Tony Laurent
JF-Expert Member
- Jan 5, 2011
- 5,606
- 7,032
kALEnga kidamali umenikumbusha mabali sana. Miaka hiyo tumekwenda machungani na watoto wenzangu tukafika mahali tukakutavkuna mti wa mwembe huko porini. Tukaoana maembe kwenye matawi ya juu yakiwa yameiva na yana mvuto hasa. ( yale maembe yanayokuwa kadhaa kwenye fungu moja)
Basi tukakubaliana tufanye mashindano ya kuuparamia ule mwembe ili kuyawahi yale maembe kule mtini. Kwamba atakayewahi kuyafikia, basi ndiye atakuwa mshindi na maembe yale yatakuwa yake. Basi nikakwea kwa spidi kubwa na kuwashinda wenzangu, huku uchu wa kula embe ukiwa umenijaa tele. Nilipoyafikia, bila kufanya ukaguzi wa mazingira ya eneo la tukio, nikayaparamia maembe ili niyachume kabla wenzangu hawajafika.
Ile nashika kile kikonyo kwa ajili ya kuchuma yale maembe, nilipigwa sindano kadhaa matata sana za manyigu, hadi nikachanaganyikiwa na kupoteza mwelekeo. Niliangua kilio kikubwa hatari. Sijui hata nilishukaje kwenye ule mti. Maana nilishitukia nipo chini. Na kichwa kilikuwa kimenyolewa upara. Manundu ya kutosha yakatokea kichwani, kichwa kinauma balaa. Habari ya kuchunga ikaishia hapo, ikabidi nirudi nyumbani huku nalia kwa maumivu makali.
Basi tukakubaliana tufanye mashindano ya kuuparamia ule mwembe ili kuyawahi yale maembe kule mtini. Kwamba atakayewahi kuyafikia, basi ndiye atakuwa mshindi na maembe yale yatakuwa yake. Basi nikakwea kwa spidi kubwa na kuwashinda wenzangu, huku uchu wa kula embe ukiwa umenijaa tele. Nilipoyafikia, bila kufanya ukaguzi wa mazingira ya eneo la tukio, nikayaparamia maembe ili niyachume kabla wenzangu hawajafika.
Ile nashika kile kikonyo kwa ajili ya kuchuma yale maembe, nilipigwa sindano kadhaa matata sana za manyigu, hadi nikachanaganyikiwa na kupoteza mwelekeo. Niliangua kilio kikubwa hatari. Sijui hata nilishukaje kwenye ule mti. Maana nilishitukia nipo chini. Na kichwa kilikuwa kimenyolewa upara. Manundu ya kutosha yakatokea kichwani, kichwa kinauma balaa. Habari ya kuchunga ikaishia hapo, ikabidi nirudi nyumbani huku nalia kwa maumivu makali.