Tukumbuke Zamani: Historia ya Taifa letu katika picha

Tukumbuke Zamani: Historia ya Taifa letu katika picha

yaani ni ukweli kuwa vitu vingi vya zamani vilikuwa bora kuanzia elimu,uongozi,tabia za wananchi,madhari ya nchi.......hivi sasa hivi kulikoni,tumerogwa?
 
Kumbukumbu zangu siyo nzuri sana lakini wimbo huu wa Niliruka ukuta ulipigwa kati ya mwaka 1974 na 1975 wakati ambapo vijana Vijana Jazz walikuwa wakutumia mtindo wa Kokakoka. Vile vile Kamata Sukuma ulikuwa wimbo mmojawapo uliotolewa kipindi kile kile pamoja na Niliruka ukuta. Kama niko off, tafadhali niwieni radhi.

Najua kuwa Maneti alikuwa mfipa wa Sumbawanga aliyekulia Tanga; ila nadhani alitokea Morogoro ambako ama alikuwa akipiga na Cuban Marimba au Morogoro Jazz au TK Lumpompo ndipo akajiunga na Vijana Jazz. Kuingia kwake Vijana jazz kuliibadilisha kabisa bendi ile kimapigo na kumwondoa John Ondoro aliyekuwa akiingoza bendi hiyo na aliyepiga wimbo uliokuwa maarufu sana kukaribisha kipindi cha wagonjwa kule RTD.

Maneno yako ni kweli mkuu, lakini "Kamata Sukuma" ulikuwa mtindo wa kwanza wa Maneti alipoingia Vijana ni kweli alitokea Morogoro kwa sababu ninakumbuka wimbo wake mwingine wa pili katika hiyo "Kamata Sukuma" aliuimba Kuluguru, wa "Kalulu libweze dizojogolo dyangu" hata ule wimbo wa Bujumbura nao aliuimba kwa lugha hiyo hiyo ya Kiluguru,

Mtiondo wa Koka Koka, alianza alipotoa albamu ya pili, ambayo ilikuwa na wimbo wake maarufu wa "Operetion Maduka", otherwise mengine yote yako sawa na heshima mbele mkuuu.
 
Maneno yako ni kweli mkuu, lakini "Kamata Sukuma" ulikuwa mtindo wa kwanza wa Maneti alipoingia Vijana ni kweli alitokea Morogoro kwa sababu ninakumbuka wimbo wake mwingine wa pili katika hiyo "Kamata Sukuma" aliuimba Kuluguru, wa "Kalulu libweze dizojogolo dyangu" hata ule wimbo wa Bujumbura nao aliuimba kwa lugha hiyo hiyo ya Kiluguru,

Mtiondo wa Koka Koka, alianza alipotoa albamu ya pili, ambayo ilikuwa na wimbo wake maarufu wa "Operetion Maduka", otherwise mengine yote yako sawa na heshima mbele mkuuu.

Mkulu wewe mwisho.... hats off!
 
wakubwa,nakumbuka miaka ya nyuma kidogo,niliona katika magazine either Africa now au africa events, picha mbili za waanzilishi wa TANU.if my memory haijakosea the person in question was KASSELA BANTU (i stand to be corrected).kassela bantu was a founding member of tanu lakini katika hii picha hakuwepo.years later picha hiyo hiyo resurfaced,kassela bantu akiwemo,in other words hii picha mpya was doctored.mjadala ulikuwa who done it,TANU au YEYE,ANYONE REMEMBERS THIS?
 
son-of-alaska said:
wakubwa,nakumbuka miaka ya nyuma kidogo,niliona katika magazine either Africa now au africa events, picha mbili za waanzilishi wa TANU.if my memory haijakosea the person in question was KASSELA BANTU (i stand to be corrected).kassela bantu was a founding member of tanu lakini katika hii picha hakuwepo.years later picha hiyo hiyo resurfaced,kassela bantu akiwemo,in other words hii picha mpya was doctored.mjadala ulikuwa who done it,TANU au YEYE,ANYONE REMEMBERS THIS?


son-of-alaska,

..nadhani jarida unalolizungumzia ni Africa Events.

..jarida hilo ndiyo lilinifungua macho kuhusu mauaji yaliyotokea Zanzibar. pia walitoa story ya Gamal Abdel Nassar kumzidi kete jamaa aliyeitwa Mohamed Naguib ktk mapinduzi ya Egypt.

..Africa Now lilikuwa more alliagned na west africans.

..nadhani kuna watu ndani ya TANU/CCM walikuwa wakifanya huo utoto unaozungumzia.

..historia yetu haswa ya harakati za kupigania Uhuru imepotoshwa kwa kiasi fulani.

..sasa kuna ambao wamejitwika jukumu la kuirekebisha, lakini nao wana ajenda zao za ajabu-ajabu. yaani hata sijui tunaelekea wapi.
 
Na. Mohammed Said

Mwaka wa 1951 wakati Dossa na wenzake wapo katika juhudi za kuipa uhai mpya TAA Dossa aliandikiwa barua na V.M. Nazerali aliyekuwa mjumbe wa Baraza la Kutunga Sheria akimuomba Dossa aunge mkono juhudi zake na za Ivor Byaldon na Brig. Scupham za kutaka kuunda chama cha siasa kitachowashirikisha watu wa rangi zote. Bayldon na Brig. Scupham walikuwa kama alivyokuwa Nazerali, wajumbe wa Baraza la Kutunga Sheria.

