Tuliowahi kuchunga wakati tukiwa wadogo tukutane hapa

Tuliowahi kuchunga wakati tukiwa wadogo tukutane hapa

wakishua kaeni pembeni muda wa kujimwaya mwaya huu nakumbuka tulienda kuchunga na dogo mtoto wa mjomba wangu kondoo akawa anamzingua jamaa alivomkamata ikabidi amtie adabu kwa kumla kiboga dah nlicheka sana
 
Kitambo sana, Kuna kuchagua madume ya ng'ombe, kondoo au mbuzi kwa ajili ya kupigana. Nakumbuka tulikuwa na dume moja matata lilikuwa na pembe kali balaa. Kuna siku tulimpiganisha na dume kutoka Kijiji Cha jirani yule dume alichomwa pembe ya mbavuni mpaka utumbo ukawa unaonekana ndo ikawa sababu ya mpaka kuuzwa. Pia kutega tetele au mnawaita njiwa poli, mitego ya wanyama wadogo wadogo mpaka raha. kutengeneza ng'ombe wa udongo kisha unawapiganisha.
Bila shaka utakuwa mtu wa nyumbani kwetu tabora au shinyanga..
 
Sitasahau siku moja nilisikia mbwa wakitoa milio fulani hivi pembeni ya kichaka kimoja nikaenda fasta kwa bashaha zote nikajua kuna mnofu umedakwa, ile kufika asalaaaaleee! Nikakuta mbwa mmoja anamalizia kukata roho kagongwa na nyoka aina ya koboko Kubwa hilo, zile mbio nilizotoka nazo hapo ilikuwa ni hatari yaani niliondoa ng'ombe haraka na kulihama lile pori na sikuwahi rudi tena lile pori. Niliambiwa koboko akikugonga nusu saa haifiki usha fika akhera sasa nikawa nimejawa hofu hatari.
Dah! pole sana mkuu
 
Nakumbuka mengi coz am cowboy. Ntakuja na story kamili but kwa kuanzia

1. Kupewa maziwa mengi kabla ya kutoa mifugo na baada ya kumrudisha
2. Tulikuwa tunashindana nani atakaeenda ndani zaidi ya Pori
3. Kuwinda ndege na sungura
4. Kuogelea kwenye lambo la kunyweshea mifugo ,hapo panakuwaga na Mademu wanaochungaga nyumban
5. Hamna kitu raha kama mbuzi kuzaa mapacha kwenye zamu yako ,unawabeba vitoto vya mbuzi kifuani hadi nyumbani
Aisee wewe ni lijendi.
 
Dah, tulikuwa tunachunga na madada makubwa makubwa! Tukiwa machungani yanatupa tenda ya kwenda kutoa ng'ombe karibu na mashamba ya watu halafu ukirudi yanakuzawadia kwichi-kwichi hotai una-do
Magepu hayo mkuu
 
Mimi kitu yenyewe sitaisahau ile kulima na ng'ombe, unaamshwa SAA tisa au kumi usiku, tulikuwa tunaita sheli, yaana unaenda kulima ukiwa na wenge la usingizi, njiani full kufakamia visiki
 
Nakumbuka mengi coz am cowboy. Ntakuja na story kamili but kwa kuanzia

1. Kupewa maziwa mengi kabla ya kutoa mifugo na baada ya kumrudisha
2. Tulikuwa tunashindana nani atakaeenda ndani zaidi ya Pori
3. Kuwinda ndege na sungura
4. Kuogelea kwenye lambo la kunyweshea mifugo ,hapo panakuwaga na Mademu wanaochungaga nyumban
5. Hamna kitu raha kama mbuzi kuzaa mapacha kwenye zamu yako ,unawabeba vitoto vya mbuzi kifuani hadi nyumbani
Huku unalia Kama mbuzi meeeee! Meeeeee!!! Huku anakufuata
 
Nimechunga sana hadi namaliza kidato cha nne. Niliyowahi kukutana nayo au kuyatenda ni mengi sana.

Nikiwa mdogo, siku moja nachunga pamoja na babu yangu, nikasikia mbuzi Analia kwa mfululizo. Nikataka kwenda ili niangalie kulikoni mbuzi alie hivyo? Babu yangu akanizuia nisiende huko na badala yake akaanza yeye kunyata kuelekea huko, name nikimfuata kwa nyuma. Kufika tukamkuta Chatu anajiviringisha akiwa amemkaba mbuzi. Babu alikuwa napenda kuchunga na Gobole lake. Aliachia risasi ya kwanza, lakini chatu akaendelea kumkunja mbuzi, akaongeza ya pili, hapo chatu alitulia kidogo. Alipoongeza ya nne, chatu alijikunjua na kumwacha mbuzi lakini tayari akiwa ameshakufa. Chatu alihangaika na baadae akatulia nae akiwa ameshakufa.

