UMUGHAKA
JF-Expert Member
- Sep 1, 2021
- 2,753
- 12,932
- Thread starter
-
- #1,801
Kwanza kabisa nawashukuru sana ndugu zangu wote mnaopongeza uzi huu na kutoa shukurani kedekede!,ningependa mtambue ya kwamba kwangu pesa si kipaumbele ingawaje nazihitaji pesa ili kufikia vipaumbele vyangu!.Wengi walitaka angalau nitoze kiasi cha fedha,ndugu zangu sijaja hapa JF kwa ajili ya fedha,ingawa fedha ikinifuata siwezi kuikataa kwasababu pia tunakesha tukiitafuta!,Lengo la huu uzi ni kukufunza,kukuburudisha na kukuelimisha!.Nilihitaji watu wapate shule kwa yale wengine tuliyopitia huko vijijini!.
Sasa Kuna mambo baadhi naona yamewatatanisha watu au wamesshindwa kuelewa!.
1.Kulipia kiasi cha Tsh 100 kwenye banda,vijana wa 2000 wanasema haiwezekani.
2.Monica kutembea usiku ingawaje ni mtoto wa kike.
3.Msukuma kumiliki Ng'ombe zaidi ya elfu 10,vijana wa 2000 wanasema haiwezekani!.
4.Kucharazwa viboko mbele ya wanafunzi kwa kosa la nyumbani,pia vijana wa 2000 wanasema haiwezekani!.
NAOMBA KABLA SIJAJIBU NITOE KISA KIFUPI!.
Mwaka 2000 kuna kaka yangu mtoto wa baba mkubwa kazi yake ilikuwa kuzibua vyoo(mzibua vyoo)Ingawa sikuhizi ameacha,kazi hii ilimpatia pesa za kutosha kwa miaka hiyo kwasababu pale wilayani ni kampuni yao ndiyo ilikuwa ikifahamika kwa shughuli hiyo!.
Sasa nakumbuka siku moja Mzee wangu alimuita yeye na watu wa kampuni yake pale nyumbani kuja kuzibua chemba ambayo ilikuwa kwa ajili ya nyumba ya wapangaji!,pamoja na kuja kuzibua ile chemba lakini pia walitakiwa kuchora ramani kwa ajili ya kujenga chemba(shimo)nyingine!..Mzee alitaka yale mashimo yawe na uwezo wa kupokea mzigo mkubwa na ndiyo maana akataka shimo lingine liongezwe!.
Basi kazi ya kuchora ramani ikaanza,ilikuwa mida ya saa 1 asubuhi!,walikamilisha kuchora ramani saa 1:20 Asubuhi,sasa kazi rasmi ya kuchoronga na kuchimba shimo jipya ikaanza!.Sasa wakati shimo linachimbwa nakumbuka tukawa tunapiga stori za kufa mtu!,wakati wao wanachimba mimi kazi yangu ilikuwa ni kutizama na kuchangia kwenye stori walizokuwa wakipiga!,ilikuwa wakihamia kwenye mademu na mimi najifanya kuchangia kana kwamba hao mademu hata ninaweza kuwamudu!,walikuwa wakihamia kwenye siasa na mimi nimo!,wakienda kwenye habari za magari na mimi nimo!.
Sasa kuna muda mada za kaka yangu huyo na wale jamaa wenzie zikaamia kwenye vyakula,na mimi nikawa mchangiaji!.
Brother "Yanii muda huu nikipata donati 10 na vikombe angalau vitatu vya chai ya maziwa ndipo moyo wangu utasuuzika"
Basi baada ya kusikia ile kauli umughaka mimi nikaanza kumzodoa brother huku nikibisha,sasa kiukweli kukawa na ubishani mkubwa mno!.
