Tukumbushane tukio la Ujambazi pale Ubungo Mataa mwaka 2006

Tukumbushane tukio la Ujambazi pale Ubungo Mataa mwaka 2006

Miaka hiyo nafanya kazi dsm posta huko.

Ujambazi ulienea kila upande wa jiji.

Kwa simulizi ya baba aliyekuwa ndani ya daladala sekeseke lilipoanza abiria walilala chini.

Huyo baba alisema alipolala akaja mama mmoja kibonge akalala juu yake.

Alipoinuka alikuta amelowa mikojo mwili wote.

Was so bad. Sijui alikuwa nani President that time
Mzee wa msoga Jeiiii Keiiiii

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Wengine kipindi hicho tulikuwa hatujafika mjini bado, tulikuwa Sitimbi...ngoja tuwe wasomaji
 
Hapa mnachanganya matukio kuna la wizi NBC ubungo na Wizi hela za NMB ifakara or kilombero tukio lilifanyika ubungo mataa
 
Aisee umenikumbusha hii siku, na namkumbuka sana Marehemu Michael (R.I.P) nitaeleza kuhusu marehemu Michael hapo mbeleni.

Basi, ilikua siku za kawaida tuu, mwaka huu nilikua bado mwanafunzi maeneo ya Mjini kati. Kwaiyo nilikua na urafiki wa karibu na Marehemu Michael ambaye baadae alinitambulisha kwa Solomon.

Ilikua ni utaratibu kwamba Michael akitoka kwake anapita mitaa ya home saa 11 asubuhi anaita dogoooo... basi nachomoka tunatembea mpaka barabarani, kama siku ana gari basi anapiga honi chap natoka ( kumbuka 11 asubuhi ni giza totoro na tulikua tunakaa shamba kabisa).

Tukifik kituoni kama hatuna gari tunasubiri gari ya solomon hii gari yake kwanza ndani ni mziki wa congo mixer speed za hatari, yani light speeed.

Sasa siku ya tukio, Marehemu Michael hakuwepo, nikamsikilizia paleeee kimya, mpaka bimkubwa nae akamaliza kujianda ikabidi nisepe na bimkubwa mpaka kituoni.

Tunafika kituoni tuu, solomon huyu hapa. Kama kawaida light speed akasalimiana na bimkubwa maana Michael alikua kashamtambulisha kua ni dada yake na mm michael nilikua namuita uncle. Basi tukaingia safari ikaanza.

Katika story solomon akawa anamwambia dada "leo niende kucheki, moyo unaniuma" bimkubwa akamwambia kacheki ndugu yangu, lakini baadae tena akasema lakini hii siku ya leo sijui imekaaje!. Yani kama anaona wenge hivi. Hapa ndio mshana anakujaga na mazaga yake ya jicho la 3.

Siku hii ndio kamanda solomon alipambana na hao mafedhuli pale ubungo.

Namkumbuka sana, Marehemu na solomon kwasaidia Elimu yangu maana usafiri haikua shida na bado walikua wanachanga wananipa mzigo wa kutumia shule.

Nilikua don na clean, because of these two great people Solomon and Michael ( R.i.p)
Usiku wake alikuwa amefiwa na kaka yake aliye mfuata kuzaliwa,aliishi nae hapo Chama kabla hajarudishwa Mbeya.
 
Hakuwa mwanajeshi na walimkamata mtu ambae anafanana sana huyo jambazi ambae tuna undugu nae. Amekaa ndani miaka kumi na tano mpka alipokuja kupatika huyu jambazi ambae alikua kikosi cha jeshi Zanzibar.
Poleni sana.
 
Lakini Magufur aliwaweza wote majambaz
Yah ukali wa Magufuli ulisaidia kwa kiasi but kikubwa kilichochangia ujambazi kuisha katikati ya mji kwanza ni watu kuongezeka,pili mitaa mingi imekuwa sehemu ya ku-park magari siyo kama wakati ule kipindi kile ulikuwa ukisimama mwanzo wa mtaa ukapiga jicho unaona mpaka mwisho wa mtaa yaani kulikuwa kweupe mtaa uliokuwa na magari mengi ni Msimbazi na Lumumba tu.

So ilikuwa rahisi kwao kukimbia ila miaka hii kila mahali pana foleni hata pikipiki haipenyi,kingine hela za kwenye simu na bank sharing (sijui kama nimeandika sahihi) zimesaidia pia maana wakati ule ilikuwa kama unanidai let's say mill 50 naingia bank A natoa hela kisha naenda bank B kukuwekea au nakufata kituo C ulipo so katikati hapa ndo matatizo yalikuwa yanatokea but leo bank yoyote ukiingia unafanya transfer yani salama kabisa.
 
Naendelea kusoma comments..
 
