Tukumbushane maisha ya UDSM enzi hizo, wazee wa Bibo na Main Campus

Tukumbushane maisha ya UDSM enzi hizo, wazee wa Bibo na Main Campus

2004/2005 tulianzishi kunji kupinga HESLB tukiongozwa na Bahati Tweve. Safari yetu ya kuelekea Ikulu kumwona Rais Mkapa kumweleza jambo letu iliishia UCLAS hatukufanikiwa kuvuka Survey...Tulipigwa na wazee wa ngunguri hatareeeee.
always kunji likianzishwa alivuki Survey,maana wanaofia kuharibu shughuri za kibiashara katikati ya mji 😂😂😂
 
Bush bwana, akaongoza mgomo wa boom, chuo wakamuangaliaaa, alipomaliza tu wakamchukua wakamuweka pale utawala ashughulikie mikopo, sasa nenda pale sijui jina lako hujaliona boom blah blah blah, anakujibu shit mpaka unataka kuzimia! Huwezi amini km ndo yeye aliyekuwa anateswa na mkopo mpaka kuwa kiongozi wa migomo!

Bush bwana alikuaga anajimwambafai sana baada tu ya kupewa kazi pale kwa dean ya mikopo, woooi
Alikua anamakasiriko tu yasiyo na maana
 
Mimi sitasahau jinsi tuliibiwa laptop nne room hall 4 nikiwa 1st year na ndio nilikua nmeachwa room peke yangu jioni, mida ya sa amoja nikasema ngoja niende chaap cafeteria kununua wali samaki, narudi room tu nikakuta mlango umevunjwa[emoji2364], hapo nilikua na laptop yangu mpyaaa hp haijamaliza ata mwezi mwizi kaiiiba na nyingine tatu za wengine[emoji2306]
 
Halafu Hapo UD vyoo vichafu miaka yote ila vijana wanahitimu fresh tu. Aisee sisi tumezoeshwa shida.
**Nakumbuka Hall 5 unaenda msalani na gazeti la Mzalendo vinginevyo jiandae kutoka na nnya ya aliyekutangulia. Same to vyoo vya CoET hakuna pa afadhali. Aisee acheni tule Pombe tu tumesoma kwa kuunga-unga jamani

[emoji23]kipindi maji hakuna tunaletewa na boza ya chumvi ukienda kuoga asbh unabakiza kwenye ndoo ya kuogea jioni[emoji23][emoji23][emoji23], mimi vyoo nilikua naenda vile vya department ya chemistry vilikua visafi[emoji16]
 
Odong nae alikuwa na nyota mganda yule! Kipindi cha kunji kabla hatujatimuliwa ilikuwa usiku main campus mtu anapiga ile 'Odooooong' kutokea hall five, sauti zinajibu kutoka hall 2 , 'Odwaaaaaaaaa', hahahaaa, ilikuwa burudani sana. Wakaja kumpiga deportation ya saa 24 naskia, wakamrudisha kwao kwa Idd Amin, na sijui ana udugu nae, maana alikuwa copy right na Idd Amin 🤣🤣
Jamaa sio mtz lakini almanusura awe rais DARUSO, Nilikuwa namuona kwenye tv tu
 
Halafu Hapo UD vyoo vichafu miaka yote ila vijana wanahitimu fresh tu. Aisee sisi tumezoeshwa shida.
**Nakumbuka Hall 5 unaenda msalani na gazeti la Mzalendo vinginevyo jiandae kutoka na nnya ya aliyekutangulia. Same to vyoo vya CoET hakuna pa afadhali. Aisee acheni tule Pombe tu tumesoma kwa kuunga-unga jamani
Vya pale Law vilikuwa poa Sana.Kule hall 3 maji yakikata kulikuwa na choo cha shimo,mh! Humo unamkuta sister do anakata gogo live maana vingine havikuwa na milango
 
Pale sisi tulikuwa hatuangalii uandishi ni intergral tu kila sehemu ,ndi maana sizingatii uandishi .A ya Mathematics na Physics ndio zilinipeleka pale kugonga miaka yangu minne kule bondeni Coet ,wala sio Kiswahili ambacho niliginga D O-level.

Wewe kweli ni feki wala usidanganye watu kuwa ulikuwa wa Physics and Mathematics maana hata neno ‘ integral’ limekushinda na kuandika ‘intergral’. Hakuna ‘inter..,’ bali kuna ‘inte...’!
 
Wewe kweli ni feki wala usidanganye watu kuwa ulikuwa wa Physics and Mathematics maana hata neno ‘ integral’ limekushinda na kuandika ‘intergral’. Hakuna ‘inter..,’ bali kuna ‘inte...’!
Watu wa Zoom College utawajua tu,mnapenda kushadadia nyuzi zisizo wahusu😂😂😂
 
Dogo upo so arrogant kwa kaka zako!!mimi nimesoma UD ya VC ni Luhanga,CACO ni Mkunya na CADO ni Mkude,Rais ni Mkapa!!nadhani nahitaji Shikamoo yako

Sisi tuliohitimu 1985 tuchangie wapi hapa maana Chuo Kikuu Mlimani na Muhimbili jumla tulikuwa 2320 kwa miaka yote! Nyinyi mnaongea ya jana ambapo Chuo kins wanafunzi zaidi ya 16,000!
 
Back
Top Bottom