Tuliowahi kuchunga wakati tukiwa wadogo tukutane hapa

Tuliowahi kuchunga wakati tukiwa wadogo tukutane hapa

Mbio.za kumuacha koboko ukiwa na ng'ombe,au uliwaacha kwanza?
Kundi la mbwa ndio lilisaidia kupoteza makini ya koboko, yaani mbwa wawindaji huwa hawashindwi kizeme walikuwa bado wakimzonga zonga licha ya kuwà mbwa mmoja aligongwa na kupoteza maisha,

Nikatumia nafasi hiyo kukimbia na kuzifuata ng'ombe zilizokuwa umbali wa kama mita 200 hivi niliwatandika bakola za maana ili nao waikimbie hatari ile, na kama ningewaacha nisingeweza rudi tena lile eneo maana ake ingekuwa ni vigumu kujua mdudu yule kuwa kahificha wapi
 
Mleta mada hoyeee!

Basi bwana nilikuwa sipendi kuchunga yaani nikisikia kuchunga kwangu ni majanga hataree! ila wakati mwingine ilikuwa starehe lk mda mwingi majanga kwangu! sababu kubwa nyota yangu!

Siku moja tuko porini bana tuna chunga kundi kubwa sana la ngombe wa Babu takribani kama 200 hivi kwa uchache, kure kwetu mara Kiribho-Tarime ilikuwa kawaida sana tulijigawa kwa makundi! kma matatu hivi! Basi..wakati tunacheza mara

Kwa mbaaali tulisikia watu wanakuja wanaongea kwa sauti za chini mara wanyamaze! bila kusita tukapanda kunako miti mirefuuu sana, kwa mujibu wa mafunzo ya awali ktk lile kundi tuligundua liliambatana na mashangazi zetu km watatu hivi waliungana na wale watu kuja mahali tulipokuwa Marishoni,

kama mnavyo jua zamani tulikuwa tuna chunga mbaliii sana na home porini haswa! kukutana na chatu macho kwa macho, sijui chui , simba ilikuwa kawaida sana ila tuliandaliwa vyema kukabiliana na hii hali kichawi! wanyama wa mwituni walituogopa sisi!

Pia zamani wanyama hatari walikuwa wengi Sana na popote! kwa wafugaji hatukushangaa lkn ukizaliwa huko unatengenezwa kuendana na mazingira yao! hasa kwa mila za huko! km wamasai wa serengeti NP wana zao.

sometimes mnaweza kulala na kula huko huko marishoni sababu mnaondoka na chakula full ngwamba! kwa mfano zamani kuna sehemu iliitwa kun'genyi Kiribho!

yaani huko yalikuwa ni machimbo ya udongo wenye chumvi chumvi mifugo walikula na kunywa kiukweli walikuwa wanapendeza sana hata kwa macho, pia hawaugui hovyohovyo! watu wa Tarime team mnajua hili!

mizigo km hii ya chakula na malazi ya mchungaji walibeba punda maalum wenye mafunzo! kulingana na ukubwa wa kundi la walishaji, kama ilkitokea zamu yako ngombe wamezaa sana ilikuwa sababu pekee ya wewe kupeleka kundi la mifugo karibu na nyumbani kwenu mbali na hapo utasota tu porini!

Basi bwana shangazi na kundi lao kadiri walivo kuwa wana jongea walikuwa wana kaa kimya wanatafuta kimya kimya! ghafla machale yakatucheza!! mimi nikiwa kinala wa machale!

Kikubwa kilichonisaidia Bibi mzaa Mama alisha nitengeneza mwili wangu kiuchawi kitambo sana, na hata leo mwanamke mtia limbwata kwangu cha mtoto! hata humu nawajua kwa kungalia tu,

na wakati huu ulikuwa ni wakati mbaya sana wa vita kule somalia ndo imepamba moto ! yule kiongozi wa kisomali Mohamed Farah Aideed kama mnamjua alikuwa ana tamani sana mifugo kutoka kenya na TZ ili kuwalisha wapiganaji wake!

Naomba kusema kuwa Ogopa sana tena kaa mbali na kuwa mwangalifu na mtu anae kujua vyema, sijakosea narudia... mke, kaka Dada, ambae ni mwema! kwako, basi Bana Shangazi wale walikuwa wamekula cha juu kwa siri ili wauze wale mifugo kwa wapiganaji wa kisomali.

Na ili kupotezea ushahidi sisi ilikuwa tuuuawe, make tulikuwa wadogo tu by that moment! na wao ilikuwa wasepe na wasomali kusiko julikana kupitia nchini kenya, lkn baba hapa nakwambia ngoma ikawa nzito!

Nikawachezesha kichawi!! Si kawaida japo kati ya wale wasomali kulikuwa na mmoja wao alikuwa mzito sana kiuchawi lkn !! na huyu ndo alikuwa group leader wao! alie watia moyo, utajiri huu una mambo wee acha tu!! shangazi walijua fika zindiko la wale mifugo! walitaka ku haribu maksudi!

kilicho tokea jamani!! ndo maana nasemaga uchawi sijui kinga za kichawi msizidharau, Nawashauri vijana kwa wazee, wapende wote sana! but Usimwamini mtu ndugu yako wa kuzaliwa hata km ni msaada mkubwaje, amini kikuracho ki nguoni mwako hawa wahenga hawakukosea hata kidogo!

Lakini kwa wema, upole waliokuwa nao shangazi zangu usingewazania, lkn mimi nilijenga mashaka ya kimya kitambo sana ila sikujionyesha kiasi kwamba waliweza kufanya ubaya mbele yangu wakidhani bado ni mtoto! hii ilinisaidia kuwajua,

hapa napo naomba kusema kuwa hawa watoto / mtoto yeyote usiwadharau kiviiile!! eti hawajui kitu unaleta mwanaume ndani weee! wana akili hao over! na usipime! laiti shangazi yangu angejua nilivo asinge thubutu kwa aibu ile ilyomtesa maisha yake yote hadi kifo chake!!

Hata hivo mwanzoni tulishushuliwa sana, wakatetewa mno na walio watetea!! nikajribiwa pia kichawi mno lkn ikadunda!
mwanzoni lkn babu alijua kitu pale, akaingia mtamboni kimya pia alijua alivo nitengeneza hii ilitusaidia sana kufikia muafaka ..... ntarudi punde kumalizia...
 
Mimi nimechunga sana. Mwaka 1961 mwaka mzima nilichunga na sikupata kuugua. Ije mvua ije jua wewe na mifugo. Ng'ombe akizaa machungani lazima unahakikisha ndama wake anafika salama nyumbani na kama hana uwezo wa kutembea ni jukumu lako kumbeba mpaka nyumbani. Furaha ya kuchunga ni kula matunda pori huko porini na kweli yanajenga mwili sana na pia michezo mbalimbali huko porini. Kwa kweli nilipenda kuchunga.
 
Mimi nimechunga sana. Mwaka 1961 mwaka mzima nilichunga na sikupata kuugua. Ije mvua ije jua wewe na mifugo. Ng'ombe akizaa machungani lazima unahakikisha ndama wake anafika salama nyumbani na kama hana uwezo wa kutembea ni jukumu lako kumbeba mpaka nyumbani. Furaha ya kuchunga ni kula matunda pori huko porini na kweli yanajenga mwili sana na pia michezo mbalimbali huko porini. Kwa kweli nilipenda kuchunga.
Duu kweli watu tuna vipaji tofauti! tofauti kuchunga ngombe? jua lako, mvua yako!
 
Sitosahau kuna ndama mmoja alikua mkorofi balaaa.kumchunga ilikua shughuri sometime alikua ananitoa nduki hizo na akinifikia anaanza kunipiga vichwa.nilikua ndo kwanza na miaka 6.nashukurupembe hakua nazo ndo zilikua zinaota tofauti na hapo angeniua
 
Na kuliua na ngombe moja mzee nikienda nae machungani akichoka analala hapo hapo njiani kumnyanyua shida ilikua inanilazimu kumuacha palepale napeleka wengine narudi na tera la kusukumwa ngombe tunambeba
 
Nakumbuka nilikua mtoto pekee ambae sikuleta ubishi kwenye swala la kwenda kuchunga na kufanya iwe kama kazi yangu, lakini ilinifanya nichukiwe na watu wengi mtaani kwasababu mtaa wote familia yetu pekee ndiyo tulikuwa wafugaji na wengine wote wakulima. swala la kulisha kwenye mashamba ya watu kwangu ilikua kawaida sana.
Ulikuw mpumbavu Sana,unalisha Kwenye mashamba ya watu?
 
Nilikua nachunga mbuzi... Tullikua tunapenda sana kupambanisha mabeberu... Na kupandishia majike
 
Nimechunga sana mbuzi za mzee wangu..afu nilikuwa nainjoy sana kuchunga huku nawinda ndege na manati yangu shingoni
 
Jamani wale wote ambao tumewahi kuchunga wakati tukiwa wadogo kabla hatuja anza shule na hata baada ya kuanza shule yaani ukirudi shule unachunga na zile siku za wikiendi basi wewe ni kwenda porini/malishoni kuchunga mifugo kama vile ng'ombe, mbuzi na kondoo tukutane hapa kuelezea uzoefu wetu pamoja vituko, mikasa na masahibu ya huko porini/malishoni ulipokuwa unachunga.

Mimi nilikuwa nikipenda sana kutokana na zile raha za kupata kila aina za matunda huko maporini pia kulikuwa na kuwinda wanyama wadogowadogo kama vile digidigi, pimbi, sungura pamoja na kanga na kware yaani ilikuwa wewe mchungaji unaporudi unapokelewa kwa heshima Kubwa ukirudi hasa ukiwa na mnyama uliyewinda huko machungoni, yaani ilikuwa kijana anayechunga anajaliwa na kuheshimiwa nyumbani mda wote kabla ya kutoka na baada ya kurudi machungoni anapewa chakula kizuri cha kushiba bila kusahau maziwa ya kutosha hata kama chakula ni kidogo basi atakula mchungaji kwanza wengine mtasubiri baadae wasiowachungaji walitamani kuwa wachungaji kutokana na mchungaji anavyojaliwa pale nyumbani kwetu.

Kingine nilichokuwa nakipenda ni kutembea na jeshi la mbwa wakali waliofundishwa kuwinda huku kila mbwa akiwa kapewa jina lakie kama vile chui, simba, nyati, mbogo, mwitu, jeshi, polisi, n.k

Hawa mbwa kwanza wakati wa kwenda machungoni ilikuwa ni mwiko kuwapa chakula(asiwe mvivu kuwinda) yaani mbwa akiwa na njaa akifika porini dakika kumi nyingi digidigi kadakwa hapo utasikia mbwa akitoa mlio wa sauti kuashiria mimi niende kuna jambo limetokea kwani wakikamata mnyama yeyote hawamli hadi mimi niende nikamchukue kama ni kumalizia kumchinja nifanye mimi na hapo mbwa watafurahi sana kwani kichwa ,miguu,matumbo ya ndani ndio mlo wao yaani nilikuwa nawapikia supu moja matata mno, baada ya kuja huku dsm nimeshangaa kuona supu lile ndio linaitwa kongoro.

Aisee ninayo mengi, hebu share na wewe yako.
My favorite part ilikua ni wabhademi yaani ugali mkubwa wa moto wa kwenye chungu wa asubuhi ukute na maziwa au ng'homele aka bbq iliyopikwa na maziwa plus kisamvu cha kulala utachunga sana na njaa hutasikia hadi jua lizame
 
Nyaru-sare
Hao mashangazi zako walikuwa wameshikwa akili na wasomali, iweje wauze mifugo kisha watokomee kufuatana tena na hao Wasomali?

Kama walikuwa mabinti, nishajua kilichokuwa kinaendelea!
 
My favorite part ilikua ni wabhademi yaani ugali mkubwa wa moto wa kwenye chungu wa asubuhi ukute na maziwa au ng'homele aka bbq iliyopikwa na maziwa plus kisamvu cha kulala utachunga sana na njaa hutasikia hadi jua lizame

Ng’homele aka BBQ!!![emoji39][emoji39]
 
Tupo hapa. Ulichunga upande wa serengeti (ngoreme) au upamde wa tarime?
Mimi nimechungia kwetu ngoreme

Young boy miaka 10 unakabidhiwa ng'ombe 200 ukapambane porini

Enzi hizo lakini mapori hayakuwa makubwa sana

Omongoleme sekeseke kolu bholenga logholo
 
Duu nilikua na chunga mbuzi kabla si ja anza shule sita sahau nili mla kitoto cha mbuzi zizini ila utoto laha Sana ila useme sote tulikua watoto
 
Nyaru-sare
Hao mashangazi zako walikuwa wameshikwa akili na wasomali, iweje wauze mifugo kisha watokomee kufuatana tena na hao Wasomali?

Kama walikuwa mabinti, nishajua kilichokuwa kinaendelea!
Yaani wee!! acha tu! najua fika unacho waza kabisaaa!! kiukweli! Na baba yangu aliwaza hivo! hivooo!!! yaani hakuna mtu mbaya km Ndugu humu Duniani, unamsaidia unamnyanyua lkn mmm! ana akili sana aliyesema ''kikulacho.......
alikuwa na upeo sana sijui yuko wapi kwa sasa ila msemo wa ki- Mungu huu mpaka leo sina jibu halisi!

Walikuwa vijana tu mbona watafutaji, tena wakulima wazuri tu wakitumia hiyo hiyo mifugo! pale home alibakia mmoja tu! tena alikufa! over suddenly! Picha kamili ya ufisadi tulitoa sisi. nduuugu!! pwiii!!!
 
Nimechunga enzi hizo. Nilipenda sana ndama hasa wakati wakitoa mbio. Tukiwa machungani tulipambanisha mabeberu. Matunda pori na maembe, zambarau yalikua hayakatizi.
Maisha yalikua raha sana
 
1996- Tazara- Mbalizi-Mbeya -Tulienda na bro wangu kuchunga mbuzi za dingi Mlimareli karibu na Mtakuja tulipoteza mbuzi watatu wa mzee sitasaha kipigo tulichopewa na mshua...

Tabia za -Machungani
-Kugombanishwa na watu wa rika lako au waliokuzidi umri
-Kufundishwa kupekecha moto
-Kufundishwa kuogelea mitoni
-kucheza kifimbocheza ukiachia fimbo yako chini unachapwa
-kupigwa teke la matako ukiinama nao ni mchezo, kujisajili ni hiari
-Kuchoma vitu vya wizi mashambani mwa watu-mahindi, viazi au mihogo
-kupakana upupu kwenye nguo- ukizubaa mnapo ogelea nguo zako zikipakwa utakubali shoo yake- unaweza rudi nyumbani uchi...

Dah kuna michezo mingi ya kikakamavu ndio maana vijana waliozaliwa miaka ya 80 kushuka chini kuna ukakamavu fulani upo tofauti na wa 90'S na kuendelea...
 
Back
Top Bottom