Tukubabali au tusikubali, Hayati Magufuli alikuwa mkombozi wetu

Tukubabali au tusikubali, Hayati Magufuli alikuwa mkombozi wetu

Daisam

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2016
Posts
2,625
Reaction score
3,141
Ndugu zanguni, hapo nyuma kidogo na sasa kwa uchache baadhi ya watu wamekuwa wakitoa kauli za kubeza kazi nzuri zilizofanywa na JPM kwa kejeli na dhihaka.

Nadhani lengo lao kubwa ni kutaka kufuta Legacy yake. Ukweli ni kwamba, hakuna mtu awaye yote anayeweza kufuta Legacy ya JPM.

Mbaya zaidi ni kwamba,wanapozidi kumbeza JPM na kazi zake ndipo wanapozidi kuumbuka zaidi.
Hapo ni lazima tukubabali kuwa, Mungu yupo upande wa JPM.

Ikumbukwe kwamba:-
1. JPM aliingiza Nchi katika uchumi wa kati katikati ya kipindi cha CORONA, lakini sasa tunaambiwa uchumi umeshuka.

2.Wakati wa JPM, vibaka walitoweka kabisa, lakini sasa wamerudi kwa kasi ya ajabu.

3. Wakati wa JPM, watumishi wa serikali walikuwa na nidhamu na walitekeleza wajibu wao ipasavyo lakini sasa ni balaa tupu. Hata kama ilikuwa nidhamu ya woga kama wanavyosema wengine lakini ilisaidia.

4. Wakati wa JPM, bei za vitu hazijawahi kupanda kiholela holela hivi, lakini sasa kila Mtanzania anajua hali ilivyo huku mtaani. Hali ni mbaya kweli kweli.

5. Wakati wa JPM, Ajali nyingi za kijinga kijinga zilikwisha kabisa lakini sasa zimerudi kwa kasi ya ajabu na kila mtu ni shahidi.

6. Wakati wa JPM, umeme haujawahi kukatikakatika kihuni huni namna hii, lakini sasa kila Mtanzania ni shahidi.

Hayo ni machache tu, yapo mengi mazuri yaliyofanywa na JPM yaliyokuwa msaada kwa Watanzania.

Rai yangu kwa viongozi ni kwamba, fanyeni tathmini ya kina muone mmekosea wapi na mjirekebishe.

Kamwe msihalalishe UDHAIFU wenu kwa kumdhihaki JPM, haitawasaidia isipokuwa mtaharibikiwa zaidi.

Acheni visingizio vya ajabu ajabu, maana sasa kila mnapofeli jambo fulani mnasingizia CORONA kana kwamba CORONA imeanza baada ya JPM kututoka.

Hivi karibuni mmeanza kusingizia vita vya Urusi na Ukraine. Visingizio vingi ni dalili za wazi kabisa za udhaifu wa kiongozi/viongozi.

Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.
 

jibu hoja unakuwa kama wanasiasa.
Kipindi cha corona ndyo tungetegemea maisha yangekuwa magumu sana lakini Magu alidhibiti kila kitu.
Hii ina mahusiano gani na vyombo vya habari
alidhibiti nini mkuu? maana kipindi cha corona, bei ya mafuta kwenye soko la dunia ilishuka mno. makampuni ya utalii karibia yote yalifunga biashara,. alichofanya pekee magu ni kuidharau corona na kuipuuza, hicho ndio kikubwa pekee alichofanya(ingawa kilimcost maisha yake)
 
Vile mwendakuzimu amefurahia uzi wako huu kutokea huko kuzimu😁😁😁
downloadfile-4(1).jpg
 
Kwa hiyo mmekata tamaa baada ya mkombozi wenu kufariki?
Poleni sana.

Pia mkumbuke kuwa, Magufuli huyo huyo kwa watu wengine wengi alikuwa ni muuaji, mkatili, Dikteta, mfilisi na shetani.
Kama JPM alikuwa katili na muuaji, basi angeua karibu hata robo ya Watanzania, yaani Watanzania 15,000,000 au zaidi.
Usione mtu anachapwa viboko ukajikita upande mmoja tu kwamba anaonewa. Jiulize, kwa nini mtu huyo achapwe viboko?
Lakini, kwa nini awe yeye tu na si mtu mwingine?
Tusitumie mihemko kufanya judgement ya mambo nyeti.
 


alidhibiti nini mkuu? maana kipindi cha corona, bei ya mafuta kwenye soko la dunia ilishuka mno. makampuni ya utalii karibia yote yalifunga biashara,. alichofanya pekee magu ni kuidharau corona na kuipuuza, hicho ndio kikubwa pekee alichofanya(ingawa kilimcost maisha yake)
Tuliingia uchumi wa kati katikati ya kipindi cha CORONA na sasa tumeshuka.
 
Kama JPM alikuwa katili na muuaji, basi angeua karibu hata robo ya Watanzania, yaani Watanzania 15,000,000 au zaidi.
Usione mtu anachapwa viboko ukajikita upande mmoja tu kwamba anaonewa. Jiulize, kwa nini mtu huyo achapwe viboko?
Lakini, kwa nini awe yeye tu na si mtu mwingine?
Tusitumie mihemko kufanya judgement ya mambo nyeti.

Unadhani unaongea na watoto nini? Au unadhani ukisema watu wanatumia mihemko ndio itabeba hoja zako?
 
Alikuwa mkombozi wako ww na family yako na watu wako, kwangu mimi alikuwa mnyang'anyi! Alikuwa katili, alikuwa dhulumati! Kwangu mimi na family yangu na ukoo wangu na ndugu na jamaa zangu wote walikuwa waathirika wa magufuli, nili furahi alipolala yooo na ninasema am happy now Mimi na family na ukoo wangu na ndugu zangu na jamaa zangu wote we are so happy now.
 
Back
Top Bottom