na nabii feki.
ndio maana unaona watu wengi hata walioenda qatar tu worldcup waliishia kubadili dini maana walichokuwa wanadanganywa na walichokiona tofauti,
Hata mtu kama mike tyson ni muislam wa kubadili,unawezasema alikuwa anaambiwa hivi na vile kuhusu uislam kumne mwenzako alibadili kama fasheni au kama anavyobadili demu mpya😁😁.
Ndio maana unaona bado anaendelea na upandaji na uvunaji wa bangi.
Na sisi waislamu swala tano ni kila siku lazima ndio maana unaona huyo mtangazaji wa kizulu kasifia hapo kwenye kusali huwa hakuna mjadala kwa waislamu hata duka au uende na pesa , fikiria mtu yupo southafrica amenote hivyo vitu
Ndio sababu nikakwambia nyinyi ni wazuri sana katika kufuata uislam na waislam ila kuhusu kumjua Mungu ni weupe tu kama watoto.
Mngekuwa mnamjua Mungu mngekuwa jamii bora sana kuishi nayo maana imeiva ktk pendo na kujikana,ila waaaapi.
Na kuna huyu shaun king kutoka marekani juzi kasilimu baada ya kufanya research kuhusu uislamu kakuta tofauti na ujinga aliodanywa
kuna kichwa kingine kama hukijui kinaitwa andrew tate,nacho ni muendelezk wa wale waislam kisasa ambao fahari kwa waislam kama wewe.

Toa chuki jifunze kuhusu uislamu nakuahidi utaupenda
Sina chuki na uislam,na inawezekana naujua kukuzidi ila tofauti yangu na yako ni kwamba unaamini Muhammad ni mtume wa Mungu.
 
get the hell out if you are not open to criticism, humu jf tunahojiana kwa hoja, leta hoja mezani kupinga ama kusapoti, kama huwezi baki kuwa msomaji tu.
Suala si kubaki kuwa msomoaji au kwamba hatuwezi ku handle criticism, suala wewe ni mdini unayejificha kwa falsafa za kinafki.

Na kwa jinsi ulivyokuwa na nia ovu, watu wameshaanza kupararuana humu kuhusiana na imani zao. Sasa sijui umepata faida gani za kuanzisha uzi kama huu zaidi unaiamsha fitna hali ya kuwa ililala.

Na hata siku moja mtu aliye na moyo safi hawezi kuhangaika na mambo yanayoleta mkanganyiko wa namna hii kwenye jamii. Isipokuwa wale ambao nyoyo zao zina maradhi ndiyo huchagua mambo ya namna hiyo!

Na huo ni uovu.
 
Hiyo siyo sawa kwa jamii yenye watu wa dini tofauti , ila zanzibar wana tamaduni zao kidogo tofauti na huku bara , ndio maana kuna baadhi ya restaurants zipo wazi kuhudumia watu wa dini nyingine na watalii,
Zanzibar ni nchi ya kidini? Ukitoa huo utamaduni?
 
Huyu mtangazaji maarufu southafrica amekuwa muwazi na kuvutiwa na waislamu wanavyotekeleza ibada zao na ni wengi wanavutiwa hata wewe mleta hoja umevutiwa ndio maana umeamua kuja na chuki zako zisizokuwa na msingi.

View attachment 2943090
kwani mkuu huyu ni SI unit ya kivutio? ni perceptions zake NB: No insult to Islam.
 
kwani mkuu huyu ni SI unit ya kivutio? ni perceptions zake NB: No insult to Islam.
WAkristo wengi wa tanzania ukiangalia hata mada zao zimejaa wivu na chuki, ukiangalia humu 90% haipiti siku wasilete mada za kutukana waislamu lakini hukuti muislamu analeta mada za kutukana wakristo
Anafunga mwingine wewe unaumia nini ?
 
Maelezo mengi lakini sijaona namna mnavyofunga kwa kifupi wakristo hawafungi kabisa wanaacha kula chakula kimoja tu kila mtu anachagua chakula chake cha kufunga mwingine anafunga kula choroko, mwingine anafunga kula magimbi, mwingine anakunywa chai bila sukari hapo ndo wanajihesabia wamefunga.
Ivi ukila chakula ukashiba saa 11 kasoro dakika kumi asubuhi unaweza kusema umeshinda na njaa?.

Hahahaa you guys are not serious!.

Sent from my Infinix X6511B using JamiiForums mobile app
 
Embu tuonyeshe mkristo mmoja tu anayefunga hivyo? Mnavyopenda kula tangu lini mkafunga wenyewe mnajijua kama dini imeshawapita pembeni dunia mmeiweka mbele kiufupi 99% ya wakristo hawafungi funga yao ni kula ila usishibe, ndio maana hata hiyo kwaresma haieshimiwi duniani kote kwasababu hawafungi
Hii thread siyo ya afya sana inasababisha mabishano yasiyo na maana lakini kama unategemea kumuona Mkristo aliyefunga utasubiri sana na hata kama yupo anayekutangazia amefunga (ikiwa yupo katikati yako) huyo hajafunga still amekaa na njaa tu kama wengine labda amekosa chakula unatakiwa umpeleke hotel umnunulie chakula ale ashibe huku akisubiri kujifunza kufunga kwa imani.