Wanasiasa wengine walioombwa kuunga mkono juhudi hizi walikuwa Chifu Kidaha Makwaia, Liwali Yustino Mponda wa Newala, Dr. Joseph Mutahangarwa, Chifu Abdieli Shangali wa Machame, Chifu Thomas Marealle wa Marangu, Chifu Adam Sapi Mkwawa, Chifu Harun Msabila Lugusha, Dr. William Mwanjisi, Abdulkarim Karimjee, Dr. Vedas Kyaruzi, Liwali Juma Mwindadi, H.K.Viran, Stephen Mhando, Ally Sykes na Abdulwahid Sykes. Dossa na wenzake waliikataa ghilba hii kwa kuwa lengo lao lilikuwa ni kuanzisha chama cha siasa cha Waafrika wa Tanganyika kwa minajili ya kudai uhuru.

Mwalimu Nyerere alipofika Dar es Salaam kwa mara ya kwanza mwaka wa 1952 kama mwalimu wa shule ya St. Francis' College, Pugu hakuna mtu aliyekuwa anamjua au kupata kusikia habari zake katika ulingo wa siasa. Kassela Bantu ambaye alikuwa akijuana na Nyerere kwa siku nyingi alimchukua Nyerere kwa Abdulwahid Sykes kumtambulisha. Wakati ule Abdulwahid alikuwa Rais wa TAA. Nyerere mara moja akajiunga na baraza la siasa lililokuwa likifanyika Mtaa wa Mbaruku nyumbani kwa Dossa. Ikawa kila Jumapili Nyerere anakuja kutoka Pugu kuja kumtembelea Dossa.

Ilikuwa katika baraza hii ndipo Nyerere alipokutana na wanasiasa wengi wa wakati ule kama Ramadhani Mashado Plantan aliyekuwa anamiliki gazeti lililokuwa likijulikana kama Zuhra, John Rupia, Dunstan Omari, Zuberi Mtemvu na wanasiasa wengine. Fikra za Nyerere za kudai uhuru zilisikika kwa mara ya kwanza kupitia kalamu ya Mashado Plantan na gazeti lake la Zuhra lililokuwa likitoka kila siku ya Ijumaa. Fikra za Nyerere ziliingiza msisimko mpya katika baraza lile na haukuchukua muda mwaka 1953 uongozi wa ndani ukampendekeza agombee urais wa TAA.

Dossa anasema ingawa wao kwa kuwa karibu na Nyerere walikuwa wamekiona kipaji chake cha uongozi, wanachama wengi hawakumkubali mara moja na ndiyo maana katika uchaguzi wa TAA uliofanyika Arnautouglo Hall tarehe 17 Aprili, 1953 kati ya Abdulwahid aliyekuwa Rais na Nyerere aliyekuwa anagombea dhidi yake, Nyerere alishinda uchaguzi ule kwa taabu sana. Haukupita muda chama kikaanza kuzorota na mwisho kikafa. Dossa anakumbuka kuwa yeye alikuwa anawapitia viongozi kwenda kwenye mkutano. Akipiga honi ili mtu atoke waende mkutanoni kiongozi alimtuma mkewe atoke nje na aseme kuwa hakuwepo nyumbani.

Dossa anasema ilikuwa baada ya kushauriana na Abdulwahid, Makamu Rais wa TAA ndipo lilipokuja wazo kuwa ni lazima wapate nguvu ya wazee wa Dar es Salaam ili kukifufua chama.Hivi ndivyo TAA katika miaka ya mwisho ya uhai wake ilipokuja kupata kuungwa mkono na wazee wa Dar es Salaam na kupelekea kuundwa kwa Baraza la Wazee wa TANU mwaka 1955 chini ya mwenyekiti wake Sheikh Suleiman Takadir. Nyerere amepata kusema kuwa alikuwa Dossa ndiye aliyemfahamisha aache kuvaa kaptula kwa kuwa sasa atakuwa akitoka mbele ya watu wazima na hiyo si adabu nzuri.

Dossa alikuwa kati ya wale wazalendo watano, Abdulwahid Sykes, Ally Sykes, John Rupia na Julius Nyerere waliokutana ndani ya ofisi ya TAA new Street (sasa Lumumba Street) katika miezi ya mwisho ya 1953 na kwa pamoja wakapitisha azimio la siri la kuibadili TAA kuwa chama cha wazi cha siasa na kukipa chama hicho jukumu la kuiongoza Tanganyika katika kudai uhuru wake. Hili ndilo lililokuwa azimio la kwanza la busara katika historia ya Tanganyika. Azimio la pili la busara ni lile la Tabora la mwaka 1958.

Tarehe 7 Julai, 1954 wazalendo hawa wafuatao wakakutana Dar es Salaam kubadili Katiba ya TAA ili kuanzisha chama cha TANU: Dossa Aziz, Abdulwahid na Ally Sykes, Tewa Said Tewa, Patrick Kunambi, Kasella Bantu, John Rupia, Julius Nyerere, C.O. Millinga,Germano Pacha, Joseph Kimalando, Japhet Kirilo; Abubakar Ilanga, L.M.Bugohe, Saadan Abdu Kandoro, S.M. Kitwana na L.M. Makaranga. Dossa Aziz kadi yake ya TANU ni namba 4 iliyotolewa na kusainiwa na Ally Sykes.

