Tuliomtetea Kabendera tumwombe radhi mwendazake, Naanza na Pascal Mayalla nisamehe Mkuu

Tuliomtetea Kabendera tumwombe radhi mwendazake, Naanza na Pascal Mayalla nisamehe Mkuu

Kumshauri mhanga afanye anchotaka yeye si kumuonea huruma.
Ninyi mashujaa wa mitandaoni ambao mko huru mnakula kunywa na kuwa karibu na familia zenu mnataka mwenzenu aoneshe ushujaa kwa gharama ya mateso makubwa.

Mkiombwa muandamane aachiwe mnaogopa kukamatwa na kwenda jela mnakomshauri aendelee kukaa. Ninyi hamtaki kuwa mashujaa?
Tangu Lini ccm mkawa na huruma kwa Freeman Mbowe?! Na kama mna huruma kiasi hicho basi mshaurini mtemi hangaya amfutie mashtaka ya kubumba bila masharti yoyote na sio kumtega Mbowe aombe msamaha kwa tuhuma tu bila udhibitisho wa kutenda makosa
 
Kuomba radhi bila kujua kosa lako ni jambo baya sana, hasa mtu anapotoa kauli ya jumla kuwa fulani yuko ndani kwa sababu hana heshima, ni heshima gani hiyo aliyoikosa inayomgharimu kukaa jela zaidi ya miezi minne? ni vyema aijue ili kama akitolewa asijekurudia kosa bila kujua.

Habari ya Kabendera kuachiwa baada ya vikao hamsini na akaridhika hata bila kujua kosa lake hilo ni uamuzi wake, unaheshimiwa; anasema anapaogopa jela, lakini kama akitokea mwenzake akaamua kukaa jela hata kama akipewa nafasi ya kuomba msamaha mpaka atakapojua kosa lake nae pia anastahili kusikilizwa.

Kwenye maisha kila mmoja wetu hupitia njia zake kufikia malengo aliyojiwekea maishani, tusilazimishane njia aliyopitia fulani na wengine wote waifuate, huo sio ustaarabu, kila mmoja wetu abakie na uhuru wake wa kuchagua muhimu asivunje sheria.
Refer Rugemalira na uhujumu uchumi
 
Acha kupotosha. Winnie Mandela hakutaka kabisa mandela aombe msamaha. Tena hakutaka kabisa kuwe na mapatano kati ya wazungu na weusi. She was very radical on that.....
Soma au fatilia historia yako vizuri, huna haja ya kejeli nk winnie alifanya sana lobbying ili Nelson awe huru miaka ya 69 na 70, baadaye naye alipata kesi kutoka kwa apartheid regime akakaa jela kwa miezi kadhaa , hapo ndo alipata elements za radicalism ,
 
Ukiwa nje unajikuta shujaa, unajikuta huwezi kuomba msamaha kwa kile qmbacho hujatenda ili mradi utoke ndani. Ukiwa ndani unaloyaka ni kutoka nje tu kwa njia yoyote. Inafika muda uko tayari hata kukubali lolote ili uachiwe. Ndiyo maana watu wengi walikubali kuingia makubaliano ma dpp ili mradi waungane na familia zao.
Wanakutesa kisaikolojia. Mama yake alifariki na hakuruhusiwa kuhudhuria hata msiba. Hujui ni maneno gani na vitesho alivyokuwa akipewa.
Shukuru Mungu hujapitia alichokipitia.
Kuna watu uwa wanakiri hata kuua kwa kukaa tu na polisi wakafanyiwa mahojiano kumbe hata hawajaua. Na huko ni Marekani ambako polisi hakupigi katika mahojiano lakini kile kitendo cha kukaa na polisi masaa mengi mtu anajikuta anachoka akili anakubali kila wanachotaka kusikia.
Hii inafahamika mkuu
Wahenga wanasema kabla hujaanza mbio , agana na nyonga...

Kabla vijana hawajiita wanaharakati ,lazima wajue what it takes to be one ,
 
Kwa mujibu wa andiko lake , kosa la kabendera ni kuomba msamaha, ilhali hajafanya kosa au jinai
Binafsi nimemuelewa sana mtoa mada , mwanaharakati hataikiwi at any time ku compromise msimamo wake in return to anything., Tangible or intangible.

Richard nixon aliwahi kuwa padorned na rais Gerrard ford , kwa kosa ambalo hata hakuwahi kufanya .it is said to be the controversial pardon of all the times .
Hii ndio nimeiona leo lakini hata kama yamepita hoja yako ni ya kudumu.
Ni kweli, kama Mbowe angekubali kuomba ule msamaha na kutoka jela kwa msamaha kamwe asingekuwa na heshima milele na isinge futa kuwa ni gaidi maana kuomba msamaha ni kukiri kosa na watawala walitaka iwe hivyo.
 
Ila kwa leo kwa kuwa Mzee Pascally Mayalla Mwandishi mkongwe Huyu Sina budi kumwomba Radhi, ndugu, kaka yangu Pascally Mayalla nakuomba radhi, niseme wazi kama usingekuwa ulichukua kadi ya chama Cha mapinduzi na kushiriki kugombea uchaguzi mchafu ningenunua Dume la ng'ombe na kuja kwako kuomba radhi ndivyo tufanyavyo sisi wamalawi punde ukibaini ulimkosea mwanaume.

Naomba radhi ila naomba kabendera akamatwe Tena aruidishwe rumande achunguzwe.

Naitwa Sifi leo.
Apology accepted
P
 
Back
Top Bottom