Tukumbushane tukio la Ujambazi pale Ubungo Mataa mwaka 2006

Tukumbushane tukio la Ujambazi pale Ubungo Mataa mwaka 2006

Kipindi kile DSM haikuwa ajabu kusikia matukio matatu mpaka manne kwa wiki halafu yote ya hatari lazima damu imwagike,mimi huwa nashangaa mtu anaposema ujambazi umerejea leo 2022 unajiuliza huyu ana umri gani?ilikuwepo miaka mtu kutembea na 500K mfukoni unakuwa hatarini.

Nakumbuka siku ilianzwa kwa majibizano makali ya risasi pale Kariakoo mtaa wa Swahili na Mafia ambapo polisi waliondoka na point zote tatu hiyo ilikuwa mapema tu saa 8:35 asubuhi,mchana majira ya saa saba mtaa wa Livingston na Mkunguni ule muda wa kwenda msikitini jamaa wakaingia sonara moja ilikuwa kubwa sana wakati ule.

Wakauwa mlinzi mwarabu boss wakamvunja nyonga wakachukua vyao wakaondoka,huku mitaa ya Jangwani na Congo kwa wale wauza vipodozi likapigwa tukio kupishana kama dk 40 hivi alikuwaga bwashee kaambiwa akabidhi fuko la hela yeye macho yamemtoka jamaa wakaona anawachelewesha wakamchapa ya mbavu wakachukua fuko wakaondoka (huyu alipona)

Pale police Msimbazi siku hii pale counter askari walibaki wawili tu wote waliingia mtaani kipindi hiki RPC alikuwa Alfred Tibaigana nakumbuka kumuona ndani ya defender pale mtaa wa Msimbazi akiongoza kikosi.

Funga kazi ni hiyo ya Ubungo jamaa waliuwa stuff wa Nmb na askari,attacker wao alikuwa kijeba hivi amejazia amevaa kawoshi na bukta ana kipisi anamimina njugu kama ana-act movie halafu mweusii kichwani ana kipara kinang’aa!

Yupo jamaa yangu aling'ang'aniwa baada ya kuonekana pikipiki iliyoshiriki lile tukio imeingia nchini kwa jina lake alikaa jela miaka nane na matukio mengi kipindi kile wapigaji walikuwa wanashirikishwa na wabongo refer tukio la kupigwa bomu kwa ATM machine pale Temeke hospital jamaa walivyofanyiwa ambush na askari Chang'ombe waliuwawa sikumbuki idadi but mmoja wao alikuwa na id ya Rwanda.
Naona jamaa yako kahojiwa na millard ayo
 
Aisee umenikumbusha hii siku, na namkumbuka sana Marehemu Michael (R.I.P) nitaeleza kuhusu marehemu Michael hapo mbeleni.

Basi, ilikua siku za kawaida tuu, mwaka huu nilikua bado mwanafunzi maeneo ya Mjini kati. Kwaiyo nilikua na urafiki wa karibu na Marehemu Michael ambaye baadae alinitambulisha kwa Solomon.

Ilikua ni utaratibu kwamba Michael akitoka kwake anapita mitaa ya home saa 11 asubuhi anaita dogoooo... basi nachomoka tunatembea mpaka barabarani, kama siku ana gari basi anapiga honi chap natoka ( kumbuka 11 asubuhi ni giza totoro na tulikua tunakaa shamba kabisa).

Tukifik kituoni kama hatuna gari tunasubiri gari ya solomon hii gari yake kwanza ndani ni mziki wa congo mixer speed za hatari, yani light speeed.

Sasa siku ya tukio, Marehemu Michael hakuwepo, nikamsikilizia paleeee kimya, mpaka bimkubwa nae akamaliza kujianda ikabidi nisepe na bimkubwa mpaka kituoni.

Tunafika kituoni tuu, solomon huyu hapa. Kama kawaida light speed akasalimiana na bimkubwa maana Michael alikua kashamtambulisha kua ni dada yake na mm michael nilikua namuita uncle. Basi tukaingia safari ikaanza.

Katika story solomon akawa anamwambia dada "leo niende kucheki, moyo unaniuma" bimkubwa akamwambia kacheki ndugu yangu, lakini baadae tena akasema lakini hii siku ya leo sijui imekaaje!. Yani kama anaona wenge hivi. Hapa ndio mshana anakujaga na mazaga yake ya jicho la 3.

Siku hii ndio kamanda solomon alipambana na hao mafedhuli pale ubungo.

Namkumbuka sana, Marehemu na solomon kwasaidia Elimu yangu maana usafiri haikua shida na bado walikua wanachanga wananipa mzigo wa kutumia shule.

Nilikua don na clean, because of these two great people Solomon and Michael ( R.i.p)
Jitahidi sana na wewe kuwasaidia mtoto mmoja wapo wa Marehemu Michael. In this life, never forget those who once helped you when you were in need..
 
Sterling wa wizi ule bado yupo anapatikana ila hatua za kuanza kuchechemea miguu zishafika

anapatikana sana bar Moja maarufu mercury ukitokea magomeni usalama upande wa kulia kabla hujafika mercury bar ...jioni utamkuta pale anatia huruma na mkewake pale...jamaa Moja white hivi ....ukimwona tu UNAJUA huyu alikuwa mtu wa kazi
 
Nimeona hii kitu jasho jembamba limetoka ghafla, I was there; wakati huo nasoma Jitegemee A- level, that day nimepata ruhusa nikawa naenda Kimara kutembelea ndugu.