Haukupita muda mrefu TANU ikampeleka Nyerere Umoja wa Mataifa. Tarehe 17 Februari, 1955 Nyerere aliondoka Dar es Salaam na kwenda New York kuhutubia Baraza la Udhamini la Umoja wa Mataifa na ndani ya mkoba wake hakuwa na hotuba nyingine ila yale mapendekezo aliyopewa Gavana Edward Twinning mwaka wa 1950 na uongozi wa TAA.Nyerere aliporudi nchini alikuta umati mkubwa wa wananchi unamsubiri uwanja wa ndege. Haikuwezekana kwake kutoka nje ya uwanja jinsi umati wa watu ulivyojazana kumlaki.. Walinzi wa kikoloni walimruhusu Dossa aingize gari yake hadi chini ya mlango wa ndege. Nyerere akashuka na kupokelewa na swahiba wake Dossa na akaingia ndani ya gari la Dossa.
 
...ama kweli, tukigeuka nyuma twaweza geuka mawe...🙁 machifu wetu hao Usukumani, circa 1900 wakiwa mbele ya "IKULU" zao, na wazee wao wa baraza a.k.a Cabinet!

attachment.php

Chief KIKANGA wa Bukumbi

attachment.php

Chief MASUKA wa Mwanza


attachment.php

Prince MAZUNGU wa Bukumbi, na mkewe.
 
Kichuguu,

..picha ya Nyerere na Bibi Titi nadhani ilikuwa miaka ya 80 wakati Mwalimu anatangaza vita dhidi ya wahujumu uchumi.

..nyuma ya Mwalimu anaonekana Mzee Aboud Jumbe, pamoja na mpambe wa Mwalimu Major.Makwaia.
 
Na. Mohammed Said

Mwaka wa 1951 wakati Dossa na wenzake wapo katika juhudi za kuipa uhai mpya TAA Dossa aliandikiwa barua na V.M. Nazerali aliyekuwa mjumbe wa Baraza la Kutunga Sheria akimuomba Dossa aunge mkono juhudi zake na za Ivor Byaldon na Brig. Scupham za kutaka kuunda chama cha siasa kitachowashirikisha watu wa rangi zote. Bayldon na Brig. Scupham walikuwa kama alivyokuwa Nazerali, wajumbe wa Baraza la Kutunga Sheria.

Wanasiasa wengine walioombwa kuunga mkono juhudi hizi walikuwa Chifu Kidaha Makwaia, Liwali Yustino Mponda wa Newala, Dr. Joseph Mutahangarwa, Chifu Abdieli Shangali wa Machame, Chifu Thomas Marealle wa Marangu, Chifu Adam Sapi Mkwawa, Chifu Harun Msabila Lugusha, Dr. William Mwanjisi, Abdulkarim Karimjee, Dr. Vedas Kyaruzi, Liwali Juma Mwindadi, H.K.Viran, Stephen Mhando, Ally Sykes na Abdulwahid Sykes. Dossa na wenzake waliikataa ghilba hii kwa kuwa lengo lao lilikuwa ni kuanzisha chama cha siasa cha Waafrika wa Tanganyika kwa minajili ya kudai uhuru.

Mwalimu Nyerere alipofika Dar es Salaam kwa mara ya kwanza mwaka wa 1952 kama mwalimu wa shule ya St. Francis' College, Pugu hakuna mtu aliyekuwa anamjua au kupata kusikia habari zake katika ulingo wa siasa. Kassela Bantu ambaye alikuwa akijuana na Nyerere kwa siku nyingi alimchukua Nyerere kwa Abdulwahid Sykes kumtambulisha. Wakati ule Abdulwahid alikuwa Rais wa TAA. Nyerere mara moja akajiunga na baraza la siasa lililokuwa likifanyika Mtaa wa Mbaruku nyumbani kwa Dossa. Ikawa kila Jumapili Nyerere anakuja kutoka Pugu kuja kumtembelea Dossa.

Ilikuwa katika baraza hii ndipo Nyerere alipokutana na wanasiasa wengi wa wakati ule kama Ramadhani Mashado Plantan aliyekuwa anamiliki gazeti lililokuwa likijulikana kama Zuhra, John Rupia, Dunstan Omari, Zuberi Mtemvu na wanasiasa wengine. Fikra za Nyerere za kudai uhuru zilisikika kwa mara ya kwanza kupitia kalamu ya Mashado Plantan na gazeti lake la Zuhra lililokuwa likitoka kila siku ya Ijumaa. Fikra za Nyerere ziliingiza msisimko mpya katika baraza lile na haukuchukua muda mwaka 1953 uongozi wa ndani ukampendekeza agombee urais wa TAA.

Dossa anasema ingawa wao kwa kuwa karibu na Nyerere walikuwa wamekiona kipaji chake cha uongozi, wanachama wengi hawakumkubali mara moja na ndiyo maana katika uchaguzi wa TAA uliofanyika Arnautouglo Hall tarehe 17 Aprili, 1953 kati ya Abdulwahid aliyekuwa Rais na Nyerere aliyekuwa anagombea dhidi yake, Nyerere alishinda uchaguzi ule kwa taabu sana. Haukupita muda chama kikaanza kuzorota na mwisho kikafa. Dossa anakumbuka kuwa yeye alikuwa anawapitia viongozi kwenda kwenye mkutano. Akipiga honi ili mtu atoke waende mkutanoni kiongozi alimtuma mkewe atoke nje na aseme kuwa hakuwepo nyumbani.

Dossa anasema ilikuwa baada ya kushauriana na Abdulwahid, Makamu Rais wa TAA ndipo lilipokuja wazo kuwa ni lazima wapate nguvu ya wazee wa Dar es Salaam ili kukifufua chama.Hivi ndivyo TAA katika miaka ya mwisho ya uhai wake ilipokuja kupata kuungwa mkono na wazee wa Dar es Salaam na kupelekea kuundwa kwa Baraza la Wazee wa TANU mwaka 1955 chini ya mwenyekiti wake Sheikh Suleiman Takadir. Nyerere amepata kusema kuwa alikuwa Dossa ndiye aliyemfahamisha aache kuvaa kaptula kwa kuwa sasa atakuwa akitoka mbele ya watu wazima na hiyo si adabu nzuri.

