Tukumbushane maisha yalivyokuwa kabla ARV hazijaanza kutolewa

Tukumbushane maisha yalivyokuwa kabla ARV hazijaanza kutolewa

Screenshot_20250208-102604_Instagram Lite.jpg
 
Huo ulikua ukimwi wa zamani, sasa hivi watu wanaumwa na hawajijui hata wanadunda tu mtaani
kuumwa ni kama mtu hatumii dawa au awe ameacha dawa uyo ataumwa maana kinga ya mwili imeshuka. nje ya apo mtu anakuwa na afya yake njema tu.
 
kuna jamaa aliugua kwa muda mrefu sana. ilifikia wkt kila sehemu ya mwili ilikuwa imeisha amechonga mwili mzima umebaki mifupa kichwa kimekongoroka ila akawa bado yu mzima tu hafi. watu wengine wazima wanakufa yeye yupo tu.

miaka inakata yeye bado yupo! kuna wakati anaweza akaumwa sanaaa mkasema huyu kesho hataamka au wiki ijayo hafiki, lakini wapi kunakucha na mawiki na miezi na mwaka unakata jamaa yupo anadunda zake fresh tu.

alikaa kwenye hali iyo muda mrefu adi yeye mwenyewe akachoka maana maumivu yalikuwa ni makali sio ya apa kiasi hata yeye mwenyewe hafurahii tena uwepo wake apa duniani lakini ndo ivyo mungu anaendelea kumtunza. bdae sana alifariki lakini kwakweli palichimbika aisee yani acha kabisa
 
Nyege mbaya na walio oa pia wana zini nje so bora watumie mpira buko nje ila ukimwi miaka ile ulikua wa kutisha sana sahv kama haupo kumbe una tu zoom tufanye ujuha na trump kazima msaada

wakati ule kama ulikuwa na nye.ge zako au ndo umemleta dem geto kwako hlf ikatokea umeonana na mgonjwa, aisee izo nye.ge zote zinakata chap apoapo unajihisi kuingiwa na ubaŕidi maungoni na kinachofata ni kwenda kumtoa mtoto wa watu geto chap kumruhusu achape mwendo chap arudi kwao kabla mambo hayajawa mengi😁
 
wakati ule kama ulikuwa na nye.ge zako au ndo umemleta dem geto kwako hlf ikatokea umeonana na mgonjwa, aisee izo nye.ge zote zinakata chap apoapo unajihisi kuingiwa na ubaŕidi maungoni na kinachofata ni kwenda kumtoa mtoto wa watu geto chap kumruhusu achape mwendo chap arudi kwao kabla mambo hayajawa mengi😁
Sana mzee yaani mwezi mzima unajikuta huna hamu
 
Enzi hizo ukipata UKIMWI watu wanaanza kukuhesabia siku wakisema hamalizi mwaka. Kuna watu tangu enzi hizo walijulikana ni waathirika mpaka leo ni wazima tena wana afya nzuri hawana hofu ya kufa kwa ugonjwa huo
mungu wa ajabu sana kuna maza alikuwa anatoa ushuhuda amegundulika miaka ya themanini lakini yupo hata leo hii.
 
- Hizi ARV zimeanza kutolewa kwenye mwaka 2003 au 2004 hapa wenye kumbukumbu sahihi mtanirekebisha. kabla ya hapo hapakuwa na dawa za kufubaza.

- Ugonjwa huu uliogopesha sana kiasi ambacho jamii haikuwa tayari kuuzungumzia. kimya kikuu kilitanda bila shaka kila mmoja akiomba kwa mola wake amuepushe na kikombe.

- Elimu kwa jamii zilitolewa zikichagizwa na picha za kilichokuwa kinaendelea mkoa wa kagera. kwa mujibu wa taswira zìle huko kagera ugonjwa ulimaliza watu wengi na wengine hata nyumba zilifungwa hakuna aliyebaki. nyumba zingine nyingi zilibaki zikiendeshwa na watoto mayatima baada ya wazazi wote kufariki.

- Kimya kingi kilitanda huku ugonjwa ukiendelea kutafuna watu kimyakimya.

- Kwenye hatua za mwanzoni wagonjwa wengi walikuwa wakionekana kupata mkanda wa jeshi yani miaka hiyo kama wewe una mkanda wa jeshi tu basi ilikuwa ni uthibitisho tosha tayari una tatizo hilo.

- Ukiona jirani yako flani haonekani hapo mtaani hiyo ilikuwa ni ishara tosha kuwa kama jirani uyo hajasafiri basi tayari uenda mambo yameshaharibika.

- Ugonjwa ulikuwa haufichiki. Ukiwa nao utajulikana tu apo kitaani kwenu. maana mwanzoni utajifungia ndani kwako lakini bdae lazma utoe ukahemee au kupata matibabu nk. ukitoka tu habari zako zinaanza kusambaa kama moto wa nyika.

- Ili kuepuka macho na vidole vya walimwengu familia nyingi ziliwapeleka mahospitali wapendwa wao mapema alfajiri sana au hata usiku.

- Familia nyingi zilikuwa zinaepuka kuwapima wagonjwa wao maana unampimaje mtu wakati unajua ugonjwa wenyewe hauna dawa. hivyo basi familia nyingi ziliishia kuuguza tu wagonjwa wao kimyakimya hadi wagonjwa anapokutana na mwisho wake.

- Wagonjwa wengi waliisha sana miili yao. hata kama ulikuwa kibonge kama pipa mwili wote utaisha kabisa unabaki kichwa ngozi na mifupa mitupu tu. ilikuwa sio ajabu kukuta mtu mwenye mwili mkubwa kama wale mabaunsa kaisha mwili wote kiasi hata usiweze kumtambua.

- Ilikuwa kawaida tu mtu mzima kabisa mwenye mwili uliojengeka vema akamalizwa na kubaki makongoro tu kiasi ambacho akilala kitandani hlf wewe ukapita apo usimuone au kujua kama pale kitandani kuna mtu amelala. najua kuna wanaozani natania lakini iyo ndio hali ilivyokuwa wakati huo.

- Watoto wengi waliozaliwa na maambukizi hawakuweza kuishi wengi walifariki baada ya muda mfupi na wachache kwa kudra za mwenyezi waliweza kuishi na wengine wako hai hata leo hii.

Hapa tunakumbushana tu hatutishani ukimwi upo tujilinde.

***Tafadhali msiuunge uzi huu tuna vijana damu changa wengi humu wanapaswa kupata ufahamu wa kule tulikotoka.
Ilikuwa hatari Shule ya msingi Maticha kama watatu walikufa...yani walikonda hadi wanafunzi tukienda kuwasalimia mademu wanakia jinsi ticha alivoisha.
Hamna namna vijana tujikinge bila ARV hata ukipiga denda tu unao
 
Back
Top Bottom