Tulimsingizia na kumhukumu Hayati Magufuli juu ya utekaji, Je leo tutamsingizia nani? Magufuli hayupo

Vyombo tulivyoviamini visipofanya kazi zake kwa weledi wataendelea tuu kusingiziwa "kama ni kweli" tuliowapa dhamana ya kusimamia ulinzi wa uhai na mali zetu,mbona hili ni rahisi sana.
 
Kwa hiyo mtekaji ni nani sasa? Manake polisi hawahusiki, TISS hawahusiki, JW security unit hawahusiki. Mkuu wa nchi ambaye ndiyo sauti ya mwisho nchi hii naye anasema hii kitu ni drama. Kama ni vyama vya upinzani mbona hawakamatwi? Shida Iko wapi?
utatafuta majibu hapa hautapata vitu kama hivi huwa ni siri labda tu apatikane mtu anaejua aamue kushusha mambo hadharani ila wao wanajua ni nani,kwanini,wapi na sangapi!.

na hata mtu akiweza kujibu yote hayo watakutafuta!!, usionyeshe kipaji chako kwa kuandika isipokuwa kipaji chako ndio kinatakiwa kiandike!.
 
Magufuli hakusingiziwa. Kama ilikuwa haki kumsifu kwa zuri lolote lililofanyika, hali kadhalika ni haki kumlaumu kwa baya lolote lililofanyika. Na kwa principal ya M/Mungu ilivyo lazima atawajibika hamna namna. Labda kama alitubu, lakini kwa kiburi kile sidhani.
 
Kwamba ameiponya nchi na pamoja na Mbowe kufunguliwa wakati wa Samia lakini wakadai oda ilikuwa imetolewa kabla Magu hajafa.

Mungu Fundi sana naona aliyekuwa anaponya nchi ana haki ya kuagiza raia wake wauawe.

Ni kweli hata Magu alifanya makosa makubwa sana kuruhusu utekaji uwe mwingi kiasi kile. Lakini kwa sasa utekaji unatisha mwanzo tulijifanya hatuoni lakini mambo ndo yanazidi kuwa mambo. Hili linchi kwa sasa linajiendea tu halina mwenyewe, rasilimali za nchi zinaporwa na kupewa wageni huku tena tunauliwa jama kuku. Eti tuna usalama wa taifa, huo sio usalama wa taifa ni usalama wa ccm na viongozi wake.
 
Unauzungumziaje hii ya Mzee kibao kutekwa mchana kweupe kwenye bus nani unazani atakuwa muhusika
 
1. Kuna uwezekano ilifanyika kuonesha JPM ndo alikuwa mbaya ili kupata uungwaji mkono dhidi ya upinzani na mahasimu wa JPM kwenye chama kwa wakati huo
2. Sasa inawezekana reverse is true. Mahasimu wa Her Excellence ndani ya chama wameungana na wapinzani kuonesha kutokuwa na uwezo wa kuwa comfort in chief Kwa kushindwa kidhibiti uhalifu nchini hata kama unafanywa na genge la wahuni wakitokea walikotokea
3. Mama anahitaji kupata washauri wazuri asije akavurugwa halafu wahuni waseme ameshindwa kazi, hafai kuendelea 2025
 
Walimchafua Magufuli ili watimize malengo na walifanikiwa kwakua uelewa wa watu wengi sio mkubwa.

Anyways Yanga Bingwa tena.
 
Kosa la mzee wetu hayati lilikuwa sio kuteka, bali kukaa kimya na watu waka-assume yy ndio anayetoa order. Isemwe tu kama kuna kikosi rogue kimetengenezwa tujue moja
Upumbavu mwingine! Unajua nguvu alizonazo rais? Unajua vyombo vyote vya ulinzi na usalama viko chini yake? Unajua kuwa ana uwezo wa kuomba hata Scotland Yard waje kusaidia? Yule mpumbavu Magufuli alikuwa muuaji na kipindi chake utekaji ndiyo ulizidi.
 
Upumbavu mwingine! Unajua nguvu alizonazo rais? Unajua vyombo vyote vya ulinzi na usalama viko chini yake? Unajua kuwa ana uwezo wa kuomba hata Scotland Yard waje kusaidia? Yule mpumbavu Magufuli alikuwa muuaji na kipindi chake utekaji ndiyo ulizidi.
Sawa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…