Tuliooa kwa mahari ndogo tuje tuseme lolote juu ya jambo letu hili

Tuliooa kwa mahari ndogo tuje tuseme lolote juu ya jambo letu hili

Wakati unatoa mahari ya 700,000= ilikuwa Mwaka gani Mkuu?
Kwanini hukusoma vizuri nilichokiandika ? Soma tena nilichokiandika kisha uulize swali upya kwa kile nilichokiandika.
 
"Inampoteza mwanamke." How?
Msingi mama wa hizo sherehe ni kujidai wanamuonyesha Mwanamke namna gani ananyimwa haki zake, ananyanyaswa na kujilinganisha na Mwanaume.

Dhana ya haki sawa kwa wote ni sanamu la kichwa cha ng'ombe ndani ya mwili wa chui, na nyinyi mkaona yule kweli ni ng'ombe na si chui. Yaani mnachotaka nyinyi ni kufanana kwa haki na kushindana na sisi. Hiki kitendo ni kumpoteza mwanamke toka katika umbile lake.

Nidhamu ya maisha na asili haitaki kufanana bali inataka kila mtu apate haki yake. Hivi kwa akili ya kawaida,hivi ni sawa kumpa hela sawa mvivu na mchapakazi katika kazi ? Hii ni dhulma, je yuko sawa mwenye akili na asiyekuwa na akili ?Mwenye elimu na asiyekuwa na ekimu ? Jibu ni hapana. Sasa vipi awe sawa Mwanaume na Mwanamke ?
 
Chief! Siyo kwenye Uislamu tu, bali popote pale panapofungwa ndoa kuna muoaji (mtendaji) na muolewaji (mtendewa). hili neno "kuoana" ni matumizi mabovu ya kiswahili. maana msingi wa ndoa ni tendo la ndoa, tendo hilo lina mfanyaji na mfanywaji hivyo hata neno "kufanyana" (nimejaribu kutumia tafsida) ni matumizi mabovu ya lugha pia.
Umepata wapi hii habari ? Maana katika ufungaji ndoa kuna maneno hutamkwa kwa matamko ya wakati uliopita, hilo la kuoana umelipata wapi?

Kwanye Uislamu kuna kuoza na kuoa, hakuna kuozana.
 
Msingi mama wa hizo sherehe ni kujidai wanamuonyesha Mwanamke namna gani ananyimwa haki zake, ananyanyaswa na kujilinganisha na Mwanaume.

Dhana ya haki sawa kwa wote ni sanamu la kichwa cha ng'ombe ndani ya mwili wa chui, na nyinyi mkaona yule kweli ni ng'ombe na si chui. Yaani mnachotaka nyinyi ni kufanana kwa haki na kushindana na sisi. Hiki kitendo ni kumpoteza mwanamke toka katika umbile lake.

Nidhamu ya maisha na asili haitaki kufanana bali inataka kila mtu apate haki yake. Hivi kwa akili ya kawaida,hivi ni sawa kumpa hela sawa mvivu na mchapakazi katika kazi ? Hii ni dhulma, je yuko sawa mwenye akili na asiyekuwa na akili ?Mwenye elimu na asiyekuwa na ekimu ? Jibu ni hapana. Sasa vipi awe sawa Mwanaume na Mwanamke ?
Yeah, that's your opinion.
Msingi wa IWD sio kujilinganisha na wanaume wala sio kujaribu kumshusha mwanaume kwa kujifanya tupo juu au tunalingana na wanaume.

Msingi wa IWD, "is to celebrate women's achievements, to raise awareness about women's equality, lobby for accelerated gender parity ,fundraise for female-focused charities"

Sasa kwanini unadhani mwanamke anatakiwa asiwe na haki ya kwenda shule?
Asiwe na haki ya ku-vote?
Asiwe na haki ya huwa kiongozi?
Asiwe na haki ya kujishughulisha na vitu ambavyo ana uwezo wa kuvifanya kwa sababu ni mwanamke?

Kumbuka, msingi sio kumshindanisha mwanamke na mwanaume, bali ni kumwinua mwanamke kuhakikisha anapata elimu, anapata haki yake ya kumchagua nani awe kiongozi, ana pata haki ya kuchaguliwa kuwa kiongozi, anapata haki ya kushirikishwa kwenye maamuzi yanayomuhusu na vitu kama hivo.
 
Leo niko huku kwa mtindo huu, ila nasikia leo ni siku ya kina mama (Wanawake) duniani maana yake siku zilizobaki ni zetu sisi kina baba, yaani kwa thamani na nafasi ya mwanamke ambaye natakiwa kumpa mara tatu zaidi ya baba, kwa mwaka anaadhimishwa mara moja. Huu ni udogashaji na udhalilishaji wa hali ya juu, ila maskini wenyewe vipofu wanaona sawa, utawaona wamevaa vitenge na kutembea uchi. Salamu zangu ndiyo hizo nawaambia waache habari za siku ya mwanamke duniani, hii ni aina ya udhalilishaji kwake.