Dossa alikuwa kati ya wale wazalendo watano, Abdulwahid Sykes, Ally Sykes, John Rupia na Julius Nyerere waliokutana ndani ya ofisi ya TAA new Street (sasa Lumumba Street) katika miezi ya mwisho ya 1953 na kwa pamoja wakapitisha azimio la siri la kuibadili TAA kuwa chama cha wazi cha siasa na kukipa chama hicho jukumu la kuiongoza Tanganyika katika kudai uhuru wake. Hili ndilo lililokuwa azimio la kwanza la busara katika historia ya Tanganyika. Azimio la pili la busara ni lile la Tabora la mwaka 1958.

Tarehe 7 Julai, 1954 wazalendo hawa wafuatao wakakutana Dar es Salaam kubadili Katiba ya TAA ili kuanzisha chama cha TANU: Dossa Aziz, Abdulwahid na Ally Sykes, Tewa Said Tewa, Patrick Kunambi, Kasella Bantu, John Rupia, Julius Nyerere, C.O. Millinga,Germano Pacha, Joseph Kimalando, Japhet Kirilo; Abubakar Ilanga, L.M.Bugohe, Saadan Abdu Kandoro, S.M. Kitwana na L.M. Makaranga. Dossa Aziz kadi yake ya TANU ni namba 4 iliyotolewa na kusainiwa na Ally Sykes.

Haukupita muda mrefu TANU ikampeleka Nyerere Umoja wa Mataifa. Tarehe 17 Februari, 1955 Nyerere aliondoka Dar es Salaam na kwenda New York kuhutubia Baraza la Udhamini la Umoja wa Mataifa na ndani ya mkoba wake hakuwa na hotuba nyingine ila yale mapendekezo aliyopewa Gavana Edward Twinning mwaka wa 1950 na uongozi wa TAA.Nyerere aliporudi nchini alikuta umati mkubwa wa wananchi unamsubiri uwanja wa ndege. Haikuwezekana kwake kutoka nje ya uwanja jinsi umati wa watu ulivyojazana kumlaki.. Walinzi wa kikoloni walimruhusu Dossa aingize gari yake hadi chini ya mlango wa ndege. Nyerere akashuka na kupokelewa na swahiba wake Dossa na akaingia ndani ya gari la Dossa.
Mkuu Jasusi,

Heshima mbele, hii saafi sana unajua mkuu nilikuwa ninapita pita huko masehemu ninakuta kazi zako nzito sana kuhusu Mwalimu na siasa yetu bongo kwa ujumla, ukwieza mkuu tumwagie hapa naona uliziandika zamani kidogo.

Heshima mbele!
 
Je kuna anayekumbuka kuwa ule wimbo wa "Ooh TANU yajenga nchi!!," ambao ulisambaa mpaka Kenya kukawa na "Ooh KANU yajenga nchi," na re-make yake ya " CHAMA chetu cha Mapinduzi Chajenga nchi" ulitokana na wimbo wa "Ooh Sasi jabela mitwe" uliotungwa na mtemi Mirambo ukimaanisha kuwa risasi ya askari wake imevunja vichwa vya maadui?

Mtemi Mirambo alituachia pia neno "Ikulu" ambalo lilikuwa na maana ya nyumba yake kubwa ya kitemi. Watu wengine hudhani kuwa watemi hawa walikuwa tofauti sana na sisi. Hapana walikuwa ni watu wa kawaida kama sisi ila walijali sana wajibu wao kama viongozi wa raia wao kuliko interest zao binafsi kama ilivyo kwa viongozi wetu wa siku hizi. Hebu angalia Mtemi Mirambo alivyokuwa, ni kijana kabisa kuliko hata Rais wetu wa sasa hivi.

attachment.php
 

Attachments

  • Mirambo.jpg
    Mirambo.jpg
    35 KB · Views: 394
Nimshukuru FMES kwa jinsi anavyoi-direct thread hii. Waanzishaji wengine wa thread muige mfano huu. Hii imetulia na haijayumba hata kidogo, matusi, kejeli, dharau, umbea, udaku havina nafasi hata kidogo.
 
Mkuu Jasusi,

Heshima mbele, hii saafi sana unajua mkuu nilikuwa ninapita pita huko masehemu ninakuta kazi zako nzito sana kuhusu Mwalimu na siasa yetu bongo kwa ujumla, ukwieza mkuu tumwagie hapa naona uliziandika zamani kidogo.

Heshima mbele!


Hebu niambie na mimi niwe napita huko kwa vile najua kuwa Jasusi huyu ana siri nyingi kutokana ujasusi wake na kama wazee walivyotufundisha: Fuata nyuki ule asali, usifuate nyuki wakuume. Nitaka asali.
 
Huwa inatia uchungu sana kuona mambo yote mazuri tuliyokuwa nayo zamani sasa hivi ni historia. Taa za barabarani (street lights), mitaa iliyopangiliwa vizuri, barabara nzuri za mitaani, pale Chuo Kikuu Mlimani palikuwa kama peponi, wanafunzi walisoma kwa raha sana! Leo hii ukimwambia mwanafunzi wa UDSM kwamba pale Cafeteria kulikuwa na viji-fridge vinavyotoa maziwa 24/7 hatakuamini kabisa....kwani yeye hata maji ya kunywa sasa hivi ananunua!

