Tuliotembea umbali mrefu kwa miguu kwa sababu yoyote ile tukutane hapa

Tuliotembea umbali mrefu kwa miguu kwa sababu yoyote ile tukutane hapa

Wewe umewahi kutembea umbali gani kwa wakati mmoja?

Karibia wote humu tumewahi kuwa watoto wa kijijini!
Shule ya msingi niliyosoma ilikuwa 3km kutoka home,hapo Kuna watu wanakaaa mbali zaidi ya hapo lakini daily school wanaenda na kurudi.
 
Wewe umewahi kutembea umbali gani kwa wakati mmoja?

Karibia wote humu tumewahi kuwa watoto wa kijijini!
Wakati nipo primary nilikuwa natembea 6 Km daily.3Kwenda tatu kurudi.
Msimu wa kulima maharage mashamba yetu yalikuwa umbali mrefu tu lkn kwenda shamba masaaa matatu mpaka 4 kurudi masaa matatu mpaka 4.Mnatoka Nyumbani saa kumi na moja mnafika shamba saa mbili.Hapo mnachapa Mguu hasa.
Nimeenda Sekondary nilikuwa Nina kawaida ya kumwambia mzee atume nauli ili nipande basi tulikuwa tunabana hela.Tunakatiza shortcut ya pori natoka school saa kumi na mbili nafika home saa nane tisa au kumi.Huo umbali sio mdogo.Sijui ni km ngapi lakini ni nyingi
 
Samsung yangu inasema nimetembea step 346,890 sijui ni sawa na umbali gani!?
 
Nakumbuka nilikuwa kidato Cha nne wakati huo tulikuwa tunafanya mock..siku hiyo tulikuwa na mtihani tukatoka jioni..kulikuwa na mvua kubwa magari shida mjini dar..nilitembea kutoka fire to mbagala..niliumwa miguu siku mbili..
 
Niliwahi tembea nmemaliza chuo nkatoa bahasha za application zangukibao kama 20 hv nkaanzia tabata relini kuanza kutembea na kusambaza hzo applctn kwny kila kiwanda nilichokuwa nakiona nilitembea mpka airport viwanda vyote hvyo hakuna ambacho sikuingia... cha ajabu sikuwahi kuitwa hata interview tuu mpka leo hii
Mjini connection.
 
Hivi jamani hili neno ni root much au ni route xxxx... yaani hakuna hata wa kunirekebisha! Kiranga uko wapi? Halafu kuna siku niliwahi kuandika packed badala ya parked na sijamsikia mtu akinirekebisha
Warekebishaji wanadai mshahara wa Sekretari siku hizi.

Wamechoka kutoa huduma ya bure.
 
Binafsi nimewahi kutembea umbali takribani kilometer 100.

Ilikuwa ni safari ya kwenda na kurudi na ilinigharimu siku moja ya kwenda na siku ya pili ya kurudi.

ilikuwa nimeelekea msibani na nilikuwa na nauli ya kwenda tu, kwa sababu nikapata company ya mtu ambaye hakuwa hata na hiyo ya kwenda tukaungana na kuanza kupasua pori mdogo mdogo.

Safari ilihusisha kupanda na kushuka milima, mvua ilinyesha na kukatika karibu mara nne ila hatukukata tamaa.

Ninajua watu wametembea kwa miguu umbali mrefu kwa sababu nyingi zikiwemo:
kukoswa nauli
kutafuta kazi
Kuepuka hatari
hakuna namna ya kusafiri
na sababu nyingine nyingi ...

karibu utujuze
Kigarama mpaka Bukoba mjini
Bukoba mjini mpaka Kamachumu
Km 120 - kuanzia saa 11 alfajiri mpaka saa tatu usiku.. mfukoni nikiwa na sh 40.. 1988
 
Zaidi ya 120km, nilitoka wilaya ya Rungwe (saivi Busokelo) eneo linaitwa Rwangwa mpaka Mbeya mjini..bahati mbaya sijui cha shortcut wala nini kwahyo nanyoka tu na barabara. Nilitoka kule saa kumi na moja alfajiri mpaka saa mbili usiku ndo naingia Mbeya mjini, form three kipindi hicho. Nilitoroka home nikaenda kule wakawa hawanitaki kwahyo kunisema kila Siku, nikashundwa kuvumilia
Mkuu acha masikhara asee...

Lwangwa - mbambo- Tukuyu- kiwira- ndaga- uyole...

Ulitisha saana[emoji119]
 
Nilitembea kwa mguu kutoka dar mpaka zenji nilipofika zenji nikaambiwa mwenyeji wangu hayupo kwa wiki nzima ikabidi nirudi tena dar siku hiyohiyo
 
Kutembea kilometa 100 kwa siku moja ni ngumu sana. Fikiria mkimbiaji wa marathon anakimbia kilometa 42 Kwa masaa mawili.

Sasa huyo mkimbiaji km 100 anaweza kukimbia kwa saa sita.

Sasa ndo mtu wa kawaida atembee km 100 kwa siku moja??
 
Back
Top Bottom