Baada ya salamu hizo, narudi kwenye mada kwa mapito haya, asikwambie Mtu,ndoa yenye baraka ni ile ambayo kufungwa kwake mahari yake ilikuwa ndogo sana. Haya si maneno yangu, bali ni maneno yaliyotoka katika kinywa twahara.

Ni nini ndoa na kwanini tunaumizana katika kutoa mahari kubwa bila sababu za msingi hali ya kuwa sote ni wanufaika na wahitaji. Ndoa ni mkataba wa maridhiano baina ya pande mbili,mwanamke akiwa muolewaji kwa mahari waliyokubaliana na mwanamume akiwa muoaji, kwa kukubaliana waishi kwa wema, na kama ikitokea wameachana basi waachane kwa wema.

Tuliokadiriwa kutoa mahari ndogo, tuje tuwaambie vijana na watajaji mahari ya kuwa ndoa ni jambo le kheri,kwahiyo tusiumizane.

Mimi mahari niliyotoa kwa mke mkubwa ilikuwa chini ya Tsh 150,000/- pesa taslimu.

Vijana tuoeni mapema na tuoe sana, wake wawili au watatu au wanne ikibidi ila ukiwa na mmoja kuwa nae lakini uwe na simanzi kubwa ya kwanini uwe na mmoja.
Mimi nilitoa 7,000 tu (elfu saba tu)
 
Yeah, that's your opinion.
Msingi wa IWD sio kujilinganisha na wanaume wala sio kujaribu kumshusha mwanaume kwa kujifanya tupo juu au tunalingana na wanaume.
Kuna tofauti kati ya kauli na vitendo, huko juu nilisem ya kuwa dhahiri ya kauli mbiu zenu ni haki sawa (Hapa nilitumia mfano wa sanamu ya kichwa cha Ng'ombe) lakini vitendo vyenu ni kushupaza shingo zenu katika kushindana na sisi. Hapa ndipo mlipodanganywa.
Msingi wa IWD, "is to celebrate women's achievements, to raise awareness about women's equality, lobby for accelerated gender parity ,fundraise for female-focused charities"
Awareness hiyo inakuwa imemili katika mambo gani ? Kwani kujadili mafanikio ya Mwanamke mpaka iwepo siku maalumu ?

Swali la msingi, ni mafanikio gani ya Mwanamke huwa mnayasherehekea ?
Sasa kwanini unadhani mwanamke anatakiwa asiwe na haki ya kwenda shule?
Asiwe na haki ya ku-vote?
Asiwe na haki ya huwa kiongozi?
Asiwe na haki ya kujishughulisha na vitu ambavyo ana uwezo wa kuvifanya kwa sababu ni mwanamke?
Hakuna aliyepinga mwanamke kusoma.

Suala ku vote tu hili kinaangaliwa kwa jicho la akili na moyo. Kwangu mimi kupiga kura ni jambo haramu kwa wote si mwanaume wala mwanamke, yaani mfumo mzima wa Kidemokrasia ni mfumo wa kishetani (Hili linahitaji mada pweke, ila kwa mukhtasari tosheka na machache hayo kweny hili).

Kadhalika mwanamke ni kiongozi lakini si kiongozi wa umma, bali watoto wake na wale ambao wako chini yake. Kanuni zinasema hivi "Hawato faulu wale ambao jambo lao wataligemeza kwa Mwanamke (Yaani watakao mfanya Mwanamke kuwa kiongozi). Wanawake mna madhaifu mengi sana. Hapa hatuwadogoshi ila maumbile yako hivyo na huo ndiyo ukamilifu wenu.

Wanawake wanaruhusiwa kujishughulisha lakini kwa kuzingatia mazingira salama jwake yeye na si mazingira hatarishi kwake yeye, hili nyinyi hamlitazami, sababu maarifa yenu ni machache na mnaamua mambo kwa hisia na si akili na kuchunga maskahi.

Laiti kama Mwanamke mngejua hadhi na nafasi aliyopewa Mwanamke na Mola wake, hakika msingetumika kama bidhaa, leo msingesikia habari za wanawake wanajiuza, habari za wanawake kadha.
 
Nifundishe Kiswahili kaka. Ila weka akilini hili ya kuwa kuna tamko moja lenye maana zaidi ya moja kulingana na mjengeko wa sentensi au maana. Mfano wa maneno hayo ni hilo "kuoza", kama yalivyo maneno "Kaa", "Paa", "Fua" na kadhalika.

Hakuna "kuoana" katika Kiswahili, rejea kwa Waswahili upate hukumu.
kiswahili = kuoana
english =To marry each other

Hicho ni kitenzi , na ni neno ambalo lipo kwenye lugha ya kiswahili japo nadhani, kwa sababu halitumiki sana na ndiyo maana haulijui.
 
kiswahili = kuoana
english =To marry each other

Hicho ni kitenzi , na ni neno ambalo lipo kwenye lugha ya kiswahili japo nadhani, kwa sababu halitumiki sana na ndiyo maana haulijui.
Chief! Kitenzi kinatokana na kitendo, sasa katika kitendo cha ndoa kuna kufanya na kufanywa (nimetumia tafsida). Maana yangu ni kuwa kitendo cha kumuingilia mkeo ni "kumfanya" (tafsida) na mkeo anapoingiliwa na wewe maana yake "anafanywa" (tafsida) Kwa hiyo kwa nje ni kuwa wewe "umemuoa" mkeo na mkeo "ameolewa" na wewe. Neno "kuoana" limezoeleka katika jamii, lakini kifasihi ni makosa.