Ila hayo mabasi yameniumiza roho sana! Ukiviona vipanya vya Dar vilivyojichokea hutaamini kama Dar pamewahi kuwa na usafiri mzuri kiasi hicho! Something must be wrong somewhere for sure!

usinitie uchungu mtu wangu maana nikikumbuka adha ya kipanya,mhh maana ebu fikiri mimi ni mrefu wa mita1.94 na hiki kipanya kina urefu wa mita 1.20 ebu fikiria tu ninaposimama ndani inakuwaje halafu safari yenyewe ni k koo to kimara sasa hivi nina maradhi yasiyo ya lazima ya kupinda mgongo.
 
Mkuu Kichuguu, heshima mbele hii nimeikuta mahali under mkulu Jasusi, imetulia sana:-

Tanzania Election 95: 29 August 1995

Ndugu zangu wote katika ,URAIS NA HATIMA YA TAIFA

Mojawapo ya mambo ambayo nchi hii itayarithi kutoka kwa uongozi wa Rais Ali Hassan Mwinyi ni kushuka kwa viwango vya utendaji na ufanisi wa ofisi hiyo iliyo kuu kuliko zote katika nchi. Kwa kuwa Ali Hassan Mwinyi ameweza kila mtu anajiona kuwa ataweza.

Enzi za Rais Julius K. Nyerere si wengi walidhani wanaweza. Maana wengi wa hao wanaojitokeza sasa walikuwapo tangu enzi hizo na hawakuthubutu kujitokeza. Kujitokeza kugombea ni kuimarika kwa democrasia. Watu watapata fursa pana zaidi ya kuchagua mtu, siyo kwa sababu wengine hawapo bali kwa sababu miongoni mwa waliojitokeza watamwona anafaa.

Lakini hao wanaojitokeza wamejipima kwa vigezo gani hata wakaona wanafaa kuwa marais wa nchi hii? Maana tunaambiwa wamo hata wale ambao walishiriki katika kuvunja katiba waliyoapishwa kuilinda. Wamo hata walioshindwa katika nyadhifa nyingine hata ikabidi waondolewe au walazimishwe kujiuzulu. Wamo pia hata wale ambao imethibitika kuwa wamechangia katika kulipotezea taifa mapato ya kodi. Baada ya hayo yote sasa wanataka urais!

Ni kweli kuwa mfumo uliokuwapo ulikuwa wa "mizengwe" kama anavyokiri Mwalimu mwenyewe. Lakini ni lazima pia tukiri kuwa viwango vya utendaji wa ofisi hiyo vilikuwa vya juu mno kulinganisha na majukumu yaliyoikabili.

Majukumu hayo ni kama vile kupigania uhuru, kujenga taifa kutokana na mkusanyiko wa makabila, kulipa "identity" na mwelekeo taifa hilo, kujenga na kudumisha amani na utulivu, kupambana na ukoloni mamboleo na ujinga, kuleta haki na usawa, kushiriki katika kuendeleza ukombozi wa Afrika, kupambana katika vita baridi na kadhalika.

Labda athari nyingine ya utawala wa rais Mwinyi ni kwa Mwalimu Nyerere mwenyewe. Kushusha viwango vya sifa za urais wa Tanzania. Kwa maana ya kuwa Mwalimu anamwona rais ajaye kama mziba nyufa na wala siyo mjenzi wa nyumba.

ANATETEA MASLAHI YA NANI?
Ni kweli kuwa 'nyumba' yetu haiwezi kuendelea kujengwa kabla nyufa zilizojitokeza hazijazibwa. Lakini kazi ya kuziba nyufa ni kazi ndogo sana katika jumla ya majukumu ya rais. Kwa hiyo, kwa maoni yangu, kuziba nyufa alizozitaja Mwalimu ni sifa za msingi tu za kiongozi au hata mrasimu wa ngazi yoyote katika nchi.

Nadhani rais wa nchi iwayo yoyote lazima awe na zaidi ya sifa za "mshona viraka." Lazima aweze kusanifu na kushona mavazi wanayoyataka wateja wake. Yaani, lazima aweze kubainisha walimpigia kura, abainishe matakwa yao na abuni siasa na mikakati ya kutekeleza siasa hiyo. Kisha aitekeleze siasa hiyo kwa ari na uwezo wake wote.

Alipokuwa Rais, Mwalimu Nyerere alibainisha constituency yake ya kuwa wakulima na wafanyikazi. Siasa zake zililenga katika kuwanufaisha hao. Walau ndivyo alivyosema. Yawezekana matokeo ya utekelezaji wa siasa hiyo hayakuwanufaisha walengwa kwa namna alivyokusudia. Lakini hakuna ushahidi kuwa alikusudia kutenda kinyume cha hivyo alivyosema.

Nimesoma maoni ya kila mgombea aliyehojiwa katika RAI. Hakuna hata mgombea mmoja ambaye ameeleza anataka kutetea matakwa ya nani. Yawezekana kuhoji kuwa hawataji watawakilisha matakwa ya nani kama mbinu ya kisiasa ya kutotaka kuwabagua baadhi ya watu wanaowatarajia wawapigie kura.

Lakini kueleza wanasimamia matakwa ya nani ni jambo la msingi sana kwa sababu tatu. Sababu ya kwanza ni kuwa kauli kama hiyo itatusaidia kulinganisha maneno na matendo yao ya siku za nyuma na ya sasa. Kwani tunaambiwa wapo wanaoungwa mkono na mataifa makubwa ya nje. Tunaambiwa pia kuwa wapo wanaofanya kampeni kwa kutumia mapesa ya Waajemi (Iran.)

