Tulia Ackson aache upotoshaji, Kiti cha Naibu Spika kiko wazi kikatiba

Tulia Ackson aache upotoshaji, Kiti cha Naibu Spika kiko wazi kikatiba

.......Sheria iliyotungwa na bunge....
haya maneno mbona Unayaruka!!??? Tulia yupo sahihi usikitazame hichi kifungu kwa mrengo wa kichama Hakuna Sheria inayomzuia naibu spika kugombea kiti cha uspika
Ahsante sana...

Nimeshangaa sana watu wanashindwa kuona hiyo phrase... wanadhani imewekwa kwa bahati mbaya!

The problem watu wameweka akili yao YOOOOTE kwenye katiba huku wakisahau almost kila Ibara, inatungiwa sheria zake na ndo maana kila ibara kwenye katiba kushito wanataja sheria inayo-govern ibara husika!!
 
Hoja ya Naibu spika Dr. Tulia inasimama kwenye maneno mafupi anayoyachagua bila kumaliza yote katika Ibara ya 84(2) ya katiba. Maneno aliyoyachagua katika Ibara hiyo haijatoa katazo la moja kwa moja kwa Naibu spika kugombea Uspika. Waliokatazwa kwakutaja moja kwa moja ni Waziri au Naibu waziri lakini ibara hiyohiyo ina maneno mengine ili ikamilike, ambayo yanazuia watu wengine kugombea uspika kwakutumia maneno yasemayo, "..........au mtu mwenye madaraka ya aina nyingine yoyote yatakayotajwa na Sheria iliyotungwa na Bunge kwa madhumuni ya Ibara hiyo, huyu ndio hataweza kuchaguliwa kuwa Spika".

Dr. Tulia ni mwanasheria anatumia udhaifu wa Watanzania wachache na hasa Wabunge wenzake waliowengi ambao ni mbumbumbu wa Sheria anawarubuni kuwa Katiba ya Tanzania haijamzuia yeye Naibu Spika kugombea Uspika. Hivyo anaamua kutojiuzulu kwanza Unaibu Spika ndipo agombee, badala yake anaamua kwenda navyo pacha.

Dr. Tulia anajenga hoja kwamba hakuna sheria ya Bunge inayomzuia. Lakini kikatiba ni kwamba, kwa kuwa hakuna sheria iliyotungwa na Bunge kumzuia Naibu Spika kuchaguliwa kuwa Spika, ni wazi kuwa Kisheria tunalazimika kuitumia Katiba kuwa sheria kwakuwa Katiba ni sheria MAMA. Sasa kwa Mujibu wa Ibara ya 84 (2) inayosema waliokatazwa ni Waziri au Naibu waziri au mtu mwenye madaraka ya aina nyingine yoyote yatakayotajwa na Sheria iliyotungwa na Bunge kwa madhumuni ya Ibara hiyo. Maneno ya kikatiba kwamba "au mtu mwenye madaraka ya aina nyingine yoyote itakayotajwa na sheria.....", yana nguvu za kisheria.

Baada ya hapo turejee kwenye katiba, cheo cha Naibu Spika kinatambuliwa na katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Ibara ya 85 (1). Isemayo, 85.-(1) Kutakuwa na Naibu wa Spika wa Bunge ambaye atachaguliwa na wajumbe kutoka miongoni mwa Wabunge.

Hivyo ndio kusema kinatambuliwa Katiba ambayo ni sheria MAMA, na kwahivyo, Naibu Spika anaingia kwenye kundi la wanaokatazwa kugombea Uspika kupitia Ibara ya 84 (2) kwa maneno ya kikatiba yasemayo "au mtu mwenye madaraka ya aina nyingine yoyote itakayotajwa na sheria....."

Kuna athari nyingi za kisheria, kimantiki na kimaslahi ikiwa Naibu Spika ataachwa aendelee na mchakato wa kugombea Uspika,

1. Ni wakati gani Naibu Spika ataachia kiti chake ili kujinadi na kupigiwa kura kuwa Spika?

2. Je wakati anaomba kura na zoezi la kura likiwa linaendelea je ataendelea kuwa Naibu Spika?

3. Iwapo Naibu spika aamue kutokujihuzulu wakati wa mchakato wa kura mpaka matokeo kutangazwa na akashinda, maana yake ni kwamba, kwa vyovyote vile kuna muda walau hata wa dakika moja atakuwa ameshika vyeo vyote viwili kwa pamoja.

4. Mchakato hauwezi kuwa huru sana, hata kuanzia kwenye chama chake kwa kuwa watalazimika kujadili intergrity ya mtu ambaye bado ni kiongozi, je implication ya chama chake au bunge kutompitisha ni yapi?

Ukisoma ibara ya 85(4) a to c, zimeelezea events za Naibu speaker kupoteza mamlaka yake. Kitendo cha yeye kuchukua fomu kugombea U-Speaker, it means kinamfanya apoteze mamlaka yake ya Unaibu Speaker chini ya Ibara ya 85(4)(b).

Wako wanaodhani kuwa kwakuwa kachukua fomu tu kwenye Chama chake basi hajavunja sheria ambayo ndio Katiba, hadi angalau apitishwe na chama chake ndio anaweza kujiuzulu. Nooo mchakato wa Kugombea kisheria na Kikatiba unaanzia pale dakika ya kwanza unapochukua fomu tu kwenye chama chako.

Ukweli unabaki kuwa, Mamlaka ya Speaker & Deputy Speaker yamewekwa na Katiba ya JMT.
Under common Jurisprudence ya Katiba ya Tanzania haiwezekani mtu mmoja kushikiria hizi mamlaka 2 kwa wakati mmoja. Hata kwa sekunde moja tu.

Ikitokea Tulia akapata U Speaker, automatically anakua ni Speaker na Naibu Speaker at the same time, this is Constitutional breach. She is supposed to resign her current position in order to be eligible to contest nafasi ya U- Speaker.

Ili kuelewa zaidi Msimamo wa Kikatiba na Kisheria, Soma kwa Construction approach kwa pamoja Vifungu vifauatavyo;

1. Ibara ya 84 Katiba.

2. Ibara ya 85(1&2) Katiba.

3. Kif.41(2) Sheria ya Kinga, Haki na Madaraka ya Bunge.

4. Ibara 149(1)(c) Katiba.

Swali la kujiuliza ni Je, Kujiuzulu kwa Spika Ndugai kumefuta na Naibu wake Tulia Ackson automatically?

Kama Tulia hajafutiwa madaraka yake, je anagombeaje nafasi ya Spika wakati yeye kwa sasa ndiye anakaimu nafasi ya Spika kwa Kifungu cha 41 cha Sheria ya Madaraka ya Bunge.

Na Yericko Nyerere

View attachment 2080587
View attachment 2080589
View attachment 2080590
Kwa kuchukua fomu ya uspika maana yake ameshajiuzulu nafasi yake ya unaibu spika au?
 
Hata wakati wa kumpandikiza Unaibu Spika ilikuwa hivihivi.
Ndugai, katika unafiki wake, alimlinda ili asijibu maswali yaliyohusu 'uanachama wake na ushiriki wake katika siasa' akiwa bado Mtumishi wa Serikali; Ofisi ya Mwanasheria Mkuu. Tuliona pia matendo yake ya kujikomba kwa serikali, akiwa Naibu Spika kulifanya kwa makusudi Bunge kuwa dhaifu/duni katika kuisimamia serikali. Ninachokiona ni kuwa ushetani wa Tulia wazidi kuwekwa hadharani ili kutuepusha kama TAIFA kuzama zaidi huko ambako kwa uroho wake, anajitahidi kutupeleka.
Mkono wa Mungu unaendelea kutenda kazi. AMEN
sukuma gang mnahali mbaya sana aisee
 
Katibu wa bunge halioni hilo? au na yeye ni pangu pakavu kwenye Sheria na katiba?
Hako kadada ni karoho na kalafi sana,kanaweza kutemea mate chakula ili wengine wasile
 
Kwa kuchukua fomu ya uspika maana yake ameshajiuzulu nafasi yake ya unaibu spika au?
Naona hujajibiwa...

In short, Tulia hajavunja Ibara yoyote ya katiba wala sheria yoyote!

Ipo hivi...

Ibara karibu zote huwa zinatungiwa sheria! Sasa hiyo Ibara aliyoiweka Yericko, moja kwa moja inamkataza Waziri na Naibu Waziri kugombea Uspika! Hata hivyo, ibara husika haijasema chochote kuhusu Naibu Spika kukatazwa au kuruhusiwa!

Lakini kama nilivyosema hapo awali, karibu kila ibara hutungiwa sheria na ndo maana ibara husika inasema:-
Waziri, Naibu Waziri au mtu mwenye madaraka ya aina nyingine yoyote itakayotajwa na Sheria iliyotungwa na Bunge kwa madhumuni ya ibdara hii, hataweza kuchaguliwa kuwa Spika.
Hapo maana yake ni kwamba, Waziri na Naibu Waziri, kwa mujibu wa katiba HAWEZI kuchaguliwa kuwa Spika!! Wengine waliozuiliwa KAMA WAPO, basi watakuwa wametajwa na na sio Katiba. Kwahiyo mtu akitaka kusema fulani na fulani ambao sio mawaziri/manaibu waziri hawaruhusiwi kuchaguliwa kuwa spika, wanatakiwa kuonesha Sheria #12 ya mwaka 1995 Ibara ya 15, na sio katiba tena kwa sababu katiba, hususani kwa kifungu husika, kinamkataza Waziri na Naibu Waziri TU!
 
Hoja ya Naibu spika Dr. Tulia inasimama kwenye maneno mafupi anayoyachagua bila kumaliza yote katika Ibara ya 84(2) ya katiba. Maneno aliyoyachagua katika Ibara hiyo haijatoa katazo la moja kwa moja kwa Naibu spika kugombea Uspika. Waliokatazwa kwakutaja moja kwa moja ni Waziri au Naibu waziri lakini ibara hiyohiyo ina maneno mengine ili ikamilike, ambayo yanazuia watu wengine kugombea uspika kwakutumia maneno yasemayo, "..........au mtu mwenye madaraka ya aina nyingine yoyote yatakayotajwa na Sheria iliyotungwa na Bunge kwa madhumuni ya Ibara hiyo, huyu ndio hataweza kuchaguliwa kuwa Spika".

Dr. Tulia ni mwanasheria anatumia udhaifu wa Watanzania wachache na hasa Wabunge wenzake waliowengi ambao ni mbumbumbu wa Sheria anawarubuni kuwa Katiba ya Tanzania haijamzuia yeye Naibu Spika kugombea Uspika. Hivyo anaamua kutojiuzulu kwanza Unaibu Spika ndipo agombee, badala yake anaamua kwenda navyo pacha.

Dr. Tulia anajenga hoja kwamba hakuna sheria ya Bunge inayomzuia. Lakini kikatiba ni kwamba, kwa kuwa hakuna sheria iliyotungwa na Bunge kumzuia Naibu Spika kuchaguliwa kuwa Spika, ni wazi kuwa Kisheria tunalazimika kuitumia Katiba kuwa sheria kwakuwa Katiba ni sheria MAMA. Sasa kwa Mujibu wa Ibara ya 84 (2) inayosema waliokatazwa ni Waziri au Naibu waziri au mtu mwenye madaraka ya aina nyingine yoyote yatakayotajwa na Sheria iliyotungwa na Bunge kwa madhumuni ya Ibara hiyo. Maneno ya kikatiba kwamba "au mtu mwenye madaraka ya aina nyingine yoyote itakayotajwa na sheria.....", yana nguvu za kisheria.

Baada ya hapo turejee kwenye katiba, cheo cha Naibu Spika kinatambuliwa na katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Ibara ya 85 (1). Isemayo, 85.-(1) Kutakuwa na Naibu wa Spika wa Bunge ambaye atachaguliwa na wajumbe kutoka miongoni mwa Wabunge.

Hivyo ndio kusema kinatambuliwa Katiba ambayo ni sheria MAMA, na kwahivyo, Naibu Spika anaingia kwenye kundi la wanaokatazwa kugombea Uspika kupitia Ibara ya 84 (2) kwa maneno ya kikatiba yasemayo "au mtu mwenye madaraka ya aina nyingine yoyote itakayotajwa na sheria....."

Kuna athari nyingi za kisheria, kimantiki na kimaslahi ikiwa Naibu Spika ataachwa aendelee na mchakato wa kugombea Uspika,

1. Ni wakati gani Naibu Spika ataachia kiti chake ili kujinadi na kupigiwa kura kuwa Spika?

2. Je wakati anaomba kura na zoezi la kura likiwa linaendelea je ataendelea kuwa Naibu Spika?

3. Iwapo Naibu spika aamue kutokujihuzulu wakati wa mchakato wa kura mpaka matokeo kutangazwa na akashinda, maana yake ni kwamba, kwa vyovyote vile kuna muda walau hata wa dakika moja atakuwa ameshika vyeo vyote viwili kwa pamoja.

4. Mchakato hauwezi kuwa huru sana, hata kuanzia kwenye chama chake kwa kuwa watalazimika kujadili intergrity ya mtu ambaye bado ni kiongozi, je implication ya chama chake au bunge kutompitisha ni yapi?

Ukisoma ibara ya 85(4) a to c, zimeelezea events za Naibu speaker kupoteza mamlaka yake. Kitendo cha yeye kuchukua fomu kugombea U-Speaker, it means kinamfanya apoteze mamlaka yake ya Unaibu Speaker chini ya Ibara ya 85(4)(b).

Wako wanaodhani kuwa kwakuwa kachukua fomu tu kwenye Chama chake basi hajavunja sheria ambayo ndio Katiba, hadi angalau apitishwe na chama chake ndio anaweza kujiuzulu. Nooo mchakato wa Kugombea kisheria na Kikatiba unaanzia pale dakika ya kwanza unapochukua fomu tu kwenye chama chako.

Ukweli unabaki kuwa, Mamlaka ya Speaker & Deputy Speaker yamewekwa na Katiba ya JMT.
Under common Jurisprudence ya Katiba ya Tanzania haiwezekani mtu mmoja kushikiria hizi mamlaka 2 kwa wakati mmoja. Hata kwa sekunde moja tu.

Ikitokea Tulia akapata U Speaker, automatically anakua ni Speaker na Naibu Speaker at the same time, this is Constitutional breach. She is supposed to resign her current position in order to be eligible to contest nafasi ya U- Speaker.

Ili kuelewa zaidi Msimamo wa Kikatiba na Kisheria, Soma kwa Construction approach kwa pamoja Vifungu vifauatavyo;

1. Ibara ya 84 Katiba.

2. Ibara ya 85(1&2) Katiba.

3. Kif.41(2) Sheria ya Kinga, Haki na Madaraka ya Bunge.

4. Ibara 149(1)(c) Katiba.

Swali la kujiuliza ni Je, Kujiuzulu kwa Spika Ndugai kumefuta na Naibu wake Tulia Ackson automatically?

Kama Tulia hajafutiwa madaraka yake, je anagombeaje nafasi ya Spika wakati yeye kwa sasa ndiye anakaimu nafasi ya Spika kwa Kifungu cha 41 cha Sheria ya Madaraka ya Bunge.

Na Yericko Nyerere

View attachment 2080587
View attachment 2080589
View attachment 2080590
Unaharaka na papara sana
Dr. Tulia anagombea Uspika wapi?
 
Haiwezekani mtu anavunja katiba na anaachwa tu na wanasheria wapo na chama chao kimekaa kimya.

Tabia hii ya kuwaacha hawa waarifu wa kikatiba ndio inafanya tuwe laugh stock of East Africa,mko wapi wanasheria?

Pelekeni hii kesi mahakamani ASAP!
Tumia akili kidogo ndugu yangu na uuache mihemuko- Tulia anagombea Uspika wapi? au ameomba kuteuliwa ili akagombee Uspika- Una fail wapi?
 
Tumia akili kidogo ndugu yangu na uuache mihemuko- Tulia anagombea Uspika wapi? au ameomba kuteuliwa ili akagombee Uspika- Una fail wapi?
Hiyo process tu ya kupitia kwenye chama inamuweka kwenye orodha ya wagombea.

Ina maana akiingia bungeni tayari anakuwa ni mgombea,kaimu na naibu spika! Na katiba hairuhusu ata kwa dakika moja mtu mmoja kuwa ivyo,maana najua wajinga wengi wanatetea eti atajihudhuru ndani ya bunge,tayari ni kosa!

Ungelijua hili usingeandika tu km headless chicken
 
Hiyo process tu ya kupitia kwenye chama inamuweka kwenye orodha ya wagombea.

Ina maana akiingia bungeni tayari anakuwa ni mgombea,kaimu na naibu spika! Na katiba hairuhusu ata kwa dakika moja mtu mmoja kuwa ivyo,maana najua wajinga wengi wanatetea eti atajihudhuru ndani ya bunge,tayari ni kosa!

Ungelijua hili usingeandika tu km headless chicken
Unahaki na maoni yako- ukweli unabaki pale pale Tulia hagombei Uspika bali anaomba kuteuliwa kugombea Uspika.
 
Back
Top Bottom