Nikiwa mkubwa nachunga mwenyewe, siku moja nikiwa nimetulia juu ya kichugu na mbwa wawili niliokuwa nao, niliwaona mbuzi wakiwa wanakimbia kutoka kichakani. Nikiwa nashangaa na kujiuliza kulikoni, mara mbwa mmojawapo alitoka juu ya kichuguu kwenda kule mbuzi wanakokimbia. Ghafla nilimsikia akitoa kilio cha uchungu sana. Kuchunguza vizuri nikiwa juu ya kichunguu, nikamwona nyoka akiwa amemng’ata yule mbwa na alipomwachia, nilimwona mbwa anadondoka chini na akawa anaangaza angaza tena. Nikawaza hapa nitafuatia mimi. Nilitoka nduki kwa spidi ambayo sijui ilitoka wapi. Nilienda mbali sanakuleamabko ng’ombe walikuwa wakielekea ng’ombe kuwasubiri wanifikie.

Niliwahi kuwapeleka ng’ombe kunywa maji mtoni, mto ambao una vichaka sana. Ng’ombe waliingia kunywa maji name nikabaki ng’ambo nawasubiri. Ajabu ni kwamba walirudi wachache sana kuliko idadi yao. Nikaingia mtoni na kufuata uelekeo walioufuata kunywa maji. Nikawaona ng’ombe wengi wako ng’ambo nyingine ya mto kwenye shamba la Mwalimu Nyerere. Niliwafuata na kuwaondoa kwa woga sana, maana sikutegemea kuwamaliza mle shambani bila kukamatwa. Nikawa nikiwapeleka pale natangulia huko wanakovukia kuingia shambani.

Nimekula sana karanga, Mihogo na Mahindi kwenye mashamba ya watu na hata ya kwetu.

Nimecheza michezo mingi sana huko, nimewinda wanyama na ndege na kuloa samaki kwenye mabwawa.
 
Jamani wale wote ambao tumewahi kuchunga wakati tukiwa wadogo kabla hatuja anza shule na hata baada ya kuanza shule yaani ukirudi shule unachunga na zile siku za wikiendi basi wewe ni kwenda porini/malishoni kuchunga mifugo kama vile ng'ombe, mbuzi na kondoo tukutane hapa kuelezea uzoefu wetu pamoja vituko, mikasa na masahibu ya huko porini/malishoni ulipokuwa unachunga.

Mimi nilikuwa nikipenda sana kutokana na zile raha za kupata kila aina za matunda huko maporini pia kulikuwa na kuwinda wanyama wadogowadogo kama vile digidigi, pimbi, sungura pamoja na kanga na kware yaani ilikuwa wewe mchungaji unaporudi unapokelewa kwa heshima Kubwa ukirudi hasa ukiwa na mnyama uliyewinda huko machungoni, yaani ilikuwa kijana anayechunga anajaliwa na kuheshimiwa nyumbani mda wote kabla ya kutoka na baada ya kurudi machungoni anapewa chakula kizuri cha kushiba bila kusahau maziwa ya kutosha hata kama chakula ni kidogo basi atakula mchungaji kwanza wengine mtasubiri baadae wasiowachungaji walitamani kuwa wachungaji kutokana na mchungaji anavyojaliwa pale nyumbani kwetu.

Kingine nilichokuwa nakipenda ni kutembea na jeshi la mbwa wakali waliofundishwa kuwinda huku kila mbwa akiwa kapewa jina lakie kama vile chui, simba, nyati, mbogo, mwitu, jeshi, polisi, n.k

Hawa mbwa kwanza wakati wa kwenda machungoni ilikuwa ni mwiko kuwapa chakula(asiwe mvivu kuwinda) yaani mbwa akiwa na njaa akifika porini dakika kumi nyingi digidigi kadakwa hapo utasikia mbwa akitoa mlio wa sauti kuashiria mimi niende kuna jambo limetokea kwani wakikamata mnyama yeyote hawamli hadi mimi niende nikamchukue kama ni kumalizia kumchinja nifanye mimi na hapo mbwa watafurahi sana kwani kichwa ,miguu,matumbo ya ndani ndio mlo wao yaani nilikuwa nawapikia supu moja matata mno, baada ya kuja huku dsm nimeshangaa kuona supu lile ndio linaitwa kongoro.

