Tukiwa jamii iliyostaarabika, lipi ni kosa kubwa na zito zaidi kwetu kati ya kuua mtu au kuchana kitabu cha dini kama Quran au Biblia?

Tukiwa jamii iliyostaarabika, lipi ni kosa kubwa na zito zaidi kwetu kati ya kuua mtu au kuchana kitabu cha dini kama Quran au Biblia?

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Ukituhumiwa kuua mtu, (au kumnyang'anya mtu haki yake ya kuishi) tunategemea utafikishwa mahakamani na kujibu mashataka ya kosa la kuua. Inawezekana kabisa, hukumu ya kesi yako ikawa ni kuachiwa huru kwa kuwa katika ushahidi uliotolewa ulionyesha labda ulisingiziwa, au uliua kwa kujitetea maisha yako, au uliua katika mazingira tunayoita "upotevu wa akili wa ghafla" au temporary insanity. Hivyo unaachiwa huru kwa kuwa mahakama haijakutia hatiani.

Ukituhumiwa kuchana Biblia au Quran - pia tutategemea ufikishwe mahakamani na kujibu mashitaka ya kuchana Biblia au Quran. Sasa hapa suala la kujiuliza ni kwamba, je inawezekana katika ushahidi kutolewa mahakamani, ikaonekana kuwa hiyo Biblia au Quran hukuchana wewe ila ulisingiziwa, au uliichana katika mazingira tunayoita "upotevu wa akili wa ghafla" au temporary insanity, na ukaachiwa huru kwa kuwa mahakama haijakutia hatiani?

Lakini kwetu sisi kama jamii ya karne ya 21, ni lipi lapaswa kuwa kosa kubwa na jambo zito zaidi - kuua mtu au kuchana Biblia au Quran? Binafsi, naona kwamba kuchana Biblia au Quran ni jambo la kukosa heshima na ustaarabu, lakini hata siku moja siwezi kusema kuua mtu ni jambo la kukosa heshima na ustaarabu.

Kama ni hivyo, kwa nini basi mtu atakaetuhumiwa kukosa heshima na ustaarabu kwa kuchana Biblia au Quran tumchukulie kama ni mbaya zaidi sana kuliko hata yule ambae atakuwa ametuhumiwa kuua (au kumnyang'anya mtu haki yake ya kuishi)?

Je, ni kweli tuna mapenzi sana na Biblia au Quran, vitabu tunavyoona ni vya Mungu, na tunaumizwa sana tukiona vinachanwa kuliko hata kuuawa kwa wanadamu walioumbwa na Mungu? Tuangalie tusije tukaonekana wanafiki mbele za Mungu kwa ajili tu ya umaarufu wa mitaani au kiki za kisiasa!
 
Kuna thread imetoka humu JF kwamba jamaa aliyechana Quran hivi karibuni alirogwa, jambo linaloashiria "mental instability".

Sasa imagine raisi unaenda kuongea mambo mengi kumbe mtu ana tatizo la kichwa. Kwa nini usifanye subira upate angalau taarifa kamili? Huyu mtu anahitaji msaada sio amri za ukali kwa ajili ya kiki za kisiasa.

Usipoangalia siku moja utakuja kutoa amri wagonjwa wa Milembe watiwe ndani kwa kumwaga chakula!
 
Kuna maneno haya nimeyasema mahali baada ya madai kutokeza kwamba kuna mtu amechana Biblia basi Raisi Magufuli amchukulie hatua kali kama yule aliyechana Quran;

"Wakristo huwa hawana mukali na vitu kama hivi na raisi akijua hili wala hawezi kuogopa kukosa kura za Wakristo kwa jambo kama hilo la kutokemea mtu fulani asiye na heshima na ustaarabu kwa kuchana Biblia. Kwa hiyo akijua hawezi kupata kiki ya kisiasa toka kwa Wakristo kwa jambo kama hilo hawezi kusema wala kufanya kitu kuhusu huyo aliechana Biblia.

"Kuwa na uchungu na kitabu badala ya ujumbe ndani ya kitabu kwetu sisi Wakristo ni ibada ya sanamu. Kitabu, hata iwe Biblia, ni wino juu ya karatasi tu, vitu vya kidunia/kimwili. Uichane, uichome, uitemee mate nk haifanyi neno la Mungu likabadlika. Sisi hatuwezi kuwa askari wa Mungu wa kimwili wa kulinda mali zake, na hili la watu kuchana Biblia tutamwachia Mungu mwenyewe tukijua huyo aliechana anaweza kuja kuwa mtumishi mzuri tu wa Mungu. Sisi ni nani hata tumhukumu mtu wa namna hiyo? Kuchana Biblia sio kosa juu ya wanadamu - labda kwa kiasi tu linakuwa kosa kwa mwanadamu kwa kuharibu mali ya mtu aliyoitolea fedha kuinunua. Sasa hilo tutaliona kama mtu kukuchania shati lako.

Watu waliojikita ibada ya sanamu (idol worship) ndio wanathamini kitabu kilichoandikwa neno la Mungu kuliko hata kutii neno la Mungu au ujumbe uliomo ndani ya Biblia, kitu ambacho tunapaswa kuona unafiki wake. Acha wanasiasa wawatumie watu kama hao kwa maslahi yao binafsi.

"Sasa kama kuna watu wanaoona kupigia kelele kuchanwa kitabu cha Mungu kwao ni utumishi uliotukuka kwa Mungu kuliko wao kutii amri za Mungu - acha wawe wafu wanaoendelea kuzika wafu wao."

Ni wazi katika enzi za Wakristo wa kale, watumishi wa Mungu waliponyanyaswa walichaniwa Biblia zao - lakini wapi katika Biblia umeona hilo likifanywa jambo kuu? Lakini ona kwamba ukatili uliofanywa ili kuwaua ndio ulioandikwa ili tujifunze jambo. Kwa hiyo jinsi tunavyowatendea binadamu wenzetu ni jambo kubwa kwa Mungu kuliko kuchana au kuchoma kitu kama Biblia ambayo hata ukichana ngapi bado zitachapishwa nyingine, tofauti na kuua binadamu mwenzako kwa sababu za kisiasa au nyinginezo.
 
Kila mtu anajua kuwa siasa chafu imeshika hatamu katika hili.
 
Back
Top Bottom