Tuliowahi kudhulumiwa na Mtandao wa Tigo Tanzania tukutane hapa

Tuliowahi kudhulumiwa na Mtandao wa Tigo Tanzania tukutane hapa

Mwaka jana mwezi wa 11 nilinunua kifurushi cha tigo 5000 kwa njia ya tigo-pesa mpaka leo sijapata hiyo huduma nimepga huduma kwa wateja mpaka leo naambiwa 24hrs
Huu ndio mchezo wao Mimi naugulia kwa zaidi ya wiki 2 sasa
 
Niliambiwa kuna tatizo la kimtandao baada ya kujiunga bando la 2000 na kuwasha data kwamba wangenitaarifu mtandao ukikaa sawa
Lakini sikuona hiyo sms hadi siku ya nne nilipoamua kujiunga tena na mtandao ulikuwa umerudi na maisha yakaendelea kwa hiyo elfu mbili ilienda kavu
Tunaweza vp kuwashtaki hawa watu au serikali inamikakati gani kudhibiti hii

Sent using Jamii Forums mobile app
Naamini TCRA watapita katika uzi huu na kujiuone vilio vya Watanzania wachache tunaowakilisha wengi walionje ya JamiiForums
 
Daah hii ilinitokea pia 2017 nlituma hela haikwenda na majibu yao ndo hayo hayo wanakwambia tatzo la mtandao subiri masaa 72, yakiisha ukiwafata tena wanakwambia subiri masaa 24... miezi na miaka ikapita hela yangu ikapotelea hewani.
Huu utapeli sio kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
Kumbe hili janga ni kubwa. Tigo jitokezeni mtoe majibu ya utapeli huu
 
Tigo ya mwaka gani hiyo, mbona sahiz naona wanajitahid kuliko mtandao flan wa mabosi,
Saa zingine huwa kunatokea matatizo ya kiufund tu mfano Voda tangu juzi internet haipo, kukatwa salio ndo usiseme hayo n matatizo ya kimtandao yapo kwote,

Sent using Jamii Forums mobile app
Mzee si unaona nimeweka hadi tarehe? Unadhani sijui ninachoandika
 
Nishawai enda pale makumbusho ,hakuna mlinzi aliyeweza zuia nikuwa mkali kupita maelekezo..niliweka vocha ya 5000 ghafla kifurushi kinagoma kuunganisha kutazama salio ni zero, nilianza na yule binti wa huduma kwa wateja toa maneno sana..nikamwambia kesho nakuja nimevaa hivi ukiweza andaa polisi kabisa

Walirudisha ndani ya nusu saa
Kumbe ndio dawa yao
 
Na Mimi jana nimeunga bundle la Internet kupitia Tigo Pesa hadi leo sijapata na Huduma kwa Wateja wanasema wanashughulikia najua ndio imetoka hii
 
Na Mimi jana nimeunga bundle la Internet kupitia Tigo Pesa hadi leo sijapata na Huduma kwa Wateja wanasema wanashughulikia najua ndio imetoka hii
Pole sana Mkuu, karibu tuungane kufichua utapeli wa Tigo Tanzania
 
Hata Vodacom Wana tabia ukifuatilia wanakupiga kalenda.
Mnamo Jumanne ya Tarehe 11 mwezi huu (Februari 2020) nilinunua kifurushi cha Internet kwa njia ya Tigo Pesa. Ndugu zangu wana JamiiForums yakapita masaa 24 bila ya kupewa kifurushi wala kupewa taarifa yoyote.

Nilichukua hatua ya kuwapigia Huduma kwa Wateja, nikajibiwa kifurushi changu kitawezeshwa baada ya masaa 24. Kwa hakika nilidanganywa.

Nikawa nikiwapigia simu kila baada ya masaa 24 lakini hakuna nilichosaidiwa zaidi ya kuambiwa nisubiri masaa 24 mengine na hadi leo hakuna nilichorudishiwa si fedha wala si kifurushi.

Huu mtandao umekubuhu kwa huduma mbovu lakini cha kushangaza sasa wamehamia hadi kuiba fedha za wateja.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwaka 2013 nilikuwa natumia line hii 071X008580. Kuna deni nilikuwa nadaiwa kama Tshs.35,000/-, Nikamtumia mdai wangu kiasi hicho mida ya saa tano usiku, Sikupata meseji yeyote ya uthibitisho, kuwa ujumbe wangu umefika kwa mlengwa japokuwa salio langu lilikuwa limekatwa tayari, na nilipojaribu kupiga call centre niliambiwa kuna tatizo la network mafundi wanajaribu kulitatua, nitapata mrejesho baadaya ya masaa 24. Ilinibidi nizisubirie hizo saa, japokuwa mdai wangu alionyesha kama kutoniamini kwa kile nilichomwambia...baada ya masaa hayo kupita sikupokea ujumbe wowote..Nilifuatilia takribani mwezi bila ya majibu yenye uhakika..zaidi ya tatizo letu la kiufundi likitatulia utaona ujumbe huo mfupi. Nizungumzavyo mpaka leo sikupokea ujumbe wowote na hela yangu ilikatwa. ilipita mwaka sikuwa na imani tena na hii kampuni...Mpaka leo siitaki hata kuisikia...Majuzi nilipiga hiyo namba yangu ikapokelewa na bidada mmoja nasikia yupo mbeya.