Aisee ninayo mengi, hebu share na wewe yako.
Kipindi cha mvua kuchunga nikugumu unakuta Zizi limekuwa tope, huko porini sasa ndiyo balaa maji na tope, alafu bado kunyeshewa na mvua ukiwa machungani, kwenye raha nilikuwa napenda kuchunga na rafiki zangu tunaenda na kibiriti tukifika huko tunaiba Maindi na viazi, kwenye mashamba ya wanakijiji tunaenda kuchoma, kiukweli nilikuwa nainjoy, ila sitasahau kuna siku tulikuwa tukicheza mbuzi [emoji238][emoji238] wakaingia kwenye shamba la mwanakijiji mm ndiye nilikuwa mdogo nikatumwa niende kuwafuata nilikuta mwenye shamba ana panga alinikamata nakuanza kunipiga ubapa hadi alinijeruhi mkono wa kushoto, wazazi walikaa wakaongea na mambo ya kijijini yalivyo ile kesi iliisha ila hadi leo nina kovu la kukatwa na panga mkononi
 
Mimi kuchunga kulinisababishia ninusurike kufa kifo kimoja hatar sana. Tangu siku hyo mzee ilibd aajir kijana kwa ajili tu ya kuchunga mbuzi.
Huyo kijana yeye alikuwa na kinga ya kifo?
 
Sitasahau siku moja nilisikia mbwa wakitoa milio fulani hivi pembeni ya kichaka kimoja nikaenda fasta kwa bashaha zote nikajua kuna mnofu umedakwa, ile kufika asalaaaaleee! Nikakuta mbwa mmoja anamalizia kukata roho kagongwa na nyoka aina ya koboko Kubwa hilo, zile mbio nilizotoka nazo hapo ilikuwa ni hatari yaani niliondoa ng'ombe haraka na kulihama lile pori na sikuwahi rudi tena lile pori. Niliambiwa koboko akikugonga nusu saa haifiki usha fika akhera sasa nikawa nimejawa hofu hatari.
Mbio.za kumuacha koboko ukiwa na ng'ombe,au uliwaacha kwanza?
 
Sema wachungaji wengi kwenye umri wa balehe huwa wanafanyaga mapenzi na ngombe, mbuzi, kondooo, tupe hii experience mkuu.
Nyanda za juu kusini ndiyo mambo yao ili wawe kama Bakhresa,Ushirombo huku,ni chale matakoni tu,ng'ombe wanazaana hatari
 
Kama ulikuwa hudandii ng'ombe kama farasi basi hujachunga.

Kama ni mkubwa sana unavizia akiwa anakula majani unatumia kichwa chake kama ngazi,kosea timing akanyage kidole cha mguu unaouacha chini[emoji1][emoji1][emoji1],niliishatolewa kucha kwa mkasa aina hii.

Kosea mambo yote ila my friend usijevaa koti lenye kofia juu ukapita karibu na ng'ombe atakuzingua vibaya sana(sio hawa ngombe wenu wa maziwa).

Kuna mang'ombe ilikuwa ukizubaa tu yanaenda kwenye mashamba ya watu.

Kingine ngombe nayeye ana tabia kama ya mbwa,akijutisha ukajaa,anakuoshea, ila ukimkazia anatulia.
Bila kusahau walikuwa na majina.ukimuita anaitika na kutii amri
 
kALEnga kidamali umenikumbusha mabali sana. Miaka hiyo tumekwenda machungani na watoto wenzangu tukafika mahali tukakutavkuna mti wa mwembe huko porini. Tukaoana maembe kwenye matawi ya juu yakiwa yameiva na yana mvuto hasa. ( yale maembe yanayokuwa kadhaa kwenye fungu moja)

Basi tukakubaliana tufanye mashindano ya kuuparamia ule mwembe ili kuyawahi yale maembe kule mtini. Kwamba atakayewahi kuyafikia, basi ndiye atakuwa mshindi na maembe yale yatakuwa yake. Basi nikakwea kwa spidi kubwa na kuwashinda wenzangu, huku uchu wa kula embe ukiwa umenijaa tele. Nilipoyafikia, bila kufanya ukaguzi wa mazingira ya eneo la tukio, nikayaparamia maembe ili niyachume kabla wenzangu hawajafika.

Ile nashika kile kikonyo kwa ajili ya kuchuma yale maembe, nilipigwa sindano kadhaa matata sana za manyigu, hadi nikachanaganyikiwa na kupoteza mwelekeo. Niliangua kilio kikubwa hatari. Sijui hata nilishukaje kwenye ule mti. Maana nilishitukia nipo chini. Na kichwa kilikuwa kimenyolewa upara. Manundu ya kutosha yakatokea kichwani, kichwa kinauma balaa. Habari ya kuchunga ikaishia hapo, ikabidi nirudi nyumbani huku nalia kwa maumivu makali.
...kunyolewa upara tena?...wapi huko mkuu...manyigu yenyewe sawa
 
Nakumbuka nilikua mtoto pekee ambae sikuleta ubishi kwenye swala la kwenda kuchunga na kufanya iwe kama kazi yangu, lakini ilinifanya nichukiwe na watu wengi mtaani kwasababu mtaa wote familia yetu pekee ndiyo tulikuwa wafugaji na wengine wote wakulima. swala la kulisha kwenye mashamba ya watu kwangu ilikua kawaida sana.
 
Back
Top Bottom