Tukuyu: Waumini KKKT wamfukuza Baba Askofu Dkt. Edward Mwaikali

Tukuyu: Waumini KKKT wamfukuza Baba Askofu Dkt. Edward Mwaikali

Labda huelewi


Mbeya yenyewe wanataka dayosisi Yao sio kuihamisha dayosisi! Kama vile hii dayosis ilivyoombwa toka Iringa! Yaan wanakonde waliomba dayosis Yao kwani wamekuwa na wanataka wajitegemee! Hivyo hivyo mbeya wanataka dayosis Yao wajitegemee! Si kuhamisha dayosisi

Halafu unaposema dayosis ya konde! Neno konde ni eneo linalojumuisha, tukuyu, busokelo na kyela! Sasa ukileta mbeya mjini huko si konde
Huyu Askofu ametufedhehesha sana kwa kukosa hekima.
Ile kulazimisha kuhamisha Makao Makuu, kutosikiliza waumini wanasemaje, kufukuza wachungaji, hii ni kiburi.
Kiburi si sifa nzuri kwa Askofu.
Na bado alikuwa na ujasiri kwenda kule aliko wadharau, Tukuyu Cathedral.
Kilichompata hapo Tukuyu ni laana.
Askofu kuzomewa madhabahuni ni chukizo sana kwaMungu.
Na Mungu hadhihakiwi.
Mimi kwa kweli machozi yalinitoka nilipoona clips za Askofu kuzomewa.
Nimefedheheka sana.
Askofu hana jinsi, ajishushe tu.
 
Baadhi ya Maaskofu wa KKKT wanaotokea Mbeya ni controversial, Huyo, Mwaipopo wa Sumbawanga, Wa Mashariki na Pwani naona sasa upepo umetulia.
 
Kanisa ni ;
MOJA
TAKATIFU
KATOLIKI
LA MITUME.

Kanisa pekee la MUNGU baba lililoanzishwa na YESU KRISTU mwenyewe chini ya usimamizi wa MITUME na uangalizi wa ROHO MTAKATIFU.
Milele Amina
Tumsifu Yesu Kristu.

Kuna tofauti gani Kati ya Kristo na Kristu?
 
Waumini wa kanisa la KKKT Usharika wa Tukuyu Mjini ulioko Dayosisi ya Konde wamemfukuza kanisani hapo Baba Askofu wa Dayosisi hiyo Dkt. Edward Mwaikali.

Waumini hao wamedai kuwa Askofu huyo hawasikilizi na amekuwa akiwafukuza kazi wachungaji wasiomuunga mkono katika maamuzi yake.



Pia soma: Mbeya: Wachungaji 25 wa KKKT Wafutiwa ajira ya Uchungaji Dayosisi ya Konde
Mpaka kufika hatu ya kususiwa Uaskofu wako, ina maana upako umeingia dosari.
 
Yes......wananchi wanapoamua kuyamiliki mamlaka......dayosisi nyingine zijifunze kitu hapo.....MALASUSA UPOOOOO?
Malasusa ana shida gani?

Hakuna askofu mzuri kama Malasusa, labda wewe kama unamuangalia kwa jicho uchadema na uchaga!

Kuna kale kaaskofu kule Karagwe kale kafupi kama nyundo kale ni kadikteta kwenye ile dayosisi hakuna mwenye sauti.
 
KKKT siyo makondoo!

Huwa nashangaa sana eti katolic kama hujatoa michango hubatizi mtoto au jufunga ndoa. Hiyo si ni sawa na kuuza huduma ya kiroho?
Haa😂😀😁😃😁😂😀
 
Huwezi kuta upuuzi kama huu ndani ya kanisa la mitume CATHOLIC
Katolic inaendeshwa kisiasa! Waumini wake ni kama makondoo!

Utasikia padri kabaka au kulawiti na ushahidi upo lakini miumini ipo tu huku mkuu akiendelea kudhalilisha ukristo!

Mtu kama hujatoa mchango wa jumuiya huwezi kubatiza au kufunga ndoa, hiyo si ni kuuza huduma?
 
Baadhi ya Maaskofu wa KKKT wanaotokea Mbeya ni controversial, Huyo, Mwaipopo wa Sumbawanga, Wa Mashariki na Pwani naona sasa upepo umetulia.
Huyu wa mashariki na pwani zile zilikuwa ni harakati za wachaga kutaka kutawala wao!
 
Kweli nimeamini kutenganisha kanisa na serikali ni ngumu duh asikofu anataka kuhamia makao makuu, hahahaaaaaaaaaaaa hawa jamaa bana tangu wagonge ile chanjo ya bure naona sasa misalaba imewaelemea shingoni wanaanza kuwa mazombi sasa
 
Inawezekana waumini wengi wapo Rungwe kama unavyosema lakini Tukuyu ipo pembeni sana kiasi kwamba mtu wa kutoka Tunduma au Rujewa Mbarali akitaka huduma ina mgharimu pakubwa tofauti na Mbeya ambapo anweza akaenda na kurudi the same day na cost zikapungua.

Tatizo sisi wanyakyusa ubinafsi unatusumbua sana. Kwani kuna tatizo gani Dayosisi kuhamishwa sehemu nyingine? Mbona Magufuli alihamisha ofisi za serikali Dar kwenda Dodoma?
Siyo magufuli alihamisha ofisi dodoma hadi ikulu ilihamia chato kwao na uwanja wa ndege sasa wanachungia mbuzi
 
Back
Top Bottom