Kama ilivyo neno kupigana (yaani piga ni kupige) ndivyo ilivyo neno "kuoana" yaani "umeoa" na yeye "ameoa" hivyo mnatendeana kitu ambacho hakiwezekani kimaumbile. Ila ikitokea mkeo akanunua uume bandia ule wa kuvaa kama chupi halafu ukawa unamuingilia kisha ukimaliza na yeye anavaa uume wake na kukuingilia wewe, hapo ndipo mtakuwa mmekamilisha tendo la "kuoana" ila ni kharamu kwa dini zote hata kwa wapagani hivyo sikushauri ufanye.
 
mahari isizidi ngapi wanaume wenzangu ?
maana kuna mikoa wanaitisha mahari kama uhai
 
kiswahili = kuoana
english =To marry each other

Hicho ni kitenzi , na ni neno ambalo lipo kwenye lugha ya kiswahili japo nadhani, kwa sababu halitumiki sana na ndiyo maana haulijui.
Huna hoja, sasa uache kujitia ujuaji wakati hujui na hujui kama hujui.

Sisi Waswahili hatuna hilo neno "kuoana".

Pili, sarufi ya Kiswahili sawa na sarufi ya Kiingereza.
 
Leo niko huku kwa mtindo huu, ila nasikia leo ni siku ya kina mama (Wanawake) duniani maana yake siku zilizobaki ni zetu sisi kina baba, yaani kwa thamani na nafasi ya mwanamke ambaye natakiwa kumpa mara tatu zaidi ya baba, kwa mwaka anaadhimishwa mara moja. Huu ni udogashaji na udhalilishaji wa hali ya juu, ila maskini wenyewe vipofu wanaona sawa, utawaona wamevaa vitenge na kutembea uchi. Salamu zangu ndiyo hizo nawaambia waache habari za siku ya mwanamke duniani, hii ni aina ya udhalilishaji kwake.

Baada ya salamu hizo, narudi kwenye mada kwa mapito haya, asikwambie Mtu,ndoa yenye baraka ni ile ambayo kufungwa kwake mahari yake ilikuwa ndogo sana. Haya si maneno yangu, bali ni maneno yaliyotoka katika kinywa twahara.

Ni nini ndoa na kwanini tunaumizana katika kutoa mahari kubwa bila sababu za msingi hali ya kuwa sote ni wanufaika na wahitaji. Ndoa ni mkataba wa maridhiano baina ya pande mbili,mwanamke akiwa muolewaji kwa mahari waliyokubaliana na mwanamume akiwa muoaji, kwa kukubaliana waishi kwa wema, na kama ikitokea wameachana basi waachane kwa wema.

Tuliokadiriwa kutoa mahari ndogo, tuje tuwaambie vijana na watajaji mahari ya kuwa ndoa ni jambo le kheri,kwahiyo tusiumizane.

Mimi mahari niliyotoa kwa mke mkubwa ilikuwa chini ya Tsh 150,000/- pesa taslimu.

Vijana tuoeni mapema na tuoe sana, wake wawili au watatu au wanne ikibidi ila ukiwa na mmoja kuwa nae lakini uwe na simanzi kubwa ya kwanini uwe na mmoja.
Ukipendwa na demu wa kimasai Raha sana.
Yaani hata mahali ni ndogo sana.
 
Kusheherekea jmsiyo jambo ubaya ni nini unasherehekea na je ulazima wa kufanya hilo upo na je kuna natija ya kufanya hivyo ?

Ni ipi maana ya kusherehekea siku ya Wanawake duniani ? Sijaona haja hiyo na sababu ninazo.
My dear.. Wacha watu waishi watakavyoo..kusherekea women's day Kuna muuzi Mungu?... Kufanya Sherehe sijui ya birthday Napo.. masheikh wanapinga.... Je nikisherekea kufauli mtihani... nikisherekea mavuno ....

Kuna tatizo Fatawa zimekuwa nyingi... Usisherekee lizika na iddi mbili TU... kusherekea Kuna tatizo gani.....?
 
Mimi hizo zote ulizo zitaja sisherehekei hata moja. Mimi nina sikukuu tatu tu basi kwa mwaka,nazo ni :

1. Kila siku ya Ijumaa kwangu ni sikukuu
2. Idd al Fitri
3. Idd al Adh'ha (Idd ya kuchinja)

Sasa maswali yako yanatakiwa yatokee katika hizo sikukuu tatu hapo juu.

Tanbihi : Hivi sahihi ni "Sherekea" au "Sherehekea" ?
Jurjani...kuwa was Kati na Kati katika Dini...

Mtu akiamua kusherekea achana nae.
.Mimi nafurahi Mwenyezi Mungu kunifikisha mwaka Mpya... Napika pilau langu na soda nakunywa...NALALA.

Hapa kosa langu lipowapi?
 
Back
Top Bottom