Tunaambiwa wapo wanaofanya kampeni kwa mapesa ya mabepari wenye asili ya Kiasia wa humu humu nchini. Tunaambiwa wapo wanaofanya kampeni kwa mapesa ya mabepari "wazawa." Tunaambiwa wapo wanaofanya kampeni kwa mapesa ya mabepari wenye asili ya Kiasia kutoka Kenya. Je, matakwa ya hao wanaotoa mapesa hayo ni sawa na matakwa ya wakulima wa Serengeti?

Sababu ya pili ni kuwa baada ya miaka mitano, au hata kabla, tutahitaji vigezo vya kutusaidia kuwahukumu hao tutakaokuwa tumewachagua. Je, matakwa watakayokuwa wameyawakilisha ni hayo hayo waliyosema watayawakilisha? Ikibidi yafaa watu wapate fursa ya kumuondoa madarakani kwa taratibu nzuri za kidemokrasia kiongozi atakayethibitika kuwa amekwenda kinyume na matakwa yao.

Kitendo cha kukataa kusema wanataka kuwakilisha matakwa ya nani ni sawa na kukataa kujiwekea malengo, au hawana kabisa malengo? Ni sawa na kusema na kukataa kujiwekea vigezo vya kujipima. Ni sawa na kusema kuwa watang'ang'ania madaraka hata ikithibitika kuwa hawafai, kama ilivyoonekana katika uongozi unaomaliza muda wake. Ni sawa na kukaribisha uwezekano wa wao kuondolewa madarakani kwa njia zisizo za kidemokrasia.

Sababu ya tatu inatokana na hali ya kisiasa nchini. Katika kipindi cha uongozi wa rais Mwinyi, hasa katika miaka mitano ya mwisho, matakwa ya mabepari wa kimataifa yalizingatiwa mno hata pale ambapo yaliathiri matakwa ya wananchi kwa nchi hii. Siyo siri kuwa ubinafsishaji, kadri unavyotekelezwa sasa, umewanyang'anya wananchi mali yao na kuikabidhi mikononi mwa wageni.

Siyo siri kuwa pale wanaponufaika wananchi imekuwa siyo katika umoja wao bali mmoja mmoja. Wengi wa hao mmoja mmoja wamekuwa ni wale ambao ni wachuuzi na siyo wazalishaji. Tena wengi wa hao walionufaika wamekuwa ni wenye asili ya Kiasia. Kwa hiyo sambamba na matakwa ya mabepari wa nje, yamezingatiwa sana matakwa ya kundi moja la mabepari wa ndani.

Siyo siri kuwa siasa ya "soko huria" kadri inavyotekelezwa sasa imeligeuza taifa kuwa jaa la kina aina ya bidhaa hata zile zilizooza na zenye madhara ya kiafya kwa watumiaji. Hili limesababisha uzalishaji wa humu nchini kufa kabisa. Lakini yapasa tujiulize: Hao wanaotuuzia bidhaa zao tunawalipa na nini? Tutaendelea kuwalipa na nini? Hao wanaotaka kuwa viongozi wetu wanalo jibu?

Matokeo ya ubinafishaji wa soko huria ni ukosefu wa ajira, kupunguzwa kwa maendeleo ya vijijini kulikozua "umachinga," kulitumbukiza taifa na watu wake katika umaskini uliokithiri, na kuzua itikadi na dhana za kibaguzi kama "wazawa" na "magabacholi" zinazoweza kuliangamiza taifa.

Binafsi siamini hayo ndiyo matakwa ya wananchi wa nchi hii. Kutobainisha ni matakwa ya nani wagombea wetu wanataka kuyasimamia ni sawa na kusema kuwa mambo kadri yalivyo sasa ndiyo murua na kwamba wataendelea kusimamia matakwa yanayosimamiwa na uongozi wa sasa. Hii ni kusema kuwa wanadhamiria kuendelea kuliangamiza taifa.

Kutokana na urithi wa democrasia ya chama kimoja na itikadi ya CCM yawezekana baadhi ya hao wagombea wakahoji kuwa watasimamia matakwa ya kitaifa. Hii itakuwa ni kudanganya kwa sababu mbili. Sababu ya kwanza ni kuwa hakuna matakwa ya kitaifa. Kila tabaka lina matakwa yake. Na tutake tusitake viongozi huwakilisha matakwa ya tabaka hili au lile.

Matakwa ya mkulima wa pamba hayawezi kuwa sawa na matakwa ya mchuuzi wa pamba. Hili linajulikana wazi. Wakulima wa wilaya ya Serengeti kwa mfano, wanajua kuwa wachuuzi wa pamba ambao sasa wamejivisha ngozi ya kondoo na kujiita wakombozi wa wakulima hawawakilishi matakwa yao. Kwa kujua hivyo wachuuzi hao sasa wanatumia itikadi ya ukabila kujihalalisha.

Sababu ya pili ni kuwa siasa haiendeshwi kwa makubaliano. Serikali ni mkondo mmoja tu wa dola ambayo jukumu lake ni kusimamia matakwa ya tabaka moja dhidi ya matakwa ya matabaka mengine. Hii ndiyo sababu tunadai kujua wanaogombea urais na hata ubunge wanawakilisha matakwa ya nani.