Brother alikuwa akisema kwamba anao uwezo wa kumaliza Donati 10 na vikombe 3 vya chai ya maziwa!,mimi nilikuwa ninabisha,wale wenzie wakanitaka tusiandikie mate wakati wino upo!.wakapendekeza tuweke dau la kila mmoja shilingi elfu 2,kwa mwaka huo nadhani ndugu zangu mtaelewa namna shilingi elfu 2 ilivyokuwa na thamani!.
Sasa tukakubaliana ya kwamba,ikifika saa 5 asubuhi tuelekee mjini kwa ajili ya kumnunulia brother donati 10 na vikombe vitatu vya chai ya maziwa,donati wakati huo kwa moja ilikuwa inauzwa Tsh 200,na chai ya maziwa kikombe ilikuwa inauzwa Tsh 100,na endapo asipoweza kumaliza basi angelipia hela niliyokuwa nimenunulia vitafunwa vile pale mgahawani na angenipatia Tsh elfu 2 kama tulivyokubaliana!.
Ilipofika mida hiyo kweli tukaelekea mjini kwa ajili ya kuupa muda na nafasi kwa ajili ya ule ubishi wangu kwa brother!.Niliagiza vile vitafunwa kama tulivyokuwa tumekubaliana!.
Ilikuwa ni ajabu kumuona brother akimaliza zile donati ndani ya muda mfupi kuliko nilivyodhani!,vile vikombe vya chai ya maziwa vilimpungua ikabidi nimuongezee vingine vitatu!,wakati huo kamaliza zile donati 10 ambazo mle kwenye mgahawa kila mtu alibaki kumshangaa kama ni binadamu wa kawaida au alikuwa kiumbe wa ajabu,cha kushangaza pamoja na kumaliza lakini alidai bado hajashiba hivyo alisema atangojea nyumbania ugali uive ili ajazilizie mapengo ya nafasi tumboni!.
Pamoja na yote lakini pia nilimpatia Tsh elfu 2 kama ilivyokuwa ahadi yetu.
SASA NILICHOTAKA KUSEMA NI NINI?
Tangu siku hiyo huwa sibishi ovyo ovyo tu kama punguani!.Yaani tumbo lako halafu nikubishie?,yaani mimi kama nakula robo wali nianze kubisha wewe kumaliza Nusu wali?,uenda nitakuwa mwendawazimu!.
Sasa nimeamua kuutoa huo mfano ili watu wajifunze jambo,usibishe jambo lolote kama hujawahi kupitia!,yaani wewe uzaliwe Magomeni ambako unashindia kutwa dagaa mchele halafu unambishia mtu aliyekulia huko UKILI GURU anayeshindia mihogo kwamba hawezi kuilima!.
Ikiwa kuna maisha hujawahi kuyaishi nikutaadharishe usije kubisha kwasababu watu watabaki kukushangaa na utaoneka Kituko mbele ya wanaume!.
1.Mimi binafsi nimeanza kushangilia mpira kwenye TV mnamo mwaka 1996 tena wakati huo nilikuwa naipenda sana Liverpool,ila ilipofika mwaka 1998 nikaanza kushabikia timu ya Arsenal!.Sasa mwaka 2004 ninaposema bandani nilikuwa nalipa Tsh 100 naamanisha!,siyo kwamba naigiza ndugu zangu!,na ndiyo maana nikamuomba huyo jamaa anayebisha yeye aje atuambie huo mwaka huko alikokuwa alikuwa analipa kiasi gani?,kama hana majibu basi atulie aache ubishi!,haiwezekani wewe uje uanze kuangalia mpira mwaka 2013 halafu ubishie watu tulioanza kuingia mabandani mwaka 1996!.
2.Suala la Monica kutembea usiku eti mtu anashangaa!,yaani leo mabinti kulala nje na kukesha kwa wanaume unadhani ni jambo jipya?,yaani binti ambaye kwao walikuwa washirikina na hakuwa na baba,yeye kutembea usiku unaona kuna uongo?,watanzania ni nani katuroga?,Mbona alivyolala na Ema pale kwa rafiki yake Jack usiku kucha mpaka kupelekea ugomvi na Deborah hamkuhoji?,mmeona muhoji mimi kukutana naye usiku kule mnadani!,Aiseee kuna sehemu vijana wa hili taifa wanapaswa kurekebisha ili mambo yaende sawa!.
