Tukutane hapa wapenda ujasiriamali

Pesa ipo kwenye uzalishaji mbadala wa vitu vilivyo pata bei, mfano vifaa vya ujenzi, mafuta ya kula, petrol, dizeli na gas
 
Pisi wapia naweza pata viatu vya michezo kwa bei za jumla
 
Moja katika vitu bora kusoma humu JF, hata kama mtu si mjasiriamali ila unafunguka akili. Ahsante sana boss

Me naweza nkachangia kidogo katika biashara ya chakula japo mtaji wake sio mdogo kama biashara tajwa hapo juu.
Katika zama hizi za njaa nenda mikoani kanunue mahindi kwa bei ya chini kisha yauze mjini japo hutopata faida kubwa sana ila itakupigisha hatua. Na kama una connection nje ya mipaka ya TZ basi umetusua sana.
 
Una itwa mataa wa narung'ombe ,kituo msimbas B
mwendokas

Sent from my SM-G960U using JamiiForums mobile app
 
Uzi ulikuwa na mchango mkubwa sana ila watu waliutelekeza na kwenda kula tunda kimasihara kule kwa rikiboy
 
Mtaa wa Narung'ombe kariakoo ndo wa viatu bei ya jumla na rejereja
 
Pisi kali naomba kama una namba za wauza chupi jumla, pia wale wanaouza vitambaa vya kushona pazia
 
Asante sana wazungu wanasema sharing is caring
80% ya hizo ideas hapo nimefanya kwa alipenda chochote hapo aje nimpe uzoefu
Dada wewe ni mpambanaji haswaaa.
Mimi naomba idea ya pants, kuuza chupi na tights tu. Ningependa nifungue mtaani (actually a busy street) kama wauza vipodozi wapo na wanauza nywele na vya kupaka. Je, chupi na hizo tights ntatoboa?

Kuna siku nilienda kumtafutia vyupi mamsapu wangu nikakuta muuzaji ana chupi za hadi sh 2,000 pale Kinyerezi pembeni ya Ikupa Supermarket. Tupe uzoefu kidogo.
 
biashara cha kwanza inatakiwa ujue unawalenga kina nani? Yaani wateja wako kina nani, na kipato chao maana kuna pants hadi za 30k pisi moja na kuna pants za 1k pisi moja

Kwa uzoefu wangu kuhusu pants hizi za bei chee zitakuchelewesha labda kama unapeleka kwenye minada au mikoani huko unaenda kuwasambazia kwa jumla lakin hasa minadani sawa yaani wewe monday to sunday unakuwa unazunguka minada lakin kama una hela yakueleweka fungua lengirie shop na unaweza anzia online
 
Asante sana
Bei chee lengo ni kuwapata hao hao wa kipato cha chini. Masikini ndio wenye hela kuipata kwake ni rahisi, mimi naamini hivyo. Angalia bidhaa za MO. Cha kufanya wewe wape solution ya kinachowasumbua.
Chupi za buku 2 au tatu wanazimudu.
Idea ya Lingeria pia sio mbaya lakini.
 
sawa mkuu komaa,

Nb: mo anazalisha basic needs sasa wewe ndugu yangu vyupi ni vya muhimu kweli πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
 
Mimi binafsi naamini katika kuzalisha na kuuza kuliko kununua na kuuza, aheri ununue kisha uzalishe ndio uuuze.
 
Biashara ya kutegemea watu ngumu sana kwenye kuikuza hasa sisi watoto wa mama ntilie
Bila watu hatufiki popote ila watu wa aina gani hio ndio changamoto.
Lakini kwa mtazamo wangu mtu yoyote anayetaka kufika mbali awe mzalishaji na sio mlanguzi.
 
Bila watu hatufiki popote ila watu wa aina gani hio ndio changamoto.
Lakini kwa mtazamo wangu mtu yoyote anayetaka kufika mbali awe mzalishaji na sio mlanguzi.
oops sikuwa na maana ya kwamba hatuhitaji watu, nimeweka biashara za watu kwa ku maanisha kulangua kwa watu
 
oops sikuwa na maana ya kwamba hatuhitaji watu, nimeweka biashara za watu kwa ku maanisha kulangua kwa watu
Wewe Jane Msowoya nimekupenda kweli hebu nipe ushauri nina kama 3ml, napenda sana biashara za kuzalisha mali, hasa vipodozi vya kina mama/dada, kama anti aging oils, scrubs, mpaka dawa za kuzuia ndevu kuota how could I start, nahisi I can do wonder!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…