NI ITIKADI AU USOKWE MTU?
Nadhani hata leo ukimwuliza Mwalimu Nyerere atakuambia kuwa yeyeni mjamaa. Sio wengi watakaokataa. Watakaoafiki watafanya hivyo siyo kwa sababu yeye hujiita hivyo. Bali ni kwa sababu ya kauli pamoja na matendo yake. Historia imempiga mhuri huo.

Lakini siasa ya ujamaa haikunyesha kama mvua. Wala Mwalimu hakuipata katika ndoto. Mwalimu siyo ujamaa na ujamaa siyo Mwalimu. Ujamaa ni siasa iliyoibuka na kuhalalishwa na mazingira maalumu ya kisiasa. Kwa kifupi mazingira hayo yalikuwa yale ya taifa lililokuwa linaibuka kutoka katika ukoloni na ambalo lilikuwa linahangaika kutafuta mwelekeo na identity yake isiyofungamana na ubepari wala ukomunisti.

Karl Marx alipata kuulizwa kama yeye ni mfuasi wa itikadi ya Ki-Marx. Akajibu akasema:"Nashukuru Mungu Siyo." Asingeweza kuwa mfuasi wa siasa ya ki-marx kwa kuwa yeye ndiye Marx. La ajabu ni kuwa wagombea wetu wa urais wanaona fahari kujibandika lebo.

Horace Kolimba anajiita "social democrat." Edwin Mtei anajiita "liberal democrat." Kwanza hizi si itikadi zao. Ni mikondo mbalimbali tu ya itikadi za kibepari. Wanaweza kuhoji. Ah! kwani kuafikiana na itikadi fulani ni dhambi? La hasha. Ni halali kabisa.

Lakini walipaswa wazijue na waweze kuzieleza na kuzitetea. Wajue historia yake na zinasimamia nini kwa sasa. Kwa maelezo yao wenyewe ambayo hatuna haja ya kuyarejea hapa, ni dhahiri kuwa hawazielewi. Kwa hiyo wanachofanya Horace Kolimba na Edwin Mtei ni usokwe mtu tu: kuiga hata jambo wasilolijua. Nukta.

Nafasi haitaruhusu kufafanua historia ya mikondo hiyo ya itikadi za kibepari. Inatosheleza tu kueleza kuwa social democrat ni itikadi iliyoibuka kulitaka tabaka la mapebari kulitupilia makombo kidogo tabaka la wafanyikazi katika nchi zenye viwanda katika nyakati ambapo matabaka hayo yalikuwa yakikinzana vikali.

Vyama vinavyojulikana kama "conservative" ni panya wa kuuma. Wakati vyama vinavyojulikana kama social democratic panya wa kupulizia, kulipunguzia makali ya kunyonywa tabaka la wafanyikazi.

Lakini vyote vinatumikia mfumo ule ule, tena kwa uaminifu mkubwa. Kwani ikibidi huungana kuwakandamiza wafanyikazi, hasa mfumo huo unapopata mtikisiko. Mara kadhaa huko Ujerumani vyama hivi vimeungana kwa nia tu ya kuzuia vyama vingine, hasa vyenye kuhoji mfumo wa ubepari, kuchukua madaraka.

Liberal Democrat ni itikadi ilyoibuka kama wasuluhishi au wasawazishaji wa 'ugomvi' baina ya conservative na social democrat. Wao huchukua msimamo wa kati. Hawa ni ndumiakuwili wa kwelikweli kama ilivyojidhihirisha huko Ujerumani. Hujiunga na kila anayekuwa madarakani.

Kolimba na Mtei walipaswa watuambie kama mazingira hayo yapo hapa kwetu. Kila mtu anajua kuwa hayapo. Kwa hiyo lebo walizojibandika zinadhihirisha ni kiasi gani walivyo mufilisi wa itikadi. Hawawezi kubuni itikadi zao ila kujibandikiza za wenzao.

Pengine wamenunuliwa au wanataka kujipendekeza kwa wakubwa. Lakini wakubwa hao hao ndiyo wetu ajae anatakiwa kulumbana nao kuhusu uwiano mbaya wa biashara duniani, uchafuzi wa mazingira, mgawanyo usio wa haki wa maarifa hasa ya sayansi na teknolojia, umaskini uliokithiri katika nchi zetu, udunishaji wa akina mama, mfumo usio wa haki wa maamuziki katika mashirika ya kimataifa hasa Umoja wa mataifa na kadhalika.

Licha ya itikadi za Kolimba na Mtei za kisokwe-mtu, mantiki yake ni 'kutia sumu kisimani kabla watu hawajachota maji.' Yaani wanataka watu wawahukumu kutokana na lebo walizojibandikiza na siyo kutokuwa na kauli na matendo yao. Kwa kuwa Kolimba na Mtei wamekuwapo tangu zamani tunajua kabisa kuwa kauli na matendo yao yanawasuta kuhusu hilo.

Kolimba amekuwa mwanachama na kiongozi wa siku nyingi wa chama kilichopata kujiita cha wakulima na wafanyikazi. Haijatokea hata mara moja chama hicho kikajibandika lebo ya social democrat. Je, huo ndio msimamo mpya wa chama chake? Kama siyo kwa nini tusimwite kinyonga kwa kujibandika rangi yoyote ili muradi tu inamnufaisha kwa wakati huo? Kwa nini asichukuliwe hatua za kinidhamu kwa kukiuka itikadi ya chama chake? Au chama hicho sasa ni 'kapu kubwa' la zoa zoa ya kila itikadi?

MWELEKEO

Rais Mwalimu Nyerere alikuwa kiongozi. Kwa maana aliweza kubuni au kutengeneza mazingira yaliyowezesha mwelekeo wa taifa kubuniwa, kujadiliwa, kutekelezwa na kutathminiwa. Mwelekeo huo ulikuwa wa siasa ya ujamaa na kujitegemea.