3 Suala la Msukuma kumiliki ng'ombe zaidi ya elfu 10 mwaka 2003-2004 mtu anabisha,huyohuyo mtu ukimuuliza kwamba amewahi kufika Tabora au sehemu nyingine ya usukumani atakwambia bado,halafu anabisha!,na huyu ni msomi mzima anashangaa kabisa!.Atahoji hadi sisi kupewa lita 5 za maziwa bure kila siku pale kwa Headmaster atakwambia ni uongo!,Kama hujawahi kutembea kwenye hii nchi nikuombe usije nyanyua mdomo wako ukabisha!.Kuna mtu ukimwambia pale Geita na Mwanza kuna watu wanahela chafu kuliko huyo anayejiita Mo Dewji bado watakuja hapa kubisha kana kwamba huyo Mo ni baba yake!.
4.Kwamba mimi kuchwapwa mbele ya wanafunzi ilikuwa ni stori ya kutunga!,Hii nchi kuna watu wanashida kubwa mno!,kwamba unataka kusema kwakuwa wewe umekulia na kusomea mjini unadhani watu wote tumesomea mjini?,Kuchwapwa mbele ya kadamnasi haikuwa mjadala!,na wala si mbele ya wanafunzi tu!,yaani stiki ulikuwa unakung'utwa hata sokoni kama ukileleta ukora!,Vijana kama hamjui vitu tuambieni tuwaelekeze muweze kuvifahamu.
Mimi nimesoma shule ya kata isiyokuwa na maabara(laboratory)masomo ya sayansi (pcb) na nilifaulu ufaulu mzuri tu wa dvs 2 sema baadae nilifeli form 6 kwasababu ya mapenzi ya mwanamke wa kitanga.Sasa hivi vijana nyie hamuwezi kufaulu masomo ya sayansi bila maabara!.
KAMA HUJAPITIA MAISHA FULANI USISIMAME NA TUMBO LAKO UKAANZA KUBISHA MBELE YA WANAUME,UTATIA AIBU!.
NI HAYO TU.
Sasa Kuna mambo baadhi naona yamewatatanisha watu au wamesshindwa kuelewa!.
1.Kulipia kiasi cha Tsh 100 kwenye banda,vijana wa 2000 wanasema haiwezekani.
2.Monica kutembea usiku ingawaje ni mtoto wa kike.
3.Msukuma kumiliki Ng'ombe zaidi ya elfu 10,vijana wa 2000 wanasema haiwezekani!.
4.Kucharazwa viboko mbele ya wanafunzi kwa kosa la nyumbani,pia vijana wa 2000 wanasema haiwezekani!.
NAOMBA KABLA SIJAJIBU NITOE KISA KIFUPI!.
Mwaka 2000 kuna kaka yangu mtoto wa baba mkubwa kazi yake ilikuwa kuzibua vyoo(mzibua vyoo)Ingawa sikuhizi ameacha,kazi hii ilimpatia pesa za kutosha kwa miaka hiyo kwasababu pale wilayani ni kampuni yao ndiyo ilikuwa ikifahamika kwa shughuli hiyo!.
Sasa nakumbuka siku moja Mzee wangu alimuita yeye na watu wa kampuni yake pale nyumbani kuja kuzibua chemba ambayo ilikuwa kwa ajili ya nyumba ya wapangaji!,pamoja na kuja kuzibua ile chemba lakini pia walitakiwa kuchora ramani kwa ajili ya kujenga chemba(shimo)nyingine!..Mzee alitaka yale mashimo yawe na uwezo wa kupokea mzigo mkubwa na ndiyo maana akataka shimo lingine liongezwe!.
