Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 17,048
- 22,790
Ngoja nitumie TANO bora zangu vizuri hapa.
(3) Kwa waliokuwa wafuasi wa Marquiz na Double "O," je mnafahamu huyu dada ni nani na alikuwa akifanya nini kwenye picha hii, na sasa hivi yuko wapi?
![]()
Ili kupata majibu ya maswali yenu, nipeni mji.
Baada ya dada za Frank Humplick kuacha kujishughulisha na mambo ya muziki mwanzoni mwa miaka ya sitini, wanawake wa kitanzania hawakujishughulisha tena na sanaa hiyo kwa muda wa takriban muongo mmoja hadi mwishoni mwa miaka sabini ambapo mwanadada Tabia Mwanjelwa aliibuka kama mmojawapo wa waimbaji katika safu ya Marquis. Kuanzia Tabia ajiunge na muziki Tanzania, wanawake wa kitanzania wameendelea kuwa msitari wa mbele katika fani hiyo kiasi kuwa hivi sasa wanawake wanashikilia chati za juu sana. Inawezekana kabisa kusema kuwa muasisi wa muziki kwa wanawake wa Kitanzania ni huyu Tabia Mwanjelwa. Katika picha hiyo alikuwa akiimba na bendi ya Orchestra Double 'O' iliyokuwa imeanzishwa na Kivumbi Mwanza Mpango King Kikii, baada ya kuhama Marquis alikotamba na kibao chake cha 'Safari Sio Kifo'.
Tabia alitoweka jijini Dar es Salaam mwaka 1987 akavumishiwa kuwa amefariki kwa Ukimwi; ninakumbuka kukutana na jamaa fulani kwenye baa moja pale Kinondoni akidai kwa nguvu kabisa kuwa alikuwa ametoka kwenye mazishi ya Tabia Mwanjelwa, na alikuwa ameshiriki kwa mkono wake kumzika. Baada ya uvumi kusambaa kwa nguvu, ndipo dada yake akaukanusha na kusema Tabia alikuwa mzima ila yuko Ulaya matembezi. Kuanzia wakati huo Tabia hajarudi Tanzania na kwa sasa hivi anapiga solo na inasemekana ameolewa huko Ujerumani mjini Saabrucken. Website yake ni TabiasSite