Siyo wote tulioafikiana naye. Lakini tuliufahamu mwelekeo huo. Pia tulijua, ingawa si wote tulioafiki, mbinu na mikakati ya kulifikisha taifa huko. Yaani mali ya umma, ujamaa vijijini, elimu ya kujitegemea, huduma za jamii kama vile elimu na afya zilizogharimiwa na serikali na kadhalika.

CCM walibadili itikadi hiyo. Wala hawakuona haja ya kutafuta itikadi nyingine badala ya hiyo. Kwa sababu hiyo taifa hili sasa linashutumiwa kwa kutokuwa na mwelekeo. Kwa hiyo, kwangu mimi sifa ya kwanza kabisa ya rais lazima iwe kututangulia na sisi tukamfuata, au kutuonyesha njia na sisi tukaifuata. Yaani awe na uwezo wa kubuni na kusimamia usanifu wa mwelekeo wa nchi.

Katika wagombea wote waliohojiwa ni Joseph Sinde Warioba tu aliyetamka neno mwelekeo. Anasema ana mawazo kuhusu mwelekeo wetu katika miaka ijayo. Kwake yeye mwelekeo huo ni umoja, amani na utulivu. Haya ni maneno mazuri sana masikioni lakini yasiyokuwa na maana yoyote kichwani.

Kwanza, Umoja, amani na utulivu haviwezi kuwa mwelekeo wa nchi. Hizo ni hali. Siyo lengo bali ni hali inayoruhusu malengo kutimizwa. Warioba na wagombea wengine wote wanapaswa watuambie, je kukisha kuwa na amani, umoja na utulivu kutafuata nini? Ni taifa lenye mahusiano gani ya kijamii litakalojengwa?
 
Nimshukuru FMES kwa jinsi anavyoi-direct thread hii. Waanzishaji wengine wa thread muige mfano huu. Hii imetulia na haijayumba hata kidogo, matusi, kejeli, dharau, umbea, udaku havina nafasi hata kidogo.

Mkuu WC,

Heshima ikurudie, na I am humbled kwa sababu ninaamini in the end hii thread itatuasaidia wananchi wengi kuelewa chanzo cha matatizo mengi tuliyonayo sasa katika sekta mbali mbali za taifa letu, na pia kwa nini tume-advance katika some of the sektas,

Binafsi nimejifunza mengi sana humu, hasa kuhusu Zanzibar, ukweli ni kwamba nilikuwa mtupu sana na historia za huko, na ninawashukuru wananchi waote tunaoshirikiana hapa, ni kwamba tunawasaidia wengi sana hapa na in the process tunajielemisha na sisi pia,

Heshima ikurudie mkuu, na tunaendelea pole pole chombo changu bado hakija kaa vizuri otherwise bado nina picha nyingi sana za ukumbusho, kitakapotengemaa tu nitazimwaga zaidi, ile tule historia zaidi.

Ahsante Wakuu.
 
...historia ya Ukristo Zanzibar

View attachment 2355
Circa 1800 Kiungani Zanzibar, UMCA (United Missionaries of Central Africa)

Sultan Seyyid Said aliona Zanzibar kama kama ni Oasisi katika bahari. Alisimamia mipango mikubwa ya upandaji miti, alichimba visima vya maji vyingi tu na kujenga nyumba nyingi ambazo zilitosha mamia ya wageni. Sultan alitambua wageni watakaa na kujiliwaza katika Oasisi. Kama ni makaribisho mema ya wageni wengi katika Oasisi yake. Sultani aliruhusu watu wa imani zote kuendesha shughuli zao za kidini walivyopenda.

View attachment 2357

...na hii inaelezea chimbuko la (baadhi ya) Wazanzibar wenye asili ya Malawi,...
Slavery in Malawi

The Atlantic slave-trade may have ended 200 years ago, but in Malawi it went on for another 90 years, finally ending when the stockade at Karonga was destroyed in 1895. 19,000 slaves from Nyasa region passed through Zanzibar Custom House alone, though most slaves from Malawi were shipped from Mozambican ports. Thousands more were killed or died in the slave gangs and Livingstoke thought that probably not one-tenth of those captured survived to become slaves.

View attachment 2356

Petro Kilekwa was captured near Lake Bangweulu in Zambia in about 1870 and marched 1,000 miles to Samama on the southern shore of Lake Malawi. There he was made to sleep alongside his owner who had gone down with smallpox, because it was unfitting for a slave to survive his master. His owner died but Petro survived. He was twice resold, and finally marched down to the Portuguese coast and taken by a dhow to the Persian Gulf. There he was freed by a British naval vessel, on which he visited Baghdad and later, as the admiral's cabin boy sailed on HMS Bacchante for Bombay, Colombo, and Madagascar.

At Zanzibar Petro was put ashore into a UMCA school for released slaves where he ended as a teacher and then made his way back to Malawi. He pioneered the work in the hills at Ntchisi as teacher, deacon and priest. This is now the strongest archdeaconry in Malawi and this year is celebrating the centenary of its foundation by Petro.

In 1929 as priest-in-charge of Nkope he became the first African to head a mainland mission. He retired in 1951.

View attachment 2358
 
Eti ni kweli kwamba Karume na Mwalimu, original yao ni Malawi na kwamba ndio maana walielewana sana na Kambona mwanzoni au?
 
FMES,
Hapana. Mwalimu asili yake si Malawi. Ni Burundi.
 
Back
Top Bottom