W
View attachment 1597425
Mdau najua wewe ni shahidi.Kila makao makuu ya mkoa anapopita Mgombea wa CCM na mgombea mwenza kumekuwa na tabia ya kuachisha masomo wanafunzi na kusombwa kuhudhulia mkutano.
Hii sio haki kwani hii ni mikutano ya kichama na inavuruga mwenendo wa masomo yao.
Mwalimu mmoja jana akanitaka kama nipo karibu na Tundu Lissu nimuombe akemee jambo hili ili lisiendelee. Nami nimemtaka Mtumishi wetu Tundu Lissu akeeme jambo hili haraka,kama ulivyokemea udhalilishaji kwa kina mama nk.
Weka ushahidi wa picha .
Lakini pia uchaguzi wa mwaka huu Watanzania wanauchukulia poa lakini huu ni uchaguzi kati ya wema na ubaya.
Ni kati ya waliotenda mabaya kwa nusu karne na waliotendewa mabaya . Waliofurahiya Kuuawa kwa akina Alfonsi Mawazo ,Azori Gwanda, Ben Saanane na kupigwa risasi Tundu Lisu nldhidi ya wale waliohuzunishwa.
Ni uchaguzi kati ya Wasiopenda haki dhidi ya wapenda haki!
Ni uchaguzi kati ya wanaolipwa mishahara mikubwa serikalini dhidi ya wale wanaolipwa kishahara isiyotosha kula kwa Siku mbili Mjini Dodoma kwa Wabunge na mawaziri.
Mwaka huu ni uchaguzi kati ya Ubaguzi wa Kivyama na Usawa.
Ubaguzi kati ya visasi na msamaha.
Kifupi kama miaka mitano iliyopita ya utawala wa awamu hii ilikua na mambo mema na ya amani basi wakirudi tena yatakua mema mara dufu . Lakini kama ya yalikua kabaya basi watu wajiandae . Kama walipigwa risasi mchana kweupe kwa wakati ambao watu walikua wanautukuza utawala wao basi wajiandae wakati huu ambao watu wamejitokeza hadharani kwa maelfu kumwita Lisu Rais.
Kumbukeni wale walioimba tunaimani na Lowasa walifanywaje na alisema waoitakiwa wafanyweje?
Atakayelunusuru Taifa hili ni Mungu pekee lakini kuwategemea Watu wanaowaza Madaraka na mali tuu ni vigumu sana kulirejesha taifa hili kwenye maisha ya upendo ,haki,amani na umoja!
Miaka mitano Bunge limehubiri Chuki kwa vitendo mpaka kuombeana watu kuuawa, serikali imehubiri chuki kwa vitendo kwa kupuuza wanapouawa wapinzani au kupigwa .
Watanzania ni vyema kabisa tukaipumzisha CCM na wabunge wake ili wajifunze kuwa wao ni binadam kama walivyowengine! Lakini kwa hali ilivyokuwa au itakavyokuwa CCM wakirudi watahalalisha kila aina ya uovu waliokua wanaufanya na na mateso yatakua ni jambo la kawaida. Pia CCM itakua na maandalizi ya kumpata wa 2025 - 2030 ambapo watumia kila hila kuwapata watakaowalinda.
Wakirejea CCM kwa hila na sifa wanazozipata kwa kuzuia vyombo vya habari kuwapa wananchi fursa ya kupata taarifa za upande wa Pili hali itakua tete sana.