Nimepanda hiace nikakaa siti ya nyuma kabisa, tuko pale mataa tunasubiri gari za kutoka Mwenge zilikuwa zina cross kuelekea mitaa ya Mabibo hostel ( hii njia nimeisahau jina) na mengine yana cross toka Sam Nujoma kuelekea Kimara.

Ghafla nikasikia sauti nikahisi tairi la gari limepasuka, nikaisikia tena, mara tena, na tena, nikajua hapa sio poa, kuna shida, natazama nje, naona kupitia dirishani barabara nyeupe hakuna mtembea kwa miguu hata mmoja, nikatoka kule nyuma nilipokuwepo nikaenda zile siti mbili pale mbele nyuma ya siti ya dereva, sio kukaa kujibanza pale chini abiria wanapoweka miguu..

Wale jamaa waliokuwa nimekaa nao, na siti iliyofuata nao wote wakanifuata, tukajazana wote pale mbele wake kwa waume, nilifanya vile nikijua risasi inaweza kutoboa bati la gari nyuma ikanila mgongo ndio maana nikakimbilia mbele, tumekaa pale km dkk kumi ni majibizano tu ya risasi nje, wote kimya hakuna anayeongea na mwenzake wala nini.

Baada ya muda nikasikia ukimya umekuja, sasa nani aanze kunyanyua kichwa, nachungulia pembeni kumbe kondakta nae alikimbia akaacha mlango wa gari wazi hata sikujua, baadae ndio nasikia km sauti za wawili watatu wanaongea nje ndio tukapata nguvu tukaanza kujiinua pale chini, tukatoka nje eneo lote la ubungo anzia pale jengo la Tanesco, mataa, kote hapakuwepo na mtu hata mmoja barabarani nakumbuka ilikuwa kam saa sita mpk nane mchana hivi, palikuwa peupe..

Nimetoka pale naanza kuangalia baadhi ya magari nayaona yana matundu ya risasi, ndio nikajua huu mchezo uliokuwa unachezwa hapa haikuwa movie, na traffic mmoja ndio alisimamia ile show sijui alipata wapi silaha wakati ule, wale abiria wenzangu nao sijui walipotelea wapi.

Hakuna aliyeongea na mwenzake wala nini, kila mmoja alikula kona yake hakuna aliyekuwa na hamu ya barabara tena siku ile, baadae ndio nasikia ni majambazi waliiba NBC Ubungo branch walisababisha yote yale, na mmoja wao aligundulika alikuwa mwanajeshi Mgulani JKT baada ya kukamatwa ila sikumbuki km walifungwa au vipi..
mada inahusu pesa za Nmb zilizokuwa zinaenda Wami Dakawa Morogoro,hill ma NBC ni lingine.
 
Ingia youtube search jina Mussa Chesa ana page yake na picha utapata simulizi alizofanya channel zote kuanzia cloud fm, RFA, davistar mata mikasa, promover TV. Ndie aliyepiga lile tukio la ubungo mataa akiwa kashika smg pia kaeleza matukio yote ya ujambazi aliyofanya ndie aliyemuua Mzungu kahama. Ili asikamatwe kwenye ujambazi akaingia kwenye uchawi akafanya vizuri sana hadi kupewa kitengo cha kusimamia misukule nchini kafanya biashara nyingi Sana za misukule na wachungaji wengi sana, alimtoa mtoto wake kafara Ili awe msanii mkubwa Sana nchini alizidiwa nguvu na diamond na amewahi taka pigana studio na diamond baada ya kukuta diamond anatumia biti yake kuingiza nyimbo studio kabla diamond ajawa star. usanii ulikoma baada ya kukosea masharti ya mganga sababu alilewa akajisahau.
Alikuwa na kikosi tabora cha kuiba kwenye treni tabora Kigoma vijana wanaiba wanarejesha kwake hesabu. Amewasumbua Sana police Kigoma risasi zilikuwa hazipenyi, kaua watu wengi sana kwa uchawi pia kwa bunduki, ameteka mabasi na magari mengi Sana Kigoma,tabora, kahama,nk.
Musa Chesa mzaliwa wa kazuramimba kigoma alijulikana kwa ujambazi kote kigoma,tabora,burundi, kahama,nk.Akiwa kwenye mambo ya kichawi alipigwa nguvu moja hatari shetani akamtoroka na hakumsaidia aliponea kwa watumishi wa Mungu akaacha uchawi akachoma moto zana zote za kichawi picha zipo alipokuwa akizichoma, akasalimisha bunduki police ambao nao awakuamini ikabidi apelekwe hadi kwa Mkuu wa Mkoa Kigoma akawahakikisha ametubu na ameacha vyote na akawa mstari wa mbele kuwakamatisha majambazi kwa police na pia ndipo hata wizi kwenye treni tabora ukatoweka.
Leo ni mtumishi wa Mungu anamuhubiri Kristo huku akitoa Siri zote za mambo ya giza na ameapa kupambana na shetani kwa mda wake wote uliobaki dunia. Anajutia Sana kwani na linamumiza Sana kupoteza watoto wake watatu kichawi Ili afanikiwe kwenye muziki, ujambazi, nk.
Ana mengi Sana muhimu sikiliza shuhuda zake yupo huru kutoa huduma na kujibu maswali yote. 0758238524 wasap pia.
Ye ndie aliyepiga tukio la ubungo mataa kalieza na hadi alivyofukuzana na police mitaa mbalimbali na kuwatoroka.
Amecheza movie matukio yake.Ametoa kitabu,ameonyesha kwa picha alipomua Mwenyekiti wa kijiji,alipotekea magari, alipokuwa akioshea misukule,nk.








Aisee
 
Back
Top Bottom