Maili tatu
JF-Expert Member
- Aug 8, 2020
- 830
- 1,070
Hakuna mfugo uliokuwa unanikera kama mbuzi kipindi tunachunga..mbuzi wetu hao sijui walikuwa ni mbuzi wa aina gani,ukienda nao maporini huko wanakupa kashkash sana , Mara mbuzi ishrini wamekimbia vle,kumi wameingia mashambani yan tafrani tu walikuwa hawashib sijui na huku una kazi ya kufanya umepewa shuleni inabidi uifanye huko huko machungoni mana ukirudi bomani kwenu hamna uhakika wa kusoma kwani taa ni moja tu na labda utumie na kuni za jikoni...ila porini ilkuwa raha kwa kiasi chake michezo na matunda ni bwerere,shida wengine ilkuwa ni kusoma halafu muda huo huo unatakiwa uchunge mbuzi kibaooo....
Karibia kila aliyewahi kuchunga amekutana na hizo tamu na changamoto za kuchunga.Jamani wale wote ambao tumewahi kuchunga wakati tukiwa wadogo kabla hatuja anza shule na hata baada ya kuanza shule yaani ukirudi shule unachunga na zile siku za wikiendi basi wewe ni kwenda porini/malishoni kuchunga mifugo kama vile ng'ombe, mbuzi na kondoo tukutane hapa kuelezea uzoefu wetu pamoja vituko, mikasa na masahibu ya huko porini/malishoni ulipokuwa unachunga.
Mimi nilikuwa nikipenda sana kutokana na zile raha za kupata kila aina za matunda huko maporini pia kulikuwa na kuwinda wanyama wadogowadogo kama vile digidigi, pimbi, sungura pamoja na kanga na kware yaani ilikuwa wewe mchungaji unaporudi unapokelewa kwa heshima Kubwa ukirudi hasa ukiwa na mnyama uliyewinda huko machungoni, yaani ilikuwa kijana anayechunga anajaliwa na kuheshimiwa nyumbani mda wote kabla ya kutoka na baada ya kurudi machungoni anapewa chakula kizuri cha kushiba bila kusahau maziwa ya kutosha hata kama chakula ni kidogo basi atakula mchungaji kwanza wengine mtasubiri baadae wasiowachungaji walitamani kuwa wachungaji kutokana na mchungaji anavyojaliwa pale nyumbani kwetu.
Kingine nilichokuwa nakipenda ni kutembea na jeshi la mbwa wakali waliofundishwa kuwinda huku kila mbwa akiwa kapewa jina lakie kama vile chui, simba, nyati, mbogo, mwitu, jeshi, polisi, n.k
Hawa mbwa kwanza wakati wa kwenda machungoni ilikuwa ni mwiko kuwapa chakula(asiwe mvivu kuwinda) yaani mbwa akiwa na njaa akifika porini dakika kumi nyingi digidigi kadakwa hapo utasikia mbwa akitoa mlio wa sauti kuashiria mimi niende kuna jambo limetokea kwani wakikamata mnyama yeyote hawamli hadi mimi niende nikamchukue kama ni kumalizia kumchinja nifanye mimi na hapo mbwa watafurahi sana kwani kichwa ,miguu,matumbo ya ndani ndio mlo wao yaani nilikuwa nawapikia supu moja matata mno, baada ya kuja huku dsm nimeshangaa kuona supu lile ndio linaitwa kongoro.
Aisee ninayo mengi, hebu share na wewe yako.
Mabaharia wanajulikana tu![emoji3][emoji3][emoji3]Ngoja nisubir ushuhuda wa wale waliobaka mifugo wanayochunga
Wewe bila shaka ulikuwa unachunga ng’ombe wa shule SESESCOTumechunga sana kwenye majaruba ya mpunga kule Sengerema mwanzoni mwa miaka ya 90. Life ya kuchunga was so awesome.... Many things were happening including kukutana na wanyama wakali kama nyoka pamoja na kuzama mtoni.
"kuwanyamilija tu"[emoji3][emoji3]usukumani raha sanaMachungani 'tumebada' sana panzi, tega sana ndege na samaki (mumi/kambale), winda sana kware... tumeiba sana viazi na miwa.
Raha iliyoje kuchunga na mademu, ni zamu kwa zamu tu... kazi yako ni 'kuwanyamilija' tu unapewa tunda!
Nilikuwa shule Mkuu, ng'ombe wa shuleDah! ni hatari kwahyo ulikuwa unachunga kipindi uko shule ama nyumbani?
Ufugaji wa namna hii mara nyingi Kanda ya ziwa mikoa mingine kwa wamasai,, yaani nimekumbuka mbali sana! Maisha yale niliyafurahia sana kwa kipindi chote kile,,wazee wa lubaga mpo???Jamani wale wote ambao tumewahi kuchunga wakati tukiwa wadogo kabla hatuja anza shule na hata baada ya kuanza shule yaani ukirudi shule unachunga na zile siku za wikiendi basi wewe ni kwenda porini/malishoni kuchunga mifugo kama vile ng'ombe, mbuzi na kondoo tukutane hapa kuelezea uzoefu wetu pamoja vituko, mikasa na masahibu ya huko porini/malishoni ulipokuwa unachunga.
Mimi nilikuwa nikipenda sana kutokana na zile raha za kupata kila aina za matunda huko maporini pia kulikuwa na kuwinda wanyama wadogowadogo kama vile digidigi, pimbi, sungura pamoja na kanga na kware yaani ilikuwa wewe mchungaji unaporudi unapokelewa kwa heshima Kubwa ukirudi hasa ukiwa na mnyama uliyewinda huko machungoni, yaani ilikuwa kijana anayechunga anajaliwa na kuheshimiwa nyumbani mda wote kabla ya kutoka na baada ya kurudi machungoni anapewa chakula kizuri cha kushiba bila kusahau maziwa ya kutosha hata kama chakula ni kidogo basi atakula mchungaji kwanza wengine mtasubiri baadae wasiowachungaji walitamani kuwa wachungaji kutokana na mchungaji anavyojaliwa pale nyumbani kwetu.
Kingine nilichokuwa nakipenda ni kutembea na jeshi la mbwa wakali waliofundishwa kuwinda huku kila mbwa akiwa kapewa jina lakie kama vile chui, simba, nyati, mbogo, mwitu, jeshi, polisi, n.k
Hawa mbwa kwanza wakati wa kwenda machungoni ilikuwa ni mwiko kuwapa chakula(asiwe mvivu kuwinda) yaani mbwa akiwa na njaa akifika porini dakika kumi nyingi digidigi kadakwa hapo utasikia mbwa akitoa mlio wa sauti kuashiria mimi niende kuna jambo limetokea kwani wakikamata mnyama yeyote hawamli hadi mimi niende nikamchukue kama ni kumalizia kumchinja nifanye mimi na hapo mbwa watafurahi sana kwani kichwa ,miguu,matumbo ya ndani ndio mlo wao yaani nilikuwa nawapikia supu moja matata mno, baada ya kuja huku dsm nimeshangaa kuona supu lile ndio linaitwa kongoro.
Aisee ninayo mengi, hebu share na wewe yako.
Kizugwangoma,mwabaluhi,mwabayanda nkTumechunga sana kwenye majaruba ya mpunga kule Sengerema mwanzoni mwa miaka ya 90. Life ya kuchunga was so awesome.... Many things were happening including kukutana na wanyama wakali kama nyoka pamoja na kuzama mtoni.
Ng'wabhaluhiWewe bila shaka ulikuwa unachunga ng’ombe wa shule SESESCO