Basi kazi ya kuchora ramani ikaanza,ilikuwa mida ya saa 1 asubuhi!,walikamilisha kuchora ramani saa 1:20 Asubuhi,sasa kazi rasmi ya kuchoronga na kuchimba shimo jipya ikaanza!.Sasa wakati shimo linachimbwa nakumbuka tukawa tunapiga stori za kufa mtu!,wakati wao wanachimba mimi kazi yangu ilikuwa ni kutizama na kuchangia kwenye stori walizokuwa wakipiga!,ilikuwa wakihamia kwenye mademu na mimi najifanya kuchangia kana kwamba hao mademu hata ninaweza kuwamudu!,walikuwa wakihamia kwenye siasa na mimi nimo!,wakienda kwenye habari za magari na mimi nimo!.
Sasa kuna muda mada za kaka yangu huyo na wale jamaa wenzie zikaamia kwenye vyakula,na mimi nikawa mchangiaji!.
Brother "Yanii muda huu nikipata donati 10 na vikombe angalau vitatu vya chai ya maziwa ndipo moyo wangu utasuuzika"
Basi baada ya kusikia ile kauli umughaka mimi nikaanza kumzodoa brother huku nikibisha,sasa kiukweli kukawa na ubishani mkubwa mno!.
Brother alikuwa akisema kwamba anao uwezo wa kumaliza Donati 10 na vikombe 3 vya chai ya maziwa!,mimi nilikuwa ninabisha,wale wenzie wakanitaka tusiandikie mate wakati wino upo!.wakapendekeza tuweke dau la kila mmoja shilingi elfu 2,kwa mwaka huo nadhani ndugu zangu mtaelewa namna shilingi elfu 2 ilivyokuwa na thamani!.
Sasa tukakubaliana ya kwamba,ikifika saa 5 asubuhi tuelekee mjini kwa ajili ya kumnunulia brother donati 10 na vikombe vitatu vya chai ya maziwa,donati wakati huo kwa moja ilikuwa inauzwa Tsh 200,na chai ya maziwa kikombe ilikuwa inauzwa Tsh 100,na endapo asipoweza kumaliza basi angelipia hela niliyokuwa nimenunulia vitafunwa vile pale mgahawani na angenipatia Tsh elfu 2 kama tulivyokubaliana!.
Ilipofika mida hiyo kweli tukaelekea mjini kwa ajili ya kuupa muda na nafasi kwa ajili ya ule ubishi wangu kwa brother!.Niliagiza vile vitafunwa kama tulivyokuwa tumekubaliana!.
Ilikuwa ni ajabu kumuona brother akimaliza zile donati ndani ya muda mfupi kuliko nilivyodhani!,vile vikombe vya chai ya maziwa vilimpungua ikabidi nimuongezee vingine vitatu!,wakati huo kamaliza zile donati 10 ambazo mle kwenye mgahawa kila mtu alibaki kumshangaa kama ni binadamu wa kawaida au alikuwa kiumbe wa ajabu,cha kushangaza pamoja na kumaliza lakini alidai bado hajashiba hivyo alisema atangojea nyumbania ugali uive ili ajazilizie mapengo ya nafasi tumboni!.
Pamoja na yote lakini pia nilimpatia Tsh elfu 2 kama ilivyokuwa ahadi yetu.
SASA NILICHOTAKA KUSEMA NI NINI?
Tangu siku hiyo huwa sibishi ovyo ovyo tu kama punguani!.Yaani tumbo lako halafu nikubishie?,yaani mimi kama nakula robo wali nianze kubisha wewe kumaliza Nusu wali?,uenda nitakuwa mwendawazimu!.
Sasa nimeamua kuutoa huo mfano ili watu wajifunze jambo,usibishe jambo lolote kama hujawahi kupitia!,yaani wewe uzaliwe Magomeni ambako unashindia kutwa dagaa mchele halafu unambishia mtu aliyekulia huko UKILI GURU anayeshindia mihogo kwamba hawezi kuilima!.
Ikiwa kuna maisha hujawahi kuyaishi nikutaadharishe usije kubisha kwasababu watu watabaki kukushangaa na utaoneka Kituko mbele ya wanaume!.
1.Mimi binafsi nimeanza kushangilia mpira kwenye TV mnamo mwaka 1996 tena wakati huo nilikuwa naipenda sana Liverpool,ila ilipofika mwaka 1998 nikaanza kushabikia timu ya Arsenal!.Sasa mwaka 2004 ninaposema bandani nilikuwa nalipa Tsh 100 naamanisha!,siyo kwamba naigiza ndugu zangu!,na ndiyo maana nikamuomba huyo jamaa anayebisha yeye aje atuambie huo mwaka huko alikokuwa alikuwa analipa kiasi gani?,kama hana majibu basi atulie aache ubishi!,haiwezekani wewe uje uanze kuangalia mpira mwaka 2013 halafu ubishie watu tulioanza kuingia mabandani mwaka 1996!.
2.Suala la Monica kutembea usiku eti mtu anashangaa!,yaani leo mabinti kulala nje na kukesha kwa wanaume unadhani ni jambo jipya?,yaani binti ambaye kwao walikuwa washirikina na hakuwa na baba,yeye kutembea usiku unaona kuna uongo?,watanzania ni nani katuroga?,Mbona alivyolala na Ema pale kwa rafiki yake Jack usiku kucha mpaka kupelekea ugomvi na Deborah hamkuhoji?,mmeona muhoji mimi kukutana naye usiku kule mnadani!,Aiseee kuna sehemu vijana wa hili taifa wanapaswa kurekebisha ili mambo yaende sawa!.
3 Suala la Msukuma kumiliki ng'ombe zaidi ya elfu 10 mwaka 2003-2004 mtu anabisha,huyohuyo mtu ukimuuliza kwamba amewahi kufika Tabora au sehemu nyingine ya usukumani atakwambia bado,halafu anabisha!,na huyu ni msomi mzima anashangaa kabisa!.Atahoji hadi sisi kupewa lita 5 za maziwa bure kila siku pale kwa Headmaster atakwambia ni uongo!,Kama hujawahi kutembea kwenye hii nchi nikuombe usije nyanyua mdomo wako ukabisha!.Kuna mtu ukimwambia pale Geita na Mwanza kuna watu wanahela chafu kuliko huyo anayejiita Mo Dewji bado watakuja hapa kubisha kana kwamba huyo Mo ni baba yake!.
4.Kwamba mimi kuchwapwa mbele ya wanafunzi ilikuwa ni stori ya kutunga!,Hii nchi kuna watu wanashida kubwa mno!,kwamba unataka kusema kwakuwa wewe umekulia na kusomea mjini unadhani watu wote tumesomea mjini?,Kuchwapwa mbele ya kadamnasi haikuwa mjadala!,na wala si mbele ya wanafunzi tu!,yaani stiki ulikuwa unakung'utwa hata sokoni kama ukileleta ukora!,Vijana kama hamjui vitu tuambieni tuwaelekeze muweze kuvifahamu.
Mimi nimesoma shule ya kata isiyokuwa na maabara(laboratory)masomo ya sayansi (pcb) na nilifaulu ufaulu mzuri tu wa dvs 2 sema baadae nilifeli form 6 kwasababu ya mapenzi ya mwanamke wa kitanga.Sasa hivi vijana nyie hamuwezi kufaulu masomo ya sayansi bila maabara!.
KAMA HUJAPITIA MAISHA FULANI USISIMAME NA TUMBO LAKO UKAANZA KUBISHA MBELE YA WANAUME,UTATIA AIBU!.
NI HAYO TU.