Hakuwa mwanajeshi na walimkamata mtu ambae anafanana sana huyo jambazi ambae tuna undugu nae. Amekaa ndani miaka kumi na tano mpka alipokuja kupatika huyu jambazi ambae alikua kikosi cha jeshi Zanzibar.
Mbona huyo mwanajeshi aliyekuwa anaitwa Juma walimkamata kipindi kile kile. Baada ya tukio alikimbilia kwa Baba yake Moro. Alikamatwa na akashighulikiwa kijeshi baadae aliachiwa. Hadi sasa ni bado mwanajeshi. Namjua huyo jamaa. Tulikuwa wote utotoni.
 
Ingia youtube search jina Mussa Chesa ana page yake na picha utapata simulizi alizofanya channel zote kuanzia cloud fm, RFA, davistar mata mikasa, promover TV. Ndie aliyepiga lile tukio la ubungo mataa akiwa kashika smg pia kaeleza matukio yote ya ujambazi aliyofanya ndie aliyemuua Mzungu kahama. Ili asikamatwe kwenye ujambazi akaingia kwenye uchawi akafanya vizuri sana hadi kupewa kitengo cha kusimamia misukule nchini kafanya biashara nyingi Sana za misukule na wachungaji wengi sana, alimtoa mtoto wake kafara Ili awe msanii mkubwa Sana nchini alizidiwa nguvu na diamond na amewahi taka pigana studio na diamond baada ya kukuta diamond anatumia biti yake kuingiza nyimbo studio kabla diamond ajawa star. usanii ulikoma baada ya kukosea masharti ya mganga sababu alilewa akajisahau.
Alikuwa na kikosi tabora cha kuiba kwenye treni tabora Kigoma vijana wanaiba wanarejesha kwake hesabu. Amewasumbua Sana police Kigoma risasi zilikuwa hazipenyi, kaua watu wengi sana kwa uchawi pia kwa bunduki, ameteka mabasi na magari mengi Sana Kigoma,tabora, kahama,nk.
Musa Chesa mzaliwa wa kazuramimba kigoma alijulikana kwa ujambazi kote kigoma,tabora,burundi, kahama,nk.Akiwa kwenye mambo ya kichawi alipigwa nguvu moja hatari shetani akamtoroka na hakumsaidia aliponea kwa watumishi wa Mungu akaacha uchawi akachoma moto zana zote za kichawi picha zipo alipokuwa akizichoma, akasalimisha bunduki police ambao nao awakuamini ikabidi apelekwe hadi kwa Mkuu wa Mkoa Kigoma akawahakikisha ametubu na ameacha vyote na akawa mstari wa mbele kuwakamatisha majambazi kwa police na pia ndipo hata wizi kwenye treni tabora ukatoweka.
Leo ni mtumishi wa Mungu anamuhubiri Kristo huku akitoa Siri zote za mambo ya giza na ameapa kupambana na shetani kwa mda wake wote uliobaki dunia. Anajutia Sana kwani na linamumiza Sana kupoteza watoto wake watatu kichawi Ili afanikiwe kwenye muziki, ujambazi, nk.
Ana mengi Sana muhimu sikiliza shuhuda zake yupo huru kutoa huduma na kujibu maswali yote. 0758238524 wasap pia.
Ye ndie aliyepiga tukio la ubungo mataa kalieza na hadi alivyofukuzana na police mitaa mbalimbali na kuwatoroka.
Amecheza movie matukio yake.Ametoa kitabu,ameonyesha kwa picha alipomua Mwenyekiti wa kijiji,alipotekea magari, alipokuwa akioshea misukule,nk.







 
Nlishuhudia hili nlikuwa kwenye daladala foleni hakuna kwenda mbele wala nyuma
 
Ngoja tumsikilize muhusika aliyepiga tukio hilo akisimulia.

 
Nilishuhudia nikiwa hapo Oil com na nili craw kuanzia hapo Hadi darajani Kama unaenda chuo hii ni baada ya kukoswa chuma nikiwa natokea Changanyikeni
 
Hapa mnachanganya matukio kuna la wizi NBC ubungo na Wizi hela za NMB ifakara or kilombero tukio lilifanyika ubungo mataa

Tukio la wizi NMB Kilombero umenikumbusha mzee, nilikuwa mdogo sana nina miaka 10
 
Hili tukio lilitokea nikiwa kama mita 50 kutoka kwenye scene na nlikuwa ndania ya shuttle naelekea bibo kujipumnzisha, gari zilitupita lwegalulila kulikuwa na foleni tulipovuka daraja tu kwa mbele kidogo ndo vita ikaanza. Nina downloads za musa chesa 39 huyu jamaa alikuwa zaidi ya hatari
 
Jina hili linaanza kunikumbusha issue ya Laura Nkunda na Major General Mwakibolwa wa JWTZ alipokuwa pamoja na majeshi ya UN kule Congo. Jamaa aliibuka siku moja kwenye media akasema huyu Nkunda tutamshughulikia vizuri tu na wala hakuna shida yoyote.

Kuna watu wanaojiamini kwenye haya mambo, yaani ni professional perce
" Laurent Nkundabatware Mihigo"(loraa Nkunda)

Sent from my SM-A405FN using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom