Uchaguzi 2020 Tulia uliambiwa hukusikia, ukalazimisha kugombea Mbeya

Huihui2

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2012
Posts
7,021
Reaction score
11,475
Your browser is not able to display this video.

CCM ilifanya makosa ya wazi kulazimisha Tulia Ackson agombee Mbeya ili kumtoa Sugu. Kuna sababu 4:-

1. Siyo mzawa wa Mbeya kwa kuwa anatokea Rungwe. Hata ukisema Tanzania hakuna ukabila lakini Wasafwa ambao ndiyo wengi hawawezi kumpa kura Tulia Mnyakyusa, bora wampe Mpangwa Sugu.

2. Mfumo dume. Hata kwao Rungwe wasingempa mwanamke kutokana na mila zao.

3. Taswira ya Tulia kama Naibu Spika. Ametumika sana kuwakandamiza wapinzani kwa kuwanyima nafasi ya kuongea, kuwafukuza kwenye vikao na kupuuza hoja zao

4. Kura 100,000 za Sugu za mwaka 2015. Hawa watu waliomfanya Sugu awe the most voted MP bado wapo na Sugu hajawakwaza.

Sioni namna Tulia atapata kura za Mbeya Mjini.
 
Mmeanza ukabila sasa? Mmeshindwa kwa hoja!
 
Kazi ipo!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…