Tukumbushane dawa za zamani, naanza na chloroquine

Tukumbushane dawa za zamani, naanza na chloroquine

Chloroquine
Aspro
Cafenol
Cofta
Sulpher
Iodine
Andrews's
Salimia
Tetracycline
Dawanol
Dawaquin
Malaquine
Penicillin
Folic Acid
Mebendazole
 
Christapen sijaandika kiufasha lakini kati ya sindano nilizokuwa nashindwa kuvumilia
 
Kuna dawa moja ya majani ilikuwa inatwangwa then inawekewa tumaji kidogo halafu wanakumiminia puani na kijiko
Sikilizia sasa chafya zake lazima upone unachoumwa
 
Dah...hizi dawa kabla hata hujameza (kile kiharufu tu) unapata kichefuchefu! Na baada ya siku mbili unaaza kuwashwa🙁🙁

BTW, nimekumbuka pia zamani dispensary nyingi (hasa vijijini) hawakuwa na kipimo cha malaria (walikuwa hawapimi damu kama sasa). Nakumbuka sanasana walikuwa wanapima joto tu!
nilipokunywa mara ya kwanza niliwashwa sana nikaamua nikaoge muwasho haukuacha nilipata shida sana siku hiyo mpaka niliambiwa ninywe piriton ndiyo nikaacha kuwashwa.
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Chloroquine
Aspro
Cafenol
Cofta
Sulpher
Iodine
Andrews's
Salimia
Tetracycline
Dawanol
Dawaquin
Malaquine
Penicillin
Folic Acid
Mebendazole

Mkuu, hiyo dawaquine siisahau. Hiyo si ilikuwa tamu.? Sasa mimi nikaumwaga malaria. Nikaandikiwa hiyo dawa. Mzee, nikadhani pipi na ule utamu utakuwepo mpaka mwisho kama pipi.

Basi bwana kumungunya kwa muda nikakutana na uchungu wa shubiri. Yaani ndo ilikuwa mwisho wa kumungunya. Nilitema nikazipeleka uvunguni kuzitupa.

Haahahaa
 
Screenshot_2016-11-25-00-53-06.jpg
 
Antepa - dawa ya minyoo! Ilikuwa ya maji rangi ya blue au nyekundu na ilikuwa na utamu wa sukari uliopitiliza!
 
Back
Top Bottom