Biblia imeelekeza kila kitu kuhusu kufunga ktk Ukristo,tena aliyefunga anatakiwa awe na furaha kuliko hata aliyeshiba in short aliyefunga asiwe dhaifu hata aonekane na wengine na awe mnyenyekevu anapokwazwa.

NB;lengo siyo kubishana nimejaribu kufafanua kidogo mada hapo juu.
 
tujadiliane sio conclusive statement, Well kwangu navyoona and i am open to be criticised / kuelimishwa ni kwamba :

Huwa nashangaa sana nikiona baadhi (sio wote) waliofunga ramadan wakilalamika swaumu imetaiti (njaa), nina uhakika hawa wanaolalamika (baadhi) hawawezi kutoboa mfungo wa kikristo.

Funga ya mkristo akila saa moja jioni ni mpaka kesho tena saa moja jioni hakuna kunywa maji wala kula, na hata mle hadharani wala hapagawi au kulalamika mnamuingiza tamaa, yani mtu hajala tangu jana lakini haonyeshi dalili yoyote ya kulegea, ndio maana inakuwa ngumu sana kujua kafunga.

Upande wa pili kufungua saa moja jioni, kabla ya kulala mida ya saa nne flani hivi unatupia tena, haijaishia hapo alarm inategwa saa kumi alfajiri kuwahi kuamka kula daku, ni kama vile ratiba ya lunch inahamia alfajiri na ratiba ya chai kabla ya kulala, cha kushangaza baadhi yao hata wakiona mtu anakula hadharani tayari kuna roho ya kutamani inaingia utasikia wakilalamika "huoni aibu kula hadharani", "unahtuharibia swaumu", n.k. Zanzibar wameenda mbali zaidi ukikutwa unashushiwa kipigo.
Ishu ni kuwa kila zama zina mtume wake na kitabu chenye sheria zake!!

Mungu anasema kuwa tufunge kama walivyofaradhishiwa kufunga waliopita kabla yetu ili tupate kuwa wachamungu. Kusudi la kufunga ni kutuwekea discipline ya kuwa wachamungu...kwa maana ukifunga utaswali na kufanya ibada nyingi za kheri na pia nafsi inanyenyekea kwa mola wake kutokana na kupungua kwa matamanio mwilini.


Kila umati una mtume na kitabu chake! Umati wetu ni umati wa Mtume Muhammmad na kitabu chetu sisi ni Quran , ambayo ina sheria na taratibu zake kiibada. Tumeainishiwa kuwa tufunge pale inapoanza kuingia alfajiri ya kweli mpaka jua litakapozama.

Katika hii ibada ya funga tujizuie kula na kunywa,kufanya jimai na kushugulika na mambo ya kipuuzi katika mchana wa mwezi wa Ramadhan.Ama kwa usiku ni halali kwetu kunywa,kula,kuwaingilia wake zetu mpaka pale alfajiri itakapoingia. Pia ndani ya hii ibada ya funga tumeainishiwa kuwa ni bora zaidi kwa mfungaji kula chakula kinachoitwa Suhoor aka daku maana ni chakula chenye baraka ndani yake kwa yule anayefunga.Suhoor aka Daku ni chakula kinacholiwa muda mchache kabla ya kuanza kwa funga....yaani muda kuanzia saa 9 usiku mpka pale alfajiri ya kweli inapoingia.

Mtume Muhammad (s a.w) ameainisha kuwa umma huu tumepewa hii bonus ya suhoor tofauti na nyumati zilizopita za wana wa israel walikuwa hawajaainishiwa kula daku.

Kikubwa ni kuwa nyumati zote zilizopita ziliwekewa kipindi maalumu cha kutekeleza ibada ya funga aka swaum ila mifumo na utaratibu wa hizi funga zinatofautiana ila lengo kuu ni lile lile ili tuwe wachamungu.

Mtume Muhammad (s.a.w) alisema kuwa bora ya funga aka swaum ni ile aliyokuwa akiifunga Nabii Daud (a.s) ,katika maisha yake daud alikuwa akifunga siku moja na kula siku moja. Leo anafunga ,kesho anakula,kesho kutwa anafunga,siku inayofuata anakula.
 
Mtoa mada usitake funga aliyofaradhishiwa Mtume Muhammad (s.a.w) ifanane na funga waliyofaradhishiwa mitume ya wana wa israel.

Kwani hata ibada za swala ni tofauti, Mtume Mussa a.s alifaradhishiwa vipindi viwili tu vya swala...yaani asubuhi na jioni ila sisi umma wa Muhammad tumefaradhishiwa vipindi vitano kwa siku.

Kila Mtume na kitabu na sheria zake.
 
Mtume Muhammad (s.a.w) alisema kuwa bora ya funga aka swaum ni ile aliyokuwa akiifunga Nabii Daud (a.s) ,katika maisha yake daud alikuwa akifunga siku moja na kula siku moja. Leo anafunga ,kesho anakula,kesho kutwa anafunga,siku inayofuata anakula.
siku = masaa 24
 
Back
Top Bottom