Leo nilikua nachanganya zege kipande hiki
View attachment 1695487
haya mazingira ni unforgetable kwangu
kuna apartment ilikua inasimamishwa na boss mtasha wa pale town. Kama ilivyo kawaida watoto wa mjini hawakosi connection za madili wakanistua na mimi sikufanya kosa nikaibukia
ilikua ni ishu ya umwagaji zege tu iliyojumlisha wafanya kazi zaidi ya 50 na ndio ilikua mara yangu ya kwanza kufanya kazi na group kubwa la watu ambalo ndani yake hadi wamama na mabinti walikuwepo
Asubuhi mtasha akaja site akatangaza dau kua kila mmoja atamlipa 25k, raia wakaonekana kutoridhika mi nikawa nawashangaa kwasababu ile pesa niliiona kubwa kulingana na idadi ya watu ilivyokua niliamini ni kazi itakayo kamilishwa masaa machache tu.
zikaletwa mashine za kuchanganyia zege na mimi nikachukua chepe nikajiunga kwenye sector ya kupakia kwenye vindoo.
sasa hii zege ilikua inaenda kumiminwa kwenye floor ya pili huko juu, kwa hiyo ukatengenezwa utaratibu wa wabebaji kupanga mstari kutoka chini ambako zege inachanganywa hadi floor ya mwisho ambako zege ilikua inamiminwa
haikua rahisi kwa mmoja mmoja kubeba zege na kupanda nayo hadi juu na ndio maana uliwekwa mstari ambao mtu wa kwanza anampasia zege mtu wa pili mpaka inafika eneo inayo hitajika
Kutokana na kazi kuambatana na wanawake hasa wamama ikabidi iwekwe sheria ya kipimo cha ujazo wa zege kua ni chepe mbili tu ili kutowaumiza
baada ya masaa takribani kama saba hivi baada ya kula lunch watu wakiwa wamejipumzisha kusubiria round ya pili nikasema ngoja nipande juu nicheki tumefikia wapi maana nilikua nahesabu idadi ya mifuko 53 tuliyoitumia nikawa nishafanya estimation kua robo tatu ya kazi kivyovyote itakua imekamilika kutokana na u expert niliopata kwenye kumwaga vizege vya renta
Aisee nilipopanda kule juu nilichoka, kwani nilikuta ile foundation imesukwa kwa namna ya kipekee. Nondo zilisukwa za kutosha halafu space ya kuijaza ile zege kutoka juu mpaka chini ilikua inanifika usawa wa paja na mi nishazoea space ya renta kutoka chini ni inch 5 tu leo hii nimekutana na hii shuguli
halafu ukicheki upana wa lile eneo lilikua ni kubwa sana kiasi cha kufanya kazi tulioifanya ionekane kama ni robo kazi huku eneo kubwa likiwa tupu bila zege
Hapa nikawa nawakumbuka wale wadau waliokua wanadai pesa iongezwe nikajisema daah wale miamba walikua na jicho la tatu walifika hii angle ila kutokana na kujifanya mjuaji nikawapinga