Ooooh!! Kwa baba aisee tulikuwa na baba mpole, hakuwahi hata kunifinya na nilikuwa kipenzi chake ila kwa mama daaaah!!
Kuna siku nimetoka shule(nikiwa std2), njiani tukaamua tucheze 'marede', nikavua soksi zangu tukatengenezea mpira, nikarudi home kwa kuchelewa,mchafuuuu na soksi zimelegea, mama akajua tu kilichofanyika, tofauti na nilivyotegemea, hakuniuliza chochote.
Sasa kesho yake kulikuwa na maonyesho ya mazingaombwe shuleni, jinsi ya kuomba pesa nikashindwa maana nshalivuruga, kesho yake asubuhi wakati nataka kuondoka nikaona hela mezani, nikachukua iliyotosha kiingilio huyooo nikasepa.
Kurudi jioni, akatukalisha na kaka yangu kutuhoji aliyechukua hela yake, nikajifanya sijui, kaka akasema yeye hajachukua, sijui hata alihisi nini ila akajua tu ni mimi, akanitega nikajikuta nimejaa, weeeeeeh nilikula kichapo, akatuambia pesa yoyote ni yake, hivyo tukitaka tumuombe, ikawa hata nikiokota hela barabarani nampelekea.