Sent using Jamii Forums mobile app
daaahh pole sana rafk

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mnamo Jumanne ya Tarehe 11 mwezi huu (Februari 2020) nilinunua kifurushi cha Internet kwa njia ya Tigo Pesa. Ndugu zangu wana JamiiForums yakapita masaa 24 bila ya kupewa kifurushi wala kupewa taarifa yoyote.

Nilichukua hatua ya kuwapigia Huduma kwa Wateja, nikajibiwa kifurushi changu kitawezeshwa baada ya masaa 24. Kwa hakika nilidanganywa.

Nikawa nikiwapigia simu kila baada ya masaa 24 lakini hakuna nilichosaidiwa zaidi ya kuambiwa nisubiri masaa 24 mengine na hadi leo hakuna nilichorudishiwa si fedha wala si kifurushi.

Huu mtandao umekubuhu kwa huduma mbovu lakini cha kushangaza sasa wamehamia hadi kuiba fedha za wateja.
Tarehe hiyo hiyo mimi nimenunua luku 10 000 sijapata token wala hela haijarudi nimekua nikipiga simu kila siku mpaka customer care wakanitukana na uzuri nimewarikodi so kama kuna njia yeyote ya kupata haki yangu nijulishe nasubiri wanirudishie tu hela yangu ili nikafute usajili
 
Daah hii ilinitokea pia 2017 nlituma hela haikwenda na majibu yao ndo hayo hayo wanakwambia tatzo la mtandao subiri masaa 72, yakiisha ukiwafata tena wanakwambia subiri masaa 24... miezi na miaka ikapita hela yangu ikapotelea hewani.
Huu utapeli sio kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
me nilikwangua vocha vibaya nikawapelekea mwaka 2O13 nikaja kupigiwa simu ya kupewa vocha yangu mwaka 2O19 hata nilishasahau hivyo hata wewe vumilia tu,issue yako itasovika tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani mimi na kampani yangu soootee tumeshajitoa tigo ni bora KUBAKI BILA MAWASILIANO KULIKO KUWA NA TIGO na ndio maana tumehamia 073 home sweet home
 
me nilikwangua vocha vibaya nikawapelekea mwaka 2O13 nikaja kupigiwa simu ya kupewa vocha yangu mwaka 2O19 hata nilishasahau hivyo hata wewe vumilia tu,issue yako itasovika tu

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahahaaa serious? 2013 had 2019 mbona wana utani hawa watu.

Bas wacha niwasubrie siku wakinikumbuka watanirudshia hela yangu
 
Nilinunua kifurushi cha mini Kabang cha Sh 650 kupitia TIGOPESA, wakaja kunikata shilingi 8000. Yaani nimenunua mara moja, ila zinaingia SMS kadhaa za TIGOPESA muamala kila moja imemega salio hadi ikafika 8000.

Ilikuwa mwaka 2015 hii, nikajaribu kuwasiliana na huduma kwa wateja kupitia facebook maana kuwapigia hadi waje wapokee ni majanga. Huko wakaniambia wanashughulika nalo, ila sikuona lolote. Nikiwa nikija kuwakumbusha kuhusu hela yangu, halafu mtu mwingine yeyote akireply comment yangu wanamjibu. Ila kwangu wanauchuna kama vile hawakuiona. Tena kidharau


Nilikuja kulalamika miaka miwili baadaye yaani 2017 nikawatajia hadi mwezi tatizo lililotokea wakaniambia watanipigia simu ila hadi leo kimya.

Kiukweli namiliki line ya Tigo tu kwasababu ina watu wengi wanaijua na ndiyo namba yangu kongwe, ila isingekuwa hivyo ningekuwa nishabadili natumia line na kuivunjilia mbali

Halafu huduma kwa wateja wana mwanamke akipokea, sijui ana ugomvi huko alipotoka. Nakumbuka mwaka 2016 nilipiga nilipopata tatizo la kifurushi kupitia TIGOPESA, nilijibiwa kimkato tena kwa kisirani kisha simu ikakatwa. Yaani kama vile unamsumbua mwanamke kwa kumtongoza, akaamua kukukatia simu. Ndiyo alichofanya
 
Back
Top Bottom