Tuko tayari kuacha kazi na kujiajiri. Tupatieni fao la kujitoa

Tuko tayari kuacha kazi na kujiajiri. Tupatieni fao la kujitoa

Viongozi wetu wengi hawana MAONO na wana uwezo mdogo mno kiakili.

Hawajui wewe ukijiajiri baadae unaweza kuajiri vijana wenzako kama kumi na kiwachangia michango yao NSSF..

Yaani wana UONI HAFIFU mno na akili za KIMASKINI MNOOOO eti mtu akichukua pesa zake atasumbua mtaani baadae akizeeka halafu hana kitu. They're shortsighted wanaangalia upande mmoja tu.
...Na wakati Mwingine wanaelewa kabisa ila ROHO MBAYA TU.
 
Upo sahihi Mkuu,
Ila ukitaka kutoka nowadays fursa za kuchukua mkopo hlf unatembea ni msaada mkubwa.
 
At Least You Have Come Up With Something !! Not Like Others Who With Complaints Every Now And Then !!!
 
Katika nchi zetu hizi utumishi ni utumwa mkatae mkubali.
Na viongozi wengi kwenye hivi vyama hasa wa wafanyakazi hawapo kwa maslahi ya wafanyakazi ni vibaraka wa wanasiasa ni mabogaz sijawahi ona ...na kwakweli tusipo badilika tutakuwa watumwa mpaka tutakapo ingia kaburini ...
 
Kumekua na kauli za kubeza watumishi pindi tunapo lalakikia maslahi duni. Wanasiasa wengi na watu binafsi wanekua wakitamka kuwa asiyetaka au anaye ona mshahara haitoshi aache kazi.

Ifahamike kuwa wapo watumishi ambao tuko tayari kuachia nafasi ili na wengine wapate Ajira ili sisi tukajiajiri.

Tatizo ni vile serikali imepokonya Hali ya malipo ya FAO la kujitoa.
Haina haja jambo la kubadili kazi iwe ni kejeli na dhihaka Kwa watumishi. Kazi iwe ni Moja ya haki na uhuru binafsi wa mtumishi. Mtu awe huru kupanga namna ya kutumia muda wake hapa duniania. Mtu apenge ni lini afanye mambo yake kulingana na malengo yake.

Kama Nina wito wa kuzeekea kwenye utumishi niamua mwenyewe. Kama nataka kuwa mkulima baada ya utumishi wa miaka mitano au zaidi niamue.

Sasa tuko tayari kuacha hiyo kazi ili tubadili namna ya kulitumikia taifa Kwa njia mbadala.

Tunaomba pesa zetu huko NSSF ambazo mmezishikilia kama fao la kujitoa.

Huo mshahara wenu tunashukuru Kwa hapa tulipo fika, Sasa tupishe wengine.
Tunaomba hilo fao
Hakuna sababu za kuweka fao la kujitoa bali kupunguza Umri wa kustaafu kuwa miaka 50 au 45 .
 
Viongozi wetu wengi hawana MAONO na wana uwezo mdogo mno kiakili.

Hawajui wewe ukijiajiri baadae unaweza kuajiri vijana wenzako kama kumi na kiwachangia michango yao NSSF..

Yaani wana UONI HAFIFU mno na akili za KIMASKINI MNOOOO eti mtu akichukua pesa zake atasumbua mtaani baadae akizeeka halafu hana kitu. They're shortsighted wanaangalia upande mmoja tu.
Wala hiyo sio sababu bali Mwendazake alipora pesa zote kwenye mifuko Ili kuzuia wanaota kuacha Kazi na obligation ya serikali kuwalipa Chao ndio alikuja na huu ujinga Kwa vile mifuko haina pesa..

Baadae iki stabilise watarudisha tena.
 
Uko sahihi, niliwahi kufanya kazi Serikalini kwa miezi 8 tu ila nilijilaumu sana, kwanza unadumaza akili tu.
Hongera kwa kujikomboa ndugu. Watu wengi ndoto zao zimezimika kisa ajira. Na unadumaa kwelikweli. Mimi nilimwandikia mwajiri wangu resignation letter nilipoenda kwa boss wangu ili aipitishe akaanza kutetemeka nikashangaa. Watumishi wengi akili si zao,we wazia mtu mzima uzabwe makofi na mtu mzima mwenzio na utulie kisa ni bosi wakati zipo code of conduct kama umekosea zinazoelezea ufanywe nini.
 
Duniani kote ipo hivyo,ila huku kwetu ni tatizo kubwa sana.
Wenyewe mlimsikia Profesa akikiri kwa kinywa chake baada ya kuteuliwa kuwa waziri kuwa miaka yote aliyokuwa kwenye utumishi alikuwa jalalani. Ni hatari sana. Nakubaliana nawewe hapa kwetu tatizo ni kubwa.
 
Back
Top Bottom